double click
JF-Expert Member
- Oct 12, 2012
- 569
- 949
Kaka hzo ni hesabu za ekari au hekta?Kukodi shamba heka moja (shamba lililokaribu na chanzo cha maji/mto) 150,000/=
Mbegu 300g 220,000/=
Kulima shamba heka 50,000/=
Kufanya palizi heka 30,000/=
Kununua water pump 320,000/=
Mbolea (samadi, na za viwandani) = 300,000/=
Madawa ya wadudu+ magonjwa 200,000/=
Kuvuna heka 50,000/=
Kununua pipe za kumwagilia (150m) = 180,000/=
Gharama ya petrol (Lita 5/siku/acre)
Roughly itagharimu 650,000/=
Hela inayobaki ni ya DHARURA +CHAKULA+ NAULI
Ekari
Mkuu nimekuwa interested na hii comment yako, kama hutojali unaweza nijuza ni Dar sehemu gani wanauza gunia la karanga 40000?Hivi unajua bei ulio iweka haina tofauti na ya Dar? Kuna shida mahali katika utoaji wako wa taarifa.
Anaposema gunia la karanga hamaanish zilizo pukuchuliwa.Mkuu nimekuwa interested na hii comment yako, kama hutojali unaweza nijuza ni Dar sehemu gani wanauza gunia la karanga 40000?
Na pia hizo karanga ni nyeupe au zile nyekundu? Kwa mazingira ambayo yupo mdau nahisi yeye anaongelea karanga nyeupe, je hizo unazoongelea wewe ni zipi?
Sawa mkuu nashkuru Kwa maelekezo yako, hasa hapo kwenye kwenda mpwapwa ni kweli Kwa bei hiyo ni nzuri Kwa karanga ambazo zishamenywaAnaposema gunia la karanga hamaanish zilizo pukuchuliwa.
Gunia la karanga za maganda hutoa kilo 20 hadi 30 kama zimekomaa vizuri. Ukichukulia kiwango cha chini cha kilo 20 inamaana utakuwa umenunua kila kg elf 2 hapo hujaweka gharama za kubungua na Nauli ya kufukisha unapopeleka. Ukijumlisha vyote hivyo utagundua bei hiyo iko juu mno.
Kea halo hiyo bora uende Mpwapwa ambapo unapata kilo ya zilizokobolewa kwa 1200-1500?
Basi andika ekari ukisema heka unaharibu maanaEkari
Drip and green houses farming ni investment inayohitaji mtaji wa maana mkuu.Mtoa maada katoa andiko zuri ila limekosa nyama kabisa.Kwanini ulime horticultural crops mkoani Katavi, ambapo hayo mazao ni very perishable kama tikiti,nyanya, tango etc...?Je,target ya soko lako ni wapi?Maana kusafirisha hizo horticultural crops kutoka katavi mpk Dar ambako kuna soko la uhakika lazima mzigo uoze au kuharibika njiani.
USHAURI:
1.Kama lengo ni ulime horticultural crops (mazao ya mbogamboga) katavi siyo sehemu sahihi kwa nature hiyo ya mazao, ndio maana hata wenyeji wanalima most cereal crops like mahindi,maharage,Mpunga,karanga etc...
2.Ni vema ufanye hicho kilimo mkoa wa Pwani au Morogoro ambako ni jirani na soko,kwa maana target kubwa ya soko la horticultural crops ni masoko ya Dsm.
3.Pia ni vema ujue crop calendar vizuri na ufahamu pia ni msimu gani supply ya horticultural crops ni ndogo na demand ni kubwa,huo ndio msimu wa kupiga pesa nyingi kwenye horticultural crops,Market target ni muhimu sana na ndio uhai wa project yako.
4.Tumia drip irrigation & green houses for the better results,nje ya hapo unatafuta kesi ya kupoteza mitaji ya watu.
5.Andaa business plan nzuri yenye input,Agronomical activities,cost analysis and profit.Japo profit ya kilimo siyo guaranteed,na hapo ndio utaonyesha ukomavu wako ndugu Mwanasuaso kuwa unaweza kupata excepted profit kwa facts gani?
Dawa ni kufungua kampuni na kumgawia share za kampuni au kumwajiri kutokana na utaalam/mchango wake then ajiri Meneja, atafanya kazi tuu maana kazi zaidi na bidii zaidi atakayoweka atafaidika zaidi na hasara mtagawana sawasawa, pesa hataiona mpaka siku ya mshahara au gawioUaminifu uko kiasi gani? Kuna mwanasheria tunaweza kuandaa mkataba?
Huu Uzi uliishaje? Je, ulifanikiwa?Mawasiliano : kwanzakilimo73@gmail.com
Kwa anayehitaji namba za simu aje PM.
Habarini za mchana ndugu zangu na poleni kwa majukumu mazito ya ujenzi wa taifa.
