Mimi mkataa ndoa naangamia rohoni: Nishaurini ili nipone

Mimi mkataa ndoa naangamia rohoni: Nishaurini ili nipone

Biashara inaweza kukupa moyo miaka mitano ya mwanzo lakini baada ya hapo ikakupiga mbaya.

Nakuunga mkono kuhusu suala lako la kuacha kazi lakini sio leo, sidhan kama biashara yako imesimama kiasi kwamba ikitokea umeumwa miezi 6 biashara haiyumbi. Biashara moja sio ya kuacha kazi. Sidhan kama majukumu yako mazito kiasi cha kushindwa kufanya kazi. Kuna watu wana majukumu mazito kushinda wewe, mabalozi nje ya nchi, makatibu wakuu, wakurugenzi, wana biashara zao na kazi hawajaacha na hawana mpango wa kuacha, wewe na fremu moja tena ya kupanga unawaza kuacha kazi, kazi yako inaweza kukusaidia upenye kwa urahisi katika misukosuko ya kibiashara, najua bado hujakutana na mikikimikiki ya kibiashara.

Kuna jamaa alichukua mkopo benk akaomba na likizo ya mwezi, kaingia mtaani kusanya mazao ingia nayo kongo hapo, mzigo wa 10m karudi na zaidi ya m100, jamaa kapagawa kaona biashara ndio hii, alivyorudi kuenda kwa mwajiri wake na barua ya kuacha kazi mkononi, kaenda kukopa hela nyingine tena kwa watu ili aondoke na mzigo mkubwa zaidi na hela aliyopata huko mwanzo kaitia yote kwenye mzigo,

Wateja walionunua mzigo mwanzo walimwambia aje na mzigo kadiri ya uwezo wake kwani makuta/faranga/dorari zipo za kutosha, kumbe bwana wale walikuwa ni madalali wa waasi, na mwanzoni walimpa hela nyingi ili kumtia jamaa tamaa, ili alete mzigo mkubwa wayeyuke nao kimasta.

Jamaa kaingia kichwakichwa na mzigo kongo, fika eneo la tukio wazee wa kazi wanapakua mzigo wake chini ya ulinzi mkali kama raisi wa marekani alivotembelea yukreni, kisha walee wakasepa bila kuacha hata thumni. Kazi ikawa juu ya kazi, wenye malori hajawalipa, mzigo umetekwa, makoli hayana mafuta, hela za watu kakopa, benki ana deni, kazi ameshaicha, alichakaa ndani ya masaa machache.

Kufipisha stori alifanikiwa kurudi, lakini brek ya kwanza ikawa kwa GEORGE HURUMA MKUCHIKA, kipindi hicho ni waziri wa utumishi.
 
Usiache kazi mkuu unaweza kuomba likizo bila malipo ata miaka mitatu ukaenda kwenye biashara zako kwa huo mda then ukiwa huko naamini akili itakukaa vizuri tu
 
Kifupi huijui career path yako btn formal job and self employement (business) bado unajitafuta. Na hii ni sababu tosha ya wewe kutokuwa na maamuzi ya kuoa. Bado hujui unawezaje kuwa mume na baba wa familia. Hujui ipi ni kazi sahihi itakayokuongoza kuendesha maisha yako, unaichukia kazi kisa boss kakuudhi? Ukiudhiwa tena kwenye biashara unafanyaje? Vyote vinaenda sambamba.
Ushauri
1. Onana mwana saikolojia akusaidie ku reset your mind.
Humu wamo lakini hutakuwa na stage sessions. Maana ushauri unahatua.

2. Tafuta business consultant ongea nao kuhusu biashara yako wakupe mwanga ufanye maamuzi.
3. Achana na ujinga wa kufuata mkumbo wa mitandao ya kijamii kuhusu champain chafu za kuzuia muungano wa familia (Ndoa).
Hii champain ya kataa ndoa inaenda sambamba na rainbow rights ni sehemu ya kuharibu akili za vijana wetu ili nchi za daraja la 3 tusinyanyuke kamwe. Break the chain anza kufanyia kazi utu wako.
 
GREETINGS.
Haloo wananchi wote wa JF, hamjambo?

Baada ya salamu twende kwenye mada.

INTRODUCTION:
Mimi ni mtumishi wa umma niliye ajiriwa 2012 na fani x (diploma) kwa level za kata (Afisa wa katani @ SIO MTENDAJI KATA).

2013 nikaenda chuo na kurudi 2018 na masters (niliunga) ya fani y.

Nikiwa na furaha na niite bahati, kurudi tu kazini nikapewa ofisi ya fani y, yaani nilimaliza chuo na kurudi kazini November 2018 na January 2019 nikahamishiwa halmashauri.

