Mitume na manabii wa kileo ni viumbe waliojaa, ghiliba, uroho ubinafsi na uchoyo uliopitiliza

Mitume na manabii wa kileo ni viumbe waliojaa, ghiliba, uroho ubinafsi na uchoyo uliopitiliza

Hawa watu mbona wametajwa kwenye Quran. Quran imetaja wakristo ambao ni kweli na hawa wanaokula mali za watu pia wametajwa. Ukisoma Quran utapata majibu yote yanayohusu Ukristo. Nawakaribisha ndugu zangu wakristo someni Quran ya kiswahili itawasaidia hata katika kuifahamu ukweli wa dini yenu na viongozi wenu.


QURAN 9: 34
"Enyi mlio amini! Hakika wengi katika makuhani na wamonaki wanakula mali za watu kwa batili na wanazuilia Njia ya Mwenyezi Mungu. Na wanao kusanya dhahabu na fedha, wala hawazitumii katika Njia ya Mwenyezi Mungu, wabashirie habari ya adhabu iliyo chungu."
Wakristo wametajwa wapi hapo mbona kama una jipendekeza kwa wakristo,

Hatuhitaji kurwani kuufahamu ukristo biblia imekamilika katika kila eneo katika imani ya ukristo.

Ni kurwani pekee inayotegemea vitabu tofauti ili kuweza kujitetea bila hivyo ni kitabu cha uongo kilichojaa nadharia nafalasafa za uongo uliopindukia,ni mpuuzi pekee anayweza amini kurani.
 
Hao wala si mitume wala manabii bali majambazi na matapeli wa kawaida wanaowaliza mazwazwa na waliokata tamaa. Ni aina ya viumbe wanaoonyesha uhovyo wa nchi na watawala wake wanaowaendekeza au kuogopa kuwakataza hata kuwakamata kwa vile wote wanacheza mchezo mmoja, wizi wizi ujambazi ujambazi uchawa uchawa ad infinitum.
Wamekata tamaa so wamefuata tumaini,niwin wini situation.
 
Asante mwamposa umetujengea hospital kubwa kyela(mbeya) hospital kubwa kuliko ya rufaa ya mkoa...

Huduma nzuri, umetuletea madaktar bingwa wazungu..mwisho mdogo wangu asiependa biashara umemwajiri kwenye hospital Yako..ubarikiwe sana.

Nimeona huo mkesha wa leo,,kwa makadirio sadaka za leo utatujengea hospital nyingine Tano pale mbeya..usijali wazaramo kulalamika ndio desturi Yao na roho za wivu, sisi tunaona uwekezaji pale mbeya!!
Kama amefanya hivyo basi anauma na kupuliza ili msishituke.
 
Kama kuna watu whuni, wanyama katili na wenye rohombaya sana basi hawa ndugu wanaongoza.

Wao wanachojua ni mashindano yq kukusanya pesa tuu na kuzitumia kwenye mambo binafsi ya kifahari na kufuru ya pesa.

Wanashindana kuvaa mavazi ya bei ghali
Wanashindana kumiliki magari ya kifahari na ya gharama kubwa.

Wanashindana kuwa na mijumba ya kifahari na kila aina ya kitu cha gharama kubwa na cha thamani unachojua wewe. Mtaji wao mkubwa ni waumini na naamini fukara hohehahe wanaowaamini sana!

Kwenye makanisa yao hakuna huduma inatolewa bure.. Hata ile nakala ya fomu ya shilingi 50 au mia ya kuandika shida yako inauzwa si chini ya elfu 50... Na kila fomu ina viwango vya gharama kwa kila huduma utakayo.

Wanaotoa dau kubwa ndio hupewa kipaumbele cha kuonana na mtumishi.. Na mapato yao hayo hayatozwi kodi yoyote ya serikali. Huwezi hata siku moja ukute
Wametoa sehemu ya mapato yao kuhudumia yatima na wajane wasiojiweza.

Huwezi hata siku moja kuwakuta wakijenga vituo vya afya kuwahudumia wasio na uwezo.

Huwezi hata siku moja kuwakuta wakijenga shule na vituo vya huduma za kielimu kama msaada kwa wasiojiweza
Huwezi hata siku moja wakiwa na programu mbalimbali za Kusaidia makundi mbalimbali kwenye Jamii kama wafanyavyo kina Malisa G.J na Lions clubs kwenye nyanja za elimu, makazi, lishe, tiba na matukio ya kibinadamu ya dharura.

Ni wepesi mno wa kufarakanisha na kugombanisha familia, wanandoa, ndugu na jamaa.. Hasa kwa wale wasiopenda mambo yao na kuharibu kuwaelimisha waliokwisha tekwa!

Kukupa tuhuma za uchawi, uongo uzinzi nk kwa wenza wa wengine wao ni fasta sana.. Wameharibu ndoa nyingi na kufarakanisha ndugu wengi sana!

