Mirathi ya nyumba iliyojengwa na mjane yazua balaa; ukoo wa mume na ukoo wa mke wanaigombania

Mirathi ya nyumba iliyojengwa na mjane yazua balaa; ukoo wa mume na ukoo wa mke wanaigombania

Wachaga Wachaga Wachaga kila kona ya ugomvi wa mirathi hawana hata aibu. Kule Bagamoyo wameenda kuzika ndugu yao hata mke hayupo! Huku nako wameenda kumzika Mpogoro Moshi ili tu wajimilikishe mali. KLyn wa Mengi wanamsumbua kama hawamjui vile. Yaaani hizi mtu kwenye mali ni FISI maaaaamae zao
 
M
Habari wadau.

Kama mnavyojua swala la mirathi linavyotolewa macho hapa Tanzania.

Jirani kwetu kuna mama amefariki na kuacha nyumba nzuri tu na hajaacha mtoto hata mmoja.

Historia ya huyu mama ( kabila mpogoro) mwaka 1991 aliolewa kwa ndoa ya kanisani na mume wake ( kabila mchaga)

Baada ya kufunga ndoa walinunua kiwanja na mume wake na kuzaa mtoto mmoja wa kiume.

Mwaka 1994 mume wa huyu mama alifariki na kumuacha mke na mtoto mmoja wakiwa hai.

Taratibu za mirathi ya mume wake zilifanyika baada ya msiba. Mama na huyo mwanae wakapewa hiko kiwanja maeneo ya tegeta kikiwa kitupu hakijaanzwa ujenzi wowote.

Maisha yakaendelea. Mama huyu hakuolewa tena . Aliendelea kuishi na mwanae kwa kupanga nyumba ya NHC keko. Na mdogo mdogo akaanza ujenzi wa nyumba katika kiwanja walichoachiwa na mumewe.

Alijenga nyumba nzuri tu ya kisasa. Na zingine ndogo ndogo pembeni za kupangisha. Maana kiwanja kilikuwa kikubwa sana ( maana enzi wananunua tegeta ilikuwa pori ardhi haina thamani miaka ya 90 muuzaji anakuuzia bonge la kiwanja kwa bei ndogoo..)

Baada ya kumaliza ujenzi yeye na mwanae waliendelea kuishi nyumba ya NHC na kule tegeta walipojenga wakapangisha wapangaji kadhaa.

Mwaka 2015 mama alipata msiba mwingine wa kufiwa na mtoto wake huyo mmoja kwa ajali ya gari na hii ikamfanya mama kubaki peke yake bila mtoto wala mume.

Mama akaendelea kuishi mwenyewe mpaka na yeye mama alipofariki mwaka huu mwanzoni.

Mwili wa mama ulisafirishwa kwenda moshi kuzikwa walipozikwa mume wake na mwanae.

Shida imekuja kwenye nyumba zilizojengwa na huyo mama. Ukoo wa mume unasema ni mali zao. Na ukoo wa mke nao unasema ni mali zao maana zimejengwa kipindi mume wa huyo mama ameshafariki.

Wataalamu wa mirathi Kesi kama hii upande upi kati ya ukoo wa mume na ukoo wa mume una haki ya kurithi hizo mali za huyu mama
Mbona hiyo kesi ipo wazi Sana ! Ni kwamba huyo Mama mali kaziendeleza baada ya kuwa kapata mgao wake wa urithi kwa mmewe so ndugu wa mume hawana Chao kwani mirathi ya ndugu yao ilikwishagawanywa alipofariki kilichopo ni Cha ndugu wa mke!
 
Ndugu wa mume Wanatumia mantiki gani kudai Mali ni zao?
Mjane ni mwanamke single. Kuzikwa Moshi au Dar hakumfanyi kuwa mke wenu.

Wanadai Mtu kuolewa maana yake ni kuhamishwa ukoo.

Ile mahari waliyopokea maana yake ni mwanamke anahama ukoo wake na kuhamia ukoo wa mume.

Ndio maana hata mwili wake wameenda kuuzika moshi alipozikwa mume wake na mwanae.

Sasa kama mwili wake umzikwa kwenye makaburi ya ukoo wao. Na hata mali zake zisimamiwe na ukoo huo huo uliomzika
 
Wanadai Mtu kuolewa maana yake ni kuhamishwa ukoo.

