Miili miwili bado inashikiliwa na HAMAS, upo wa kijana Mtanzania Joshua Mollel

Miili miwili bado inashikiliwa na HAMAS, upo wa kijana Mtanzania Joshua Mollel

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
IMG_9332.jpeg

Tal Chaimi, mkazi wa Kibbutz Nir Yitzhak, na Joshua Luito Mollel, mkazi wa Kibbutz Nahal Oz , waliuawa wakati wakishikiliwa mateka na Hamas katika Ukanda wa Gaza.

Miili yao yote miwili bado inashikiliwa na Hamas. Chaimi aliaminika kutekwa nyara lakini, ushahidi mpya ulionyesha aliuawa Oktoba 7 na mwili wake ulichukuliwa na Hamas hadi Gaza.

Chaimi alikuwa sehemu ya kikosi cha dharura ambacho kilitumwa kusimamisha shambulio la Hamas hadi waweze kuongezewa nguvu.

Chaimi aliondoka asubuhi hiyo baada ya kubainika kuwa Hamas wamejipenyeza Israel na kuwaacha mkewe na watoto nyumbani.

Waliporejea kikosini, Chaimi hakuwa miongoni mwao. Kikosi hakikuweza kumwambia mkewe mahali alipokuwa.

Chaimi alikuwa mkazi wa kizazi cha tatu wa Nir Yitzhak na mzao wa waanzilishi wake. Ameacha mke na watoto watatu.

Kumbukumbu yao iwe baraka
Mollel mwanafunzi wa Kitanzania wa kilimo alikuwa amewasili Israel wiki mbili tu kabla ya Mauaji ya Oktoba 7.

Mollel alikuwa akifanya kazi huko Nahal Oz kama mfugaji wa ng'ombe wa maziwa na alikuwa kazini siku ya mauaji hayo.

Baba yake alijulishwa usiku wa kuamkia leo juu ya hatma ya mtoto wake, inasemekana haamini na ameuliza chanzo cha habari hiyo.

Babake Mollel anawasili Israel usiku huu akiandamana na wawakilishi wa wizara ya mambo ya nje, kwa mujibu wa Kituo cha Wahamiaji na Wakimbizi.

UPDATE:
Kupitia Mtandao wa X, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amethibitisha taarifa hii.

Makamba ameandika “Tumejulishwa na Serikali ya Israel kwamba Joshua Mollel, kijana wa Kitanzania aliyekuwa anasoma chini Israel, na ambaye tulipoteza naye mawasiliano tangu tarehe 7 Oktoba 2023, na ambaye Serikali imekuwa inafanya jitihada kubwa kupata taarifa zake tangu wakati huo, aliuawa mara tu baada ya kutekwa na kundi la Hamas mnamo tarehe 7 Oktoba 2023. Nimeongea na Mzee Mollel, baba mzazi wa Joshua, kuhusu ujumbe huo wa Serikali ya Israel.

Tunaendelea na mpango wa awali wa kuwapeleka Mzee Mollel na manafamilia mwingine pamoja na Afisa wa Serikali nchini Israel, kuungana na Balozi wetu na maafisa waliopo huko, kukutana na kuzungumza na mamlaka za nchi hiyo ili kupata taarifa za ziada. Kwa ridhaa ya familia, na itakapobidi, tutatoa taarifa za ziada katika siku zijazo.”
 
Tal Chaimi, mkazi wa Kibbutz Nir Yitzhak , na Joshua Luito Mollel, mkazi wa Kibbutz Nahal Oz , waliuawa wakati wakishikiliwa mateka na Hamas katika Ukanda wa Gaza.

Miili yao yote miwili bado inashikiliwa na Hamas.
Inna li Llahi wa inna Ilayhi Rajiun, wawekwe popote wanapostahili.

, wapo wengi sana hao kutoka nchi mbali mbali duniani waliouliwa na mazayuni wenyewe na mazayuni wamekiri kuuwa.

Ni mpumbavu tu ambae atapeleka mwanawe akasome israel, hivi huwa hamuelewi kuwa hiyo nchi ipo vitani kuanzia mwaka 1948?

Halafu cha kujiuliza, huyo mpumbavu alienda kusoma au kucheza disco?
 
Inna li Llahi wa inna Ilayhi Rajiun, wawekwe popote wanapostahili.

, wapo wengi sana hao kutoka nchi mbali mbali duniani waliouliwa na mazayuni wenyewe na mazayuni wamekiri kuuwa.

Ni mpumbavu tu ambae atapeleka mwanawe akasome israel, hivi huwa hamuelewi kuwa hiyo nchi ipo vitani kuanzia mwaka 1948?

Halafu cha kujiuliza, huyo mpumbavu alienda kusoma au kucheza disco?
Wewe naona zile dawa za kichina za kurejesha ubikra huzipendi ila unapenda ule ubikra unaopatikana kwa kumwaga damu ya kafri.
 
