Miezi 30 ya Rais Samia madarakani: Pamoja na kujikwaa kwenye Bandari, bado ni Rais mwenye record bora ya kukuza uchumi wa Tanzania kwa kipindi kifupi

Kichefuchefu,yaani siku nzima umeiharibu k kwngu.
Ukweeli unahubiri ukiwa umekaa kwenye kiti??NENDENI vijijini
 
Nitakubali endapo ukija na supported facts... otherwise, nakuchukulia kama uliyopotea njia kama wenzako wenye mitizamo kama wewe.

Kuandika tu 'Rubbish & nonsense' hakukufanyi wewe kuonekana bora. Zaidi zaidi inakufanya uonekane mjinga.
UMETUMWA
 
Miamia
 
Saaafi
 
Hamna jipya! Nchi haiwezi kwenda tena BOT kwishney! Dully amekatiwa madolari ghafla amegeuka mwekezaji Uganda. Mama kilaza mkubwa kiuchumi
 
Tuendelee na mtori nyama chini ziko tutazikuta tu.
Ila mmh.
 
Kwa ajili ZAKO wewe Dola sio uchumi???Eheee Pato la taifa linapimwa kwa hicho ulichoandika Hapo JUU. SHAME UPON YOU
KAKOJOE ULALE
Dola sio uchumi bwashew,Pato la Taifa linaoimwa Kwa pesa yeyote mnayotumia au hata ukitaka kupika kwa.pesa ya Urusi ni wewe tuu kucheza na exchange rates.

Huna ulijualo kwenye uchumi wewe nguchiro
 


Natoa maoni yangu nikitambua umuhimu wa miradi ya kimkakati iliyofanywa na serikali ya awamu hii. Tanzania ni yetu sote, tufurahie kasi ya mabadiliko iliyoletwa na Rais Samia.

Sekta ya ajira,
Ninacho kubaliana na wewe ni kwamba ajira za sekta ya umma zinaweza kutengenezwa na serikali. Yaani, serikali ikiamua kutengeneza ajira hizi, inacho hitaji kufanya ni kutoa kibali cha kuajiri. Kibali hiki hakitegemei sekta zingine zozote ambazo sio za serikali. Ila unaposema kwamba serikali ya awamu hii imetengeneza ajira ambazo sio za sekta ya umma, unakuwa umetu dangaya kwasababu serikali haiwezi kuamuru sekta binafsi kuajiri. Mashirika yaliyo kwenye sekta binafsi huajiri muda wowote kulinga na mahitaji yao bila idhini yoyote kutoka serikalini.

Viwanda na uzalishaji,
Elewa kwamba uchumi wa viwanda sio uzalishaji tu. Mchakato unaofuata baada ya uzalishaji ni kutafuta masoko ya bidhaa na kuweza kupiku bidhaa zingine ambazo tayari zipo sokoni. Sisemi kama hili haliwezekani ila bidhaa kuuzika sana kwenye nchi mbalimbali ni suala la diplomasia zaidi na sio kuwa na bidhaa bora. Mfano, makubaliano ya kibiashara yanaweza hutuwezesha kuwa na bidhaa ughaibuni lakini je, unamtegemea nani anunue maji ya Kilimanjaro nchini Uingereza?. Uchambuzi wako haujitoshelezi kwasababu sekta za ujenzi na nishati sio mfano mzuri wa serikali iliyo wasaidia wananchi wake kwa ufanisi katika suala zima la uzalishaji.

Sekta ya usafirishaji,
Ningependa kufahamu takwimu hii inajumuisha nini haswa kwenye sekta ya usafirishaji na mnufaika wa fedha hizi unazosema zimekusanywa. Nashindwa kuelewa serikali inaweza kuinufaika kwa njia ipi kwa kupitia sekta hii. Labda kama serikali ingekuwa ina miliki kikamilifu dadala, mabasi, reli, malori na ndege zote nchini. Labda kupitia tozo kwenye mafuta?, kwasababu serikali sio mnufaika mkuu wa mapato kwenye sekta ya usafirishaji.

Mfumuko wa bei,
Ningependa kufahamu chanzo cha kuongozeka kwa fedha kwenye mzunguko. Wanaoweza kuwa na maelezo kamili ni mabosi wa benki kuu. Vile vile fedha kuongezeka kwenye mzunguko huathiri dhamani ya sarafu yetu na kwasababu hiyo sio jambo la kusheherekea sana. Fahamu kwamba njia kuu ambayo serikali inaweza kutumia kuzuia ongezeko la bei ya bidhaa yoyote ni kupitia tozo au kodi. Mfumuko wa bei unaweza kusababishwa na kodi, kupanda kwa bei ya bidhaa kwenye soko la kimataifa, kupanda kwa gharama za uzalishaji n.k. Mara nyingi, serikali haiwezi kuingilia kati bei za bidhaa zinazouzwa kwa jumla au na wasambazaji. Hii ina maanisha kwamba uwezo wa serikali kuingilia kati bei za bidhaa za kila siku sio mzuri. Katika nchi yenye misingi ya kidemokrasia, serikali haiwezi kuwa pangia bei wafanya biashara.