Ile mahari waliyopokea maana yake ni mwanamke anahama ukoo wake na kuhamia ukoo wa mume.

Ndio maana hata mwili wake wameenda kuuzika moshi alipozikwa mume wake na mwanae.

Sasa kama mwili wake umzikwa kwenye makaburi ya ukoo wao. Na hata mali zake zisimamiwe na ukoo huo huo uliomzika
Hawa kwanini walikubali azikwe moshi wakati wanasema ni wakwao
 
mwanamke kama alilipiwa mahari hao ndugu wa mwanamke hawana wanachodai kwa upande huo alioolewa huyo mwanamke. wanachotaka kufanya hakina tofauti na wizi
Hapa bado hujatoa suluhu maana kama Mume alishafariki, nyumba imejengwa na sasa Mume, Mama na Mtoto wote hawapo..ni nani huwa ndio '"next of kin?"

Hapa kama Mama hajaacha maandishi hakika ni mtihani.
 
Hapa bado hujatoa suluhu maana kama Mume alishafariki, nyumba imejengwa na sasa Mume, Mama na Mtoto wote hawapo..ni nani huwa ndio '"next of kin?"

Hapa kama Mama hajaacha maandishi hakika ni mtihani.

Huyo mjane kazikwa wapi?
Alipozikwa mjane ndipo wenye mamlaka na Mali za marehemu
 
Wote hawana haki mkuu, win win situation apo ni mjengo tu uuzwe wagawane fungu ila umasikini ni mbaya sana aloo
Hapana mkuu wagawane kwa misingi ipi wakati unaambiwa nyumba alijenga huyo mwanamke na wakati anajenga mme wake alikuwa ameshafariki.
Hao ndugu wa mme ni njaa tu zinawasumbua mbona jambo liko wazi kabisa hata mtoto wa chekechea anaweza kusuluhisha hiyo kesi.
 
mimi sijui kabisa sheria lakini kuna maswali ya machache ya kujiuliza?
  1. je baada ya mume wa marehemu kufariki nini kiliamliwa kwenye miradhi
  2. kama mke alikubali kuwa mjane na atabaki kama mwanafamilia je wanafamilia walihusika vipi na malezi ya mtoto wa ndugu yao?
  3. mawasiliano yalikuwaje kati ya familia iliyooa na mjane wakati wa uhai wake?
  4. Je walikuwa na mchango wowote
na mengine mengi mwisho wa siku busara inaweza kutumika kwa familia zote mbili kugawana wakipata ratio ya 2:3
Hapo hakuna cha malezi wala mchango,nyumba ni ya mwanamke aliyefariki hao ndugu wa mme wanahusika vipi hapo?ndugu wa huyo mke aliyekufa ndio wenye mamlaka na hiyo nyumba very simple
 
Hapana mkuu wagawane kwa misingi ipi wakati unaambiwa nyumba alijenga huyo mwanamke na wakati anajenga mme wake alikuwa ameshafariki.
Hao ndugu wa mme ni njaa tu zinawasumbua mbona jambo liko wazi kabisa hata mtoto wa chekechea anaweza kusuluhisha hiyo kesi.
Kiwanja kilikua cha mume lakin kwa msingi huo wana haki na jasho la ndugu yao
 
Hapana mkuu wagawane kwa misingi ipi wakati unaambiwa nyumba alijenga huyo mwanamke na wakati anajenga mme wake alikuwa ameshafariki.
Hao ndugu wa mme ni njaa tu zinawasumbua mbona jambo liko wazi kabisa hata mtoto wa chekechea anaweza kusuluhisha hiyo kesi.

Kiwanja alinunua mume enzi za uhai wake. Na kwenye mirathi ya mume hiko kiwanja alipewa mtoto wa huyo mama ambae ni ukoo wao pia. Ameshafariki wamezika kwao.
 
Uhalali upo sababu mume alitoa mahari na pia mwanae kazikwa hapo. Mfumo mnaoutetea ulishapitwa na wakati.
Kama ishu ni mahari wadai hiyo mahari walipwe lakini si nyumba.
Hiyo nyumba haiwahusu kivyovyote.
 
Back
Top Bottom