Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Stori ishaanza kukosa Radha Haina hata uzuri wowte yaani ,kisa huko chini itaendelea nachokushauri usilete huo mwendelezo badala ya kusema itaendelea andika hata siku mbili au tano kabisa ikisha kamilika ndo uilete hapo hakuna hata Cha kukielewa ,smart people always doing smart thing
Mr. Smart usipangie watu maisha tafadhali, ungekuwa smart kama unavyojinadi hapa wala usingekuwa unasoma stories humu jukwaa la Entertainment, ungekuwa zako unawaza jinsi ya kujenga ghorofa angani..!

Halafu,kingereza chenyewa Mr. Smartie naona kimekukataa, usikitumie.!
 
Duu nimegundua kuwa watu wengi wanapenda stories humu ndani
Yaani mtoa hadithi usipomalizia huu mkasa utawaudhi watu wengi Sana

Hebu on a watu wanavyokutetea huku[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Hahaha, jamaa ni mshabiki wa Arsenal, chochote kinaweza kutokea.

Story yenyewe imekaa kama Isidingo, haiishi hivi karibuni.
 
Mr. Smart usipangie watu maisha tafadhali, ungekuwa smart kama unavyojinadi hapa wala usingekuwa unasoma stories humu jukwaa la Entertainment, ungekuwa zako unawaza jinsi ya kujenga ghorofa angani..!

Halafu,kingereza chenyewa Mr. Smartie naona kimekukataa, usikitumie.!

Story mbayaaaa! Tumeichoka.
 
Mimi kinachonifurahisha kuliko hata story yenyewe ni kamati ya maadili. Imejipanga kwa kweli, naona hawataki tena mambo yaliyojitokeza kwenye story ya kwanza yajirudie

Nilicheka jamaa alivyomalizia part 1 kwa hasira, watu hawajui hata mambo ya pedali yalimalizwaje.

Hata hii tutamchanganya tu baadae, ngoja na sisi ma-opposer wa motion tutafute nguvu.
 
MKASA WA PILI -sehemu ya 9

Inaendelea.............


Tulitafuta maeneo ya pale jirani walipokuwa wakiuza uji,Kuna dada tulimkuta pale na alitukaribisha.

Nilimuuliza "Uji unauzaje?".

Alituambia "Nauza shilingi 100 kwa kikombe".

Niliendelea kumuuliza "hizo karanga hapo unauzaje?".

Alijibu "karanga nazo nauza shilingi 100".

Basi nikamwambia dogo "Kwenye hili buku kila mtu atatumia 500".

Nilimwambia yule dada atuweke uji,maeneo hayo wakati sisi tunakwenda kupata uji hakukuwa na mtu yeyote,ila kadri muda ulivyozidi kwenda ndiyo vijana nao wakawa wanaongezeka kupata uji!,haikuwa ngumu mimi kutambua kwamba yule dada hakuwa mgeni hayo maeneo,kwasababu vijana wengi walionekana kumchangamkia na kuanza kutaniana.Nilitamani sana nianzishe mazoea na yule dada kwa wakati ule lakini kwakuwa vijana walikuwa wengi ilibidi nisubiri kwanza wapungue!.Kadri muda ulivyosonga vijana nao wakawa wakipungua maeneo yale,na sisi tulichokifanya ni kunywa ule uji kwa madaha,hatukuwa na haraka maana hatukuwa na mahali pakwenda usiku huo!.

Nilijikuta nimemsemesha yule dada ghafla "Unaitwa nani?".

Alijibu "Naitwa Mkami".

Nilimwambia "Dada mkami inaelekea wewe ni mcheshi sana,maana naona vijana wengi wanakutania sana".

Yule dada alianza kucheka akaniambia "Hawa tumeshazoeana nao ndiyo maana wanapenda kunitania".

Baada ya mazungumzo ya hapa na pale ilibidi nimwambie ya kwamba maeneo yale sisi tulikuwa wageni na hatukuwa na mwenyeji.

