Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Bandarini 2:3-4Joseverest andiko lako kitabu gani na mstari wa ngapi
Naye akajibu unanini nami ewe mlinda mlango?sivijui vichwa hivi.Mara jimbi akawika mara tatu. Matokeo 34:12-14.Vichwa vinakanwa mara tatu
Ndipo Barick mkuu akasema,mkiyashika mausia yangu mtakula mema ya nchi.Kuchenjua 4:5.Wakasemezana....Je sisi ni kina nani mpaka BWANA atufanyia haya yaliyo makuu kwa kutu nyunyizia mvua ya vichwa vya Treni?.....Acacia:3:2-4
[emoji13] [emoji13]34 katika mwaka wa pilii wa utawala wa mfalme Juma Nguvu Hovyo wa tano, mfalme wa nchi ya sambaratika, bandari ilikuwa tupu. hakuna mizigo iliyoingia kupitia bandari hii. mfalme na matowashi wale walikuwa katika mfadhaiko mkuu wasijue la kufanya.
35 lakini asubuhi moja katika mwezi wa sita, mlinzi wa lango kuu la bandari aliona vichwa vya treni vikiwa bandarini. moyo wake ukashikwa na hofu kuu. akageuka na kwenda kuwaambia matowashi alichokiona. nao kwa hamaki wakanyanyuka kwenda kuyaona. wakaulizana wao kwa wao "ni nani kati yetu amefanya haya?" hakuna hata mmoja kati yao aliyejua chochote.
36 habari zikamfikia mfalme nguvu hovyo, naye akafika bandarini na kuwakuta matowashi wakiwa wamekusanyika kwa fadhaa. akaviangalia vichwa vile, kisha akawageukia matowashi na kuwauliza "ni nani kati yenu amefanya haya kunijaribu mimi nisiyejaribiwa?". nao wakamjibu "ee bwana usiyejaribiwa, kama wewe uishivyo, hata sisi hatujui"
37 akavigeukia tena vichwa vile vya treni, akaviuliza "enyi mliotoka kusikojulikana, ni nani amewatuma kwangu kuja kunijaribu mimi na watu wangu, watu waliochini ya uvuli wa minyororo yangu?". kichwa kimoja kikafungua kinya chake na kunena "ewe mfalme nguvu hovyo, huoni kuwa bandari yako ilivyo tupu?, huoni watu wako walivyo na fadhaa? je, ni vibaya sisi kuja kurudisha matumaini ya watu yaliyopotea tangu ukalie kiti hicho cha enzi?"
38 maneno yale yalimfadhaisha sana mfalme, akageuka na kurudi kwenye jumba lake jeupe akiwa na gadhabu ya kiwango cha standard gauge akiwaacha matowashi na walinzi wasijue la kufanya.
MENDE MSAFI 24: 34-37
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Ndipo makada wakajipiga vifua na kugalagala kwenye mavumbi kama chatu huku wakisema, "ewe Sizonje tuchukue utumwani milele"
Lumumba 4 : 5-13
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Na akasema,ewe bwana,ewe bwana,na hivyo vichwa vya tren na vilejee vitokako."(Kibiti 57:121-123)
Navyo vichwa vikamjibu,wewe umetutoa SA,iweje usitujue?yeye aliyeniona mimi amemuona aliyenileta.makinikia 12 :Ndipo mfalme mtukufu wa makinikia akaviuliza vichwa vya treni, Nyie ni yatima au mna wazazi?
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]Wakasemezana....Je sisi ni kina nani mpaka BWANA atufanyia haya yaliyo makuu kwa kutu nyunyizia mvua ya vichwa vya Treni?.....Acacia:3:2-4
Na kwa jinsi gadhabu ya Bwana,SIZONJE ilivyo waangukia wana wa DANGANYIKA......wakaambizana ole wake atakaye vikubali na kuvitwaa VICHWA HIVYO.....Hatusomeshi Wazazi-7:28-31