Mimi ni kijana wa kiume na Mtanzania mwenye umri wa miaka 28. Nina Elimu ya chuo kikuu katika ngazi ya shahada ya kilimo na katika hali ya ndoa mimi bado sijaoa na wala sina mtoto kwasasa.
Hivi sasa ninapatikana katika mkoa wa Katavi, Wilaya ya mlele, kata ya usevya na mtaa wa kasunzulu. Ila makazi yangu ya kudumu ni Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza.
Ndugu zangu, nipo hapa kutafuta mtu yeyote ambaye ana mtaji (Rasilimali fedha) ili tuanzishe mradi wa kilimo biashara katika mkoa huu wa katavi maana ni miongoni mwa mikoa ambayo bado ina fursa kubwa za uwekezaji katika kilimo biashara.
Miongoni mwa fursa hizo ni kama ifuatavyo:-
1) Uwepo wa ardhi ya kutosha na yenye rutuba (matumizi/mahitaji ya mbolea za viwandani katika uzalishaji yapo chini sana).
2) Gharama za kukodi/kununua mashamba zipo chini sana.
3) Uwepo wa mito na schemes za umwagiliaji (mfano, KILIDA irrigation scheme na KASHISHI irrigation scheme) unatoa fursa kubwa kwa uanzishwaji wa miradi ya kilimo cha umwagiliaji.
4) Kwa upande wa kilimo biashara bei za mazao huku ziko chini sana hivyo kutoa fursa ya kununua mazao ya huku kwa bei ndogo na kusafirisha kwenye masoko ya walaji wakubwa mikoa mingine ili kutengeneza faida maradufu.
5) Gharama za kuishi katika mkoa huu zipo chini pia.
6) Urahisi wa upatikanaji wa nguvukazi (vibarua) ukilinganisha na mikoa mingine maana asilimia kubwa ya vijana wa huku wana mapenzi (passion) na kilimo.
Hivyo basi, Jukumu kubwa la muwezeshaji litakua ni kuwekeza fedha zake katika miradi pendekezwa na kujipatia faida zitakazo zalishwa na miradi pendekezwa huku mimi nikiwekeza mtaji wangu (Rasilimali muda na ujuzi) katika usimamizi wa shughuli zote za miradi pendekezwa.
Kitendo cha kutokua na mke na mtoto kwasasa kitanipa fursa kubwa ya kuelekeza focus yangu yote katika kazi na vilevile kuwa na uwezo wa kuzunguka mikoa mbalimbali katika shughuli za uendeshaji wa miradi na biashara kwa ujumla.
Penye nia pana njia, mgaagaa na upwa hali wali mkavu na mtembea bure si sawa na mkaa bure pasipo kujishughulisha.
Nakaribisha maswali, maoni na mapendekezo yeyote kutoka kwenu wakuu.
Mtu yeyote atakaye guswa na mwenye nia ya dhati ya kuisaidia serikali katika kupanua "Wigo" wa uwezeshaji vijana katika kujiajiri namkaribisha hapa au PM kwaajili ya mazungumzo ya kina.
Niko tayari kufanya kazi mkoa wowote ambapo mfadhili atapendekeza.
~Nawasilisha~ [emoji120][emoji120]
wazo lako zuri sana tunatofautiana kwenye kuwekeza pesa mm na vifaa vya kilimo kuanzia Tractrors vifaa vya kumwagilizia kupanda na kuvuna kama Drons kwajili ya kumwagilizia dawa mifumo ya umwagilizia mbegu mbolea na madawa kama uko tayari tuanze kazi pesa sinaAnaposema gunia la karanga hamaanish zilizo pukuchuliwa.
Gunia la karanga za maganda hutoa kilo 20 hadi 30 kama zimekomaa vizuri. Ukichukulia kiwango cha chini cha kilo 20 inamaana utakuwa umenunua kila kg elf 2 hapo hujaweka gharama za kubungua na Nauli ya kufukisha unapopeleka. Ukijumlisha vyote hivyo utagundua bei hiyo iko juu mno.
Kea halo hiyo bora uende Mpwapwa ambapo unapata kilo ya zilizokobolewa kwa 1200-1500?
Hivyo vyote ulivyovitaja hapo umavyo ola pesa huna. Hapo sijakuelewa kabisawazo lako zuri sana tunatofautiana kwenye kuwekeza pesa mm na vifaa vya kilimo kuanzia Tractrors vifaa vya kumwagilizia kupanda na kuvuna kama Drons kwajili ya kumwagilizia dawa mifumo ya umwagilizia mbegu mbolea na madawa kama uko tayari tuanze kazi pesa sina
Vitendea kazi vipo vyote wapi ukuelewa?Hivyo vyote ulivyovitaja hapo umavyo ola pesa huna. Hapo sijakuelewa kabisa
Nashindwa kuelewa unakua je na. Vitendea kazi vyote hivyo ukose pesa ya kuviendesha; it's a jokeVitendea kazi vipo vyote wapi ukuelewa?