mshakamshaka
JF-Expert Member
- Oct 19, 2019
- 355
- 647
Hahahahahh
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yaaani uache nyumbani kwako ukakae lodge peke yako? Utakuwa unaumwa sio bure
Hiyo hotel naijua ipo ubungo maziwa1. Demu wangu kaniambia anakuja. Hua sipendi kuleta wanawake geto. Nikaenda mtaa wa tatu kuna lodge nikachagua chumba kizuri kabisa, nikakikagua kiko safi, nikakilipia nikaondoka nikawaambia ntarudi baadae. Saa hiyo ilikua kwenye saa tisa.
Mida ya saa 1 usiku demu kanipigia amefika, nikamfuata tukaelekea lodge. Kuingia chumbani tunakaribishwa na kitanda kimevurugika, makasha ya condom sakafuni na condom used! Aisee demu alikua mbogo ananiambia ina maana ulikua na mwanamke mwingine humu. Ilikua mshike mshike. Demu akasepa usiku ule ule.
2. Niko na demu tumeenda loji usiku, tukakuta jamaa wawili. Kuulizia chumba jamaa wakaangaliana, mmoja akamwambia mwingine "wape namba 12". Tukaingia. Ile tumeanza purukushani demu akaniambia "mbona nasikia harufu ya sigara..?" Mmh.. mi siskii chochote. Nikaenda dirishani nikakuta dirisha moja kitasa kibovu halifungi. Nikalirudishia. Dakika 10 nyingi demu ananiambia tena "nasikia harufu ya sigara.. mi sipatani na sigara kabisa..!" Nikanyanyuka tena, kwenda dirishani nakuta dirisha lipo wazi. Kucheki vizuri naona jamaa limechuchumaa kwa chini ya dirisha.
3. Kuna hoteli moja ipo hapo dar (jina kapuni) karibu na kituo kikuu cha mabasi cha zamani. Hii hoteli ina balcony ambazo milango yake ni aluminium na vioo na haina pazia milangoni. Changamoto yake ni kwamba hoteli hii iko muundo wa "L". Kwakua ina madirisha makubwa ya aluminium, kuna baadhi ya vyumba ukiangalia dirishani unaona vizuri kabisa ndani ya chumba kilichopo upande wa pili kupitia mlango huo wa kioo. Tena unaona kitandani!! Pia unapata view nzuri kabisa ya chumba kilichopo floor moja chini. Ni shida.
Daah tunduma ilikuwa lodge ipi hiyo sammy , nyati au olimpiaDah mimi hiyo imenitokea juzi Tunduma. Mida ka hiyo saa 8 usiku nimelala lodge nipo mwenye nikasikia kwa nje mtu anajaribu kufungua mlango ameingiza funguo, bahati nzuri na mimi sikua nimechomoa funguo kwa ndani. Nikauliza kwa ukali wewe ni nani, nikajibiwa na sauti ya kike samahani nimekosea namba.( I was like w.t.f?)
Kusoma ni kama jambo limekukuta unakunywa kahawa.Utaliangalia tu.Ila kusoma maujinga unaweza mkuu.
Hill park panaitwa. Ipo maeneo ya Kilimanjaro wanaita.Daah tunduma ilikuwa lodge ipi hiyo sammy , nyati au olimpia
Bond kubwa ni Upendo kati yetu na sio trauma,,hizo ni kama catalyst tuu ktk mahusiano,mfano mtu anakwambia yani nampenda sana mke wangu na kilichofanya nimpende zaidi mpk kumuoa ni vile anavyochukulia matatizo yangu kama yake,au vile alivyo na huruma,au vile alivyomsafi etc...etc....Aah hiyo ndio maana ya shared trauma relationship.
Yani bond kubwa kwenye relationship ni yale matatizo mliyoyapata kama kufiwa, ajali etc.
[emoji2][emoji2][emoji2] Ilikuaje?Mwanza nilifikia hotel moja mjini pale floor ya pili, kwa chini kuna bar , nikaenda nikapata demu muhudumu pale, kumbe mtu wa jikoni ni mtu wake.
Demu walivofunga akaja kwangu, watu wakamsanua mwana...ulikua ni shida hio siku.
[emoji23]Mimi niliachia kimba juu ya kitanda baada ya mhudumu kunitolea nje nisimle [emoji2][emoji2][emoji2]
[emoji23] pole. Ila kiukweli kwenda kulala kwenye magesti kunataka moyo bora hotel kama mfuko uko njema.baada ya kukosa lodge nikapata moja mida ya saa saba, kuingia imetumika kumevurugwa, maji chapa chapa, mataulo mabichi,hewa nzito ya jasho km watu walikuamo muda si mrefu!!
Nje usalama mdogo,ikabidi nilale juu ya meza ilikuwepo room,kuskilizia ni maumivu ya mgongo isitoshe meza si kubwa yakanishinda ikabidi nigeuze godoro juu chini pakakucha kwa taaabu sana
Nilihisi kinyaaa
Enzi hizo ndo tuko chuo hela ya hotel unamaliza kibubu mnatafuta lodge nzuri tena safi mpya mpya hahaa. Ila siku hz hata niende mkoa silali lodge au guest aisee ni hotelini tena nzuri. Usalama na usafi ni muhimu.[emoji23] pole. Ila kiukweli kwenda kulala kwenye magesti kunataka moyo bora hotel kama mfuko uko njema.
Kwenye haratakati za hapa na pale nilishawahi kukutana na Mikasa kadhaa ya lodge/gest nilizowahi kulala !
Mimi kinachonipa tabu kwanza nikiwaza mashuka sijui mataulo yashatumiwa na watu kibao kabla yangu nami tena nikatumie hata kama yanafuliwa aah naona kero tu.Enzi hizo ndo tuko chuo hela ya hotel unamaliza kibubu mnatafuta lodge nzuri tena safi mpya mpya hahaa. Ila siku hz hata niende mkoa silali lodge au guest aisee ni hotelini tena nzuri. Usalama na usafi ni muhimu.
Mkoba wa mwanamke haukosi khanga. Mm hata mpk leo siwezi tumia taulo la hotel.Mimi kinachonipa tabu kwanza nikiwaza mashuka sijui mataulo yashatumiwa na watu kibao kabla yangu nami tena nikatumie hata kama yanafuliwa aah naona kero tu.
Taulo huwa sigusi issue ipo kwenye mashuka, hakuna namna.Mkoba wa mwanamke haukosi khanga. Mm hata mpk leo siwezi tumia taulo la hotel.
Hapo sister unaongelea mashuka ya mahotel makubwa ....sasa huku kwenye guest bubu unahisi hali ikoje,ni noma sana...kuna time upo mishe mishe unalala basi tu huna namnaTaulo huwa sigusi issue ipo kwenye mashuka, hakuna namna.
😂😂 Kote huko naelewa ila hotel ni safi tofauti na huko kwingine. Na kweli kuna muda unakua huna option lazima upambane nazo.Hapo sister unaongelea mashuka ya mahotel makubwa ....sasa huku kwenye guest bubu unahisi hali ikoje,ni noma sana...kuna time upo mishe mishe unalala basi tu huna namna