Mishahara ya viongozi wa Tanzania

Mishahara ya viongozi wa Tanzania

Jamani kuna mtu anayejua mshahara wa raisi wa Tanzania ni kiasi gani? Kuna mtu kaniambia ni $200,000 na kitu kwa mwaka...sikuamini lakini akanihakikishia kuwa taarifa zake ni za uhakika. Bado ninasita kuamini ingawaje sina taarifa zozote na sijawahi kuona mahala popote pale kuhusu mshahara wa raisi.

Na mshahara wa makamu wa raisi..?
Waziri mkuu..?
Spika wa bunge..?
Mkuu wa majeshi ya ulinzi, polisi,magereza..?
Jaji mkuu..?

Kama kuna mtu anayejua...ni wapi tunaweza kupata taarifa hizi?

Kwa kweli kulingana na ikama itolewayo na serikali mara kwa mara hii mishahara ni midogo kukidhi mahitaji ya kila siku kwa watumishi wote wa seikali. Inaanzia $1200 kwa KM hadi kama $5000 kwa Rais kwa mwezi.

Ila mshahara si issue kwa vile ana "entinlements" (stahili) nyingi. Zinajumuisha matumizi ya kawaida kama usafiri ulinzi, mawasiliano, kiwango cha posho ya kusafiri hata posho ya vikao. Mfano mimi kidampa mshahara wangu $100 kwa mwezi nikisafiri nje say Nairobi au Kampala nastahili kulipwa $ 230 kwa siku sawa na mishahara ya miezi miwili na zaidi. Hapo ndipo kwenye utata. Iweje posho ya kusafiri nje kwa siku izidi mshahara wa mwezi? Jibu ni kuwa watumishi wengi hawana fursa hiyo ila baadhi tu ya wanamtandao. Lakini uchambuzi wa ndani unadhihirisha kuwa viwango vya mishahara vinalingana na tija. Maana yake udogo wa mishahara unalingana na udogo wa Tija, ujuzi, uweledi fikira fupi, hata uaminifu na utiifu kwa serikali.

Nakushauri usiangalie sana viwango vya mishahara kwa sababu siyo realistic na mfumo fare na productive wa serikali makini
 
kwa nini mshahara wa rais wa tanzania mnaukokotoa kwa misingi ya dola?
 
Sorry sina jibu, ila nina swali, umewahi kuona mshahara wa Rais yeyote Duniani kuwekwa wazi? kama umefanikiwa kupata hata mshahara wa Rais mmoja wapo Duniani unaweza kupata jibu,
 
Sorry sina jibu, ila nina swali, umewahi kuona mshahara wa Rais yeyote Duniani kuwekwa wazi? kama umefanikiwa kupata hata mshahara wa Rais mmoja wapo Duniani unaweza kupata jibu,

Mishahara ya Marais inajulika sana.
US President- 400, 000 USD kwa mwaka,
Cameroun ndiyo mkubwa zaidi kwa marais wote, sikumbuki ni kiasi gani. TZ sijui
 
Sorry sina jibu, ila nina swali, umewahi kuona mshahara wa Rais yeyote Duniani kuwekwa wazi? kama umefanikiwa kupata hata mshahara wa Rais mmoja wapo Duniani unaweza kupata jibu,

Marekani si mshahara tu bali hata amelipa kodi kiasi gani inawekwa wazi! Mshahara wa rais wa Kenya unapangwa na bunge na unajadiliwa wazi. Ni hivi karibuni Kibaki amekataa nyongeza kubwa ya mshahara. Mandela nae alikataa nyongeza ya mshahara. Ni haki ya wanaomlipa mshahara (wananchi) kujua anapata kiasi gani. Kama ilivyo kwa watumishi wa umma.

Na nyie mnaouliza source, acheni uvivu. Mtandao si JF peke yake!

Amandla.
 
Kurasa 20 na bado hakuna anayejua....

labda kurahisiha anayejua TGSS J, K ,L na kuendelea. TGSS ndo salary code ya watumishi wa serikali kuu. Akitokea mtu akataw na data hizo TGSS( Tanzania Gov Salary Scale) zinawakilish kiwango gani basi tunaweza kuwa na kadirioa la karibu na ukweli nani anapata kiasi gani.

Hawa wakubwa ngazi zao za mishahara nadhani itakuwa kuanzia TGS J.

Assumption/makadirio yangu ni kuwa

TGS J= wakurugenzi wa idara kwenye wizara , DC < 1,200,000
TGS K= Makatibu wakuu makamisna ,RC < 1,400,000
TGS L= Mawaziri na wakuu wa taasisi nye < 1,600,000
Rais I assume mshahara utakuwa <4,000,000

Natoa hoja
 
Mimi ningefurahi kama Slaa angetoa ahadi ya kuweka wazi mishahara na marupurupu ya viongozi wote wajuu.

