benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,533
- 3,187
"ANDIKO HILI LIMETOLEWA NA WAFANYAKAZI WA RADIO 5 ARUSHA"
"Habari za wakati huu wanahabari wenzetu.
Sisi ni Wafanyakazi wa Radio5 Arusha iliyo chini ya TAN COMMUNICATION MEDIA ambayo inamilikiwa na Familia ya Mzee Edward LOWASSA kwa masikitiko kabisa tunalazimika kuandika ujumbe huu kueleza mateso tusiyostahili ambayo tunayapitia kwa muda mrefu sana. Tunajua kwamba hii si njia ambayo tungetamani kutumia kutatua changamoto zetu, lakini tumeona kwamba ndio njia pekee iliyosalia kufanikisha hili.
Kampuni yetu haitutendei haki na imekuwa ikifanya unyanyasaji kwa wafanyakazi kwa miaka mingi, lakini sasa hali imekuwa mbaya zaidi:-
1. Kampuni hailipi wafanyakazi. Huu ni mwezi wa 9 hawajatulipa wafanyakazi na bado wanatulazimisha kuingia kazini. Ni ngumu kwetu kuendesha maisha bila mshahara. Ni kama hawajiulizi tunakula nini, tunaishi wapi, tukiumwa tunajitibu vipi, tunasafirije kuja kazini, watoto wetu wanasomaje, familia zetu zinazotutegemea tunazimudu vipi, nk.
2. Hatuna Bima ya Afya.
Tangu Radio hii iwe chini ya familia ya Lowassa mwaka 2007, hakuna mfanyakazi amewahi kukatiwa Bima ya Afya ilhali mikataba inasema tutapewa Bima ya Afya. Haijawahi kutokea
3. Makato ya HIFADHI ZA JAMII HAYAFIKI KWENYE MIFUKO HUSIKA NA TUNAKATWA.
Kampuni hii haijawahi kupeleka hata Sh. 10 ya makato wanayotukata wafanyakazi.
Tumekuwa tukilalamika miaka yote, tukaenda Idara ya Kazi na NSSF kulalamika kwenye ofisi zao za Arusha, ila wanakuja ofisini, wanaonana na Uongozi, WANAHONGWA wananyamaza (Kwenye Hili Viongozi wa IDARA YA KAZI na MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII Tunaomba Rais SAMIA SULUHU HASSAN Awawajibishe maana Wana Michezo Hatari sana na ni WALA RUSHWA. Hawajawahi kutusaidia kabisa licha ya kuwa tumepeleka malalamiko mara kwa mara.
4. Kampuni inaingiza Fedha nyingi sana kwa mwezi sababu tuna matangazo makubwa lakini haitujali.
Radio hii haitoi nafasi za wafanyakazi kujindeleza wala haitoi fursa hata za mikopo midogomidogo kwa wafanyakazi
5. Uongozi wa Radio5 ni mbovu kiasi kwamba kila siku tunaona jinsi radio inaelekea kufa. Maelezo mtandaoni yanasema tunasikika mikoa 21, tulikuwa tunasikika mikoa 11, ila sasa tumebaki Arusha na Dar tu, na hata hiyo miwili mara leo tupo hewani kesho haipo. Vipindi havina ubora sababu wafanyakazi wengine wanashindwa kufika kazini SABABU YA KUKOSA NAULI na hata wanaobahatika kuingia kazini wana stress za ugumu wa maisha. Cha Kushangaza tunapiga kelele kila siku lakini Hawasikii
Mfano, Bob Lowassa ambaye ndiye anasimamia Radio ANA MIAKA MITATU (3) Hajakanyaga Radio5!!!!
6. Kampuni haina usafiri
Radio 5. Haina hata GARI BOVU kwa ajili ya wafanyakazi kinyume na mikataba na pia hawatoi nauli japo mkataba unasema kampuni ina gari za usafiri na pia wafanyakazi watakuwa wanapewa NAULI.
Hali hii imepelekea wafanyakazi kufika kazini kwa tabu au kutofika kabisa. Na wengine kulala ofisini hasa wale wenye vipindi vya usiku kwa kukosa namna salama ya kurudi majumbani kwao
7. Uongozi hautaki VIKAO NA WAFANYAKAZI.
Ni zaidi ya miaka mitano sasa wafanyakazi tumekuwa tunaomba kukutana na viongozi wetu haswa MD bila mafanikio.
8.Wafanyakazi hatuna mikataba, tangu ilipomalizika takribani miaka miwili sasa.
MAOMBI YETU:-
1. TUNAMUOMBA WAZIRI WA Habari MH.NAPE NNAUYE Aingilie kati hii kampuni ili wafanyakazi tupate stahiki zetu muhimu (Mishahara ya miezi 9 na mafao ambayo tunakatwa na hayapelekwi kwenye mfuko) kwani mpaka sasa hakuna wa kutusikiliza.
2. Tunaiomba Serikali ya Mama yetu mpendwa MH.SAMIA SULUHU HASSAN kuingilia Kati idara zake muhimu ambazo zinakuwa hazitimizi wajibu wao. Mfano ni kama IDARA YA KAZI na MIFUKO YA HIFADHI ZA JAMII
UJUMBE HUU TUMEANDIKA WAFANYAKAZI WA RADIO5 na hatuwezi kutaja majina yetu kwa kuhofia usalama wetu na familia zetu ila ni uhalisia kwamba tunateseka na uchunguzi mdogo unaweza kuthibitisha madai yetu yote
WANAHABARI TUMEKUWA MSTARI WA MBELE KUPAMBANIA MASLAHI YA WENGINE NA HUKU TUNATEKETEA.
