Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Nina wazo nataka kuchangia,swala la ndoa ni deni kwa mwenyezi mungu hivyo kila mtu lazima afunge ndoa,ili tuepukane na uzinifu,na swala la mtu asichangishe watu eti kisa raha atapata yeye mimi binafsi naona ni roho ya kimaskini na choyo na pia kujifanya tumeelimika sana bila kujali kuwa ni upuuzi kwa kuongea swala ambalo watu waliosoma wenzio wakilichambua wanakuona umetoa uzi wa kipuuzi,uchumi wa nchi,mifuko imetoboka,hali mbaya lazima mtu achangishe kwa wadau wake wakaribu na si lazima unaweza usitoe,kuna swala la kadi,mtu anasambaza kadi kwa watu wa karibu sana ambao ni uhakika na waliokaribu lakini sio sana sana ambao sio wa uhakika sana zinaitwa kadi za kubahatisha sasa nadhani wewe mtoa mada upo kundi la pili la watu wa kubahatishwa
Bro wewe kama kweli ni msomi basi usomi wako huutendei haki.
Watu mnataka sifa sana na hii ndio inawapelekea kufanya huu ijinga wa harusi ambazo hamna uwezo nazo kisha unaanza kusumbua kila unaemjua.
Hakuna msomi anayeweza kusanya from 1M to any amount for months kisa akaisaga ndani ya saa halafu ukasema huyo ni msomi(huyo mwite mjinga).
Ndoa ni pale unapofungiwa kanisani /msikitini .
Mtu unatumia milioni 10 ndani ya masaa halafu kesho unaanza kusumbua watu wakukope huu ni ujinga wa kutaka sifa
 
Kuna wakati hata mimi nilikuwa nadhani hivyo...

Lakini baadae nimekuja kugundua hapana. Kuchangiana ni muhimu. Nafahamu watu ambao hawana tabia ya kuchangia mtu. Lakini nikiangalia maisha yao wala hawana maendeleo zaidi kushinda wanaochangia

Kusaidiana kwenye harusi kwa kuchangia na au kushiriki kwenye shughuli za maandalizi

- Ni njia nzuri ya kupunguziana mizigo
- Ni njia nzuri ya kuonyeshana upendo
- Ni njia nzuri ya kukutana na marafiki (kwa sasa nina marafiki wengi wafanyabishara, watu wa TRA, askari, madaktari, wafanyakazi wa idara tofauti kwenye taasisi ninayofanyia kazi, wanasiasa nk (nisisitiza hii nk)) ambao nillikutana nao mara ya kwanza kwenye vikao vya harusi za ndugu, jamaa na marafiki. Marafiki hawa wamenisaidia kwenye mambo mbali mbali kama elimu na ajira ya ndugu zangu, biashara zangu, kazi zangu za ofisini, afya, matatizo ya usalama nk...

Tupende kuchangia na kushiriki kwenye vikao vya harusi
 
Kama ni harusi ya watu wa karibu pekee ni sawa, haina umuhimu wa kuchangisha lakini familia na koo zimetofautiana sana. Kuna familia ni kubwa na socially wapo close sana linapokuja suala la harusi ya mwanafamilia linakuwa ni suala la familia kuanzia muundo wa sherehe including kualika marafiki ya familia. Katika familia kama hizi kuchangisha haikwepeki.
 
Lakini sijui uwezo wako mheshimiwa labda upo kwenye kundi la watu waliobahatika kuila keki ya taifa,ila na mimi mwanzo nilikuwa na akili ya kitoto kama yako ila now nimekuwa,na pia ukigombana na mkeo unashirikisha watu?!?!
 
Kwanza naomba nimuite mtoa mada MPUMBAVU uliyeelimika kwa shida sana na ukashindwa kuitumia elimu yako vizur...swala la kuchanga harusi ni utaratibu tuliojiwekea watanzania na tunautekeleza kwa moyo mmoja kama huupendi kaishi kenya hamna kuchangia harusi!! Ujue ipo siku na wewe utahitaji hii support kwa njia moja au nyingine,utayakumbuka haya maandishi yako kuwa hutak kuchangia harusi.

Usiniwaze kama huwezi kujiwaza.

OOh give me a break; na uondokane na mawazo mgando. Naomba niite hoja yako kuwa kuwa inakinzana na elimu uliyonayo . Tena aliyeelimika kwa shida sana hawezi kuwaza kuchangia sherehe ambazo mnakula na kunywa na ndani ya 3 hours hela imeisha na hakuna any return on investment done. Aliyeelimika hawezi kupanga spending 10 M which he has less than 1% of it expecting to beg the rest of the 99%. Aliyeelimika: Anawaza michango inayogusa wengi (mfano ukimsaidia mtu shule umesaidia jamii yake), ukisaidia wazo la maendeleo umeokoa jamii, ukisaidia mgonjwa umereturn working capital and the list is endless.

