Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Wakasemezana....Je sisi ni kina nani mpaka BWANA atufanyia haya yaliyo makuu kwa kutu nyunyizia mvua ya vichwa vya Treni?.....Acacia:3:2-4
Ndipo Barick mkuu akasema,mkiyashika mausia yangu mtakula mema ya nchi.Kuchenjua 4:5.
 
34 katika mwaka wa pilii wa utawala wa mfalme Juma Nguvu Hovyo wa tano, mfalme wa nchi ya sambaratika, bandari ilikuwa tupu. hakuna mizigo iliyoingia kupitia bandari hii. mfalme na matowashi wale walikuwa katika mfadhaiko mkuu wasijue la kufanya.

35 lakini asubuhi moja katika mwezi wa sita, mlinzi wa lango kuu la bandari aliona vichwa vya treni vikiwa bandarini. moyo wake ukashikwa na hofu kuu. akageuka na kwenda kuwaambia matowashi alichokiona. nao kwa hamaki wakanyanyuka kwenda kuyaona. wakaulizana wao kwa wao "ni nani kati yetu amefanya haya?" hakuna hata mmoja kati yao aliyejua chochote.

36 habari zikamfikia mfalme nguvu hovyo, naye akafika bandarini na kuwakuta matowashi wakiwa wamekusanyika kwa fadhaa. akaviangalia vichwa vile, kisha akawageukia matowashi na kuwauliza "ni nani kati yenu amefanya haya kunijaribu mimi nisiyejaribiwa?". nao wakamjibu "ee bwana usiyejaribiwa, kama wewe uishivyo, hata sisi hatujui"

37 akavigeukia tena vichwa vile vya treni, akaviuliza "enyi mliotoka kusikojulikana, ni nani amewatuma kwangu kuja kunijaribu mimi na watu wangu, watu waliochini ya uvuli wa minyororo yangu?". kichwa kimoja kikafungua kinya chake na kunena "ewe mfalme nguvu hovyo, huoni kuwa bandari yako ilivyo tupu?, huoni watu wako walivyo na fadhaa? je, ni vibaya sisi kuja kurudisha matumaini ya watu yaliyopotea tangu ukalie kiti hicho cha enzi?"

38 maneno yale yalimfadhaisha sana mfalme, akageuka na kurudi kwenye jumba lake jeupe akiwa na gadhabu ya kiwango cha standard gauge akiwaacha matowashi na walinzi wasijue la kufanya.
MENDE MSAFI 24: 34-37
[emoji13] [emoji13]
 
Enyi watu wa nchi,msifadhaike kwa vile afanyavyo sherehe kila wiki,maana segerea inamtamani. Iptl 20:7
 
Tena amini nawaambieni yeye aliyepokea kwa mkono wa kulia atatoa kupitia tundu lolote.Na haya nimewaambieni mbele ili wakati atoapo muwe tayari kushuhudia.Naye aliyeko wodini asitoke hapo mpaka kesi yake iishe kusomwa. Mbagala 6:5.
 
Ndipo makada wakajipiga vifua na kugalagala kwenye mavumbi kama chatu huku wakisema, "ewe Sizonje tuchukue utumwani milele"
Lumumba 4 : 5-13
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Nami nilipochangia nikatoka na kwenda zangu na niliporudi jioni nikakuta jamii forum imechafuka na makada wa Lumumba wameenda kuishitaki kwa kuhani ili malaika alieshusha vichwa vya treni ashuke kuizima mitandao
Koromije 8:15
 
Wakasemezana....Je sisi ni kina nani mpaka BWANA atufanyia haya yaliyo makuu kwa kutu nyunyizia mvua ya vichwa vya Treni?.....Acacia:3:2-4
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Hahahaha hatari[emoji581] [emoji581] [emoji582] [emoji582] [emoji586] [emoji586] [emoji586]
 
Nchi ya Giningi, Watu wake wamekunywa uji Wa ndele amabo unawafanya Mzugo wao kuona nyeupe kuwa nyeusi na kinyume chake. .

Bi Kilembwe 2:6:9
 
Ndipo Farao akastaajabu kuona hakuna aliyejitokeza na kukiri vichwa vile ni mali yake,wafuasi wake wakaangaliana na kusema,"hakika Mungu yu upande wetu,ametushushia vichwa kutoka mbinguni".Nao Wadanganyika wakaangaliana kwa mshangao kwa maana waliijua kweli.Nae Erode ambaye ambaye alikuwa kipindi cha utawala wa Mroma(JK),akakaa kimya hasiseme neno maana akikumbuka kupukutika kwa nywele kichwani hana hamu....Watch Out 22:12-20
 
Wadanganyika wakasikika wakiitikia Amina Amina SIZONJE Wewe ndiye Rais wa milele wa nchi yetu utukuzwe milele na Wadanganyika wote. ZERO BRAINS 10:25-30


Na kwa jinsi gadhabu ya Bwana,SIZONJE ilivyo waangukia wana wa DANGANYIKA......wakaambizana ole wake atakaye vikubali na kuvitwaa VICHWA HIVYO.....Hatusomeshi Wazazi-7:28-31
 
Back
Top Bottom