Mifumo ya kidunia ilishaamua mwanaume aishi kwa kukandamizwa na kufanyiwa ulaghai/ udanganyifu

Mifumo ya kidunia ilishaamua mwanaume aishi kwa kukandamizwa na kufanyiwa ulaghai/ udanganyifu

Nilishakueleza sababu za mgawanyo wa mali yaweza moja kati ya hizi au zote kwa pamoja

Kuchuma mali pamoja
Kama mkeo atakuwa anafanya kazi basi maana yake utakuwa haumhudumii, na lazima kuna bills za hapa na pale alikuwa anakusaidia kwahiyo inahesabika kama mmechuma wote, hivyo mkiachana mtagawana mali kwa hicho kigezo

Mke kufanya majukumu ya nyumbani na kulea watoto
Hayo majukumu ya mke yanakuja na wajibu juu yake ya kumhudumia, kwa sababu huo muda anaoutumia kufanya hayo majukumu alitakiwa naye awe anatafuta pesa, ili siku mkiachana awe na kitu cha kuanzia maisha

Kubaki na watoto
Ndoa nyingi watu wakiachana mke ndio hubaki na watoto, ambapo ataendeleza gurudumu la malezi huku mwanaume akiwa free tu, sasa unataka huduma za watoto nani ahusike nazo

Wajibu wa mke kwa mumewe
Tamaduni zetu zinaamini kwamba mwanaume anapooa basi mke kazi yake ni kuhakikisha anamlea, anamtunza, anamliwaza na anamfariji mumewe pale anapokuwa na msongo wa mawazo, hiyo inamfanya mwanaume apate moyo na awe na juhudi zaidi ya kutafuta pesa, ambapo wanaamini mke asipofanya hayo basi mume utafutaji wake utakuwa wa kusuasusua

Sasa whether huko ndani ya ndoa mke alikuwa anatimiza hayo au hatimizi hilo haliwahusu, wenyewe wanaassume kwamba mwanamke aliyeolewa lazima anatimiza hayo majukumu ambayo kwa namna moja au nyingine, lazima tu yatamfanya awe na haki ya kugawiwa nusu ya mali zilizopatikana ndani ya ndoa

Sasa kwa mantiki hiyo wewe ulitaka ufidiwe nini hapo au labda nikuulize kama mwanamke alikuwa hatafuti pesa na alikuwa anatimiza majukumu yake, siku mmeachana hana pesa wala mali wala kazi wala biashara unategemea anapata kipi cha kufidia muda ambao alitakiwa atafute kama wewe, by the way nenda kasome sheria za ndoa na mgawanyo wa mali mimi mwenyewe siko kwenye ndoa but atleast nafuatilia baadhi ya mambo na najaribu kukuelezea katika uhalisia wake ila wewe unajadili kwa mihemko na kulazimisha assumptions zako ndio ziwe sahihi
Nikushukuru kwa kujitahidi kufafanua, sasa tuachane na sheria inavyosema ambayo ni kandamizi kwa wanaume, chukulia wanandoa hawana mtoto na mke alikuwa mama wa nyumbani, tukiachana namlipa kwasababu gani? Kisa kupika na kunipa K? Nahuku ni majukumu yake kama mke, mlitaka hizo huduma nizipate wapi? Ninachoshauri ni kila mmoja aondoke na alichokuja nacho au alichonunua, haina mantiki kumlipa mtu nahuku alikuwa anatimiza majukumu yake kama mke, kama mimi nilivyokuwa natimiza majukumu yangu kama mume (ambayo unakwepa kuyazungumzia kana kwamba hayana umuhimu)

Halafu mke akifanya kazi, pesa zake bi ngumu kupata, anatuma kwao kimya kimya, nyie wanawake hampendani hata wenyewe kwa wenyewe, itakuwa kumpenda mwanaume?
 
Mwanamke kununuliwa kama nyanya sokoni kupitia mahari ni sahihi ?

mwanamke ni mtumwa wa mwanaume kupitia kununuliwa kwa mahari hivyo anapaswa kutii kila agizo la bwana wake si ndio ?