Sijui unatumia elimu gani uliyopata kuwaza kuwa the best social thing u can do ni kuchangia harusi inayohusu watu hao wawili wanaojua fika kuwa suala lao si dharura, wanajua fika wanaishi nyumba ya kupanga, wanajua fika kipato chao hakizidi milioni na bado wanataka kutumia milioni kumi for A SINGLE DAY. Yuko radhi marafiki waone kuna bia na gari zuri ilhali kesho haijui itakuwaje, anarudhi kwenye same life huku jana ametumia TEN MILLION ZA WATU . To me this is the biggest abuse of peoples money u can ever do. Definition ya elimu na maarifa unayopata ili kukuwezesha kupambana na mazingira yako. " KUPAMBANA " Kuishi within your means , sio kupambana Kudai hela za watu for your wedding.

Utaratibu huu umejiwekea wewe na watanzania gani, wa aina gani? Una uhakika wanatoa kwa roho nyeupe?
Its just a matter of planning , unajua huna uwezo basi usisumbue watu , mtu unapiga simu kudai michango kama deni vile. Kama unataka harusi ya 10 M na wewe hata nusu huna unaanzaje kuwapangia watu kuwa kima cha chini ni laki ? Michango hii hii imefanya tukosane na ndugu na marafiki. Una rafiki wa dhati kabisa kisa hajakupa kima cha chini eti hawezi kuwa mshiriki wa sherehe yako, na unaishia kualika watu pengine hata sio close friends au ndugu kisa tu wametoa kiasi cha kadi?????? madness???? Wacha watu out of goodwill waone nia ya kukupa hata zawadi ili harusi ifane.

Pili: Kuna mambo mengi mazuri ya kusaidiana , Magonjwa, elimu , miradi NK nadhani hii ingepewa kipaumbele.Ukijikita na mawazo mgando haya kuwa sherehe utachangiwa u better think twice. Ninafahamu watu wengi tu wa dini zote waliofanya harusi simple bila kuchangisha na wana maendeleo mazuri tu na wanaishi vema na jamii. So d'ont try to fool us kuwa ni utaratibu mmejiwekea watanzania .
 
Lakini sijui uwezo wako mheshimiwa labda upo kwenye kundi la watu waliobahatika kuila keki ya taifa,ila na mimi mwanzo nilikuwa na akili ya kitoto kama yako ila now nimekuwa,na pia ukigombana na mkeo unashirikisha watu?!?!

Kwa hiyo kuchangia na kuchangisha watu michango ya harusi ndio mawazo ya kikubwa?. Jaribu kufikiri kwa kutumia kichwa tafadhali.
 
Mawazo potofu hayoo.. nadhani tatizo sio kuchangia harusi bali ni kiasi cha mchango kama mchango ni kias kidogo cha wastani hapo kama mtu mzima hamna tatizo but pale iiNapokuwa mchango ni kiasi kikubwaa saana ndo shidaaa,

Kutoa ni moyoo mchangiee ndug na jAmaa yako bhanaa acha imani potofu
 
Mwambie tu kwamba hufagilii michango ya harusi.

Tatizo michango hampendi halafu kulalamika.mnakija kulalamikia JF.

Jamii yetu inagubikwa na kutokuwa na uwazi.

Ukifanya harusi bila kuchangisha watu utaambiwa unajisikia, ukichangisha watu unaulizwa kwa nini uchangishe watu kwenye harusi yako.

Ingawa inaweza kuwa socially awkward kukataa kuchangia harusi, kama michango inakukera kweli, unatakiwa kusema hilo na kukiweka wazi kwa wahusika.

Wakijua hilo kesho hata kadi ya mchangi hawatakupa.

Kitu ambacho kitamaanisha hata kadi ya harusi unaweza usipate.

But I guess you are not too big on weddings.
 
OOh give me a break; na uondokane na mawazo mgando. Naomba niite hoja yako kuwa kuwa inakinzana na elimu uliyonayo . Tena aliyeelimika kwa shida sana hawezi kuwaza kuchangia sherehe ambazo mnakula na kunywa na ndani ya 3 hours hela imeisha na hakuna any return on investment done. Aliyeelimika hawezi kupanga spending 10 M which he has less than 1% of it expecting to beg the rest of the 99%. Aliyeelimika: Anawaza michango inayogusa wengi (mfano ukimsaidia mtu shule umesaidia jamii yake), ukisaidia wazo la maendeleo umeokoa jamii, ukisaidia mgonjwa umereturn working capital and the list is endless.

