Mikanganyiko katika Biblia ni kigezo kinachowapa watu uhalali wa kusema hakuna Mungu

Sema tuu vigezo vyako ambavyo WEWE binafsi ukiviona utaamini Mungu yupo

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
MKuu Gocha,
mungu ni mwenye nguvu zote, hakosei, habadili maamuzi, mwenye upendo wote, aliumba mbingu na ardhi

Hizo sifa zote hapo zinajikanganya yaani mungu anabadili mawazo, anaua,ana upendeleo, ana wivu ana hasira, si mwenye uwezo na nguvu zote

Je unahitaji kuona mistari na baadhi yake nimeiweka hapo juu.

Uwepo wa sifa zake unajipinga wenyewe kupitia vitabu hivyo viitwavyo vitakatifu.unaweza kumtetea vipi?
 
Mungu ana Mwili??

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
Mungu hayupo, kisichokuwepo hakiwezi thibitishwa kwa namna yoyote ile,
Huwezi thibitisha mbali na kutumia vitabu vya hekaya za kiyahudi, na cha ajabu zaidi unaletewa wewe mnyaturu.

Thibitisha huyo mungu mwenye sifa nilizotaja hapo juu Kama yupo bila kuwapo kwa contradiction?
 
Mkuu mjinga,
Ni hivi nikiwasha feni nikaweka karatasi mbele yake itapepea Nina feel upepo, upepo unaweza kupimwa.
Upepo ukiwa mkali utaona outcome majani yana ruka light object vina move.

Thibitisha mungu kwa namna yoyote ile?
Kwahiyo una sema Mungu Hana outcomes

Nimekwembia hivi Mungu yupo kwasababu kanitendea MIUJIZA hiyo ndo outcomes

Kwanini Una amini upepo upo?
Si kwasababu ya outcomes

Lakin kumbuka upepo hauinekani Wala haushikiki

Kama una amini outcomes za upepo kwann usiamini out comes za Mungu??

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
 
Kutojua ulimwengu upo hivi ulivyo haimanishi niamini majibu ya uongo, na yanajidhihirisha ni ya uongo sababu ya contradiction zake, Na mola mwenye upendo mwingi lakini huyohuyo anasimamía uwepo wa maovu ,na si tu kusimamia vilevile yeye mwenyewe anaua.Ni dhahiri mungu huyo hayupo ila tu yupo kwenye vichwa vya wale walioamua kuwa mateka wa akili na hisia.
 

Mkuu kwani Bibilia kaiandika nani?
Nani aliidhinisha huyo muandika Bibilia kuwa ndio atamsemea “Mungu” maneno yake matakatifu?

Tukijua haya basi tutajua kwanini Bibilia inajikanganya yenyewe
 
Mkuu Gocha
Nipo tayari kukosolewa utakaponionyesha sehemu nimeandika naamini upepo, ukishindwa hoja Hapana ulazima wakumsingizia mtu maneno ya uongo.

Hizo outcomes unazozisema Kwanini zisiwe kwa watu wote na zisioekane?

Huoni upepo ukipeperusha au kung’oa mabati tunaona?
ukipuliza karatasi kwa mdomo wako huoni linapepea?

Thibitisha hizo outcome?
 

Mkuu upepo ni hewa inapokua ina move...... simple as that

Hatuutambui kwa outcome tu bali upepo unaweza kuupima, kuutengeneza, kuusimamisha, kuusikia, kuuhisi, kuubadilisha nk nk

Unautumiaje huu kuthibitisha uwepo wa Mungu?
Kwamba Mungu ni kama upepo? Tunaweza kumpima? Tunaweza kumtengeneza? Tunaweza kumsimamisha? Nk nk
 
Utake usitake Yeye yupo na alikuwepo na ataendelea kuwepo.

Na utamkuta katika mengi
Kuponya kbuka yule mwanamke aliyebakiwa na mlo mmoja akila age.Alipompikia mtumishi was Bwana kila kitu kiliongezeka.Hivyo MUNGU alimponya na njaa.Maana yupo jitokeze afanye maajabu kwako kama umekwama mahali


Kuonya.Rejea Anania na Safira walidanganya(sadaka/ahadi)na walikufa ili kuwa funzo kwa wengine kujua yupo na anatenda kazi
 
Tafiti zinaonyesha kwamba...
1. Dini ya Kikristo inaongoza Kwa kuzalisha Atheists wengi.

2. Asilimia kubwa ya Atheists wa Jamii Forum wana background ya Kikristo.


Hypothesis:- data zinaonyesha kwamba sababu kubwa ya atheists wengi kuwa na background ya dini ya Kikristo ni contradictions nyingi zilizojaa kwenye kitabu chao,.hali inayofanya wengi kushindwa kuelewa mafundisho yao.
 
 
Mkuu uthibitisho wako ni Anania na safira ndio unathibitisha mungu yupo?
 
Inaweza kuwa ni maneno yako tu binafsi.

Unaweza ukafungua uzi wenye kuonyesha mungu wako asiye na mikanganyiko tukajadili.

Karibu tujadili mada mkuu.
 
Mbona unaongea maneno tupu bila uthibitisho wowote? Haina tofauti na maneno ya kanga.

Muhamad hakuwahi kuisoma Biblia wala hata hakujua kusoma wala kuandika.
Na wala yeye hakuandika Quran maana Quran ilikuwa inashushwa na malaika
 
Inaweza kuwa ni maneno yako tu binafsi.

Unaweza ukafungua uzi wenye kuonyesha mungu wako asiye na mikanganyiko tukajadili.

Karibu tujadili mada mkuu.
Yes ni maneno binafsi yenye ukweli ndani yake...mfano mzuri hata wewe Kwa zaidi ya 60% I bet una background ya Kikristo ndiyo maana umekuja na mada hii Kwa kuwa kitabu unachotumia kimekuchanganya.


Tukiacha ushabiki usio na maana yoyote,.. Qur'an ndiyo imeelezea na kujibu maswali yote ambayo watu wanayajengea hoja., Kuanzia kile mnachoita problem of evils, existence of disasters,maradhi, vifo na kadhalika kwamba Kwa nini vinatokea,...na kwanini MUUMBAJI mwenye uwezo wa kuzuia vitu hivyo anaruhusu vitokee.

NB:- Huo ni mtazamo wangu naamini nipo sawa,. wewe pia una mtazamo wako unaamini upo sawa.. mwisho wa siku tupo hapa kujadili na ikishindikana kukubaliana basi itabidi tukubali kutokukubaliana.
 
Maneno binafsi hayawezi kuwa yana ukweli ! Ukweli unabaki kwako wewe mkuu.
Unaweza ukaanzisha uzi tukaona hicho unachoita ngano za kiarabu wewe mmakonde useme ni za kweli.

Karibu mkuu tujadili mada iliyopo.
 
Allah huyo, Anashushaje Quran kwa lugha moja tu ya kiarabu?

Allah huyo, Hakujua kwamba Duniani kuna watu wa lugha mbalimbali?

Allah huyo, Alishindwaje kushusha Quran hiyo kwa watu wote duniani wa lugha zote akaeleweka na watu wote kwa wakati mmoja?
Napita tu🏃
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…