Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Hii michango imekuwa mingi sana. Kibaya zaidi ni pale mtu anakutafuta hata kama hamjaongea miaka 5. Na hizi sms za kukumbushia michango zinaudhi sana. Mtu alikuwa hakujulii hali hata siku noma, leo hii unapata sms ya good morning everyday. Unafiki mtupu. Mimi nikioa nitafanya harusi kwa uwezo wangu. Watakaonichangia nitashukuru lakini sitaki ufahari wa kusababisha kero kwa wenzangu.
 
Kinachokera zaidi ni pale unaletewa kadi ya mchango wa harusi ya mtu hata humjui na kupakaziwa maneno ya "ndugu na rafiki wa karibu" halafu harusi yenyewe inafanikia Ukerewe na send off Ukara! Bado utasumbuliwa kwa meseji zikikumbushia, hivi raha za mtu kuoa zinawahusu vipi wengine!!! Cangieni mambo mengine ya maendeleo kama Elimu watoto yatima, wajane na wenye shida na mungu atawazidishia,
 
Niko tayari kuchangia endapo nitapewe mwaliko kushiriki zoezi la kuijaza dunia
 
Kuna sehemu mmeambiwa ni lazima kuchangia?????!!!!
Umewahi kumjibu mtu kuwa hutaki kumchangia na akaendelea kukukumbusha???!!!


Michango sio taabu mnafiki ni wewe uliyepokea kadi ya kwanza mpaka ya tisa halafu unakuja kulalama huku

Olesaidimu mh, hivi unafikiri waomba michango lazima wakupe card mkononi! si unaikuta tu nyumbani au ofisini kama anafahamu hom or ofc iko wapi! culture an kuoneana aibu ndio imetufikisha hapa, tena kuna mwingine hata hajakuzoea kivile, anaanza kujichekesha akijua kesho anakuzukia na card. Sema cha muhimu sasa tuamue kubadilika wote, kuanzia waoaji na waolewaji hadi wachangaji, hii kitu tuikatae tu, kwenye ukoo ukikataa wenzio wakitoa unajua kutengwa? halafu hawakutengi wakikungojea kuoa/olewa au mtoto wako akioa/olewa, wanakutenga hadi kwenye ishu zingine kwamba huna ushirikiano.
Halafu eti budget za siku hizi umeziona 30 to 100m ni sawa kweli? walao kwa usawa huu kama mchango ni 10,000 kwenda mbele kadri ya uwezo poa, watu wanaweka limit utafikiri wamekutafutia kazi au wamekusomesha! its high time we Tanzanians to change.
Hata misiba nayo haihitaji ufahari, tumepoteza ndugu,rafiki, wafanyakazi wenzetu ni huzuni, mbwembwe za nini? wengine wanashona nguo, sare, watu full demonstration na mapose why? sasa mwingine afe mwingine afanye marketing ya sura jamani? Mabadiliko yaanze kangu kwako na kwa wote
 
KWELI JAMANI ASANTE MDAU kwa mada.mimi inanikera sana siku zote mtu hakutafuti kabisa ikikaribia harusi yake anajifanya kukukumbuka ili mwisho wa siku uchange.kila siku msg za kukumbushia michango hadi kero mishahara yenyewe midogo majukumu kibao.akhaaaaa.......tupumzisheni kidogo raha mpate wenyewe usiku kucha.
 
Na wote wanochangia hii mada waliooa na kuolewa walichangiwa lol mbona mnakuwa wachoyooooooooooooo embu tuchangieni na sisi alafu tukiwa ngoma droo wote tuacheeeeeeeeeeeeeeeeeeee.
 
Kama ulichangiwa jiandae kulipa madeni ya watu,
 
Ndiyo majukumu yenyewe hayo. Mbona mkialikwa kwenye kikao mnapleji mahela kibaao, huku jukwaani mnalalamikia kadi.....

Na wanapigiwa makofi kwa mbwembwe na ukizingatia kikao cha kwanza kuna makulaji na manywaji ya bwerere, ukitakiwa ukamilishe ahadi yako unaanza kulalamika, pleji hata elfu kumi au tano kulingana na uwezo wako
 
Yaani hii makitu nilishaikataa longtime, potelea mbali japo imenifanya baadhi ya watu wanichukie kwa kutochangia harusi zao! Urafiki wa namna hii ya kuchunana kinamna siutaki, bora nikusaidie wakati wa shida, kama hauna uwezo, kwa nini utake li-harusi kuuuuubwa?
 
This is stupidity of africans, kutwa kucha ni kuwaza harusi n sherehe, hamna kingine cha maana, msimu mzima ni vikao vya kamati tu,
UJINGA!!, say NO to michango ya harusi.
yaani me jamani niliachaga kuchangia harusi atakae nichukia poa tu. Sababu mimi mwenyewe nafight kupata maendeleo kamshahara kadogo bado hakohako nianze kugawa eti kufanikisha kuona kwa watu wengine nimejuana nao miezi michache tu. Lo! Sifikirii kumchangisha mtu kwenye harusi yangu nitakaoweza kuwaalika ndo haohao. Harusi zenyewe tunupoteza pesa na muda mwingi alafu zinadumu kwa muda mfupi. Aaaagh! Sitoka nichange.. tubadilike jamani,hii nchi.....
 
Ni utamaduni wa kuzika kabisa huu wa kugongea fedha ya kuoa. Mbaya zaidi hata kama huna kabisa tayari mtu anakuwekea bifu ambalo haliishi moyoni mwake as if alikuwa anakudai. Mwingine akiwa tu na namba yako hata kama hakujui kivile atakusumbua huyo!
 
Si wewe tu utakuja jamaa na tumbo kubwa linakuletea kadi tena na kiwango wamekiweka,baadae kila siku linakuja kudai! Mimi hadi nimevunja urafki na rafki yangu baada ya kumwambia kwa sasa sina. Hivi nauliza unaponidai kama nimekopa FINCA utaniazima mke wako japo usiku mmoja?
 
Unasapoti tuchangie sawa, shemu na yeye tuchangie? Au ndo methali isemayo mzigo wa chizi huishia kichwani?
 
Hii mada nadhani ni mara ya 10 kama si zaidi kuwekwa humu!!!!. Mkuu kama mtu anakukera mpe laivu, kuja kulalamika lalamika hapa hakusaidii kitu. Kama hutaki kuchanga acha PERIOD.
Na wewe KJ tu huna lolote. Sikiliza kibao "majanga" labda utaelimika
 

Mkuu ulichokisema ni kweli ila pia kujitenga sana na jamii iliyokuzunguka si vyema hata kama hutaki jumuika nao hata kwa shingo upande tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…