Uchaguzi 2020 Mitandao ya kijamii Tanzania yawa restricted. YouTube, WhatsApp, Twitter, JamiiForums na Telegram zimeguswa - Oktoba 27, 2020

Uchaguzi 2020 Mitandao ya kijamii Tanzania yawa restricted. YouTube, WhatsApp, Twitter, JamiiForums na Telegram zimeguswa - Oktoba 27, 2020

Najaribu kuingia YouTube lakini inagoma, kama nusu saa iliyopita nilikuwa naipata.

Kuna yeyote anapata tatizo kama langu?

Natumia mtandao wa Tigo
Alafu tukisema Magufuli hafai kuwa Rais watu wanasema tuna chuki naye. Haya sasa mmeyaona mwenyewe. Nawaambia watanzania kesho tukapigeni kura kwa wingi kumuondoa huyu fedhuli madarakani na tuzilinde kura zetu kwa nguvu zote
 
Kuna muda nilishangaa mdomo wangu unatoa matusi bila kutarajia. Nimepanga kukutana na hubby sehemu, nimefika hiyo sehemu simu hazitoki. Na yeye ananitafuta sipatikani. Bahati nzuri alikua anazunguka zunguka akaniona.
Yan huu upuuzi wa kuzimiana mitandao ni wa kishamba sana. 2020 tunazimiana mitandao kweli watu wengine biashara zinategemea mitandao watakula mawe. Jiwe et al. ni wehu sana
Yaani baby niliwaza sana why wanafanya hivi?..nikaona nizunguke kidogo labda nitakuona na kweli nikakuona na moyo wangu ukatulia. Nakupenda sana kipenzi, take care.
 
Nimetest ni kweli in load tu labda itakuwa kwa baadhi ya watu maana Kuna muda watu walikuwa wakilalama mitandao haifanyi kazi Ila wakati mimi nilikuwa napeta.. so i think kutakuwa na katatizo ka mtandao
Ili kuficha aibu ya kutetea ushetani mnalalazimika kulalamika kimoyomoyo

Poleni sana shetani hana rafiki
 
Nchi zote duniani watu wenye akili timamu huwa wanawalinda raia wao
Watu wa siasa hawazidi hata million 5
Wachochezi katika siasa hawazidi hata 100
Athari ya mitandao ya kijamii hasa twitter, facebook, na social media zingine ni kubwa mno hasa kipindi hiki cha uchaguzi
Kuna watu ni machizi lakini wanatumia hii mitandao
Taarifa wala hazijathibitishwa tayari machizi wameshazisambaza social media wakidhani ni sifa kumbe wanaliingiza taifa katika machafuko yasiyo ya lazima
Kwangu mimi ni sawa tu TCRA Piga Ban kila kwenye viashiria vya kuvunja Aman
Sio kila mtanzania ni mwana siasa.
 
Najiuliza sipati jibu.
Ni jambo jipya ambalo halijapata kuwepo nchini tangu mitandao hii ianze.
Ndivyo tunavyotakiwa kulinda amani yetu, umoja wetu na Taifa letu?
Hofu yetu kubwa ni nini hasa juu ya mitandao hii?
Huyu ndie ana waambia mkimpa ridhaa ya tano tena ata kuwa mtiifu. Leo hamja piga kura ana wazimia mitndao mliyo lipia pesa kupata taarifa.
Akili kichwani.. Keaho mpe kura atakae toa haki.
 
Back
Top Bottom