Tal Chaimi, mkazi wa Kibbutz Nir Yitzhak , na Joshua Luito Mollel, mkazi wa Kibbutz Nahal Oz , waliuawa wakati wakishikiliwa mateka na Hamas katika Ukanda wa Gaza.

Miili yao yote miwili bado inashikiliwa na Hamas.

Chaimi aliaminika kutekwa nyara lakini, ushahidi mpya ulionyesha aliuawa Oktoba 7 na mwili wake ulichukuliwa na Hamas hadi Gaza.

Chaimi alikuwa sehemu ya kikosi cha dharura ambacho kilitumwa kusimamisha shambulio la Hamas hadi waweze kuongezewa nguvu.

Chaimi aliondoka asubuhi hiyo baada ya kubainika kuwa Hamas wamejipenyeza Israel na kuwaacha mkewe na watoto nyumbani.

Waliporejea kikosini, Chaimi hakuwa miongoni mwao. Kikosi hakikuweza kumwambia mkewe mahali alipokuwa.

Chaimi alikuwa mkazi wa kizazi cha tatu wa Nir Yitzhak na mzao wa waanzilishi wake. Ameacha mke na watoto watatu.

Kumbukumbu yao iwe baraka​

Mollel mwanafunzi wa Kitanzania wa kilimo alikuwa amewasili Israel wiki mbili tu kabla ya Mauaji ya Oktoba 7.

Mollel alikuwa akifanya kazi huko Nahal Oz kama mfugaji wa ng'ombe wa maziwa na alikuwa kazini siku ya mauaji hayo.

Baba yake alijulishwa usiku wa kuamkia leo juu ya hatma ya mtoto wake, inasemekana haamini na ameuliza chanzo cha habari hiyo.

Babake Mollel anawasili Israel usiku huu akiandamana na wawakilishi wa wizara ya mambo ya nje, kwa mujibu wa Kituo cha Wahamiaji na Wakimbizi.

===

Sijui wanataka walipwe nini ili waachie mwili ultwe Afrika na kuzikwa walipozikwa mababu zake....

 Tal Chaimi and Joshua Luito Mollel, both murdered on October 7, their bodies remain in Hamas captivity. (photo credit: Bring Them Home Now)



Chanzo:
FaizaFoxy Kwa muisrael kuuawa najua inakuongezea furaha na amani.

Vipi kuhusu kuuawa Mtanzania mwenzako?
 
Naona hawa vijana wetu walitumwa kufanya kazi nyingine huko Israel, yaani kweli ameenda kufuga ng'ombe wa maziwa?

Inaumiza sana.

Hiyo wizara ya nje nayo ina tatizo, inaruhusu tena mzazi kwenda kufuatilia mwili wa mwanae, wizara inafanya nini.
 
Wale waliotaka kuandamana hapa tanzania kwa ajiri ya hamas wako wapi..?........waambie ile maiti ya mtanzania inawasaidia nini katika kupata mabikira 70?
Methali 18:7
Kinywa cha mpumbavu humwangamiza mwenyewe; mdomo wake ni mtego wa kumnasa yeye mwenyewe.
 
Jarida ni la Jerusalem oneni uongo huu ,wameshindwa kujua mateka wapo wapi wakawakomboe ,eti wametrack na kujua kwamba wawili wamekufa 😅😅😅.

Huu utoto anakusapot ni mjing wa kiwango cha juu, yaani wamshindwa kuwaokoa na hiyo miili wanayo wao mda sana ,wamekufa kweny ardhi yao .
 
Inna li Llahi wa inna Ilayhi Rajiun, wawekwe popote wanapostahili.

, wapo wengi sana hao kutoka nchi mbali mbali duniani waliouliwa na mazayuni wenyewe na mazayuni wamekiri kuuwa.

Ni mpumbavu tu ambae atapeleka mwanawe akasome israel, hivi huwa hamuelewi kuwa hiyo nchi ipo vitani kuanzia mwaka 1948?

Halafu cha kujiuliza, huyo mpumbavu alienda kusoma au kucheza disco?
bibi we ni mpumbavu samahani lakini
 
Wameuliwa Tangu oktoba 7 ,eti Hamas wamechukua miili yao na kukaa nayo mpaka leo ...Huu ujinga labda asiyejua kusoma ndio anaweza kuelewa .

Yaani Hamas kukamata mateka waache wazima wachukue miili ya waliokufa tangu oktoba 7 😅😅😅..

Dead bodies are everywhere na zinaachwa kusambaa watu waje kuokota maiti .

Simple ni kwamba israel wameua watanzania wote wawili....walichoandika labda uwe mjinga ndio utakubali .


Yaani mtu kauliwa oktoba 7 wao Hamas washikilie miili ya hao maiti kwa miezi 2 ,ili wapate nn tena?😅😅
 
Back
Top Bottom