Michango ya Rambirambi za Misiba kwenye makundi ya Whassap imegeuka mzigo kwa wachangiaji

Michango ya Rambirambi za Misiba kwenye makundi ya Whassap imegeuka mzigo kwa wachangiaji

Mimi binafsi Sina magroup na wala Sina mpango wa kua na magroup sijui ya tuliosoma nao, mara nyingi huwa ni umbea tu unaendelea humo, watu niliosoma nao primary mpaka chuo na tukawa marafiki Basi tunawasiliana binafsi,sio mpaka tukutane kwenye group, Nina group Moja tu la ofisini ambako ni lazima kujoin, Hilo ndo hua nachangia hata misiba na harusi maana ni watu ambao nipo nao Kila siku na Ninajua nikipatwa na jambo watanibeba.
Lakini mtu ambae tangu tuachane shule hajawahi hata kunijulia hali, halafu from nowhere naombwa mchango wa harusi kwangu ni big NO.(bora hata rambirambi nitachangia lakini sio harusi)
Kama hayo magroup yanatija kwenye maisha yako endelea nayo lakini Kama unaona kabisa mzani haubalance yaani faida yake ni ndogo Sana ukilinganisha na stress unayopata kwasababu yake achana nayo,Baki na magroup machache yenye tija.
 
d
Kuna group lilianzishwa miaka ya 2017 la members wa hapa JF lilikuwa na members 75 kama sijasahau, ila kila siku huku kwenye group kila member kafiwa anahitaji mchango, sasa nani atamchangia mwingine? Baadae tukaamua kuweka utaratibu wa kuchanga 10k kila mwezi kuwe na shida kusiwe na shida. Baada ya miezi kama mitano admin akadelete group lile la whatsapp na hela zetu kamega. Ukija huku jukwaani JF anajifanya great thinker sana. Baada ya kuopoa kimwana humu kapotea jukwaani na iD kaitelekeza, kumbe alienda unganishwa kwenye gridi ya taifa bila kujijua. Saivi anashinda huko X ana kazi ya kuretweet maneno ya biblia. Hela za rambi rambi sio za kuzila. 😏
duu hahaha
 
Kuna group lilianzishwa miaka ya 2017 la members wa hapa JF lilikuwa na members 75 kama sijasahau, ila kila siku huku kwenye group kila member kafiwa anahitaji mchango, sasa nani atamchangia mwingine? Baadae tukaamua kuweka utaratibu wa kuchanga 10k kila mwezi kuwe na shida kusiwe na shida. Baada ya miezi kama mitano admin akadelete group lile la whatsapp na hela zetu kamega. Ukija huku jukwaani JF anajifanya great thinker sana. Baada ya kuopoa kimwana humu kapotea jukwaani na iD kaitelekeza, kumbe alienda unganishwa kwenye gridi ya taifa bila kujijua. Saivi anashinda huko X ana kazi ya kuretweet maneno ya biblia. Hela za rambi rambi sio za kuzila. 😏
Nani huyo?? 😡
 
Ukiwa member wa makundi ya Whassap, ya kifamilia, ukoo, mliosoma wote primary, O-Level, High School, Chuo, Kazini, Mtaani Kuna mzigo mzito sana wa michango ya rambirambi inakungoja.

Kila kundi unakuta lina wastani wa watu 20 mpaka 50 na mengine yanafika watu 100. Katika makundi haya, ndani ya miezi miwili unakuta angalau kuna msiba katika kundi mojawapo. Wakati mwingine unakuta zaidi ya makundi 3 kuna msiba na unahitajika mchango!.

Michango ya misiba imekuwa ni kitanzi kizito sana kwa members ila wanaugulia kimyakimya ili wasionekane wabaya.

Na Michango ya Rambirambi kimsingi imetengenezwa in such a way siyo ya hiyari kivile japo haluna kulazimishwa kwa nguvu bali kuna kulazimishwa kisaikolojia na pia jinsi hiyo michango ilivyo haiko kwa namna ya kuonyesha upendo au kuguswa na msiba, bali imegeuka kuwa kama VIKOBA kuwa Ukichanga basi na wewe utachangiwa!. Usipochanga basi hakuna hata kuitisha rambirambi kwenye kundi ili kila mtu atoe kwa hiyari yake bila kujali policy ya kundi!.

Katika maisha haya ambayo uchumi unazidi kuwa mgumu, Hii michango ya rambirambi katika makundi ya Whassap imegeuka shubiri kwelikweli.
Jitoe tu kwenye hayo makundi acha kutuchosha. Kwani imelazimishwa kuingia?

