Naunga mkono hojaTunaishi kwenye combination ya Monarchy mated with Oligarchy in stealth mode ila nchi inaitwa ni ya kidemokrasia mbele ya macho ya dunia.
Kuna mizee yenyewe imejikasimisha madaraka na inataka wao na vizazi vyao waendelee kuhodhi madaraka while the rest of us just toiling hard to make ends meet.
Option pekee naona ni umwagaji damu tu. Without it hakuna mabadiliko yatatokea. Ni hadi makundi haya mawili ya clash. Maskini wachoke kuburuzwa waamue kustrike iwe balaa.
Umetumia njia ndefu Sana kufika kwenye hili hitimisho ambalo hasa ndiyo linatakiwa kuwa kiini cha mjadala huu.Uchumi wa nchi unapimwa kwa uzalishaji na ufanisi wa balance of trade.
Mbona nimeanza kulisema hilo awali kabisa kwa kutumia mfano hai kabisa wa China?Umetumia njia ndefu Sana kufika kwenye hili hitimisho ambalo hasa ndiyo linatakiwa kuwa kiini cha mjadala huu.
Jee udhaifu wa sarafu yetu unasababishwa na sababu Gani ya kiuchumi!??
Maana uimara ama udhaifu wa sarafu ya nchi yoyote ile duniani hautokei kusikojulikana, bali huwa na chanzo chake cha kiuchumi.
China inazalisha kwa wingi bidhaa mbali mbali tena kwa gharama ndogo kwa Teknolojia ya kisasa na bora kabisa.
Sisi tunazalisha ama tunauza nini kwenye soko la kimataifa. Urari wetu wa kibiashara (balance of payment/trade) kimataifa ukoje!?
Kwa mtazamo wangu badala ya kujikita kujadili thamani ya sarafu yetu kimataifa, basi tujadili kwanza thamani ya uchumi wetu kimataifa.
Hizi hadithi za kwenye vijiwe vya kahawa usilete kwenye mjadala wa mada makini kama hii.Mwalimu hakuwahi kuza uchumi wowote zaidi ya kutumia hazina aliyoachiwa na wakoloni akaitumia vibaya kutaka kumrejesha swahiba wake madarakani dhidi ya idi amini zingine akazitapanya kwenye ukombozi wa nchi za Africa
Naam, umeniita?Labda watakuja, ngoja nikwaalike FaizaFoxy , Lucas Mwashambwa , chiembe ,Huihui2 , Erythrocyte Pascal Mayalla nk nk, ingawa tutegemee na matusi pia!!
Hakuna aliyekuita, Kuna mtu alikutaja kimakosa kuwa nawe ni chawa!!Naam, umeniita?
Tatizo nini?
Kabisaukiifatilia sana hii nchi uatagombana hadi na mkeo
acha ninywe bia mi
Kwanza ujinga sanaUnawezaje kukopa ukajengee vyoo vya mashuleni?
Shule ni huduma Si biashara,
Ulitakiwa tukope kuwezesha mitaji kwenye MABENKI yashusge interest rates za mikopo Ili watu wapate mitaji Uchumi ukue Kisha Serikali ichukue pesa kiduchu Toka faida kujenga vyoo,
Sasa kukopa ukaenda kujenga, huo Si Uchumi.
Weka account ya dollar upige hela.Salaam shalom!!
Tulipopata Uhuru wa Nchi yetu, hatukuwa na wawekezaji wengi wa kuwekeza kwenye migodi, Serikali ilihodhi vitega Uchumi vyote na kusimamia, Hawa wawekezaji wa sasa, nionavyo Si HAKI kuwaita wawekezaji Bali waporaji, na uporaji huo unashirikisha viongozi wetu wa ndani. Tulipopata uhuru, Dola Moja ya kimarekani, ilibadilishwa Kwa Tshs 7 tu!!
Nisikuchoshe, hii hapa ni historia ya Exchange rate tangu Uhuru Hadi hii Leo, chama Cha MAPINDUZI kikiwa madarakani.
1961.
1usd=7 Tshs
1971
1usd= 7.14 Tshs
1981
1usd=8.2 Tshs
1991
1usd=219 Tshs
2001
1 Usd=876.4 Tshs
2005
1 Usd=1,128.9 Tshs
2010
1usd =1,434.7 Tshs
2012
1usd= 1,600Tshs
2015
1usd=2,037.1 Tshs
2020
1usd=2,330.5
2024
1usd= 2,615 Tshs.
Source: Google, average Exchange Rate, University of Pennsylvania.