Nilimwambia "ningeomba uwe mwenyeji wetu dada Mkami".

Aliniuliza "Kwani nyinyi mnatoka wapi?".

Ilibidi nimdanganye kwamba tulikuwa tumetokea Musoma na tulikuja hapo kumfata jamaa mmoja ambaye tulikuwa tunamdai pesa,tulipofika kumtafuta kwenye simu akawa kazima simu hakupatikana na hatukuwa na pesa yeyote ya kuturudisha Musoma.Dada Mkami alionekana kushangaa sana.
Aliniuliza "Kwahiyo haya maeneo nyinyi ni wageni?".

Nikamjibu "Ndiyo".

Nilijaribu kuongea na kuonyesha huzuni ili angalau huruma imwingie aone namna ya kutusaidia,nilijikaza kisabuni nikamuomba atusaidie tu sehemu ya kulala kwa usiku huo ili asubuhi tungejua la kufanya.Mkami alituambia kwamba yeye anakaa na mama yake na nyumba wanayokaa kuna chumba kimoja na sebule hivyo ingekuwa ngumu sisi kupata nafasi kwa usiku huo pale kwao!.

Alituambia "Ngoja kuna kijana mmoja huwa anakuja kunywa uji hapa tunafahamiana naye,akija nitajaribu kumueleza najua atawasaidia".

Baadae kidogo mida ya saa 3 usiku alikuja jamaa mmoja wakaanza kuongea,jamaa alimuuliza "Mtoto anaendeleaje?".

Kwa yale mazungumzo yao kwa haraka haraka nikajua yule jamaa atakuwa mpenzi wake na Mkami japo ilionesha hawakai wote,kapo Mkami yeye hakutuambia lakini kwakuwa mimi nilikuwa mtu mzima tayari nikaelewa!.Basi baadae tukasalimiana na yule jamaa pale na ukimya ukatawala kidogo!,tulikaa pale mpaka mida ya saa 4 usiku ndipo yule jamaa akataka kuondoka,Mkami alimuita akamueleza hali halisi kuhusu sisi,jamaa kiukweli nilimpenda sana maana hakuwa na maneno mengi.

Alituambia "Twendeni nyumbani".

Alituuliza "Vipi,mmekula?".

Nilimjibu "Tushakula bro".

Nilimshukuru sana Mkami kwa wakati ule maana sikutegemea sana,Yule jamaa ilionekana alikuwa mnyenyekevu sana maana hata wakati tukiwa njiani tulikuwa tukipiga stori na ilionekana na yeye kuna mambo mengi tu ya maisha alikuwa kapitia hivyo alikuwa akitutia moyo!.Tulifika hapo geto kwake na jamaa alituelekeza tukachote maji kwenye kisima kilichokuwa nje ya hiyo nyumba kwa ajili ya kuoga kuondoa uchovu!,kiukweli mimi nguo zangu zilishaanza kutoa harufu kwa ajili ya jasho.

Jamaa wakati tukiwa njiani tunaelekea kwake alituambia yeye jina lake ni Mashauri na sisi pia tulimtajia majina yetu.Usiku ule mimi nilimwambia Mashauri atusaidie sabauni kama anayo ili tuweze kufua nguo zetu,jamaa alituletea kipande cha Sabuni tukaanza kufua huku mastori yakiendelea kama kawaida.Mashauri alituambia ya kwamba yule dada Mkami alikuwa mpenzi wake na walifanikiwa kupata mtoto mmoja ambapo kwa wakati ule wa kuuza uji mtoto huwa anamwacha nyumbani na bibi yake.Katika maongezi nilimwambia jamaa kwamba tulikuwa na safari ya kwenda Bunda,kwakuwa Mkami alikuwa keshamueleza kuhusu sisi,nilimwambia baada ya kumkosa mtu tuliyemfuata hapo Ikizu ilibidi tuondoke kuelekea Bunda halafu ndiyo tungerudi Musoma,sikutaka sana kupindisha uongo ambao nilikuwa tayari nilikuwa nishamdanganya Makami.Mashauri alituambia kama tunaenda Bunda,asubuhi tujitahidi kuamka mapema ili twende naye mpaka kile kijiji cha Nyamuswa tungepata gari.