Amandla.....
 
labda kurahisiha anayejua TGSS J, K ,L na kuendelea. TGSS ndo salary code ya watumishi wa serikali kuu. Akitokea mtu akataw na data hizo TGSS( Tanzania Gov Salary Scale) zinawakilish kiwango gani basi tunaweza kuwa na kadirioa la karibu na ukweli nani anapata kiasi gani.

Hawa wakubwa ngazi zao za mishahara nadhani itakuwa kuanzia TGS J.

Assumption/makadirio yangu ni kuwa

TGS J= wakurugenzi wa idara kwenye wizara , DC < 1,200,000
TGS K= Makatibu wakuu makamisna ,RC < 1,400,000
TGS L= Mawaziri na wakuu wa taasisi nye < 1,600,000
Rais I assume mshahara utakuwa <4,000,000

Natoa hoja

2005 Tuliambiwa na CUF kuwa mshahara wa Rais Karume ni 7M kwa vyovyote J.K atakuwa analamba zaidi.
 
Hivi mishahara na marupurupu ya viongozi wa juu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania inajulikana? Viongozi hawa ni Rais, Waziri Mkuu, Jaji Mkuu na Spika. Nauliza kwa sababu nadhani mishahara wa marais nyingine inakuwa wazi. Kwetu ikoje?

Mishahara ya serekali iko kwenye salary scale,kila kiongozi anaongozwa na hii salary scale.
 
Mishahara ya serekali iko kwenye salary scale,kila kiongozi anaongozwa na hii salary scale.

Mheshimiwa Rais yuko kwenye salary scale ipi? Na wapi imeelezwa hivyo? Hawa viongozi wanalipwa kutokana na kodi na mapato mengine yanayotokana na jasho la wananchi wao kwa hiyo ni haki yetu kujua wanalipwa kiasi gani kwa kila hali.

Mshahara wa mtumishi wa umma hata siku moja hautakiwi kuwa siri.Uwazi huu utazuia hisia kuwa wanajinufaisha kutokana na hayo madaraka tuliyowapa.

Amandla.
 
labda kurahisiha anayejua TGSS J, K ,L na kuendelea. TGSS ndo salary code ya watumishi wa serikali kuu. Akitokea mtu akataw na data hizo TGSS( Tanzania Gov Salary Scale) zinawakilish kiwango gani basi tunaweza kuwa na kadirioa la karibu na ukweli nani anapata kiasi gani.

Hawa wakubwa ngazi zao za mishahara nadhani itakuwa kuanzia TGS J.

Assumption/makadirio yangu ni kuwa

TGS J= wakurugenzi wa idara kwenye wizara , DC < 1,200,000
TGS K= Makatibu wakuu makamisna ,RC < 1,400,000
TGS L= Mawaziri na wakuu wa taasisi nye < 1,600,000
Rais I assume mshahara utakuwa <4,000,000

Natoa hoja

Hiyo TGSS inapatikana wapi?
 
Duh na marupurupu?

Marupu rupu yanakuwa mengi na yanaweza kuzidi mshahara.
Gari- Land cruiser sijui wanawekewa lita ngapi kwa wiki inategeama na cheo
Nyumba- ya kiwango ambazo sijui hata kama wanalipia maitanace charge
Safari za mikoani na nje ya nchi perdiem?
Lazima kutakuwa na kitu kama overtime
 
Na hili ndo tatizo kwanini mshahara uwe siri, wa mbunge wanasema 7m, ina maana wanamzidi rais mshahara?
 
Kwa kumbukumbu zangu iliwahi kutajwa mishahara ya rais Mkapa pamoja na gavana wa benki kuu marehemu Bilali; Mshahara wa Mkapa ilikuwa ni dola za kimarekani $15,000 kwa mwezi bila kodi na mshahara wa Bilali ulikuwa $ 12,000 kwa mwezi.

Hivyo naamini kabisa rais Kikwete hakupunguza hicho kiwango ila yawezekana aliongeza.
 
Tatizo siyo mshahara......ishu zote zipo kwenye marupurupu.....ndiko mapigo yalipo....
 
Sorry sina jibu, ila nina swali, umewahi kuona mshahara wa Rais yeyote Duniani kuwekwa wazi? kama umefanikiwa kupata hata mshahara wa Rais mmoja wapo Duniani unaweza kupata jibu,

I once read somewhere (nadhani kwenye yahoo news) kuwa mshahara wa obama ni dola laki nne...nadhani article ile ilianzia kwenye issue nzima ya wamarekani kuhoji spending ya kiwango chake ya presidaa wao wakati fulani wa holiday..so kwa america si issue i think, na hata wa vice presidaa wao waliuonyesha na hata wa seneta.

ila huku kwetu duu..balaa..kuna mshikaji wangu alishawahi kufika scandinavian country (sijui ipi) anasema unaweza jua income ya mtu (incuding mshahara wake) kwenye mtandao tuu, wako very transparent..
 
Back
Top Bottom