Niite bahati kwasababu, imekua ngumu kwa watumishi wengi kutoka Shule tu na ofisi zao za Utumishi wakawabadilishia Kazi zao (rectegorization au kuwahamishia kwenye vitengo walivyosomea).

Nilifanya Kazi kwa furaha na juhudi sana na 2019 nikapokea barua ya kubadilishiwa muundo (recategorization).

Niliona zile ndoto zangu za kuwa mkubwa kama zinaanza kutimia hivi na nilifanya Kazi kwa juhudi sana.

Fani y ndio niliyokuwa naipenda.

Fani x nilisomea tu kwa vile nilikuwa yatima na nilikosaga ada ya kusomea fani y miaka hiyo.

Ila hiyo fani x ndio iliniingiza serikalini.

SCENARIO:
2020 likatokea jambo kazini, mara TAKUKURU hao, mara CAG huyo, mara kamati ya kutuchunguza hiyo, mara usalama wa taifa huo.

Kifupi vitu vilikuwa vingi, ila iliamriwa tusimamishwe Kazi.

Tukiwa tumesimamishwa Kazi niliamua kufungua biashara.

Baada tu ya kusimamishwa Kazi nilitumia wiki 2 kutafuta frame na kuanza biashara.

Baada ya miezi 7 nikarudishwa kazini na mambo yakaendelea.

Ila biashara yangu ilikuwa ya moto sanaa (inauza sanaa).

PROBLEM
Baada ya kurudi kazini Kuna mambo nikaona yamebadilika.

1. Upendo na ile Kazi ukapoteaaa kabisaa

2. Nilikuwa mtoro balaa mpaka Mkurugenzi aliandika barua kwenda Utumishi ya Mimi kuvuliwa madaraka na kupewa mwengine.

Yaani aliyekuwa kijana wangu wa chini sasa hivi ni boss wangu.

3. Kuona hii ajira siipendi Tena, nikaona nitafute uhamisho, changamoto sasa, Mkurugenzi kagoma kabisaa kusaini barua zangu za kuniruhusu nikatafute post kwengine.

Anasemaga "bado nakuhitaji sanaa na siwezi kukuruhusu uondoke"

4. Nakiri; kunivua madaraka hata sijamlaumu, kiukweli kabisa nimekuwa mtoro balaa, siipendi Kazi Tena (kwasasa napenda sanaa biashara yangu na wanangu).

5. Yaani kazini naweza pitisha wiki sijasaini daftari la mahudhurio maana naingia saa 3 au 4 asubuhi na "ole wako uniulize lolote juu ya hilo..!!""

6. Yaani kwasasa siipendi Tena hii halmashauri, siipendi Tena hii Kazi (niliyokuwa naiwaza kuifanya miaka hiyo), kifupi HII OFISI NA KAZI YA SERIKALI SIVIPENDI KABISAAA.

BIG PROBLEM
Kuona nawaze kujiharibia future kazini nikaona nishirikishe wakubwa.

Hao wakubwa nao wamenipa ushauri ambao HATA SIJAUKUBALI.

Ninachonipa "Huu ukichaa wa kutopenda Kazi" ni kwamba NAHITAJI KUWA HURU.

Nahitaji kuwa kwenye biashara zangu masaa 24,
Nataka chochote kinachotokea kwenye biashara nikione, KIFUPI BIASHARA IMENIMEZAA HASAA yaani ROHONI na NAFSINI NAWAZA BIASHARA ZANGU.

Naweza kuwa ofisini kuanzia asubuhi mpaka jioni ila nikaishia ku-google na kusoma mambo ya biashara hiyo, nikaishia kupiga simu dukani na Kwa wateja badala nifanye Kazi za watu..!!!

Ushauri..
1. Shangazi yangu aliniambia "NIOE" halafu mke ndio asimamie halafu Mimi niendelee kupambana na ajira.
HUU USHAURI NILIGOMA KABISAAA

2. Boss mmoja, aliniambia nitafute uhamisho ili niwe karibu na biashara yangu.
Nikaona hili wazo ni sahihi, kwa maana biashara yangu ipo mkoa wa jirani na niliko.
Ila sasa tokea 2021 nianze harakati za kuhama basi Mkurugenzi kagoma kabisaaa kunisainia barua ya uhamisho ili nikatafute post kwengine (mkoa ilipo biashara yangu), hili swala LIMEFANYA NIMCHUKIE KABISA.

Nikawaza kuacha Kazi.

Nina watoto wawili mmoja darasa la 3 mwengine la 2.
Hawa watoto nawaelewa sanaa, nawasomesha Shule ada Mil 2.7 *2 (Mil 5.4, WANASOMA SHULE MOJA).

