Mimi kada wa CCM lakini mauaji ya kada wa CHADEMA Ali Kibao limetukera

Mimi kada wa CCM lakini mauaji ya kada wa CHADEMA Ali Kibao limetukera

Kondoo alikuwa anapita akamuona simba akilia akiwa amenasa kwenye boksi la chuma(grili), simba akamsihi sana kondoo amuokoe na kumuahidi kuwa hatamuua wala kumla, lakini kondoo akakataa.... Baada ya simba kubembeleza sana na kwa upumbavu wa kondoo, akafungua lile boksi la chuma.

Sasa simba alikuwa na njaa kali mno baada ya kukaa kifungoni kwa siku kadhaa bila kula chakula... Mara moja alimrukia kondoo na kukaribia kumuua ili amle, lakini kondoo alimkumbusha kiapo chake.

Waliendelea kubishana hadi wanyama wengine waliokuwa wanapita wakauliza kulikoni? Basi simba na kondoo wote wakaelezea jinsi ilivyokuwa, lakini kwa hofu ya simba na kutaka kupata huruma machoni pa simba, wanyama wote wakamsapoti simba isipokuwa kobe ambaye alidai kuwa hakuelewa mazingira na stori yenyewe.

Sasa kobe akamuomba simba aoneshe mahali alipokuwa kabla ya kondoo kumuokoa, simba akamuonesha kobe kwa mguu wake wa mbele, pale... Kobe akamuuliza tena, "ulikuwa ndani ama nje kabla ya kondoo kuja??"...Simba akamjibu, "nilikuwa ndani".

Kobe akamuuliza tena simba, "sawa, embu ingia tena ili tuone jinsi ilivyokuwia vigumu kukaa ndani ya grili kwani sielewi stori hii yote vizuri"... Simba akaingia, na mara moja(chapu!), kobe akafunga lile boksi la chuma (grili)... Na simba sasa alikuwa amenasa tena!!

Kwa mshangao mkubwa, wale wanyama wengine wakamuuliza kobe "Kwanini?" na kobe akawajibu..."Kama tukimruhusu simba amle kondoo leo, bado atasikia njaa tena kesho na hatujui kati yetu ni nani atakayeliwa kesho..!!"

#FUNDISHO

Usiunge mkono uovu leo kwa vile haukuathiri moja kwa moja, pengine kesho inaweza kuwa zamu yako.!!

Nafikri tunahitaji kobe wengi zaidi katika jamii yetu. Umejifunza nini?
Upo sahihi sana.

Hawa watu wanateka na kuua wakosoaji wa Serikali na watawala. Je, ndani ya CCM hakuna wakosoaji? Kwa hali ilivyo sasa, huenda zamu ya Mpina ipo karibu.

Bila kujali upo chama gani, hawa mashetani wanaweza kukufikia kwa kupanga au kwa kukosea. Kama ikitokea, hata humu ndani ya CCM, akatokea hayawani mmoja akaenda akawajaza maneno kuwa wewe unamkosoa Rais au Serikali yake, ujue watakufikia.

Kwa wenye akili, wajiulize, Zacharia alikuwa CHADEMA?
 
Huyu muuaji sio mtoto mdogo, atakua Ni MTU mwenye 50+ years.
Ina maana hapa duniani Hana zaidi ya miaka 25 ya kuishi. Hivi kweli unamwaga damu ya mtu ili ui njoi kwa miaka 25 tu.?
Nadhani huyu muuaji atakua na familia, nyumba na account nzuri benki, hivi kuua kutamuongezea furaha ya kuishi siku zake chache zilizobaki?

KARMA IS A BITCH.
 
Hivi 4R maana yake nini kwa sasa sijui maana yake nini.

Mauaji ya kada wa CHADEMA Ali Kibao, mauaji ambayo yanaashiria kufanyika na state agents si suala la kulifumbia macho.
Kwa kawaida state agents wanaagizwa operation za kutekeleza.

Kama tumeanza kuingia katika mauaji ya kisiasa hata mimi mwa CCM siliungi mkono hilo.
Na kwa vyovyote mauaji haya hayaashirii upepo mzuri kwa uchaguzi mwakani na hali ya utulivu kuweza kuharibika.

Kuna wanaotaka kuleta mchafuko wa kisiasa maana siamini kwamba operations kama hizi mama Samia anaweza kuziagiza zitekelezwe.
Wambieni wanachama wenzako mkitumaliza ndio hamtakufa?
 