Mashauri alituambia yeye ni dalali wa Mbuzi,hivyo huwa anaenda huko vijijini anawakusanya kisha anawapeleka hapo Nyamuswa kuna eneo maalumu wanawekwa halafu yeye hupewa chake.Hivyo akatuambia kwakuwa kesho kuna magari yangekuja kuchukua mbuzi angetuombea tupate lift mpaka Bunda,Kiukweli nilimuona Mashauri ni muungwana sana.

Nilipomaliza kufua nilihakikisha zile nguo zangu nazikung'uta kisawasawa,hiii yote nilitaka kwa usiku ule ziwahi kukauka kwa upepo maana hakukuwa na jua.Baada ya shughuli za kufua na kuoga zilipokamilika tuliingia geto kwa Mashauri ambako kulikuwa kumenakishiwa vizuri kwa magazeti ukutani!,japo ile nyumba ilikuwa niya nyasi lakini kijana mwenzetu alikuwa kajitahidi sana kupendezesha geto lake,kwakuwa alikuwa na kitanda kidogo nilimwambia yeye alale na dogo na mimi kuna jamvi lilikuwa pale nje aliniletea nikatandika chini akanipa na shuka mrume ndago nikauchapa usingizi!.Usingizi japo ulikuwa wa mang'amu ng'amu lakini nilimshukuru sana Mungu maana kupata sehemu ya kulala kwa usiku ule halikuwa jambo jepesi,tena kwa mtu ambaye tulikuwa hatufahamiani.

Usiku huo jamaa alifungulia redio yake iliyokuwa ikitumia betri akaweka stesheni fulani hivi tukaanza kusikiliza miziki,nilipitiwa na usingizi nikajikuta nashituka kushakucha.Mashauri yeye aliwahi kuamka,mimi na dogo tuliamka mida ya saa 1 asubuhi ndipo Mashauri alisema tujiandae twende kwao Mkami akatupikie uji tunywe kisha tuelekee Nyamuswa.Basi tulijiandaa pale japo nguo zangu hasa suruali ilikuwa haijakauka vizuri nilivaa hivyo hivyo,dogo naye mambo yalikuwa yale yale!.Tuliondoka na Mashauri mpaka kwao Mkami asubuhi hiyo na tulipofika tulimkuta Mkami na mama yake na yule mtoto wa Mashauri,kilikuwa kibinti cha miaka 3 hivi!.
Basi Mashauri akaanza kuongea na Mkami kilugha,baadae mkami aliondoka na jembe pale nyumbani ambapo hakupita muda alikuja na mihogo mibichi!,Kumbe kwa wakati ule inaonekana jamaa alimwambia akachimbe mihogo aje atupikie ili tule tuondoke.

Baada ya kuwa tumemaliza kupata uji na mihogo ya kuchemsha tulianza sasa kutembea kuelekea Nyamuswa,wakati tunaenda nilimshukuru sana Mashauri,jamaa alikuwa ni mtu mmoja muungwana sana,ile roho aliyokuwa nayo Mashauri sijui kama vijana wa leo wangekuwa nayo!.Tulitembea kwa muda kidogo na hatimaye tukafika hapo Nyamuswa,tulifika mpaka mahala wanapowahifadhi wale mbuzi,jamaa akatuambia tusubilie gari la kubebea mbuzi maana halikuwa mbali.Gari lilipofika mbuzi walianza kupakiwa kwa kuhesabiwa na sisi ilibidi tuanze kumsaidia Mashauri kupakia wale mbuzi kwenye ile fuso,tulipomaliza ile kazi Mashauri aliongea na yule dereva kwamba sisi ni ndugu zake na akifika Bunda atuache.Kabla ya kuingia kwenye lori nilimuomba Mashauri namba yake ya simu nikamwambia tungekuwa tunawasiliana.