Wapo Dar kwa mama zao (kila mmoja na mama ake), ila tunawasiliana kila siku.

Nahitaji kuhama niende kwenye biashara zangu halafu niwavute wanangu ili niishi nao.
NAWAPENDA SANAA WANANGU.

Nawaza kuacha Kazi ili nikakomae na biashara yangu.

CONCLUSION.
Sina wazo la kuoa na wala sitaki kuoa, hivyo sihitaji kuwa na mtu wa kusimamia biashara sijui kunisaidia kulea.

Nikiangalia Kazini napata hela na biashara napata pesa.

Kwahiyo nipo dilema, nikisema niache Kazi Kuna pesa itapwaya tu kwenye maisha yangu, sasa naona kama duka litahelemewa na majukumu.

NIA YA KUACHA KAZI NINAYO, ILA SABABU SINA.

Ukicheki nilisoma sanaa kwasababu ya hii Kazi ila SIIPENDI TENA.

Mpaka muda mwengine nawaza KWANINI SASA NALISOMA SANAAA HIVI?

Ushauri wenu na MSAADA WENU MUHIMU SANAA.

Asanteni.

#YNWA
Mrejesho vipi sasa 🤔
 
GREETINGS.
Haloo wananchi wote wa JF, hamjambo?

Baada ya salamu twende kwenye mada.

INTRODUCTION:
Mimi ni mtumishi wa umma niliye ajiriwa 2012 na fani x (diploma) kwa level za kata (Afisa wa katani @ SIO MTENDAJI KATA).

2013 nikaenda chuo na kurudi 2018 na masters (niliunga) ya fani y.

Nikiwa na furaha na niite bahati, kurudi tu kazini nikapewa ofisi ya fani y, yaani nilimaliza chuo na kurudi kazini November 2018 na January 2019 nikahamishiwa halmashauri.

Niite bahati kwasababu, imekua ngumu kwa watumishi wengi kutoka Shule tu na ofisi zao za Utumishi wakawabadilishia Kazi zao (rectegorization au kuwahamishia kwenye vitengo walivyosomea).

Nilifanya Kazi kwa furaha na juhudi sana na 2019 nikapokea barua ya kubadilishiwa muundo (recategorization).

Niliona zile ndoto zangu za kuwa mkubwa kama zinaanza kutimia hivi na nilifanya Kazi kwa juhudi sana.

Fani y ndio niliyokuwa naipenda.

Fani x nilisomea tu kwa vile nilikuwa yatima na nilikosaga ada ya kusomea fani y miaka hiyo.

Ila hiyo fani x ndio iliniingiza serikalini.

SCENARIO:
2020 likatokea jambo kazini, mara TAKUKURU hao, mara CAG huyo, mara kamati ya kutuchunguza hiyo, mara usalama wa taifa huo.

Kifupi vitu vilikuwa vingi, ila iliamriwa tusimamishwe Kazi.

Tukiwa tumesimamishwa Kazi niliamua kufungua biashara.

Baada tu ya kusimamishwa Kazi nilitumia wiki 2 kutafuta frame na kuanza biashara.

Baada ya miezi 7 nikarudishwa kazini na mambo yakaendelea.

Ila biashara yangu ilikuwa ya moto sanaa (inauza sanaa).

PROBLEM
Baada ya kurudi kazini Kuna mambo nikaona yamebadilika.

1. Upendo na ile Kazi ukapoteaaa kabisaa

2. Nilikuwa mtoro balaa mpaka Mkurugenzi aliandika barua kwenda Utumishi ya Mimi kuvuliwa madaraka na kupewa mwengine.

Yaani aliyekuwa kijana wangu wa chini sasa hivi ni boss wangu.

3. Kuona hii ajira siipendi Tena, nikaona nitafute uhamisho, changamoto sasa, Mkurugenzi kagoma kabisaa kusaini barua zangu za kuniruhusu nikatafute post kwengine.

Anasemaga "bado nakuhitaji sanaa na siwezi kukuruhusu uondoke"

4. Nakiri; kunivua madaraka hata sijamlaumu, kiukweli kabisa nimekuwa mtoro balaa, siipendi Kazi Tena (kwasasa napenda sanaa biashara yangu na wanangu).

5. Yaani kazini naweza pitisha wiki sijasaini daftari la mahudhurio maana naingia saa 3 au 4 asubuhi na "ole wako uniulize lolote juu ya hilo..!!""

6. Yaani kwasasa siipendi Tena hii halmashauri, siipendi Tena hii Kazi (niliyokuwa naiwaza kuifanya miaka hiyo), kifupi HII OFISI NA KAZI YA SERIKALI SIVIPENDI KABISAAA.