Awamu ya kwanza ya utawala wa mwalimu Nyerere Kwa miaka yote 24 aliyokaa madarakani, Dalar halikuwahi kubadilishwa Kwa zaidi ya Tshs 10 pekee!! Na wakati huo, Aliendesha Uchumi Kwa KILIMO PEKEE!! Uchumi wetu ulitegemea zaidi KILIMO Cha biashara na chakula, Tuliuza millions ya tons za mazao ya KILIMO na biashara.
Mambo yameanza kuharibika pale tulipoamua kuingiza sera za ubepari Uchwara, Tukaanza kuruhusu waporaji kushika uchumi wetu Kwa mlango wa Uwekezaji. Alipoingia tu Mzee Ruksa, ikapaa Kutoka Sh 10- tsh 200 kubadili Kwa 1 Usd. Kumbe tulitakiwa tuunde na kuwajenga wazawa ndio wapewe mashirika ya umma kujenga Nchi na kubakiza pesa nchini.
Tungetegemea, Uchimbaji wa Madini usaidie kuimarisha pesa yetu na Uchumi, lakini Cha kushangaza, Dhahabu inachimbwa, lakini Serikali inakosa pesa ya kufadhili budget na kulazimisha kukopa nje, sasa hiyo migodi Si ingefungwa tujue Moja? Tusubiri wazaliwe Watanzania ambao watakuwa na uwezo wa kuchimba Dhahabu yetu wenyewe, ituzwe benki kuu baada ya kununuliwa na Serikali Toka Kwa wachimbaji hao. Pesa yetu irudi kuwa yenye nguvu tena kama zamani.
Nchi yetu tunawezaje kusema tuna wawekezaji ambao hawaleti mchango wowote kwenye kuimarisha pesa yetu na Uchumi wetu?
Iweje tuwape wageni Bandari zetu kwamba wakusanye mapato Kwa weledi mkubwa Kisha tukose pesa ya kufinance budget yetu Kwa mwaka Hadi tulazimike kukopa tena?
SOLUTION.
1. Turudi na kukaa kama nchi na kutafakari tena kuhusu sera zetu za kiuchumi, maana uwekezaji haujaleta TIJA yoyote muhimu zaidi ya kutufanya kuwa maskini zaidi, tunahitaji Sera ambazo ni Mixture ya Ujamaa na Ubepari. Na ubepari huo uwe wa kudeal na Wazalendo wa ndani ya nchi ,wafadhiliwe mikopo Ili waendeshe Uchumi wa Nchi yetu.
2. MIKOPO ya nchi yetu isimamishwe. Iundwe Taasisi huru kikatiba, Taasisi hiyo impore Rais mamlaka ya kujihusisha na mikopo ya nchi, Taasisi hiyo ichakate taarifa nyeti na kuona namna Bora ya kujitegemea wenyewe tukishirikisha matajiri wazawa wa nchini, Dhahabu yetu na Raslimali zetu zimilikiwe na wazawa, hao ndio wafadhili budget ya Uchumi wetu.
3. Tukipumzishe chama Cha MAPINDUZI kuongoza nchi, nasisitiza point hii no 3!!
Vyama vya upinzani pia viangaliwe UPYA, maana Sera na maono Yao kiuchumi ni Yale Yale ya kuamini kuwa tunaweza kuleta wawekezaji Toka nje Kisha tukapata faida za kiuchumi kupitia uwekezaji Uchwara tukiweka rehani raslimali zetu Kwa wageni, tunahitaji vyama vya upinzani vyenye sura ya kizalendo na kuwa na Political na Economical INDEPENDENCE!! Vyama vya siasa nchini visizidi VITATU PEKEE!!!
4. Tupate Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote. Nchi yetu tusiwape wageni kiutawala kupitia sera mbovu na RUSHWA Kwa viongozi wetu ilhali Uchumi na Raslimali za nchi zinazidi kuondoka mikononi mwetu.
5. Tuongeze hasira juu ya Wala RUSHWA!! Rais asione haya kusaini death sentence, watu Wala RUSHWA wa level zote na uhujumu Uchumi wanyongwe, wasiogope, ukinyonga Wala RUSHWA watu hawataisha nchini, Bali wataacha vitendo vya RUSHWA.!!
Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿
Karibuni🙏
Badala ukope Kisha Benki zipewe pesa hizo na kupunguza interest rates Ili sekta ya Uchumi ikue,Kwanza ujinga sana
Unakopa kujenga vyoo kweli ,halafu unakusanya tozo kununua VX ,si upumbavu huu jamani
Nchi hii inakera sana
Hutopata muwekezaji huyoUpo sahihi. Tena afadhali wawekezaji wa migodini ambao bidhaa wanazizalisha zinaingiza dola. Fikiria tunaleta muwekezaji anazalisha bidhaa anazouza humu humu ndani au anachezesha kamari. Huyu anatuuzia bidhaa kwa Tsh halafu anapopeleka faida kwao anazibadili kuwa dola na kuondoka nazo. Matokeo yake mahitaji ya dola na thamani yake inazidi kupanda na Tsh inazidi kushuka.
