Vijisenti kama uliozeshwa ndoa ya mkeka hilo ni lako. watu lazima tuonyeshe solidarity kwa kuchangiana.
wewe katika kuchangia harusi mimba inakukwaza nini?!! binafsi huwa sichangii kabisa harusi, ukiniletea kadi ya mchango iliyoandikwa na kiasi sichangi kabisaa, ni heri uiandike kama kunijulisha tu kama nitajiskia kuchangia nichangie chochote, siyo uniambie double laki moja, single elfu hamsini...wtf!! yaani mimi kuja kuhudhuria harusi yako mpaka nichange, kwa umuhimu upi ulionao?!!! fanya harusi iliyo ndani ya uwezo wako, vijijini harusi hazina kadi na wanakijiji wanakula wanakunywa na kusaza, mtu analisha kijiji kizima sembuse mjini ambapo hata ukitoa kadi vinywaji kujitegemea marafiki watafika tu, cha muhimu ndoa, harusi mbwembwe!
yaani tatizo lako wewe ni mimba umesahau kuwa mimba ni matokeo ya sex, mtu akibort je achangiwe? au wanao sex bila mimba je wachangiwe? Nazani kama unataka kuisaidia jamii ni kuuangalia mzizi wa tatizo sio matokeo ya tatizo. Sishabikii watu waolewe na mimba ila sioni kwa nini iwe ni tatizo kama kuna aliyeolewa na kaabort. Kama unamchangia mtu, mchangie tu na kama hutaki usitoe tu, mimba isiwe sababu.huu mchezo uliozuka sasa wa watu kupeana mimba kwanza kisha ndiyo kuanza kutukaba tuwape michango ya harusi mi sikikubali hata kidogo. Huu siyo utaratibu mzuri kabisa ambao sisi watanzania inabidi tuufuate.
Ndoa nn harusi nn changanua
Hiyo ndio shida ya umasikini,ukiwa na pesa vyote unafanya Wenyewe halafu unakaribisha watu kunywa tu.
dah, we ni mtanzania kweli kaka?! ndoa ni ahadi, harusi ni sherehe.
wala shida siyo umaskini, shida ni ufahari!
wewe katika kuchangia harusi mimba inakukwaza nini?!! binafsi huwa sichangii kabisa harusi, ukiniletea kadi ya mchango iliyoandikwa na kiasi sichangi kabisaa, ni heri uiandike kama kunijulisha tu kama nitajiskia kuchangia nichangie chochote, siyo uniambie double laki moja, single elfu hamsini...wtf!! yaani mimi kuja kuhudhuria harusi yako mpaka nichange, kwa umuhimu upi ulionao?!!! fanya harusi iliyo ndani ya uwezo wako, vijijini harusi hazina kadi na wanakijiji wanakula wanakunywa na kusaza, mtu analisha kijiji kizima sembuse mjini ambapo hata ukitoa kadi vinywaji kujitegemea marafiki watafika tu, cha muhimu ndoa, harusi mbwembwe!
wazee wenu walichangisha UMMA au ni immediate family ndio iliwajibika?My note: tujaribu kuangalia wazee wetu waliishije na walifunga vipi ndoa zao kwa maadili yapi.
Ushaoa lakini!!!Mi sichangii harusi ng'o, na wengi wananinunia eti kisa sijachangia harusi zao shenzi wala sina habari ukinuna nuna tu.
Yaani nikipata m/ke asiyependa miharusi nitafurahi!!!!!!!!