Mishahara imekatwa: Poleni Watumishi watia nia

Mishahara imekatwa: Poleni Watumishi watia nia

Pitapita zangu hapa jijini Mwanza zimenikutanisha na watumishi wa umma wenye huzuni, chuki, hasira na kisasi mioyoni baada ya mishahara yao kukatwa kwa sababu walitia nia.

Wanasema, mishahara yao ndo uhai wa familia zao, ndiyo uzima wa Babu na Bibi zao vijijini. Wanasema wanawagonjwa wanaowategemea.

Wako walioomba ruhusa kwa mujibu wa waraka. Wako waliokuwa likizo za kawaida za mwaka.

Wamerudi makazini, walikipenda Chama cha Mpainduzi, wakavaa nguo za kijani, wakaamuka na CCM OYEEE, NG'ARA CCM ng'ara CCM na mengine kadhaa.

Wafanyakazi wanalia, wanasikitika kwanini imekuwa hivi. Wanaona hata yanayoitwa majonzi ya kitaifa ni majonzi yao wao huku na si ya kila mtu.

Taifa kinahitaji uponyaji

Cc: Katibu Mkuu Utumishi
Ninachofahamu japo sijasoma sheria yenyewe mtumishi akifanya kazi chini ya siku 15 anatakiwa kulipwa nusu mshahara Happ Sina hakika kwakweli
 
Sifurahii watumishi was umma kukatwa mishahara yao ya mwezi julai ila sheria ni msumeno
 
Mkuu kabla hujalalamika unafahamu taratibu za utumishi wa umma kuhusu mtu ambaye anataka kugombea nafasi yoyote ya uongozi kwa vyama vya siasa ?


Maana tunaweza kuanza kulaumu watu wengine kumbe makosa yapo upande wetu kabisa
Kuchukua fomu na kuchaguliwa kugombea ni vitu viwili tofauti.Hiyo sheria inapingana na katiba.

Ibara ya 21 ya Katiba: 21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.
 
Eti kisasi!! Huyu mtumishi wa umma wa tz mwente kisasi ni mwalimu au dakrari?? Yani hata wasingepewa mishahara mpaka oct bado watachagua CCM!
 
Ni sheria ipi walivunja mpaka wakasimamishiwa mishahara? kwani hawawezi kushitaki?
Usitugombanoshe na serikali yetu. Ngoka tuvumilie hilo lipite. Tunashukuru kwa kuwa ni mwezi mmoja. Kidumu chama cha Mapinduzi.

Mtia nia.
 
Wambie washukuru pia mwezi ujao watapata mshahala, je wangetimuliwa saivi nadhani wangekuwa ICU.
Kina katika, matambiko, Elia Michael et al nao mwezi ujao watarudishwa kwenye payroll?
 
Kina katika, matambiko, Elia Michael et al nao mwezi ujao watarudishwa kwenye payroll?

🤣🤣🤣🔨🔨🔨 akina kafulila, makonda hao waendelee kuwa jobless hadi hapo Jiwe akipata nafasi ya kuwapa tena
 
Pitapita zangu hapa jijini Mwanza zimenikutanisha na watumishi wa umma wenye huzuni, chuki, hasira na kisasi mioyoni baada ya mishahara yao kukatwa kwa sababu walitia nia.

Wanasema, mishahara yao ndo uhai wa familia zao, ndiyo uzima wa Babu na Bibi zao vijijini. Wanasema wanawagonjwa wanaowategemea.

Wako walioomba ruhusa kwa mujibu wa waraka. Wako waliokuwa likizo za kawaida za mwaka.

Wamerudi makazini, walikipenda Chama cha Mpainduzi, wakavaa nguo za kijani, wakaamuka na CCM OYEEE, NG'ARA CCM ng'ara CCM na mengine kadhaa.

Wafanyakazi wanalia, wanasikitika kwanini imekuwa hivi. Wanaona hata yanayoitwa majonzi ya kitaifa ni majonzi yao wao huku na si ya kila mtu.

Taifa kinahitaji uponyaji

Cc: Katibu Mkuu Utumishi
Umetumwa kutusemea?
 
Kuchukua fomu na kuchaguliwa kugombea ni vitu viwili tofauti.Hiyo sheria inapingana na katiba.

Ibara ya 21 ya Katiba: 21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.
Mistari 3 ya mwisho "kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria."

UTARATIBU uliowekwa kwa watumishi wa umma kuhusu kutaka kugombea nafasi za uongozi wa siasa ndo uko Kama nilivyo eleza katika post ile uliyo i-quote
 
Sheria inasema
Mtia nia yoyote aliyeajiliwa anatakiwa aache kazi ndipo aingie kwenye shuguli za siasa
Washukuru ata wamepunguziwa na sio kuachishwa
Siyo Kweli Mkuu! Anaruhusiwa kuanza michakato ya kuingia kwenye siasa akiwa bado mfanyakazi kwa kuomba ruhusa au likizo isiyokuwa na malipo,akishafanikiwa kuchaguliwa kwenye nafasi ya kisiasa hapo Sasa anatakiwa aache kazi.
 
Sheria inasema
Mtia nia yoyote aliyeajiliwa anatakiwa aache kazi ndipo aingie kwenye shuguli za siasa
Washukuru ata wamepunguziwa na sio kuachishwa
Hakuna sheria inayosema hivyo. Standing orders za civil servants zinasema wakati wa mchakato wa kura za maoni mtumishi anapaswa kuomba likizo ya bila malipo. Hivyo kukatwa mshahara kwa siku ambazo hawakuwapo kazini ni sahihi kabisa, lakini siyo kufutwa utumishi. Mgombea atatakiwa kuacha kazi mara chama chake kikimpitisha kugombea ubunge au udiwani.
 
Ile sheria nimeisoma. Ni sheria ukiangalia kwa makini utagundua ilitungwa kuzuia flow ya wafanyakazi kukimbilia siasa. Ubaya wa sheria nikwamba inawanyima haki wafanyakazi ya kushiriki kuchaguliwa kwenye siasa. Ni sheria ya kibaguzi flani.

Upande mwingine ,wahanga walijua kitachofuata wasimlaumu mtu. Ni mpaka sheria ibadilishwe
Sheria mbona iko straight forward, tatizo watu wanataka kumwibia mwajiri. Kuna mambo wanayotakiwa kuyafanya kabla ya kuingia kwenye mchakato wa kura lakini wanataka kujifanya hawajui. Nasema tena sheria haimzuii mtumishi kuingia siasani!
 
Back
Top Bottom