Mjadala huru: Kwanini vifo vya Mkapa na Magufuli vilifuatana?

Huyu ni mwafrika anayeamini kila kifo kina mkono wa mtu. Covid imeua mabilionea wa Italy na Ulaya nzima ingeshindwa kuwaua wasaidizi wa JPM wa ikulu ya Tanzania!!.

Hizi sababu za vifo vya watu zinazotolewa hapa TZ ndizo zinazowafanya washirikina wakawepo kwa wingi mpaka leo. Msingi wa uwepo wao ni akili zetu mbovu zisizotaka kufikiria kwa kina.
 
Nakuomba ufatilie documentary ya vifo vya ndugu wawili waliokuwa na nguvu kubwa marekani mmoja akiwa Rais huku kaka mtu akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (The Kennedy Brothers) kisha utagundua kuna mambo huwa hayatokei kwa bahati mbaya
Kennedy Brothers walitaka kuwashughulikia mafia wa wakati ule kina Giancana, waligusa mahali pa juu kabisa pasipogusika hovyo. Mpaka leo CIA wanaficha sababu haswa na nani aliyemuua Kennedy Rais.
 
Vipi kuhusu vifo vya wengine ndani ya miezi mitatu. Sasa hivi hakuna kiongozi anyekufa na Corona, ugonjwa wa moyo, ugonjwa wowote.
Ni ugonjwa wa msimu, sio tu kwamba watu hawafi na corona ndani ya Tanzania, dunia kote watu hawaugui tena ugonjwa huu labda utokee mlipuko mwingine.
 
Kennedy Brothers walitaka kuwashughulikia mafia wa wakati ule kina Giancana, waligusa mahali pa juu kabisa pasipogusika hovyo. Mpaka leo CIA wanaficha sababu haswa na nani aliyemuua Kennedy Rais.
Huyu anataka kulinganisha vifo vya akina Kennedy na hawa wa kwetu? Vifo vyao wote ni vya kupigwa risasi hadharani na kwa sababu ambazo conspiracy theories nyingi zimejitokeza.

Hawa wa kwetu mmoja alikuwa 80+ (umri umekwenda) na mwingine alikuwa na pacemaker (matatizo ya moyo) na huku kutwa kucha yuko barabarani (kwa hivyo chances za kupata infection ni kubwa), hivi hapa tena unasema kuna mkono wa mtu ulipita?

Tumuamini Mungu tuepukane na dhana mbovu. Kufa kila mmoja atakufa kwa wakati wake ulioandikwa.
 
Ukifikiria angalau kidogo tu unagundua ukweli kuwa hawa walikuwa viongozi wenye sababu za vifo vyao ingawa kimaadili huwezi kuzianika hadharani.

Mkapa alikuwa na miaka 81 akielekea 82 hakuwa ni kijana kwa namna yoyote ile. JPM kama ulivyosema alikuwa na pacemaker, na kipindi kile cha kampeni za 2020 alikuwa akiugua mara kwa mara.

Kina Kennedy waliruhusu mazingira ya mafia kuingilia uongozi wa juu wa USA, walikuwa ni watu wazima fulani wahuni wasio na maadili wakiwa mbali na kamera za TV lakini zikiwa karibu yao wanageuka ni viongozi wenye heshima. Waliishi aina ya maisha ambayo ni maarufu kwa Kingereza kama DOUBLE LIFE, na matokeo yake yakapigwa risasi.
 
Kifo humpasa mwanadamu kumfika hilo halina ubishi.

Lakini kwa nini kifo cha Mkapa na Magufuli vilifuatana?!
Inawezekana kwa sababu ya janga la Corona au inawezekana kwa sababu ya laana ya utawala wa kidhalimu wa JPM akisaidiwa nyuma ya pazia na BWM

Kazi kwako kuangalia ni ipi sababu kati ya hizo mbili, pia unaweza kuangalia mabadiko hayo[emoji116]


 
Tena bora walikufa
 
Labda walimalizana wao kwa wao na COVID ikafanywa sababu
Why only politicians ndio walipukutika sana
 
Ubishi na jeuri zao

Waliona ni kikohoo ama
Over 70 wamekataa kukaa makwao na kupima upepo mpaka kikawakuta
Wengi walifuata mkumbo likawaondoa na aliekuwa anapinga zaidi likammaliza mwisho
Ila ukweli utakuja julikana tu maana mpaka wazungu walitukanwa sana wakijua fika wazungu kwa fitna ndio wenyewe [emoji23]
 
Hii mada ipo mpaka leo?, Asee Suzy Elias una bahati sana au mods walikuwa lunch/dinner time.

Mada kama hii nimeshuhudia zikiliwa kichwa hata kabla jogoo hajawika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…