Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Jana tu nimemwambia rafiki yangu mmoja sitaweza kukuchangia kwa vile nina majukumu muhimu kwa familia yangu...jibu lake lilikuwa "kwa kweli sitakuelewa" Nikamwambia huo ndio ukweli nina malengo ambayo siwezi kutoa hata 10,000/= kwa ajili ya jambo tofauti kwa sasa. Akasema ananiachia uamuzi huo mwenyewe - Nahisi kanielewa na urafiki utaendelea.
 
tujifunze kujitegemea kwa vitu ambavyo havina faida, harusi ni overnight tu....sichangii ng'o....tamaduni nyingine ni za kuachwa kama hii
 
Lakini sio ishu sana kwa mtu wako wakaribu kumchangia
kwa malalamiko haya mwishowe mtaanza kuona uvivu hata
kutoa sadaka ukiwa nacho unatoa tu haina majasho!!!!
 
kweli michango imeshakua tatizo la kijamii, mtu akikupa card anakudai utafikiri kakukopesha huo mchango sasa anataka hela yake maana hutapumua.
 
too much hela hakuna michango mikubwa wanafaidi wanakamati mwingine unaishia kula vitakataka ambavyo hata kumi elfu havifiki lol! i cant, mie wala sitafanya harusi ya style hii sababu kama harusi za ufahari zilisha kuwepo toka enzi za kina mbiliabeli, unakuta lijitu umelichangia 50,000/ alafu mwezi mmoja yameachana lol whatzc?
 
jukumu la harusi ni la bwana arusi na nduguze. Turudi kwenye sherehe za kimila.

Nimekusoma sana bujibuji, hata ulipouliza utamaduni huu ulitoka wapi, nadhani haihitaji kuumiza kichwa - HUU NI WA KUTOKA UZARAMONI- kwa watanizangu. Angalia kuanzia zile ngoma za kumtoa mwali, jando na hatimaye harusi, ni kwamba wanachangiana kwenye koo zao na kuhakikisha shughuli nzima inanoga na kuweka rekodi fulani (sifa ni muhimu hapa). Kwa kuwa wazaramo ni wenyeji wa pwani hususani dsm utamaduni huu umekuwa ukiboreshwa siku hadi siku na hivyo kuvutia watu wa makabila mengine waishio dsm.

Siku za mwanzo shughuli zote zilikuwa zinafanyika nyumbani kwa mhusika, lakini kadili miaka ilivyosonga ukichanganya na mabolesho ya kutaka kuvunja 'rekodi' polepole zikaanza kutafutwa kumbi za kufanyia sherehe, ukizingatia wengine ni wapangaji tu kwenye nyumba wanazokaa hivyo hawezi kwenda na cherekochereko za ngoma na midundiko mtaani kwake 'mtogole' ... kilichofuata hapo kila mtu anajua, kwamba inafika mahali kumbi zimejaa miezi 3 mbele.
Basi mimi huwa nawauliza jamaa zangu kuwa ikiwa wewe una mpango wa kuoa na unahitaji mfano hizo 10 m unaomba kuchangiwa, na mimi nina mpango wa kununua gari kwa hiyo hiyo 10 m atanichangia nani. Mpango wa kuoa ama kuolewa ni wa mhusika mwenyewe na nduguze wa karibu
Nakubaliana na wale wanaosema tuchangie kwenye elimu na maendeleo hiyo ndiyo sahihi, tuendelee kuelimishana tu .

Amani yetu inatumiwa vibaya.
 
Lakini sio ishu sana kwa mtu wako wakaribu kumchangia
kwa malalamiko haya mwishowe mtaanza kuona uvivu hata
kutoa sadaka ukiwa nacho unatoa tu haina majasho!!!!
hiyo hummer kwenye avatar ni la kwako ...na uliza tu
 
kweli michango imeshakua tatizo la kijamii, mtu akikupa card anakudai utafikiri kakukopesha huo mchango sasa anataka hela yake maana hutapumua.
Nasikia ukiipokea tu tayari ni deni na usipo irudisha itabidi aliekupa alipe kimo cha chini....
 
Mimi naona kuchangia ni vizuri, ila ni kuangalia mfuko wako kwanza, wakisema minimum 50,000/= na we una 20,000/= toa tu kisha ukumbini si lazima, cha msingi hudhuria tukio la arusi mfano kanisani au msikitini kama wanaruhusu wasio wa dini hiyo kuingia kwenye hiyo ibada!
 
Yes umesema! But can we do without it?

I think we should contribute where we can and to the people we are close....

Ama sivyo, utahama mtaaa... mimi nika kadi 10 za michango kwa sasa, na sijui nichange zipi niache zipi????
 
Kuna bwana mmoja harusi yake ilikusanya zaidi ya milioni 45, ndoa haikufika hata mwaka


and the list is endless.. watu wa design hii ni kama ma celebrity wa Hollywood....wao kuachana ni kawaida kabisa, ndoa za mikataba...
 