Umefika wakati sasa tupaze sauti pia kwa ajili yetu."
Asante
"Habari za wakati huu wanahabari wenzetu.
Sisi ni Wafanyakazi wa Radio5 Arusha iliyo chini ya TAN COMMUNICATION MEDIA ambayo inamilikiwa na Familia ya Mzee Edward LOWASSA kwa masikitiko kabisa tunalazimika kuandika ujumbe huu kueleza mateso tusiyostahili ambayo tunayapitia kwa muda mrefu sana. Tunajua kwamba hii si njia ambayo tungetamani kutumia kutatua changamoto zetu, lakini tumeona kwamba ndio njia pekee iliyosalia kufanikisha hili.
Kampuni yetu haitutendei haki na imekuwa ikifanya unyanyasaji kwa wafanyakazi kwa miaka mingi, lakini sasa hali imekuwa mbaya zaidi:-
1. Kampuni hailipi wafanyakazi. Huu ni mwezi wa 9 hawajatulipa wafanyakazi na bado wanatulazimisha kuingia kazini. Ni ngumu kwetu kuendesha maisha bila mshahara. Ni kama hawajiulizi tunakula nini, tunaishi wapi, tukiumwa tunajitibu vipi, tunasafirije kuja kazini, watoto wetu wanasomaje, familia zetu zinazotutegemea tunazimudu vipi, nk.
2. Hatuna Bima ya Afya.
Tangu Radio hii iwe chini ya familia ya Lowassa mwaka 2007, hakuna mfanyakazi amewahi kukatiwa Bima ya Afya ilhali mikataba inasema tutapewa Bima ya Afya. Haijawahi kutokea
3. Makato ya HIFADHI ZA JAMII HAYAFIKI KWENYE MIFUKO HUSIKA NA TUNAKATWA.
Kampuni hii haijawahi kupeleka hata Sh. 10 ya makato wanayotukata wafanyakazi.
Tumekuwa tukilalamika miaka yote, tukaenda Idara ya Kazi na NSSF kulalamika kwenye ofisi zao za Arusha, ila wanakuja ofisini, wanaonana na Uongozi, WANAHONGWA wananyamaza (Kwenye Hili Viongozi wa IDARA YA KAZI na MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII Tunaomba Rais SAMIA SULUHU HASSAN Awawajibishe maana Wana Michezo Hatari sana na ni WALA RUSHWA. Hawajawahi kutusaidia kabisa licha ya kuwa tumepeleka malalamiko mara kwa mara.
4. Kampuni inaingiza Fedha nyingi sana kwa mwezi sababu tuna matangazo makubwa lakini haitujali.
Radio hii haitoi nafasi za wafanyakazi kujindeleza wala haitoi fursa hata za mikopo midogomidogo kwa wafanyakazi
5. Uongozi wa Radio5 ni mbovu kiasi kwamba kila siku tunaona jinsi radio inaelekea kufa. Maelezo mtandaoni yanasema tunasikika mikoa 21, tulikuwa tunasikika mikoa 11, ila sasa tumebaki Arusha na Dar tu, na hata hiyo miwili mara leo tupo hewani kesho haipo. Vipindi havina ubora sababu wafanyakazi wengine wanashindwa kufika kazini SABABU YA KUKOSA NAULI na hata wanaobahatika kuingia kazini wana stress za ugumu wa maisha. Cha Kushangaza tunapiga kelele kila siku lakini Hawasikii
Mfano, Bob Lowassa ambaye ndiye anasimamia Radio ANA MIAKA MITATU (3) Hajakanyaga Radio5!!!!
6. Kampuni haina usafiri
Radio 5. Haina hata GARI BOVU kwa ajili ya wafanyakazi kinyume na mikataba na pia hawatoi nauli japo mkataba unasema kampuni ina gari za usafiri na pia wafanyakazi watakuwa wanapewa NAULI.
Hali hii imepelekea wafanyakazi kufika kazini kwa tabu au kutofika kabisa. Na wengine kulala ofisini hasa wale wenye vipindi vya usiku kwa kukosa namna salama ya kurudi majumbani kwao
7. Uongozi hautaki VIKAO NA WAFANYAKAZI.
Ni zaidi ya miaka mitano sasa wafanyakazi tumekuwa tunaomba kukutana na viongozi wetu haswa MD bila mafanikio.
8.Wafanyakazi hatuna mikataba, tangu ilipomalizika takribani miaka miwili sasa.
MAOMBI YETU:-
1. TUNAMUOMBA WAZIRI WA Habari MH.NAPE NNAUYE Aingilie kati hii kampuni ili wafanyakazi tupate stahiki zetu muhimu (Mishahara ya miezi 9 na mafao ambayo tunakatwa na hayapelekwi kwenye mfuko) kwani mpaka sasa hakuna wa kutusikiliza.
2. Tunaiomba Serikali ya Mama yetu mpendwa MH.SAMIA SULUHU HASSAN kuingilia Kati idara zake muhimu ambazo zinakuwa hazitimizi wajibu wao. Mfano ni kama IDARA YA KAZI na MIFUKO YA HIFADHI ZA JAMII
UJUMBE HUU TUMEANDIKA WAFANYAKAZI WA RADIO5 na hatuwezi kutaja majina yetu kwa kuhofia usalama wetu na familia zetu ila ni uhalisia kwamba tunateseka na uchunguzi mdogo unaweza kuthibitisha madai yetu yote
WANAHABARI TUMEKUWA MSTARI WA MBELE KUPAMBANIA MASLAHI YA WENGINE NA HUKU TUNATEKETEA.
Umefika wakati sasa tupaze sauti pia kwa ajili yetu."
Asante