Sekta ya kibenki,
Graph yako moja inaonyesha kwamba mikopo kwa sekta binafsi imeongezeka. Mikopo hii ni afya kwa sekta binafsi na ni chachu katika ongezeko la fedha kwenye mzunguko. Lakini je, mikopo hii inatoka serikali au inatoka kwenye sekta binafsi?. Mikopo hii inawa wezesha wananchi kufanya shughuli zao kwa wepesi lakini huwezi kuitunuku serikali kwa hatua hii. Kama nilivyo changia awali, ongezeko la fedha kwenye mzunguko ni ishara ya kupungua kwa dhamani kwa sarafu yetu. Ili kuhakikisha hii, tutazame exchange rate ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani kuanzia mwaka 2000 mpaka 2023 ambayo ndiyo reference point. Utagundua kwamba dhamani ya shilingi ya Tanzania imepungua sana.

Nafikiri badala ya benki kuu kuendelea kutoa nakala mpya za fedha kwenye mzunguko, ni vyema kufahamu kwamba "The government is always the biggest spender". Serikali inatakiwa ijitahidi kuwekeza zaidi kwenye sekta mbali mbali. Hii ni njia "Natural" ya kuongeza fedha kwenye mzunguko bila kuharibu dhamani ya sarafu au kuingilia mifumo huru ya kiuchumi. Elewa kwamba unaweza kuongeza fedha kwenye mzunguko lakini ukiitoa hii fedha, huwezi kuirudisha benki kuu tena.

Uchambuzi huu umefanywa kwa kutilia maani kazi iliyofanywa na serikali ya awamu hii. Fahamu kwamba National Bureau of Statistics pekee ndiyo yenye uwezo wa kuchapisha takwimu za Tanzania. Uchambuzi siyo mbaya, ila nina mashaka ya chanzo cha takwimu zako
 
Kichefuchefu,yaani siku nzima umeiharibu k kwngu.

Ukweeli unahubiri ukiwa umekaa kwenye kiti??NENDENI vijijini
Sasa Kwa taarifa Yako huko Vijijini ndiko wanamtambua Samia ni nani.

Huko wamechongewa Barabara ambazo hazikuwepo Sasa Wana uhakika wa kuuza mazao.

Huko Vijijini wamefungiwa minara ya simu ambayo haikuwepo Sasa hakuna Utapeli wa bei

Huko Vijijini wamefikishiwa umeme ambao haukuwepo,Sasa Kijijini ni kama mjini

Huko Vijijini wamejengewa Zahanati na Vituo vya Afya wakapelekewa na matabibu hakuna kwenda mjini

Huko Vijijini wanafikishiwa maji ya Bomba via Rukwasa wanamtambua Samia ni mkombozi

Nyie wa Mjini ambao hata kura hampogi ndio mnaeopoka upuuzi tuu
 
Jibu la vyote hivyo hapo Juu ni
kuongezeka Kwa utitiri wa miradi across sectors sio Jiwe alikuwa na visingizio viingi vya kujenga bwawa na Sgr tuu.

Maelfu ya Ajira Mpya,kulipa malimbikizi,kupandisha madaraja vyote hivi vimeongeza aggregate demand mtaani bila kuisahau sensa.

,kupanuka Kwa sekta ya Kilimo

,kurejea Kwa sekta ya makazi/real estates iliyokuwa imejifia,

na kikubwa kuliko vyote kilichochochea hivyo vingine ni kurejea Kwa uwekezaji

kutokana na policy stability za awamu ya 6 hivyo kuchochea expansion ya uchumi kiujumla.
 
Uchambuzi hafifu kama mtaa wa Lindi na Msimbazi
 
Vitu vingi Samia alivyofanya alikuwa anamalizia pale alipoishia hayati, kwahiyo hamna jipya atoke tu MADARAKANI.
Anamalizia?! Bwawa la Nyerere alilikuta likiwa limefikia asilimia ngapi? SGR aliikuta ikiwa imefikia asilimia ngapi?! Yaani mtu anayetoka Dar kwenda Mwanza unasema anamalizia safari yake wakati ndo kwanza yupo Morogoro?! Pole sana, Samia kama ilivyo kwa Magufuli wote wametekeleza ilani ya chama chetu kwa sababu hata Magufuli na yeye kuna mengi sana aliyofanya lakini yalianzia utawala wa JK, na kuna wengine watafuata kumalizia ya Samia, na hata wakiingia CHADEMA nao yapo ya Samia watakayomalizia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…