Nyuma ya lile lori kulikuwa na jamaa wengine wawili ukiacha sisi,jumla tulikuwa 4,Kuna jamaa nilimuuliza kwa wakati ule walikuwa wakielekea wapi baada ya hapo?,jamaa alisema wanaelekea Tabora ila katikati ya safari kabla ya kufika Bunda kuna vituo viwili wangesimama kuchukua mbuzi wengine.


Itaendelea.................
 
Stori ishaanza kukosa Radha Haina hata uzuri wowte yaani ,kisa huko chini itaendelea nachokushauri usilete huo mwendelezo badala ya kusema itaendelea andika hata siku mbili au tano kabisa ikisha kamilika ndo uilete hapo hakuna hata Cha kukielewa ,smart people always doing smart thing
"Always doing"😂😂😂 my shit.. !
 
MKASA WA PILI -sehemu ya 9

Inaendelea.............


Tulitafuta maeneo ya pale jirani mahala walipokuwa wakiuza uji,Kuna dada tulimkuta pale na alitukaribisha!,Nilimuuliza uji anauzaje,Alisema "Nauza shilingi 100 kwa kikombe",Na hizo karanga hapo unauzaje?,niliendelea kumuuliza!,Pia alituambia karanga anauza 100!

Basi nikamwambia dogo "Kwenye hili buku kila mtu atatumia 500",Nilimwambia yule dada atuweke uji!
Maeneo hayo kiukweli wakati sisi tunakwenda hapo kupata uji hakukuwa na mtu yeyote ila kadri muda ulivyozidi kwenda ndo vijana nao wakawa wanaongezeka kupata uji!,Haikuwa ngumu mimi kutambua kwamba yule dada hakuwa mgeni pale maana vijana wengi walionekana kumchangamkia na kuanza kutaniana!
Nilitamani sana nianzishe mazoea nae kwa wakati ule lakini kwakuwa vijana walikuwa wengi ilibidi nisubiri kwanza wapungue!

Kadri muda ulivyosonga vijana nao wakawa wakipungua maeneo yale,na sisi tulichokifanya ni kunywa ule uji kwa madaha,hatukuwa na haraka maana hatukuwa na pa kwenda!

Nilijikuta nimemsemesha yule dada ghafla "Unaitwa nani"?,Naitwa "Mkami" yule dada alijibu!

"Dada mkami inaelekea wewe ni mcheshi sana,maana naona vijana wengi wanakutania sana",Yule dada alianza kucheka akanambia "Hawa tumeshazoeana nao ndo maana wanapenda kunitania"

Baada ya mazungumzo ya hapa na pale ilibidi ni mwambie ya kwamba maeneo yale sisi ni wageni na hatuna mwenyeji na ningeomba yeye awe mwenyeji wetu!
Aliniuliza "Kwani nyinyi mnatoka wapi",Ilibidi nimdanganye kwamba Tunatoka Musoma na tulikuja hapo kumfata jamaa mmoja ambaye tulikuwa tunamdai na tulipofika na kumtafuta kwenye simu akawa kazima simu hakupatikana na hapo hatukuwa na pesa yeyote ya kuturudisha Musoma,Dada Mkami alionekana kushangaa kidogo,Aliniuliza "Kwahiyo haya maeneo nyinyi ni wageni"?,Nakamwambia "Ndiyo"

Nilijaribu kuongea na kuonyesha uzuni ili angalau huruma imwingie ili aone namna ya kutusaidia!,Nilijikaza kisabuni nikamuomba atusaidie tu sehemu ya kulala kwa wakati huo ili asubuhi tutajua la kufanya!

Mkami alituambia kwamba yeye anakaa na mama yake na nyumba wanayokaa kuna chumba kimoja na sebule hivyo ingekuwa ngumu sisi kupata nafasi kwa usiku huo pale kwao!,Ila alituambia "Ngoja kuna kijana mmoja huwa anakuja kunywa uji hapa tunafahamiana naye,akija ntajaribu kumueleza najua atawasaidia".

