Misafara ya viongozi inachosha, inatesa na kurudisha nyuma maendeleo, IGP Sirro peleka Traffic Sweden kujifunza misafara ya wenzetu, Time is Money!

Hii siku ilitesa watu sana. Msamvu ilisimama tangu saa 12 asbh mabasi yaliondoka saa tano.. Kuna umuhimu wa kufanya hii misafara isitese watu.
 
Mkuu Pascal kulaumu traffic wetu na Sirro ni kazi bule ,utawala wa awamu hii unapenda misafala ya ndani zaidi wakati awamu iliyopita ilipenda misafala ya nje. Sirro na traffic wake wanapewa amri tu ya kusafisha njia na kama unavyo jua amri toka juu za awamu zinavyotisha...😀😀😀
 
Nani humu keshakutana na adha ya motorcade ya Rais au Makamu wa Rais wa Marekani?

Kama mtu unalalamikia misafara ya Tanzania, basi hujaona kero wewe!
 
Hii siku ilitesa watu sana. Msamvu ilisimama tangu saa 12 asbh mabasi yaliondoka saa tano.. Kuna umuhimu wa kufanya hii misafara isitese watu.
Chakushangaza msafara unagar zaid ya 10na pikipiki lkn bado watu wanawacwac
 
Point, na tupate definition ya kiongozi ni nani. Kuwe na viongozi wawili tu kitaifa wenye motorcade na outriders
 
Usalama wa viongozi hususani no.1 ni wa lazima. Nashauri polisi na vyombo usalama watumie tekinolojia zaidi.Wanavyotoa muda mwingi alert ni hatari zaidi. dakika 10 zinatosha safisha njia.
 
Hakika inachosha tena haswa hii njia ya posta-airport (gongo la mboto) aisee inawaumiza sana watu wanaotoka njia ya ilala kwenda veta.
Unakuta mtu umetoka mikochen labda unaenda mbagala, ukifika pale mataa ya veta unaweza ganda pale hata kwa 2 hours kupisha hawa wanatoka na kwenda njia ya airport.
So disguisting kwakwel
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…