Huyu muuaji sio mtoto mdogo, atakua Ni MTU mwenye 50+ years.
Ina maana hapa duniani Hana zaidi ya miaka 25 ya kuishi. Hivi kweli unamwaga damu ya mtu ili ui njoi kwa miaka 25 tu.?
Nadhani huyu muuaji atakua na familia, nyumba na account nzuri benki, hivi kuua kutamuongezea furaha ya kuishi siku zake chache zilizobaki?

KARMA IS A BITCH.
Mkuu wanakwambia Life is Short live it to the fullest.......Hapo wanaongezwa vyeo kwenye category yao. Achana na Pesa mamilioni ya kula bata baada ya kazi nzuri
 
Je marehemu alikuwa na bifu na serikali
 
Hivi 4R maana yake nini kwa sasa sijui maana yake nini.

Mauaji ya kada wa CHADEMA Ali Kibao, mauaji ambayo yanaashiria kufanyika na state agents si suala la kulifumbia macho.
Kwa kawaida state agents wanaagizwa operation za kutekeleza.

Kama tumeanza kuingia katika mauaji ya kisiasa hata mimi mwa CCM siliungi mkono hilo.
Na kwa vyovyote mauaji haya hayaashirii upepo mzuri kwa uchaguzi mwakani na hali ya utulivu kuweza kuharibika.

Kuna wanaotaka kuleta mchafuko wa kisiasa maana siamini kwamba operations kama hizi mama Samia anaweza kuziagiza zitekelezwe.
Muuaji atafahamika tu.
 
Ile sheria iliyopitishwa Bungeni kuhusu Usalama wa Taifa ilikua ni mwiba sana
 
Hivi 4R maana yake nini kwa sasa sijui maana yake nini.

Mauaji ya kada wa CHADEMA Ali Kibao, mauaji ambayo yanaashiria kufanyika na state agents si suala la kulifumbia macho.
Kwa kawaida state agents wanaagizwa operation za kutekeleza.

Kama tumeanza kuingia katika mauaji ya kisiasa hata mimi mwa CCM siliungi mkono hilo.
Na kwa vyovyote mauaji haya hayaashirii upepo mzuri kwa uchaguzi mwakani na hali ya utulivu kuweza kuharibika.

Kuna wanaotaka kuleta mchafuko wa kisiasa maana siamini kwamba operations kama hizi mama Samia anaweza kuziagiza zitekelezwe.
Unakumbuka ile kauli ya mwenzeni '...tukiwapoteza msiwatafute?'
 
Hakika inasikitisha na kuumiza sana, mhimu ni wahusika kukamatwa na kufikishwa mbele ya Sheria na pengine kunyongwa ikibainika na kuthibitika KWa waliofanya mauaji ya raia na mtanzania mwenzetu.siasa za majitaka kamwe zisipewe nafasi katika nchi yetu.
 
Wajinga wanadhani wanamsaidia Samia kumbe ndo wanamharibia kabisa!
Mimi ni mwana CCM ujinga huu ukiendelea wenye akili ndani ya CCM itabidi wampinge Samia kwa nguvu zote!
Hata tamko alilotoa linaonyesha hayuko serious ! Na ni kama Kuna kitu anakijua upfront!
Uraisi au siasa haziwezi kufanya watu wauwawe kinyama hivi!
Huyo Mzee Kibao hakustahili kuuwawa kinyama hivyo ndani ya Nchi yake kwasababu za kisiasa!
Vyombo vya usalama inaonekana kumejaa watu wajinga sana!
Mara wanauwa watu , mara wana FIRA watu ,ni ujinga mtupu!!!!
Wanauwa na kufira watu halafu hawafanywi chochote
Wanapongezwa
 