Wewe ni supporter wa mfumo dume, mfumo jike au 50/50 au ni nini hasa unacho support ?
Mahari siyo kumnunua mwanamke wala haina uhusiano wowote na mke kuwa mtumwa wa mume, kama hamtaki kutoa mahari basi mfute utaratibu wa watoto kutumia majina ya ukoo ya mume bali watumie majina ya koo zote mbili, maana kwa tamaduni zetu hiyo ndiyo sababu kubwa ya kutoa mahari
 
Nguvu ya mwanaume ipo katika kuoa wake wengi. Mila ya kiafrika iliyoachwa
 
Mahari siyo kumnunua mwanamke wala haina uhusiano wowote na mke kuwa mtumwa wa mume, kama hamtaki kutoa mahari basi mfute utaratibu wa watoto kutumia majina ya ukoo ya mume bali watumie majina ya koo zote mbili, maana kwa tamaduni zetu hiyo ndiyo sababu kubwa ya kutoa mahari
Tamaduni zenu wewe na nani ?
 
Siyo omba omba ni mgawanyo wa majukumu tu, siku wanaume mkianza kuyachukulia majukumu ya wanawake kama yenu, basi hata nao wataanza kuyachukulia majukumu yenu kama ya kwao
Majukumu gani hayo yanayo fanya kuwa ombaomba ?
 
Nikushukuru kwa kujitahidi kufafanua, sasa tuachane na sheria inavyosema ambayo ni kandamizi kwa wanaume, chukulia wanandoa hawana mtoto na mke alikuwa mama wa nyumbani, tukiachana namlipa kwasababu gani? Kisa kupika na kunipa K? Nahuku ni majukumu yake kama mke, mlitaka hizo huduma nizipate wapi? Ninachoshauri ni kila mmoja aondoke na alichokuja nacho au alichonunua, haina mantiki kumlipa mtu nahuku alikuwa anatimiza majukumu yake kama mke, kama mimi nilivyokuwa natimiza majukumu yangu kama mume (ambayo unakwepa kuyazungumzia kana kwamba hayana umuhimu)

Halafu mke akifanya kazi, pesa zake bi ngumu kupata, anatuma kwao kimya kimya, nyie wanawake hampendani hata wenyewe kwa wenyewe, itakuwa kumpenda mwanaume?
Mkuu mbona nimeshakuelezea kwamba katika mazingira ambayo mke ni mama wa nyumbani na hamna watoto, mkiachana mke atapewa mali kwa hicho kigezo cha kufidia muda wake ambao alitakiwa atafute pesa kama wewe lakini akawa anatimiza hayo majukumu, sawa ni majukumu yake lakini ndio ukubali sasa kwamba siku mkiachana lazima mtagawana mali kwa hicho kigezo

Vinginevyo msiachane au usifanye makosa makubwa ya kumfanya yeye atake muachane, wangesema kila mtu aondoke na alichokuja nacho ingekuwa ni uonevu kwa wanawake ambao ni wamama wa nyumbani, kwa sababu huwezi kumkataza mtu asitafute pesa akae nyumbani akuhudumie halafu eti mkiachana usimpe chochote wakati ni wewe ndio ulimzuia asitafute pesa

Hayo ya mke kufanya kazi halafu asichangie pato la familia nalo haliwezi kuwa utetezi wa kuaminika, kwa sababu mwanaume yeyote tu anaweza akatumia huo utetezi hata kama ni uongo ili mradi tu mkewe asipate chochote, huwa wanaamini haiwezekani katika muda wote ambao mmeishi na huyo mke eti awe hajawahi kuchangia chochote kwenye familia lazima tu kuna sehemu naye alichangia

Kuhusu hayo ya wanawake kutokupendana nazo ni propaganda kama propaganda nyingine kwa sababu ukiangalia hali halisi mazingira ambayo yanafanya wanawake waonekane hawapendani, utakuta ni mazingira ambayo hata ingekuwa ni wanaume nao wangefanya hayo hayo ambayo wakifanya wanawake wanaonekana hawapendani, labda wewe uniambie ni katika mazingira gani ambayo wanawake hawapendani na ni kwa sababu ya kufanya vitu gani

Halafu siyo kwamba majukumu ya mwanaume hayahesabiki au hayana umuhimu ila kumbuka jukumu lenu pekee hasa wanaume wa kiafrika ni kutafuta pesa tu, sasa niambie ni pesa kiasi gani inayoweza kulingana na majukumu ya kufanya kazi za nyumbani, kutii mume, kubeba mimba, kuzaa, kunyonyesha, kulea watoto nk sasa hata kama utakuwa unamhudumia utakuwa unampa pesa kiasi gani ya kufidia majukumu yote hayo
 
Tamaduni za kiafrika

Majukumu ya mwanamke ni yapi
Sidhani hata unajua unacho tetea au wajiandikia tu.

