Michae Maluwe kumbe na wewe hujui Kingereza?

Michae Maluwe kumbe na wewe hujui Kingereza?

Huyu Michael Maluwe wa zamani Sana. Nilianza kumuona anatangaza kipindi Cha michezo ITV 1999/2000 miaka Kama 24 iliyopita
Tamasha la Michezo ITV,,kila jumapili Saa nane Mchana
 
Nashangaa mtangazaji upo AZAM unashindwa kwenda kwa rasi simba kuna gift macha kuna Patrick nyembera yaani mtangazaji wa AZAM akiongea kiingereza natamani nijifiche chini ya meza.
 
Mlishawahi sikia kiingereza cha mama yenu Ndalichako au Magufuli ?

"I will put you in ze kongrachulasheni "
 
Una Mawazo Kama Majirani zetu Wakenya.....!

Inaitwa assimilation..! Wenyewe wanatuona WaTz tuko nyuuuuma eti hatujui Kiingereza...teh teh..!

Sasa Nenda Kwa Wenye kujiamini na Lugha zao kama India,China n.k ..Hawa hawashobokei Lugha za Watu..!

Ifike Mahali tujiamini na Lugha zetu.
Unawezaje kujiamini na lugha ya kimaskini kama kiswahili? Hii lugha ni ya humuhumu tu.. ukivuka tu Nakonde border haina maana.
 
Mimi ninadhani kutojua kiingereza vizuri itangazwe tu kama aina mojawapo ya ULEMAVU.
 
Sasa hapo unashangaa nini? Kwani kiingreza ni lugha yake? Kwani muingreza akikosea kiswahili naye utamcheka? Wakati wa ukoloni kulikuwa na watu wanaitwa manyapala, walikuwa wakijua kuongea kiingreza hata cha kuombea maji wakajiona wazungu wakatumika na wazungu kunyanyasa wasiojua kizungu! Naona na wewe uanajiona mzungu kwa kujua kizungu! Pole sana kwa utumwa huo!!!
Manyapala = Manyapara
Mbona na wewe hata kiswahili tu haujui..!!😛😛😛
 
Mechi ya KenGold inaisha
Mtangazaji Michael Maluwe anamuuliza kocha mzungu
""You create the chance.......
Badala ya ''you created some chances.....

Kweli lugha ngumu
Kwani lazima uongee kama wazungu!!?

Kwani hao wazungu wanaongea kiswahili hizuri kama sisi!!?

Bado tunaushamba wa kufikiri kuongea kiingereza kizuri ndio kuelimika sio!!?

Kwani wachina,warusi.wanongea kiingereza kama wazungu!!?nani anawazodoa!!?wakenya na wanaijeria je!!?

Tuache ushambaw mkuu!

Kwani we hapo hujaelewa Nini sasa!!?
 
Kukosea kidogo lugha ambayo tunajifunza darasani haikutakiwa tujihisi aibu.

Nadhani kuna tatizo fulani kwenye kichwa cha Mwafrika. Kuna ubaya gani kuongea kiingereza kama vile Mzungu anavyoongea kiswahili?
 
Mwanzoni angeweka "actually " kama jamaa mmoja aliyehojiwa na radio moja huko Kenya. Actually zilikuwa zaidi ya 100.
 
Mechi ya KenGold inaisha
Mtangazaji Michael Maluwe anamuuliza kocha mzungu
""You create the chance.......
Badala ya ''you created some chances.....

Kweli lugha ngumu
Hivi ni mchaga wa wapi tena?
 
Nimeshawahi kuwa na demu wa kizungu alikuwa ana enjoy sana broken ingilishi yangu nashangaa wewe mswahili unajifanya much know kupitiliza
Kabisa
Hata mie na English yangu ya ku unga unga na ni mbovu kweli kweli lakini kuna waJamaica walikuwa wanaifurahia sana MAn....
 
Mechi ya KenGold inaisha
Mtangazaji Michael Maluwe anamuuliza kocha mzungu
""You create the chance.......
Badala ya ''you created some chances.....

Kweli lugha ngumu
Toa maelezo yote ili ueleweke vizuri ni nini kinaongelewa baina ya wahusika. Unaonaje kwa ambayo angeanza na 'did you...?' hiyo ndio ingeonesha ni swali.
 
Toa maelezo yote ili ueleweke vizuri ni nini kinaongelewa baina ya wahusika. Unaonaje kwa ambayo angeanza na 'did you...?' hiyo ndio ingeonesha ni swali.
Did you?hapo haiitajiki maana football ni mchezo wa wazi kila mtu kaona walivyo create some chances ila wakashindwa kuzitimia
 
Back
Top Bottom