Sijui unatumia elimu gani uliyopata kuwaza kuwa the best social thing u can do ni kuchangia harusi inayohusu watu hao wawili wanaojua fika kuwa suala lao si dharura, wanajua fika wanaishi nyumba ya kupanga, wanajua fika kipato chao hakizidi milioni na bado wanataka kutumia milioni kumi for A SINGLE DAY. Yuko radhi marafiki waone kuna bia na gari zuri ilhali kesho haijui itakuwaje, anarudhi kwenye same life huku jana ametumia TEN MILLION ZA WATU . To me this is the biggest abuse of peoples money u can ever do. Definition ya elimu na maarifa unayopata ili kukuwezesha kupambana na mazingira yako. " KUPAMBANA " Kuishi within your means , sio kupambana Kudai hela za watu for your wedding.

Utaratibu huu umejiwekea wewe na watanzania gani, wa aina gani? Una uhakika wanatoa kwa roho nyeupe?
Its just a matter of planning , unajua huna uwezo basi usisumbue watu , mtu unapiga simu kudai michango kama deni vile. Kama unataka harusi ya 10 M na wewe hata nusu huna unaanzaje kuwapangia watu kuwa kima cha chini ni laki ? Michango hii hii imefanya tukosane na ndugu na marafiki. Una rafiki wa dhati kabisa kisa hajakupa kima cha chini eti hawezi kuwa mshiriki wa sherehe yako, na unaishia kualika watu pengine hata sio close friends au ndugu kisa tu wametoa kiasi cha kadi?????? madness???? Wacha watu out of goodwill waone nia ya kukupa hata zawadi ili harusi ifane.

Pili: Kuna mambo mengi mazuri ya kusaidiana , Magonjwa, elimu , miradi NK nadhani hii ingepewa kipaumbele.Ukijikita na mawazo mgando haya kuwa sherehe utachangiwa u better think twice. Ninafahamu watu wengi tu wa dini zote waliofanya harusi simple bila kuchangisha na wana maendeleo mazuri tu na wanaishi vema na jamii. So d'ont try to fool us kuwa ni utaratibu mmejiwekea watanzania .

Mi nadhani mjomba asiyekuelewa is out of place and out of time at the same damn time! Unaeleweka sana sema watu wanajitoa ufahamu tu! Ndo maana kabla ya kuanza kuwasumbua watu na simu ,message zisizokwisha utadhani unadai madeni kwanza jipange ndugu. Jikamilishe zen watu wata do the rest. It's really the biggest abuse of folks money, especially wewe mwenyewe mwenye shughuli ukiwa below that amount. Unachoma leo 10mls afu kesho warudi kwenye nyumba yako ya kupanga na madeni juu. Mi nimekuelewa sana.
 
hahahaha
hlo nalo neno,
siku hiz michango imekuwa mingi mpaka inaboa...
Sherehe kubwa ya harusi sio lazima, kama huna hela fanya tafrija ndogo tu, tusiumizane wacha tuwekeze kwenye mambo ya maan, ndo zenyewe zinvunjika kila iitwapo leo....
 
Sometimes michango inaleta uhusiano mzuri baina ya ndugu na marafiki,wengine fahari yao ni kuchangiana,kwani michango lazima bhana kama hutaki unaacha,kwanza michango mingi si ya kushtukiza unaambiwa kabla,sasa kama mchango tu kumsaidia ndugu yako au rafiki hutaki je utaishije na majirani katika kusaidiana.
 
Binafsi sioni tatizo la michango ya Harusi, nachoona hapa ni tatizo la wabongo wengi kutokupenda kuwa wa wazi na wa kweli, kwanini mtu usijiwekee utaratibu wa kusema hapana kwani lazima uchangie kila kitu?
"The man who complains about the way the ball bounces is likely to be the one who dropped it."
— Lou Holtz​
 
Mleta uzi, inaonekana wewe umeshaoa siku nyingi bila kufuata utaratibu rasmi, sasa ynaona wanaotaka kuoa kwa utaratibu rasmi wanakusumbua.

Anyway, kuwachangia sio lazima, ukipewa kadi usipeleke mchango, ukialikwa kwenye kikao usiende. Lkn kumbuka kuna siku utahitaji watu wakuchangie michango.

Vv
Kuchangia sio mbaya ila kunataasisi wanalazimisha sana haya mambo
Kuna sehem nilifanya kazi mkuu wa idara kidogo anifukuze kazi sababu sikuchangia harusi ya mwanae .
Kuna mambo ya msingi ya kuchangia kama magonjwa ,
Shule na matatizo mengine kwenye jamii . Nashangaa jinsi tunavojitahidi kuchangia Arusi kuliko wagonjwa wetu wanaohitaji msaada wa upasuaji
 
Back
Top Bottom