Tamaduni za kiafrika una generalize tu mambo.

Hebu tuliza kichwa na ujibu nacho kuuliza
 
Mwanaume kama huna akili timamu na ya kiume ndo utayumbishwa......tofauti na hapo hakuna la kunitisha...
 
Kama umeshindwa hoja sema acha hizi porojo za kusema napenda ligi, wewe ungekuwa hupendi ligi tusingefika hapa ungeshaacha kunijibu tangu mwanzo, kufika hapa maana yake wote tumebishana by the way kwani niliyoyaandika ni uwongo
Haya umeshinda mkuu
 
Sidhani hata unajua unacho tetea au wajiandikia tu.

Tamaduni za kiafrika una generalize tu mambo.

Hebu tuliza kichwa na ujibu nacho kuuliza
Ndio hivyo kwa tamaduni za jamii nyingi za kiafrika mahari ni kama fidia kwa familia ya mke kwa kulose ilihali ya mwanaume imegain, unaweza kuamua tu kukataa ila wewe kukataa haibadilishi ukweli wa hilo jambo, mahari siyo kumnunua mwanamke wala haihusiani na mwanamke kuwa mtumwa wa mumewe
 
Mwanamke kununuliwa kama nyanya sokoni kupitia mahari ni sahihi ?

mwanamke ni mtumwa wa mwanaume kupitia kununuliwa kwa mahari hivyo anapaswa kutii kila agizo la bwana wake si ndio ?


Wewe ni supporter wa mfumo dume, mfumo jike au 50/50 au ni nini hasa unacho support ?
Hajui anasupport nini uyo jamaa. Yeye anachotaka ni kuoneshana umwamba tu tu ndani ya nyumba
 
Mahari siyo kumnunua mwanamke wala haina uhusiano wowote na mke kuwa mtumwa wa mume, kama hamtaki kutoa mahari basi mfute utaratibu wa watoto kutumia majina ya ukoo ya mume bali watumie majina ya koo zote mbili, maana kwa tamaduni zetu hiyo ndiyo sababu kubwa ya kutoa mahari
Kwahiyo kutolewa mahari ndo unarejea utamaduni, ila mke kuwa submissive kwa mume pmj na kufanya kazi za ndani, tukikwambia kuwa nao ni utamaduni wa kiafrika unapinga, unahoji eti ni nani anayeamua kuwa gender roles za mwanamke ni hizi na za mwanaume ni hizi.
 
Hatushindani tunajadili hoja
Wewe unataka mashindano. Ndio maana nimeona nikuache labda hao wengine wanaweza kukuelewesha. Hivi unajua kwann hata wanawake hawajitokezi kwenye comments? Wanajua hoja imewapiga kwenye mshono hawana cha kuchangia vinginevyo wangeshakuja kutapika hapa.
 
Mkuu mbona nimeshakuelezea kwamba katika mazingira ambayo mke ni mama wa nyumbani na hamna watoto, mkiachana mke atapewa mali kwa hicho kigezo cha kufidia muda wake ambao alitakiwa atafute pesa kama wewe lakini akawa anatimiza hayo majukumu, sawa ni majukumu yake lakini ndio ukubali sasa kwamba siku mkiachana lazima mtagawana mali kwa hicho kigezo

Vinginevyo msiachane au usifanye makosa makubwa ya kumfanya yeye atake muachane, wangesema kila mtu aondoke na alichokuja nacho ingekuwa ni uonevu kwa wanawake ambao ni wamama wa nyumbani, kwa sababu huwezi kumkataza mtu asitafute pesa akae nyumbani akuhudumie halafu eti mkiachana usimpe chochote wakati ni wewe ndio ulimzuia asitafute pesa

Hayo ya mke kufanya kazi halafu asichangie pato la familia nalo haliwezi kuwa utetezi wa kuaminika, kwa sababu mwanaume yeyote tu anaweza akatumia huo utetezi hata kama ni uongo ili mradi tu mkewe asipate chochote, huwa wanaamini haiwezekani katika muda wote ambao mmeishi na huyo mke eti awe hajawahi kuchangia chochote kwenye familia lazima tu kuna sehemu naye alichangia

