Kweli au si kweli ni sijui maana mimi si mtaalam wa mambo haya. Hata hivyo, sidhani kama ni sahihi kukana moja kwa moja uwezekano wa mimba kuwa ya hiyo rafiki yako. Ukweli ni kwamba kila mtu anayo namna yake ya mwili kutoa mrejesho wa mambo mbalimbali yanayoendelea ndani yake.
Kwa kuwa tunajaribu kuelimishana na kubadilishana uzoefu, nitatoa mfano unaonihusu mimi mwenyewe. Nina make na watoto watatu. Siku mke wangu anaposhika ujauzito kwa mara ya kwanza alilala usingizi mzito mno tofauti na siku nyingine zote. Na kesho yake aliamka na mafua makali sana. Hali hii ilijirudia siku aliposhika ujauzito wa pili na watatu (nilikuwa nafuatilia kwa ukaribu sana).
Kutokana na hali hii kujirudia consistently, naweza ku-conclude kuwa haikuwa coincidental. Hii ilikuwa namna ya mwili kutoa mrejesho, na mrejesho huo unaweza kutofautiana kutoka kwa mwanamke mmoja hadi kwa mwingine. Zaidi nawaachia wataalam.