Mitambo ya kuzuia vurugu za uchaguzi wa Rais mwaka 2025 iliyonunuliwa na Serikali inatisha sana, vyama pinzani vitakapoleta vurugu vitaishia pabaya

Mr Why

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2019
Posts
2,235
Reaction score
4,252
Mitambo ya kuzuia ghasia za uchaguzi wa raisi mwaka 2025 iliyonunuliwa na Serikali inatisha sana, vyama pinzani vitakapoleta vurugu vitaishia pabaya

Vyama pinzani mkiwemo CHADEMA na vinginevyo nendeni pole pole ndugu zangu kwasababu mitambo ya kupambana na vurugu iliyomwagwa Jeshi la Polisi ni hatari sana na mbaya zaidi Polisi wetu wanafanya kazi kwa hasira sana ndugu zangu mnaweza kudhurika vibaya mtakapoleta vurugu

Tangu niifahamu Tanzania na Jeshi la Polisi sijawahi kuona mitambo hatari kama hii iliyonunuliwa miaka hii 2024 - 2025
 
Weka picha tuione,picha itanoga zaidi
Team Samia,2025,Ushindi lazima
 
Pia soma Video: Magari Mapya ya Polisi Tayari Kukabiliana na Watakaojaribu Kuvuruga Uchaguzi wa Oktoba 2025
 
Upumbavu. Hospitali havina madawa. Wanafunzi wanakaa chini na wengine kukosa au kucheleweshewa mikopo mnajifia upumbavu na ufisadi huu! Aibu na ajabu. Wanaosifia ukumbuvu huu ni machawa na makunguni. Sifa nyingine hata chizi hawezi kuzitoa hata kuzikubali. Anyway, mshukuruni rais dk wenu kwa kuwapenda wananchi hadi ananunua siasa za kuwaumiza kwa fedha zao. Sijui nani aliwaroga watanzania.
 
Mnajitekenya na kucheka wenyewe
 
Inachekesha sana, kwanini tunajiandaa na vurugu na sio kuweka mazingira vizuri kusiwe na vurugu?

Ninavyofahamu, UCHAGUZI UKIWA HURU, WAZI NA HAKI HAKUWEZI KUTOKEA VURUGU.
 
Nani alikuambia vurugu lazima vianzishwe na vyama, lile kombora lililofyatuka na kuua askari ndani ya gari la polisi lililokuwa limeegeshwa pembeni ya uwanja nani alilifyatua?
 
Huku tunalilia hela za Trump.

Mmabo kama haya ni matumizi ya hovyo sana.
 
Tumeipenda wenyew ndi-ndi🎵
Wacha waisome number eeeh🎵
Fisiem mbele Kwa mbeleeeee!🎵
 
Nani alikuambia vurugu lazima vianzishwe na vyama, lile kombora lililofyatuka na kuua askari ndani ya gari la polisi lililokuwa limeegeshwa pembeni ya uwanja nani alilifyatua?
Mleta uzi anafikiri mfano itokee watu milion 25 nchi nzima waingie mitaani,anafikiri hyo mitambo itasaidiaaa sana sana wenye mitambo wataikimbiaaq na kuziacha 😄

Ova
 
Tumeshindwa kuchonga hivi vitu pale Nyumbu kweli?
 
Yote haya sababu ni moja tu! "Kwenda choo"
 
Wangetoa order yatengenezwe yenye sura ya kutisha kama Makamu
 
Nchi zenye wananchi wake chini ya dolla moja zina mbwembwe za kijinga sana.

Yote ya nini? Wakati vituo vya afya vinakosa vifaa tiba na mashule kukosa vifaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…