Wengi walio CCM ni kwasababu ya njaa ila hawaipendi toka moyoni
 
Ninaweza kuandika kwamba Yeye kama Mwenyekiti wa Chama kinachounda serikali inayosimamia vyombo vya ulinzi na usalama wa nchi yetu ana taarifa za kutosha juu ya hiki kinachoendelea nchini kwa sasa kwa muktadha ufuatao.
Ni sahihi kwamba kazi ya idara ya usalama wa taifa ni kukusanya taarifa, kuzichanbua na kuishauri serikali juu ya hatua za kuchukua. Kwa maana hiyo ili taarifa zipatikane watu wa idara ya usalama wa taifa wamesambazwa na wanafanya kazi katika idara zote za serikali kuanzia sehemu za kisekta ikiwemo siasa na kuanzia ngazi ya juu kabisa mpaka ngazi ya mtaa tunapoishi.
Kila siku Rais huwa anapokea briefing au muhtasari wa mambo yote yanayoendelea nchini kisiasa,kiuchumi na kijamii pamoja na yale yanayoendelea nje ya nchi au katika mataifa mbali mbali na hatua zinazochukuliwa ndani na nje ya nchi. Na katika briefing hizo idara ya usala wa taifa ni mojawapo ya idara zinazotoa taarifa kwake. Hii ni kutokana na ukweli mabadiliko ya sheria ya idara ya usalama wa Taifa yaliyofanyika yaliifanya idara hiyo iwe chini ya Rais.
Rais ni Amiri Jeshi Mkuu wa vyombo vya ulinzi na usalama ikiwemo idara ya usalama wa Taifa. Kwa msingi huo IGP humpatia hali halisi ya usalama wa ndani na mwenendo wa shughuli mbali mbali ikiwemo shughuli za vyama vya siasa na hatua zinazochukuliwa.

Rais pamoja na nafasi hizo alizonazo kikatiba pia ni mwenyekiti wa Chama Kinachotawala nchi. Katika chama kuna idara mbali mbali zikiwemo za usalama wa chama propaganda na zile za kupanga namna gani ya kushughulika na wapinzani wa kisiasa. Hivyo katibu mkuu wa chama huripoti kwa Mwenyekiti juu ya mambo hayo na hatua zinazochukuliwa kila wakati. Kwa msingi ni vigumu kutofautisha chama na serikali au serikali na chama.

Hivi karibuni viongozi na wajumbe wa kamati kuu ya chama akiwemo Speaker alikua na kauli mbiu ya "pita nao wote wanaokosoa utendaji kazi wa serikali' Huyu ni kiongozi wa juu wa serikali ambaye anasimamia chombo kinachotunga sheria ikiwemo sheria ambayo ambayo imetungwa ya kuwapa kinga wafanyakazi wa idara ya usalama wa taifa kutoshtakiwa kwa makosa ya jinai ikiwemo mauaji wakati wanatimiza majukumu yao pamoja na kuwa na mamlaka ya ukamataji kama askari polisi. Kwa ufupi imekua ni jeshi kama majeshi mengine. Mwenye kuipeleka sheria hii bungeni ni Rais kupitia waziri mwenye dhamana husika.

Ni hivi majuzi tu Rais alitamka wazi wazi kwamba wanaodhaniwa kuwa wametekwa ni drama na Tanzani ni mahala salama ambapo vitendo vya utekaji na mauaji haviwezi kufanyika. Lakini uwkeli ni kwamba alisikia Yowe na sauti hiyio kwamba watu wanaotekwa wapo na hasa wale ambao wapo kinyume na sera za chama chake pamoja na ugumu wa maisha ambao haushabihiani na utajiri wa nchi anayoiongoza.

Ni hivi karibuni tuu viongozi wawili waandamizi katika chama na serikali yake wametoa matamshi tata ambayo yananasibishwa na mauaji na utekaji na hakuwahi kutoka hadharani kukekemea na wala vyombo vya dola anavovisimamia havikuwahi kuchukua hatua yoyote juu ya watu hao. Hii ni picha halisi kwamba anahisika na anajua yale ambayo yanatokea ila anaamua kukaa kimya kwa sababu ya maslahi ya chama chake. Mathalani kule kanda ya Ziwa kiongozi wa chama alisikika wazi wazi akiwataka jeshi la polisi kutowatafuta watu ambao kwake aliwaita wanaomtusi Rais pindi watakapowapoteza. "kukosolewa kwao hutafsiri kama matusi" ingawa hakuna hata mtu mmoja alishwahi kuburuzwa mahakamani na akathibtika bila mashaka yoyote kuwa amemtusi Rais au mtawala.
Kiongozi mwingine ambaye alifutwa kazi au alibadilishiwa majukumu ni DC wa huko kanda ya Kaskazini aliyeeleza wazi wazi mambo yanayofanyika maaporini ili kuhakikisha ushindi unapatikana.

Hayo ni machache yanayoonesha kwamba Rais anajua kinachoendelea juu ya uhalifu huu dhidi ya binadamu. Hii ni dhahiri kwamba majaji ambao ni wateule wake wametupilia mbali kesi inayotaka ufafanuzi juu ya maswala haya ya utekaji na wakati huo huo Speaker anatupilia mbali mjadala unawowasilishwa na mbunge juu ya vilio vya utekaji.