BIG PROBLEM
Kuona nawaze kujiharibia future kazini nikaona nishirikishe wakubwa.

Hao wakubwa nao wamenipa ushauri ambao HATA SIJAUKUBALI.

Ninachonipa "Huu ukichaa wa kutopenda Kazi" ni kwamba NAHITAJI KUWA HURU.

Nahitaji kuwa kwenye biashara zangu masaa 24,
Nataka chochote kinachotokea kwenye biashara nikione, KIFUPI BIASHARA IMENIMEZAA HASAA yaani ROHONI na NAFSINI NAWAZA BIASHARA ZANGU.

Naweza kuwa ofisini kuanzia asubuhi mpaka jioni ila nikaishia ku-google na kusoma mambo ya biashara hiyo, nikaishia kupiga simu dukani na Kwa wateja badala nifanye Kazi za watu..!!!

Ushauri..
1. Shangazi yangu aliniambia "NIOE" halafu mke ndio asimamie halafu Mimi niendelee kupambana na ajira.
HUU USHAURI NILIGOMA KABISAAA

2. Boss mmoja, aliniambia nitafute uhamisho ili niwe karibu na biashara yangu.
Nikaona hili wazo ni sahihi, kwa maana biashara yangu ipo mkoa wa jirani na niliko.
Ila sasa tokea 2021 nianze harakati za kuhama basi Mkurugenzi kagoma kabisaaa kunisainia barua ya uhamisho ili nikatafute post kwengine (mkoa ilipo biashara yangu), hili swala LIMEFANYA NIMCHUKIE KABISA.

Nikawaza kuacha Kazi.

Nina watoto wawili mmoja darasa la 3 mwengine la 2.
Hawa watoto nawaelewa sanaa, nawasomesha Shule ada Mil 2.7 *2 (Mil 5.4, WANASOMA SHULE MOJA).

Wapo Dar kwa mama zao (kila mmoja na mama ake), ila tunawasiliana kila siku.

Nahitaji kuhama niende kwenye biashara zangu halafu niwavute wanangu ili niishi nao.
NAWAPENDA SANAA WANANGU.

Nawaza kuacha Kazi ili nikakomae na biashara yangu.

CONCLUSION.
Sina wazo la kuoa na wala sitaki kuoa, hivyo sihitaji kuwa na mtu wa kusimamia biashara sijui kunisaidia kulea.

Nikiangalia Kazini napata hela na biashara napata pesa.

Kwahiyo nipo dilema, nikisema niache Kazi Kuna pesa itapwaya tu kwenye maisha yangu, sasa naona kama duka litahelemewa na majukumu.

NIA YA KUACHA KAZI NINAYO, ILA SABABU SINA.

Ukicheki nilisoma sanaa kwasababu ya hii Kazi ila SIIPENDI TENA.

Mpaka muda mwengine nawaza KWANINI SASA NALISOMA SANAAA HIVI?

Ushauri wenu na MSAADA WENU MUHIMU SANAA.

Asanteni.

#YNWA
unataka tukushauri nini?
 
Pole kwa changamoto. Kwa mazingira hayo lazima kazi uichukie sababu ulisimamamishwa kwa tuhuma lkn umerudi ktk mazingira yaleyale . Kisaikolojia tu lazima ari ya kufanya kazi ipungue au ishuke kabisa.

Pili kama ulikopa mkopo mrefu na biashara bado haijaanzaa kuzaa matunda na huku mshahara unamakato pia lkn kazi uione changamoto.

Biashara ni rahisi kufanikiwa kama tu utaweka nidhamu katika pesa. Na kama huna tegemezi wanaokutegemea. Changamoto kwa familia zetu za kiafrika tuna ndugu jamaaa wadogo zetu. Sasa kama.

Kama inawezekana jaribu kuomba uhamisho japo wa ndani ya mkoa uende halmashauri nyingine. Usiache kazi kwanza ilihali hujapata uzoefu ktk biashara. Ukishapata uzoefu wa kujua changamoto,,,na mambo mengine. Ndipo ufanye maamuzi ya kuacha.

Siku zote simamia kile unachokiamini kwa maana hata ukikosea huwezi mlaumu mtu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila wafanyakazi wa serikali ni waogaa Jamani [emoji119]

Imagine anaogopa mpaka ndoa

Nani kakwambia kuwa naogopa kuoa?
Lini nimekwambia kuwa naogopa kuoa?

Kifupi:-
Sioni Sababu ya kuoa
Sina Nia ya kuoa
SIHITAJI KUOA.

Sio wote tuwe wanamuziki, wengine tubaki mashabiki.

#YNWA
 
Back
Top Bottom