Baadae kidogo kama mida ya saa 3 usiku alikuja pale jamaa na wakaanza kuongea na jamaa ilionekana anamuuliza "Mtoto anaendeleaje"?,Kwa yale mazungumzo yao kwa haraka haraka nikajua yule jamaa atakuwa Mpenzi wake na Mkami japo ilionesha hawakai wote,Japo Mkami yeye hakutuambia lakini kwa mimi ni mtu mzima tayari nshaelewa!

Basi baadae tukasalimiana na yule jamaa pale na ukimya ukatawala kidogo!,Tulikaa pale mpaka mida ya saa 4 usiku ndipo yule jamaa akataka kuondoka,Mkami alimwita akamwambia situation iliyotukuta na jamaa kiukweli nilimpenda sana maana hakuwa na maneno mengi,Alituambia "Twendeni Nyumbani",Alituuliza pale "Vp mmekula"?,Nilimwambia "Tushakula bro"

Nilimshukuru sana Mkami kwa wakati ule maana sikutegemea sana,Yule jamaa inaonekana alikuwa mtu wa watu maana hata wakati tukiwa njiani tulikuwa tukipiga stori na ilionekana na yeye kuna mambo mengi tu ya maisha alikuwa kapitia hivyo alikuwa akitutia moyo!
Tulifika hapo geto kwake na jamaa alituelekeza tukachote maji kwenye kisima kilichokuwa nje ya hiyo nyumba kwa ajili ya kuoga kuondoa uchovu!,kiukweli mimi nguo zangu zilishaanza kutoa hatufu kwa ajili ya jasho na dogo nae vile vile!

Jamaa wakati tukiwa njiani àlituambia anaitwa Mashauri na sisi pia tulimtajia majina yetu!

Usiku ule mimi nilimwambia Jamaa atusaidie sabauni kama anayo ili tuweze kufua nguo zetu,jamaa alituletea kipande cha Sabuni tukaanza kufua pale huku mastori yakiendelea kama kawaida!
Mashauri alituambia ya kwamba yule Dada Mkami alikuwa demu wake na wamefanikiwa kupata mtoto mmoja ambapo kwa wakati ule wa kuuza uji Mkami mtoto huwa anamwacha nyumbani na Bibi yake!,Basi tuliendelea sana kupiga stori na jamaa alikuwa mtu wa watu sana!

Katika maongezi nilimwambia Jamaa kwamba kesho sisi tunasafari ya kwenda Bunda na kiukweli sikutaka kabisa kumweleza chochote kuhusu kilichotupeleka kule!,Jamaa alituambia kama tunaenda Bunda Asubuhi twende nae mpaka kijiji kimoja kinaitwa Nyamuswa kwani yeye anafanya biashara ya mbuzi na kuzipeleka hapo baadae kuna magari yanakuja kufata kupeleka Mwanza na sehemu nyingine!,Mashauri alivyotuambia kwamba yeye ni kama dalali wa Mbuzi,hivyo huwa anaenda huko vijijini anawakusanya kisha anawapeleka hapo Nyamuswa huwa kuna eneo maalumu wanawekwa halafu yeye hupewa chake!
Hivyo akatuambia kwakuwa kesho kuna magari yangekuja kuchua mbuzi pale angetuombea tupate lift mpaka Bunda,Kiukweli nilimuona Mashauri ni muungwana sana!

Nilipomaliza kufua nilihakikisha zile nguo zangu nazikung'uta kisawasawa,Hii yote nilitaka kwa usiku ule ziwahi kukauka kwa upepo!