Kuna haja gani kuingia kwenye Group ambayo hamuwezi kuchangia kwenye raha na shida.
 
Wamekutema kwa sababu huchangii hela au huchangii hata salamu?
Kutoa salamu nilikuwa mara chache labda mara moja kwa mwezi, Nadhani ilikuwa ni kuhusu michango, maana walikuwa wanawazodoa wote ambao hawakutoa na nilikuwa naona jina langu kwenye list ya wasiotoa michango lakini napiga kimya, ikaeenda mpaka wakanichoka na kunitema.
Nilikuwa natoa michango kama naona ni sahihi kutoa kama kufiwa mtoto au mzazi, sasa ikawa hata ya hospitali na ya harusi nikaona hii sasa ni kuchoshana
 
Kutoa salamu nilikuwa mara chache labda mara moja kwa mwezi, Nadhani ilikuwa ni kuhusu michango, maana walikuwa wanawazodoa wote ambao hawakutoa na nilikuwa naona jina langu kwenye list ya wasiotoa michango lakini napiga kimya, ikaeenda mpaka wakanichoka na kunitema.
Nilikuwa natoa michango kama naona ni sahihi kutoa kama kufiwa mtoto au mzazi, sasa ikawa hata ya hospitali na ya harusi nikaona hii sasa ni kuchoshana
Kuweka list ya wasiotoa michango, kuishi maisha ya kutegemea michango, ni kuendekeza umasikini.

Kila mtu anatakiwa kuwa na bima ya maisha si tu kuweza kukidhi gharama za mazishi, bali pia hata kuacha kiasi fulani kwa familia.

Na hata vikundi vinavyochangishana vinaweza kununua bima za maisha za vikundi ambazo zitakuwa na gharama rahisi zaidi, zinazotabirika zaidi na zenye ufanisi zaidi.

Tunapenda mifumo ya kijima tu ya kuchangishana kwa tukio hata kama kuna mifumo mipya yenye ufanisi zaidi.
 
Kule X anajiita nani?

Kuna group lilianzishwa miaka ya 2017 la members wa hapa JF lilikuwa na members 75 kama sijasahau, ila kila siku huku kwenye group kila member kafiwa anahitaji mchango, sasa nani atamchangia mwingine? Baadae tukaamua kuweka utaratibu wa kuchanga 10k kila mwezi kuwe na shida kusiwe na shida. Baada ya miezi kama mitano admin akadelete group lile la whatsapp na hela zetu kamega. Ukija huku jukwaani JF anajifanya great thinker sana. Baada ya kuopoa kimwana humu kapotea jukwaani na iD kaitelekeza, kumbe alienda unganishwa kwenye gridi ya taifa bila kujijua. Saivi anashinda huko X ana kazi ya kuretweet maneno ya biblia. Hela za rambi rambi sio za kuzila. [emoji57]
 
Kuweka list ya wasiotoa michango, kuishi maisha ya kutegemea michango, ni kuendekeza umasikini.

Kila mtu anatakiwa kuwa na bima ya maisha si tu kuweza kukidhi gharama za mazishi, bali pia hata kuacha kiasi fulani kwa familia.

Na hata vikundi vinavyochangishana vinaweza kununua bima za maisha za vikundi ambazo zitakuwa na gharama rahisi zaidi, zinazotabirika zaidi na zenye ufanisi zaidi.

Tunapenda mifumo ya kijima tu ya kuchangishana kwa tukio hata kama kuna mifumo mipya yenye ufanisi zaidi.
Wabongo wameshazoea kupewa msaada na kuombaomba
Hii nchi wakiona mtu anaendesha maisha yake mwenyewe wanaanza uchuro wa anajifanya anaringa subiri apate shida tutamuona anakuja kuomba msaada, huyo wanaemuogelea hivi unakuta kajitosheleza na wala hawezi hata siku moja kuomba asaidiwe.
Huu ujamaa ulitulemaza sana, sasa mtu ukishaamua kuwa na familia, inakuwaje siku una mgonjwa hospital unategemea eti washkaji ndio wakuuguzie mtoto wako au mke wako, wakati anaoa na kuzaa hakujua kuwa hii kazi yake kuwahudumia.
 
Dah! Mleta uzi inaonekana unakereka sana watu wanavyofiwa. Kama hutaki kuchangia hata msiba wewe ni mtu wa hovyo. Pia kulikuwa hakuna haja ya kuleta huu uzi wa kipumbavu hapa... ukiona grupu linakuboa unajitoa tu. Mimi nilijitoa magrupu yote ya watsapp hadi la familia. Ila niliwaambia mkinihitaji nipo mnicheki.
 
Back
Top Bottom