Kuhusu hayo ya wanawake kutokupendana nazo ni propaganda kama propaganda nyingine kwa sababu ukiangalia hali halisi mazingira ambayo yanafanya wanawake waonekane hawapendani, utakuta ni mazingira ambayo hata ingekuwa ni wanaume nao wangefanya hayo hayo ambayo wakifanya wanawake wanaonekana hawapendani, labda wewe uniambie ni katika mazingira gani ambayo wanawake hawapendani na ni kwa sababu ya kufanya vitu gani

Halafu siyo kwamba majukumu ya mwanaume hayahesabiki au hayana umuhimu ila kumbuka jukumu lenu pekee hasa wanaume wa kiafrika ni kutafuta pesa tu, sasa niambie ni pesa kiasi gani inayoweza kulingana na majukumu ya kufanya kazi za nyumbani, kutii mume, kubeba mimba, kuzaa, kunyonyesha, kulea watoto nk sasa hata kama utakuwa unamhudumia utakuwa unampa pesa kiasi gani ya kufidia majukumu yote hayo
Ndo ujibu sasa huo muda wa kumlipa mwanamke kama fidia una mantiki gani nahuku kiutamaduni ni jukumu lake kufanya kazi za nyumbani? Mbona umesema vzr tu jukumu letu ni kutafuta pesa, basi jukumu la mwanamke ni kazi za nyumbani, halafu unadharau hizo pesa anazotafuta mwanaume nahuku tunahudumia familia tatu, ya mke wangu, familia niliyotoka, pamoja na familia ya mke wangu mizinga napigiwa? Unahesabia mke tu?

Kwahiyo kwenye ndoa mwanaume hana mchango wowote mpaka mali zake zipokonywe na asipate fidia yoyote pale wanapoachana? Narudia tena usirejee sheria za kitapeli ambazo ni kandamizi kwa wanaume, ongea uhalisia, eti mwanamke anakazi kubwa kubeba mimba na kulea, kwahiyo ukitaka mwanaume ndo abebe mimba? Si ni asili Mungu kaumba watu hivyo?

Maswali hayo mawili kuhusu mantiki ya kumlipa mwanamke kisa kazi za ndani nahuku ndo jukumu lake ni lipi? Mchango wa mwanaume kwenye ndoa kwanini hauhesabiki? Aya hii ya mwisho ndo summary ya maswali niliyouliza tangu jana unakwepa hujibu, jibu sasa bila kuandika gazeti ambalo halina hoja za msingi.
 
Chukulia mfano suala la sex, ile ni starehe ya wote lakini dunia imekua brainwashed kwa kuaminishwa mwanaume anafanyiwa favor ambayo in return inatakiwa kulipia posho, hii posho ya sex wadada wa mjini siku hizi wanaiita matunzo.

Mambo yapo ivyo karibu kila nyanja zinazohusu masuala ya kijinsia na mahusiano. Taasisi zinatetea haki za watoto ukiangalia mkazo mkubwa wameuweka kwa watoto wa kike.

Wanandoa mkiachana kama mali ni za mwanaume zinapigwa pasu kwa pasu ila kama ni za mwanamke hapo mwanaume hapati chochote. Wanasema sababu ni kwamba mwanamke ana haki ya kufidiwa muda na jitihada zake kipindi cha ndoa cha kushangaza muda na gharama alizotumia mwanaume kwenye ndoa iyo iyo hapati fidia yoyote.

Ukiangalia mchakato mzima before, during and after marriage mnufaika mkubwa ni mwanamke lakini jamii imetengenezewa fikra ionekane ananufaika ni mwanaume, ndo hapo mwanaume anatishiwa akiwa bachelor atakapoumwa hakuna wa kumuuguza utafikiri uko kwenye ndoa wanaumwa wanaume tu.

Kwenye suala la DNA napo nishawahi kusikia majibu yakionesha mtoto sio wa mwanaume husika basi mwanaume uyo atadanganywa kuwa ni mtoto wake, wanasema wanalinda masilahi ya mtoto.

Ukija kwenye nasaa za kimaisha tunaambiwa mwanaume kaumbiwa mateso mara kitanda hakizai halamu. Kwamba nibebe mzigo ninaoweza kuuepuka kwa sababu mimi mwanaume? kwamba mwanamke afanye umalaya wake nilee mtoto sio wangu, eti kitanda hakizai halamu.! That is totally bullshit.