Wakati hayo yakiendelea na vijana kuendelea kutekwa mitaani Jeshi la polisi linakataa uhusika wake lakini halitoi taarifa ni watu gani wanahusika na matukio hayo na kwanini yawalenge watu fulani pekee na sio ordinary citizens. Maswali hayo yakiwa hayajapata majibu tuanapata taarifa ya Kutekwa mzee kada wa chadema katika mazingira ambayo ni sahihi yanahusishwa na vyombo vya ulinzi na usalama. Uwepo wa askari wa usalama barabarani, gari za polisi kuhusika, marehemu kufungwa pingu, wahusika kuwa na silaha ni maswali ambayo hayana majibu.

Jeshi la polisi halitoi state warning or alert isipokua linatoa taarifa ya kufanya uchunguzi juu ya tukio hilo ma siku chache mtu anakutwa marehemu tayari, katika maeneo ambayo Roma Mkatoliki alitelekezwa na akakimbia nchi mpaka leo. Jeshi hilo hilo la polisi limejitokeza na taarifa nyepesi huku likitumia nguvu kubwa pale Mwananyamala hospitali kutotaka postmortem huru ifanyike kabla ya mwili kuchukuliwa na kwenda kuhifadhiwa.
ikiwa Amiri Jeshi Mkuu hajui na vyombo vyake havijui basi Taifa liko hatarini.
Hatuna usalama wa Taifa bali kuna usalama wa serikali, polisi pia wako kwa ajili ya usalama wa serikali sio raia - kama ni raia kweli leo pangekua na hekaheka. Hatuna bunge kama chombo kinachoithibiti serikali bali bunge la sasa ni mkono au mwendelezo wa serikali - suala la speaker husika..kipindi cha kinBa Samweli Sitta, Mama Makinda kidogo bunge lilikua balanced - bunge la sasa ni kama kikao cha secretariat ya CCM.
Baba wa Taifa alitusaidia katika kuvunja ukabila na kuleta usawa lkn kwenye suala la Usalama alivuruga sana - system alizoasisi ndo hizi zinazotusumbua mpaka sasa - vyombo vya ulinzi viko katika kulinda sana serikali na viongozi wake kuliko raia...
Njaa, uoga, umaskini nako ni changamoto - huwezi ukasikia kiongozi yoyote mkuu wa serikali kaongelea hili suala mfano : waziri mkuu, makamu wa Rais, IGP, Kamanda wa polisi - wote hawa wabahibernate kabisaaaa..ndo muone jinsi bado tuko nyuma sana...
 
Hivi 4R maana yake nini kwa sasa sijui maana yake nini.

Mauaji ya kada wa CHADEMA Ali Kibao, mauaji ambayo yanaashiria kufanyika na state agents si suala la kulifumbia macho.
Kwa kawaida state agents wanaagizwa operation za kutekeleza.

Kama tumeanza kuingia katika mauaji ya kisiasa hata mimi mwa CCM siliungi mkono hilo.
Na kwa vyovyote mauaji haya hayaashirii upepo mzuri kwa uchaguzi mwakani na hali ya utulivu kuweza kuharibika.

Kuna wanaotaka kuleta mchafuko wa kisiasa maana siamini kwamba operations kama hizi mama Samia anaweza kuziagiza zitekelezwe.

UPDATE
Tayari nchi imechafuliwa kimataifa.View attachment 3090846View attachment 3090848View attachment 3090848

YAANI WAFANYE HAYO RAIS ASIJUE? WEWE UNAFANYA MASIKHARA SANA. RAIS SI ALISHASEMA HIZO NI DRAMA SI MAMBO YA KWELI. AKINA SOKA WANAPIGIWA KELELE WAACHILIWE RAIS HAJUI? YEYE ANAISHI WAPI?
 
Hivi 4R maana yake nini kwa sasa sijui maana yake nini.

Mauaji ya kada wa CHADEMA Ali Kibao, mauaji ambayo yanaashiria kufanyika na state agents si suala la kulifumbia macho.
Kwa kawaida state agents wanaagizwa operation za kutekeleza.

Kama tumeanza kuingia katika mauaji ya kisiasa hata mimi mwa CCM siliungi mkono hilo.
Na kwa vyovyote mauaji haya hayaashirii upepo mzuri kwa uchaguzi mwakani na hali ya utulivu kuweza kuharibika.

Kuna wanaotaka kuleta mchafuko wa kisiasa maana siamini kwamba operations kama hizi mama Samia anaweza kuziagiza zitekelezwe.

UPDATE
Tayari nchi imechafuliwa kimataifa.View attachment 3090846View attachment 3090848View attachment 3090848
Mwambie aache kutoa amri kuwateka watu.
 
Back
Top Bottom