Baada ya shughuli na kufua na kuoga zilipokamilika tuliingia geto kwa Mashauri na kulikuaa kumenakshiwa vizuri kwa magazeti ukutani!,Japo ile nyumba ilikuwa niya nyasi lakini kijana mwenzetu alikuwa kajitahidi sana kupendezesha chumba chake!,kwakuwa alikuwa na kitanda kidogo nilimwambia yeye alale pale na dogo na mimi kuna jamvi lilikuwa pale nje aliniletea nkatandika chini akanipa na shuka Mrume ndago nkauchapa usingizi!
Usingizi japo ulikuwa wa mang'amu ng'amu lakini nilimshukuru sana Mungu maana kupata sehemu ya kulala kwa usiku ule ilikuwa ni ishu!

Usiku huo jamaa alifungulia redio yake mmoja hivi iliyokuwa ikitumia betri na akaweka stesheni fulani hivi tukaanza kusikiliza!,Nilipitiwa na usingizi na nimejikuta nashituka kushakucha!

Mashauri yeye aliwahi kuamka,Mimi na dogo tuliamka mida kama ya saa 1 asubuhi ndipo Mashauri alisema tujiandae twende kwao Mkami akatupikie uji ili tuelekee Nyamuswa!

Basi tulijiandaa pale japo nguo zangu hasa suruali ilikuwa haijakauka vizuri nilivaa hivyo hivyo,dogo nae mambo yalikuwa yale yale!
Tuliondoka na Mashauri mpaka kwao Mkami asubuhi hiyo na tulipofika tulimkuta Mkami na Mama yake na yule mtoto wa Mashauri,kilikuwa kibinti kama cha miaka 3 hivi!
Basi Mashauri akaanza kuongea na mkami pale kilugha baadae mkami aliondoka na jembe pale nyumbani,Baadae kidogo alikuja na mihogo mibichi!,Kumbe kwa wakati ule inaonekan jamaa alimwambia akachimbe mihogo aje atupikie ili tule tuondoke!

Hivyo ndivyo ilivyokuwa ndugu zangu!


Baada ya kuwa tumemaliza kupata uji na mihogo ya kuchemsha tuliagana pale na kuanza sasa kutembea kuelekea Nyamuswa!,wakati tunaenda nilimshukuru sana Mashauri!,Jamaa alionekana ni mtu wa watu kweli!,Hii roho sijui kama vijana wa leo wangekuwa nayo!

Tulitembea kwa muda kidogo na hatimaye tukafika hapo Nyamuswa!,tulifika mpaka mahala wanapowahifadhi wale mbuzi na jamaa akasema ngoja tusubilie gari la kubebea mbuzi maana halikuwa mbali sana na pale!

Gari lilipofika mbuzi walianza kupakiwa kwa kuhesabiwa na sisi ilibidi tuanze kumsaidia Mashauri kupakia wale mbuzi kwenye ile fuso!
Tulipomaliza ile kazi Mashauri aliongea na yule dereva pale kwamba sisi ni ndugu zake na akifika Bunda atuache!,Basi kabla ya kuingia kwenye lori nilimuomba Mashauri namba za simu na akanipa nkamwambia tutawasiliana!,Nyuma ya lile lori kulikuwa na jamaa wengine wawili ukiacha sisi,Jumla tulikuwa 4!,Kuna jamaa nilimuuliza kwa wakati ule walikuwa wakienda wapi?,Jamaa alisema wanaelekea Tabora ila humo katikati kabla ya kufika Bunda kuna vituo kama viwili watasimama kuchukua mbuzi!


Itaendelea.................
Hata kama wana kamati watachukia lakini lazima tukubali maelezo yamekuwa mengi yasiyo na maana yoyote[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
 
Hata kama wana kamati watachukia lakini lazima tukubali maelezo yamekuwa mengi yasiyo na maana yoyote[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
Achana nayo tu.
 
Kuacha ni ngumu maana nina uraibu na usomaji wa stori wakuu
 
Hata kama wana kamati watachukia lakini lazima tukubali maelezo yamekuwa mengi yasiyo na maana yoyote[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
ukiyaona yaruke tuachie sisi....wacha magugu na ngano vikue pamoja
 
Back
Top Bottom