Yapo mengi sana yanamkandamiza mwanaume lakini dunia imepotoshwa yaonekane ni kawaida tu. Suala hili halikuonekana tatizo uko zamani kwa sababu mwanamke alikua inferior na mtiifu sana kwa mwanaume.

Kutokana na sera ya 50/50 kushika hatamu kwa sasa wanawake wamekua wabinafsi, wamepandindikizwa chuki na feminists kwamba wanaume ndio wabaya wao hii imewafanya kuwa na roho za kikatili mbaya zaidi washaona mifumo ya kidunia ina loopholes ambazo wakizitumia kimkakati zinaweza kuwapa pesa rahisi au kupata huruma kwa mabaya waliyoyafanya.

Mifano ipo mingi familia ya mzee mengi nusura ipigwe na kitu kizito na klyn, ukiangalia kwa jicho la kosheria inawezekana klyn inawezekana akawa sawa lakini kwa utashi wa kiubinadamu akaonekana ni matapeli.

Dunia ya sasa kwa mwanaume yoyote mwenye ndoto kubwa za kufika mbali kiuchumi basi ndoa ni mtego ambao unaweza kuja kuiangusha himaya yako aliyoijenga kwa miongo mingi.

Kupitia sera ya 50/50 wanawake washapewa access zote za kiuchumi, kijamii na kisiasa binafsi sioni kama kuna haja tena ya kuwapa victim status kama zamani.

Mifumo ifumuliwe mwanamke nae aangaliwe kama predator kama ilo haliwezekani basi ni wajibu wetu wanaume kuishi na wanawake kwa tahadhari kubwa sana ili tusitumike kama levarage.

Mwanaume tambua ya kwamba mpenzi sio mama yako atakaekua upande wako katika kila hali siku zote za maisha yake. Mpenzi anaweza kusitisha mahusiano muda wowote bila kujali umejitoa au umempambania kwa kiasi gani na hakuna utakachoweza kumfanya.

Hivyo basi ukiamua kumwinua mpenzi wako(kumsomesha, kumfungulia biashara, kumtafutia kazi, kumjengea nyumba n.k) basi fanya hivyo kwa kiasi ambacho unaweza kuhimili maumivu ya kukipoteza.

Mwanaume usiweke malengo yako kwa mpenzi/mke, hitaji lako kwa mwanamke liishie kwenye kampani ya kijinsia na kuendeleza kizazi chako tu.
Ni kweli. Hapa solution ni kukataa ndoa tu.
 
Heshima na majukumu ya kimaadili kila upande unawajibika ilo sipingani nalo kabisa. Huwezi ukamtaka mmeo akutengee chakula maana inajulikana huo ni wajibu wa mwanamke vivyo hivyo yanapotokea majukumu yanayoitaji nguvu mfano gari ya familia imepata hitilafu labda tusemale pancha haiwezekani mume akamwambia mkewe abadilishe tairi maana inajulikana ilo ni jukumu la mwanaume au kaingia mwizi ndani ya nyumba haiwezekani mume akamwambia mkewe aende kupambana nae Gender roles sio utumwa ni wajibu ambao unakuja automaticaly tu kutokana na misingi ya jamii iliyokukuza., unachotaka kusema hakiwezekani kwenye jamii zetu za kiafrika kwamba mume amtengee mkewe chakula.! msilazimishe mambo ambayo mnajua kabisa hayawezekani
We are challenging those stereotypes, nikutengee chakula maana yake nitoe vyombo nioshe. , don't you know this is TIME??? Kwa nini mnakataa mtu asilipwe 50 baada ya huu utumwa????? ..kubali hizo gender role zinamkandamiza mwanamke, and recognising this hence malipo ya 50/50 yanawekwa in place sasa ndio useme sasa ulitumia muda lini kufukuza mwizi na mara ngapi katika mahusiano yenu....

Anyway ulisema mwanamke kumtii mwanaume ni gender role nakuuliza ulikua unamaanisha nini, maana nilidhani umemaanisha wanawake ni weaker beings ila ukanirudisha ni respect nikakwambia ni reciprocal sasa hivi naona unanirudisha kwenye tamaduni za kiafrica, hizi zinazokandamiza wanawake all in the name of gender roles...????? Please ulikua unamaanisha nini unaposema mwanamke kumtii mwanaume ni gender role ili twende sawa.
 
Back
Top Bottom