Miezi mitatu nimetotolesha vifaranga 500 vya kuku wa kienyeji

Miezi mitatu nimetotolesha vifaranga 500 vya kuku wa kienyeji

Nakupa mbinu

Nirahisi hakikisha unakuwa na kuku kwaajili ya kuatamia tu na wengi kwaajili ya kutaga tu sasa Unafanya vipi 👇🏼
Chukulia mfano wa kuku 30 Tenga 15 wa kutaga na 15 kuatamia Hawa 15 wa kutaga wapatie Kila tete 5 jogoo mmoja hii ni kupata mayai Bora yenye mbegu za kutoa vifaranga Hawa kuku wafungie sehemu Moja baada za zoezi la utagaji kuku wakianza kuatamia wawekee mayai ya kisasa matatu au mawili ili kuwasubirisha wote 15 waanze kuatamia kwa pamoja wakitimia wagawie mayai kulingana na umbo LA kuku hakika mayai haya hayavuki siku Saba Hadi 10 tangu yatagwe utawawekea wote kwa siku moja baada ya zoezi hili hakikiksha kuku wale wengine 15 unawarudisha kwa jogoo baada ya siku 14 wataanza kutaga mayai tena sasa hayo unaweza kuuza kwasababu wale wengine Bado hawajaanza kutotoa ikifika siku ya 7 tangu waanze kuatamia unaweza kwenda kuangalia mayai yenye vifaranga na kutoa yale yasio na vifaranga utatumia kwa Chakula sasa ikifika siku ya 21 kuku wote watakuwa wameanza kutotoa hakikisha kila kifaranga aliyekamilika unamtoa na kupeleka kwenye bluda (sehemu ya joto) ili kuacha nafasi na kumfanya kuku yule aendelee kuatamia akijua Bado hajapata watoto Fanya hivyo kwa kuku wote Hadi mayai uliyowapatia yatotolewe yote kabla ya mayai hayo kuisha muwekee mayai yale ya kisasa ili aendelee kubaki pale kwenye kiota baada ya kuwa mayai yote yametotolewa sasa unaweza chukua mayai mengine kutoka kwa wale kuku 15: wa kutaga na kuwagawia tena kuku hawa waendelee kuatamia kwa mwenzi mwingine hakikiksha mayai hayavuki siku saba tangu yatagwe utarudia zoezi la ukaguzi kama kawaida baada ya siku saba ili kutoa mayai yasiyokuwa na vifaranga unaweza fanya zoezi la kutotolesha kwa namna hii kwa miezi 3 ndio unawatoa wale kuku kwenye viota ili wapumzike kwa mwenzi mmoja tena au miwili kwa namna hii utapata kuku wengi
Asante sana kwa darasa, naomba kujifunza utaalamu wa kuchanganya chakula kwa kuku wa kienyeji ili kupunguza gharama
 
Nzuri sanaa mali inapatikana shambani hii ndo maana yake.
 
Kheri kwenu wapendwa nimeamini kila kitu ni nia na kujituma.

Mwezi wa saba nilinunua tetea 30 na jogoo 3 wanaotetea mwezi wa nane nikapata vifaranga 280 na mwezi huu wa tisa 220.

Na bado naendelea kuatamishiae. Lengo kufika mwezi wa kumi na mbili niwe na kuku 1000 wa kienyeji pure.

NJIA NAZOTUMIA KUFANIKISHA MALENGO HAYA
1: Mimi mwenyewe ndiyo msimamizi mkuu naamka saa11 alfajili kuosha makopo na kulisha chakula.

2: Nimetenga kuku 15 wanaoatamia na wengine15 wanataga tu.

3: Vifaranga navilea kwa joto la mkaa.

4: Kwenye mabanda ya vifaranga kwa siku nafanya ukaguzi Mara 4.

5: Eneo la kufugia ni kubwa na nimezungushia fesi.

6: Dawa za kuku zipo za kutosha za maji na unga.

Karibuni
Hongera Sana Mkuu Haya ndo mambo nayopenda kuyasikia Usisahau Tu Kumrudishia Mungu Kadiri ya Wema alokutendea kwa Mwaka ulopita
 
Kuku wa kienyeji jau sana
Mara wanakula mayai
Wanagombania sehemu ya kutaga na nimetenga sehemu nyingi

Majogoo yanapigana
Mara vifaranga kukanyagwa

Dawa ni mashine tuu ya kutotoleshea
 
Kheri kwenu wapendwa nimeamini kila kitu ni nia na kujituma.

Mwezi wa saba nilinunua tetea 30 na jogoo 3 wanaotetea mwezi wa nane nikapata vifaranga 280 na mwezi huu wa tisa 220.

Na bado naendelea kuatamishiae. Lengo kufika mwezi wa kumi na mbili niwe na kuku 1000 wa kienyeji pure.

NJIA NAZOTUMIA KUFANIKISHA MALENGO HAYA
1: Mimi mwenyewe ndiyo msimamizi mkuu naamka saa11 alfajili kuosha makopo na kulisha chakula.

2: Nimetenga kuku 15 wanaoatamia na wengine15 wanataga tu.

3: Vifaranga navilea kwa joto la mkaa.

4: Kwenye mabanda ya vifaranga kwa siku nafanya ukaguzi Mara 4.

5: Eneo la kufugia ni kubwa na nimezungushia fesi.

6: Dawa za kuku zipo za kutosha za maji na unga.

Karibuni
Bila picha na video sasa sisi tutaamini vipi huu ufugaji wa pdf?
 
Nifanyaje nitoboe?
Kuna kuku ambao ni maalumu kwa ajili ya utotoleshaji vifaranga (PARENTAL STOCK) sasa Hawa kuwapata huwa ni issue, kuku wakwanza akishatotoa , nahuyo kifaranga akija kua mkubwa nae akaanza kutaga akitotoa vifaranga mara nyingi huwa haviwi imara, Kinga yao ya mwili inakua dhaifu natural.

Tafuta parental stock ndio wawe maalumu kwa ajili kutaga mayai kisha utotoleshe vifaranga.
 
Back
Top Bottom