Ilitakiwa muwekezaji asiruhusiwe kuondoka na dola zaidi ya anazozalisha kwenye business yake au alizokuja nazo kama mtaji.
Wahusika wapo bize na campaigh. One thing nimejifunza kuna ka utamaduni, kiongozi (si wote) akijua kazingua anakaa kimya, wenyewe wanasema (upepo upite), aka mbongo asahau.Rate ya Bank inasoma hivyo ila mtaani watu wanauziana 2882 ilikua juzi hii ukitaka kwa hiyo ya Bank hauwezi kupata kitu naona inakimbilia Tsh 3000 kwa 1 usd...
Ukiwa na akili za aina hiyo unaweza hata kufanya biashara haramu ya drugs,au hata kuuza viungo vya binadamu.Weka account ya dollar upige hela.
Viongozi wenyewe hawana uchungu na nchi halafu wewe ndiyo una uchungu na nchi.
Piga hela angalia maisha yako na kizazi chako
Bado hata huko kwenye exportation bado tabu tupuZaidi ya 70% ya export yetu inatokana na Madini,ambayo yanachukuliwa hapa kwenda kuuzwa huko Ulaya-kwa maana hii hizi export ni kama namba tu ambazo hazina impact yyt kiuchumi ndani ya nchi.
Kama wanunuzi wangekuwa wanakuja kununua haya madini hapa Nchini basi wangenunua kwa fedha yetu na fedha yetu ingepanda thamani.Vilvile Kama hii migodi ingekuwa inamilikiwa na Wawezekazi wa ndani hata kama wangekwenda kuuza nje basi wangerudi ndani wakileta hizo USD zinazotokana na faida na mwishowe wangepandisha uchumi na shilingi ya Nchi.
The so called uwekezaji kwenye Nchi aina ya Tanzania yenye viongozi wala rushwa na wananchi wajinga ni utahira.
Kama anataka kuondoka na dola basi afanye biashara ya kuingiza dola. Yaani export business. Unaalika mtu kuja kuendesha mwendokasi. Anaingiza Tsh halafu wakati wa kuondosha faida anabadilisha kuwa dola!! Mbona tunakuwa tunafanya biashara kichaa.Hutopata muwekezaji huyo
Sasa hapo atakua amefanya nini
Yaani aje na Dola 1M mathalani ,apambane apate faida halafu siku ya kuondoka aondoke na Dola 1M ile ile , we kuweza mkuu?
Maparachichi njia rahisi ni kuyatoa kupitia Mombasa aisee yanatoka na box za Nairobi wakati yanatoka hapo Njombe na Moshi Nchi ngumu sana hii vitu vya kuingiza fedha za kigeni kupata vibali kama sijui unatoa kitu gani wakati SA ukitaka kufanya Export yeyote kibali ni siku moja kinafanyiwa kazi na unawaambia utatoa kwa mpaka upi ili ikiwezekana upewe na agent kabisa na vitu vyote ni bure kasoro gharama ya Agent huko Mpakani nilienda na Jamaa mmoja kutoka Iringa alidhani ile huduma tuliyopewa tunalipia kumbe ni free of charge harafu jamaa wapo serious kweli..Bado hata huko kwenye exportation bado tabu tupu
Ukiwa na maparachichi Yako unataka uyauze uingereza kupata export permit ni mzunguko
Ukiwa na mahindi Yako unataka uyapeleke Kenya au Ethiopia shughuli yake si mchezo
Ukiwa na ngozi za ng'ombe unataka uwapelekee Gucci au LV kupata kibali sahau
Kwa hiyo hata export inauliwa na hao hao wanaotorosha dhahabu sababu ya ukiritimba na roho mbaya, matokeo yake tunabakia hoi kama nchi
Ndio hapo ,Kwa hakika sisi watanzania tuna matatizo sanaMaparachichi njia rahisi ni kuyatoa kupitia Mombasa aisee yanatoka na box za Nairobi wakati yanatoka hapo Njombe na Moshi Nchi ngumu sana hii vitu vya kuingiza fedha za kigeni kupata vibali kama sijui unatoa kitu gani wakati SA ukitaka kufanya Export yeyote kibali ni siku moja kinafanyiwa kazi na unawaambia utatoa kwa mpaka upi ili ikiwezekana upewe na agent kabisa na vitu vyote ni bure kasoro gharama ya Agent huko Mpakani nilienda na Jamaa mmoja kutoka Iringa alidhani ile huduma tuliyopewa tunalipia kumbe ni free of charge harafu jamaa wapo serious kweli..