Hawa si watumishi wa kweli maana hawahubiri upendo, amani na mshikamano kwa vitendo
Hawa ni watu wa makafara ya kutisha,ibada za siri, washirikina wakubwa!

Ni wachafu na ni walafi wanaofanya mambo machafu na mabaya kizani..
Kuwanyesha waumini wao vitu vichafu kwao ni kawaida kabisa.

Maji yaliyochanganywa na maji yaliyooshea maiti;
Maji yaliyochanganywa na manii au uchafu uliotoka ukeni;
Maji yaliyooshea miguu au mikono ya nabii au mtume nknk

Ni wezi wakubwa!

Udongo uliochimbwa na scavator na kuusafirisha kwa roli kisha kuwauzia Watu kijiko shilingi elfu moja.. Huu ni zaidi ya wizi na utapeli wa kiwango kikubwa sana

Kuna mafuta ya upako, sabuni za upako, leso za upako.. Nknk vyote hivyo ni biashara kubwa isiyochajiwa kodi yoyote na serikali

Naendelea…
Hawa manabii na mitume wa mchongo wamejaa sana hapa nchini kwa kuwa nchi imesheheni wapumbavu wa kutosha. Wapuuzi hawa huwezi kuwakuta kule Kenya na n nchi nyingine zinazojitambua.
 
Unajua kwanini kina Mwamposa wanateka sana watu!!?
Ni kwasababu anaombea mijibaraka kwa wote, wazinzi, walevi, mashoga, wasagaji, malaya , wezi nyote pale mtapewa mibaraka bila kujali uhusiano wako na Mungu, hutaaswa kuacha ufanyacho na kujikabidhi kwa Mungu kuacha mabalaa yako.

We haijalishi ni mdhambi kiasi gani, hata kama ukitoka kupokea mibaraka ukaenda kufirimbwa bado utautumia udongo/maji/ mafuta ya upako kutatua shida zako bila kufeel guilty ya dhambi uliyofanya.

Ni rahisi kupita njia ya Mwamposa kuliko kujipitisha kwenye tanuri kwa kuacha dhambi zako uzipendazo, ni rahisi tu kwenda kuchukua wese kunyunyiza, sijui kupaka ukinuia kuliko kuacha umalaya na mabalaa yako.
 
Hata siku moja huwezi kumkuta Mwam akikemea matendo machafu yeye Sadaka mbele
Unajua kwanini kina Mwamposa wanateka sana watu!!?
Ni kwasababu anaombea mijibaraka kwa wote, wazinzi, walevi, mashoga, wasagaji, malaya , wezi nyote pale mtapewa mibaraka bila kujali uhusiano wako na Mungu, hutaaswa kuacha ufanyacho na kujikabidhi kwa Mungu kuacha mabalaa yako
 
Hata siku moja huwezi kumkuta Mwam akikemea matendo machafu yeye Sadaka mbele
Hicho ndo wanampendea, watu hawapendi ukweli mkuu.

Na maombi yao makubwa ni kuukemea uchawi na mapepo, vitu ambavyo huwezi viona wala kuthibitisha kua ndiyo vinakuletea matatizo.
Umbali tuliojiwekea na Mungu ndo tatizo, tunataka baraka bila kuacha choyo, tunataka baraka bila kuacha unafiki na umbeya, na vimizigo vingine vidogo vidogo lakini vitamu.
 
Hawa manabii na mitume wa mchongo wamejaa sana hapa nchini kwa kuwa nchi imesheheni wapumbavu wa kutosha. Wapuuzi hawa huwezi kuwakuta kule Kenya na n nchi nyingine zinazojitambua.
Wapuuzi hawa huwezi kuwakuta kule Kenya na n nchi nyingine zinazojitambua.📌🔨
Hata Rwanda pia hawatii pua kule
 
Hili nadhani acha tu kila Mjinga apigwe atajijua mwenyewe maana hamna anayelazimisha watu kutoa izo sadaka.
 
Hawa watu mbona wametajwa kwenye Quran. Quran imetaja wakristo ambao ni kweli na hawa wanaokula mali za watu pia wametajwa. Ukisoma Quran utapata majibu yote yanayohusu Ukristo. Nawakaribisha ndugu zangu wakristo someni Quran ya kiswahili itawasaidia hata katika kuifahamu ukweli wa dini yenu na viongozi wenu.


QURAN 9: 34
"Enyi mlio amini! Hakika wengi katika makuhani na wamonaki wanakula mali za watu kwa batili na wanazuilia Njia ya Mwenyezi Mungu. Na wanao kusanya dhahabu na fedha, wala hawazitumii katika Njia ya Mwenyezi Mungu, wabashirie habari ya adhabu iliyo chungu."
Bora kondoo kuliko mbwa mwitu mkali aliyemezeshwa mistari ya kuuwa wenzie
 
Back
Top Bottom