MKASA WA PILI -sehemu ya 9
Inaendelea.............
Tulitafuta maeneo ya pale jirani mahala walipokuwa wakiuza uji,Kuna dada tulimkuta pale na alitukaribisha!,Nilimuuliza uji anauzaje,Alisema "Nauza shilingi 100 kwa kikombe",Na hizo karanga hapo unauzaje?,niliendelea kumuuliza!,Pia alituambia karanga anauza 100!
Basi nikamwambia dogo "Kwenye hili buku kila mtu atatumia 500",Nilimwambia yule dada atuweke uji!
Maeneo hayo kiukweli wakati sisi tunakwenda hapo kupata uji hakukuwa na mtu yeyote ila kadri muda ulivyozidi kwenda ndo vijana nao wakawa wanaongezeka kupata uji!,Haikuwa ngumu mimi kutambua kwamba yule dada hakuwa mgeni pale maana vijana wengi walionekana kumchangamkia na kuanza kutaniana!
Nilitamani sana nianzishe mazoea nae kwa wakati ule lakini kwakuwa vijana walikuwa wengi ilibidi nisubiri kwanza wapungue!
Kadri muda ulivyosonga vijana nao wakawa wakipungua maeneo yale,na sisi tulichokifanya ni kunywa ule uji kwa madaha,hatukuwa na haraka maana hatukuwa na pa kwenda!
Nilijikuta nimemsemesha yule dada ghafla "Unaitwa nani"?,Naitwa "Mkami" yule dada alijibu!
"Dada mkami inaelekea wewe ni mcheshi sana,maana naona vijana wengi wanakutania sana",Yule dada alianza kucheka akanambia "Hawa tumeshazoeana nao ndo maana wanapenda kunitania"
Baada ya mazungumzo ya hapa na pale ilibidi ni mwambie ya kwamba maeneo yale sisi ni wageni na hatuna mwenyeji na ningeomba yeye awe mwenyeji wetu!
Aliniuliza "Kwani nyinyi mnatoka wapi",Ilibidi nimdanganye kwamba Tunatoka Musoma na tulikuja hapo kumfata jamaa mmoja ambaye tulikuwa tunamdai na tulipofika na kumtafuta kwenye simu akawa kazima simu hakupatikana na hapo hatukuwa na pesa yeyote ya kuturudisha Musoma,Dada Mkami alionekana kushangaa kidogo,Aliniuliza "Kwahiyo haya maeneo nyinyi ni wageni"?,Nakamwambia "Ndiyo"
Nilijaribu kuongea na kuonyesha uzuni ili angalau huruma imwingie ili aone namna ya kutusaidia!,Nilijikaza kisabuni nikamuomba atusaidie tu sehemu ya kulala kwa wakati huo ili asubuhi tutajua la kufanya!
Mkami alituambia kwamba yeye anakaa na mama yake na nyumba wanayokaa kuna chumba kimoja na sebule hivyo ingekuwa ngumu sisi kupata nafasi kwa usiku huo pale kwao!,Ila alituambia "Ngoja kuna kijana mmoja huwa anakuja kunywa uji hapa tunafahamiana naye,akija ntajaribu kumueleza najua atawasaidia".
Baadae kidogo kama mida ya saa 3 usiku alikuja pale jamaa na wakaanza kuongea na jamaa ilionekana anamuuliza "Mtoto anaendeleaje"?,Kwa yale mazungumzo yao kwa haraka haraka nikajua yule jamaa atakuwa Mpenzi wake na Mkami japo ilionesha hawakai wote,Japo Mkami yeye hakutuambia lakini kwa mimi ni mtu mzima tayari nshaelewa!
Basi baadae tukasalimiana na yule jamaa pale na ukimya ukatawala kidogo!,Tulikaa pale mpaka mida ya saa 4 usiku ndipo yule jamaa akataka kuondoka,Mkami alimwita akamwambia situation iliyotukuta na jamaa kiukweli nilimpenda sana maana hakuwa na maneno mengi,Alituambia "Twendeni Nyumbani",Alituuliza pale "Vp mmekula"?,Nilimwambia "Tushakula bro"
Nilimshukuru sana Mkami kwa wakati ule maana sikutegemea sana,Yule jamaa inaonekana alikuwa mtu wa watu maana hata wakati tukiwa njiani tulikuwa tukipiga stori na ilionekana na yeye kuna mambo mengi tu ya maisha alikuwa kapitia hivyo alikuwa akitutia moyo!
Tulifika hapo geto kwake na jamaa alituelekeza tukachote maji kwenye kisima kilichokuwa nje ya hiyo nyumba kwa ajili ya kuoga kuondoa uchovu!,kiukweli mimi nguo zangu zilishaanza kutoa hatufu kwa ajili ya jasho na dogo nae vile vile!
Jamaa wakati tukiwa njiani àlituambia anaitwa Mashauri na sisi pia tulimtajia majina yetu!
Usiku ule mimi nilimwambia Jamaa atusaidie sabauni kama anayo ili tuweze kufua nguo zetu,jamaa alituletea kipande cha Sabuni tukaanza kufua pale huku mastori yakiendelea kama kawaida!
