Mikasa iliyotokea kipindi wanaigiza filamu za Yesu

Mikasa iliyotokea kipindi wanaigiza filamu za Yesu

Hapo ndipo wanapochanganya na kuona wakristo wanakufuru wakati ni imani tofauti.

YESU NI MUNGU.


Luka 18
19 Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna mtu aliye mwema ila Mungu peke yake.
Yohana 17
3 Na huu ndio uzima wa milele: wakufahamu wewe ambaye pekee ni Mungu wa kweli, nakumfahamu Yesu Kristo ambaye umemtuma.


Hapa Yesu alikua anamzungumzia Mungu gani?
 
Subiri waje wakuulize , Mungu anazaliwa ? Mungu anakubali kufa kizembe bila kujitetea?

Yesu ni Mungu kamili ila tu alipovaa mwili wa kibinadamu akaonekana ni binadamu kamili.
Kumbe mara nyingine Mungu wenu huwa anauvaa ubinadamu na huyo huyo mwasema hafananishwi!?

Mna taabu sana waamini
 
Achana na Titanic... Filamu ya Yesu ya mwaka 1979 ndio inaongoza kwa kutazamwa zaidi Duniani

Titanic ilikuwa inashikiliwa record ya filamu yenye mauzo makubwa, ila badae 2010 Movie ya AVATAR ikapindua na kuvunja record ya Titanic na kuifanya AVATAR kuwa ndio filamu yenye mauzo ya juu zaidi.

Jua kutofautisha Filamu kutazamwa zaidi na Filamu kuuza zaidi... Hivyo ni vitu viwili tofauti.

Filamu ya YESU ya mwaka 1979 imetazamwa karibia Duniani kote, na bado inazidi kutizamwa
Tunajuje kama imetizamwa zaidi bila kuuzwa zaidi?
 
Tunajuje kama imetizamwa zaidi bila kuuzwa zaidi?
Filamu ya Yesu haikutengenezwa kibiashara kwa ajili ya kuuzwa bali ilikua ni mission ya kutangaza Injili ...ndiomana huko vijijini watu huwa wanakusanyika kuangalia sinema ya Yesu free of charge
 
Haikuwa kazi nyepesi kuigiza movie za Yesu. Songombingo lilianza katika ile scene ya msalabani. Scenes zote ilikuwa rahisi sana isipokuwa ile ya msalabani.

Kwenye ile movie ya mwaka 1979 ya Yesu iliyoigizwa na Decon, Brian Deacon anasimulia kwenye interview kuwa wakati wa scene ya msalabani haikuwa nyepesi kuigizwa kwani walikumbana na dhoruba kubwa la radi kiasi cha kushindwa kuigiza hivyo wakasubiri siku inayofuata. Haikubadilika, Hali ilitulia lakini baada ya Decon kuwekwa msalabani upepo mkali ulivuma, lakini hawakukata tama. Movie ya yesu ya Brian Deacon ndio movie mpaka sasa inayoshikilia rekodi ya Dunia ya kutazamwa mara nyingi na pia inashikilia rekodi ya movie iliyotafsiriwa kwenda lugha mbalimbali Duniani. Movie hii ilichezewa huko katika milima ya nchini Israel. Na mpaka leo hii Director (Muongozaji) wa filamu huyo hajulikani ni nani. Na baadhi ya waigizaji walishafariki na muigizaji mkuu aliyeigiza kama Yesu sasa ana takribani miaka 75 mwaka huu 2024.

Mikasa Haikutokea kwao tu kina Deacon bali hata kwenye movie ya Passion of Christ ya 2004, Muandaaji wa hiyo filamu, Mel Gibson alielezea songombingo la namna hiyo, walisitisha kuigiza filamu hiyo kwa siku tatu mfululizo kutokana na radi za mara kwa mara zilizoibuka tu na tetemeko la ardhi, anasema hata Jim Caviezel aliyeigiza kama Yesu alinusurika kuuwawa na radi. Pia alikumbwa na magonjwa mbalimbali ya mapafu ikiwemo Pneumonia, pamoja na kuishiwa joto la mwili. Filamu hiyo iliigizwa huko Italia katika kipindi cha majira ya baridi kali.
Hivi ni mtangazaji gani aliyetafsiri filamu ya Yesu kwa Kiswahili...jamaa alitisha sana aisee
 
Achana na Titanic... Filamu ya Yesu ya mwaka 1979 ndio inaongoza kwa kutazamwa zaidi Duniani

Titanic ilikuwa inashikiliwa record ya filamu yenye mauzo makubwa, ila badae 2010 Movie ya AVATAR ikapindua na kuvunja record ya Titanic na kuifanya AVATAR kuwa ndio filamu yenye mauzo ya juu zaidi.

Jua kutofautisha Filamu kutazamwa zaidi na Filamu kuuza zaidi... Hivyo ni vitu viwili tofauti.

Filamu ya YESU ya mwaka 1979 imetazamwa karibia Duniani kote, na bado inazidi kutizamwa
Ona hiyi
IMG_20240107_092740.jpg
 
Soma Mwanzo 1:1-14...

Hapo mwanzo kulikuwa na neno naye neno alikuwa kwa Mungu, naye neno alikuwa Mungu..
Yesu kabla ya kuja duniani alikuwepo mbinguni kama kiumbe wa roho,na yeye ndio kiumbe wa kwanza kabisa kuumbwa kabla ya kitu chochote kile,Methali(Mithali)8:22-31,baada ya Yesu kuumbwa yeye pia alikuwa anashirikishwa katika kazi ya uumbaji,kama hiyo mistari ilivyoeleza Yan alikuwa msaidizi, ndiomaana Kuna mistari inayosema "Tumfanye mtu Kwamfano wetu" hapo Mungu alikuwa anamwambia Yesu,,lakini pia Mungu hawezi kufa ila Yesu alikufa siku3,,soma hapa kidogo Yohana20:17 'Yesu akamwambia acha kuning'ang'ania,kwamaana Bado sijaoanda kwenda kwa Baba.Lakini nenda kwa ndugu zangu,nawe uwaambie,Ninapanda KWENDA KWA BABA YANGU NA BABA YENU na kwa MUNGU WANGU NA MUNGU WENU"
 
Luka 18
19 Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna mtu aliye mwema ila Mungu peke yake.


Yohana 17
3 Na huu ndio uzima wa milele: wakufahamu wewe ambaye pekee ni Mungu wa kweli, nakumfahamu Yesu Kristo ambaye umemtuma.


Mathayo 27:46​

Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
Fikiria vizuri kabla ya kumuita Yesu kuwa ni Mungu
Mungu anaukuu wa hali ya juu na hafanishwi na kitu chochote!
Andiko lipo linaloonesha yesu ni Mungu, wakiristo wamegawanyika,wapo wanaamini yesu Mungu na wapo wanaamini ni mwana wa Mungu,na wote wapo sahihi kwa mujibu wa biblia
 
Back
Top Bottom