Lakini sio ishu sana kwa mtu wako wakaribu kumchangia
kwa malalamiko haya mwishowe mtaanza kuona uvivu hata
kutoa sadaka ukiwa nacho unatoa tu haina majasho!!!!

Kwa hadhi yako, hutakiwi kabisa kukimbia michango midogo midogo! You are driving a 500 millions car, no problems...
 
Bora uchangie anayeoa kwa mara ya kwanza, kuna msg kila baada ya siku mbili jamaa aliwahi kuniomba mchango wa jubilee ya ndoa miaka 50, na leo nimepokea msg ya jubilee ya ndoa ya miaka 60. Baya zaidi yuko bush ambako hata kigeregere siwezi toa. Si afanye inayo lingana na uwezo wake? Mtaani noma, make ubatizo, kipaimara, kuvunja ungo, kuingia kwenye nyumba mpya, kumaliza darasa la saba, form iv, vi, na degree, wote wanataka michango, kama ya pinda vile!
 
Ni kipindi kingine cha mwaka ambapo kila mwisho wa mwaka kadi za michango ya harusi inakuwa mingi, inakuaje mtu anataka kufanya sherehe kubwa na hana uwezo?

Kwanini usifanye hiyo harusi kutokana na uwezo wako ulionao, ni mpaka usumbue watu wakuchangie?

Tena kinachoudhi ni mtu ameshakaa na mke/mme na wana watoto anataka kupasha kiporo chake nae anataka afanye sherehe kubwa na anachangisha!!

Na kero nyingine mtu anakupa kadi ya mchango wa ndugu yake ambaye humjui.

Sijawahi kupewa au kuona mtu akichangisha kwa ajili ya maendeleo kama vile ada ya shule etc kama majirani zetu na harambee zao zenye maendeleo, sijui wenzangu mnafikiria vipi.
 
ni kipindi kingine cha mwaka ambapo kila mwisho wa mwaka kadi za michango ya harusi inakua mingi, inakuaje mtu anataka kufanya sherehe kubwa na hana uwezo?? kwa nini usifanye hiyo harusi kutokana na uwezo wako ulionao, ni mpaka usumbue watu wakuchangie??? tena kinachoudhi ni mtu ameshakaa na mke/mme na wana watoto anataka kupasha kiporo chake nae anataka afanye sherehe kubwa na anachangisha!!! na kero nyingine mtu anakupa kadi ya mchango wa ndugu yake ambaye humjui. Sijawahi pewa au kuona mtu akichangisha kwa ajili ya maendeleo kama vile ada ya shule etc kama majirani zetu na harambee zao zenye maendeleo, sijui wenzangu mnafikiria vipi.

Hili jambo linakera sana...Kama hatutabadilika tutaishia kufa kwa BP baada ya kustaafu kwa sababu tunashindwa ku-save kwa sababu ya hizi gharama zisizo za lazima.

Siku hizi watu wameamua pia ku-complicate mambo ya mazishi...Shame on us!
 
Ndugu wana JF, hili suala la michango ya harusi naona hivi sasa inashika kasi kwa kasi ya ajabu, nikifikiria kwa makini kabisa naona ni kitu ambacho hakina tija hata kidogo, kwana mwisho wa siku zinapatikana pesa nyingi sana ambazo zinaenda kuteketezwa kwa anasa ya siku moja tu. Wakati huohuo unakuta mtu unamichango lukuki kwa mwezi, mpaka unatoa michango karibu nusu ya mshahara wako, hivyo tunajikuta tunafanya kazi ili kuziendeleza hizi anasa zisizokuwa na maana.

Mimi napendekeza, kama mtu unataka kuoa hakikisha umekusanya pesa za kutosha kulingana na aina ya sherehe unayoitaka. Mtu unataka kufanya harusi ya Mil 30 halafu wewe mwenyewe una laki tano, huku ni kuwapa stress watu wengine tu. MKE NI WAKO, KUOA UMEAMUA WEWE MWENYEWE,KULALA UTALALA NAE PEKE YAKO, HALAFU MIMI NISIPOKUCHANGIA HELA UNANINUNIA.

kUANZIA LEO, MIMI NITAPOKEA KADI ZA MICHANGO YA VITU VIFUATAVYO:
1. Kuchangia Ada mtu aliyepungukiwa
2. Mgonjwa anayehitaji huduma ya dharura ambayo ni ghali
3. Misiba
4. Na vitu kama hivyo

Hii ni kwa sababu, mengi ya mambo haya yanakuja bila ya muhusika kujiandaa kifedha na masuala mengine, na yasipotatuliwa basi tunampoteza mwenzetu in case ya ugonjwa, au mtoto atashindwa kwenda shule. Lakini Harusi, watu wanakuwa wameshafanya uzinzi weeee, wakinogewa basi wanapanga tufunge ndoa mwezi ujao. Hili ni suala ambalo mnatakiwa mjiandae wenyewe, na ufanye kulingana na uwezo wako!!!

WATANZANIA MICHANGO YA HARUSI NI KERO SANAAAAAAAA!!!!!!
 
Back
Top Bottom