Mashauri alituambia ya kwamba yule Dada Mkami alikuwa demu wake na wamefanikiwa kupata mtoto mmoja ambapo kwa wakati ule wa kuuza uji Mkami mtoto huwa anamwacha nyumbani na Bibi yake!,Basi tuliendelea sana kupiga stori na jamaa alikuwa mtu wa watu sana!
Katika maongezi nilimwambia Jamaa kwamba kesho sisi tunasafari ya kwenda Bunda na kiukweli sikutaka kabisa kumweleza chochote kuhusu kilichotupeleka kule!,Jamaa alituambia kama tunaenda Bunda Asubuhi twende nae mpaka kijiji kimoja kinaitwa Nyamuswa kwani yeye anafanya biashara ya mbuzi na kuzipeleka hapo baadae kuna magari yanakuja kufata kupeleka Mwanza na sehemu nyingine!,Mashauri alivyotuambia kwamba yeye ni kama dalali wa Mbuzi,hivyo huwa anaenda huko vijijini anawakusanya kisha anawapeleka hapo Nyamuswa huwa kuna eneo maalumu wanawekwa halafu yeye hupewa chake!
Hivyo akatuambia kwakuwa kesho kuna magari yangekuja kuchua mbuzi pale angetuombea tupate lift mpaka Bunda,Kiukweli nilimuona Mashauri ni muungwana sana!
Nilipomaliza kufua nilihakikisha zile nguo zangu nazikung'uta kisawasawa,Hii yote nilitaka kwa usiku ule ziwahi kukauka kwa upepo!
Baada ya shughuli na kufua na kuoga zilipokamilika tuliingia geto kwa Mashauri na kulikuaa kumenakshiwa vizuri kwa magazeti ukutani!,Japo ile nyumba ilikuwa niya nyasi lakini kijana mwenzetu alikuwa kajitahidi sana kupendezesha chumba chake!,kwakuwa alikuwa na kitanda kidogo nilimwambia yeye alale pale na dogo na mimi kuna jamvi lilikuwa pale nje aliniletea nkatandika chini akanipa na shuka Mrume ndago nkauchapa usingizi!
Usingizi japo ulikuwa wa mang'amu ng'amu lakini nilimshukuru sana Mungu maana kupata sehemu ya kulala kwa usiku ule ilikuwa ni ishu!
Usiku huo jamaa alifungulia redio yake mmoja hivi iliyokuwa ikitumia betri na akaweka stesheni fulani hivi tukaanza kusikiliza!,Nilipitiwa na usingizi na nimejikuta nashituka kushakucha!
Mashauri yeye aliwahi kuamka,Mimi na dogo tuliamka mida kama ya saa 1 asubuhi ndipo Mashauri alisema tujiandae twende kwao Mkami akatupikie uji ili tuelekee Nyamuswa!
Basi tulijiandaa pale japo nguo zangu hasa suruali ilikuwa haijakauka vizuri nilivaa hivyo hivyo,dogo nae mambo yalikuwa yale yale!
Tuliondoka na Mashauri mpaka kwao Mkami asubuhi hiyo na tulipofika tulimkuta Mkami na Mama yake na yule mtoto wa Mashauri,kilikuwa kibinti kama cha miaka 3 hivi!
Basi Mashauri akaanza kuongea na mkami pale kilugha baadae mkami aliondoka na jembe pale nyumbani,Baadae kidogo alikuja na mihogo mibichi!,Kumbe kwa wakati ule inaonekan jamaa alimwambia akachimbe mihogo aje atupikie ili tule tuondoke!
Hivyo ndivyo ilivyokuwa ndugu zangu!
Baada ya kuwa tumemaliza kupata uji na mihogo ya kuchemsha tuliagana pale na kuanza sasa kutembea kuelekea Nyamuswa!,wakati tunaenda nilimshukuru sana Mashauri!,Jamaa alionekana ni mtu wa watu kweli!,Hii roho sijui kama vijana wa leo wangekuwa nayo!
Tulitembea kwa muda kidogo na hatimaye tukafika hapo Nyamuswa!,tulifika mpaka mahala wanapowahifadhi wale mbuzi na jamaa akasema ngoja tusubilie gari la kubebea mbuzi maana halikuwa mbali sana na pale!
Gari lilipofika mbuzi walianza kupakiwa kwa kuhesabiwa na sisi ilibidi tuanze kumsaidia Mashauri kupakia wale mbuzi kwenye ile fuso!
Tulipomaliza ile kazi Mashauri aliongea na yule dereva pale kwamba sisi ni ndugu zake na akifika Bunda atuache!,Basi kabla ya kuingia kwenye lori nilimuomba Mashauri namba za simu na akanipa nkamwambia tutawasiliana!,Nyuma ya lile lori kulikuwa na jamaa wengine wawili ukiacha sisi,Jumla tulikuwa 4!,Kuna jamaa nilimuuliza kwa wakati ule walikuwa wakienda wapi?,Jamaa alisema wanaelekea Tabora ila humo katikati kabla ya kufika Bunda kuna vituo kama viwili watasimama kuchukua mbuzi!
Itaendelea.................