Mjadala kuhusu Babu wa Loliondo na dawa yake.


Acha uzushi, huna hata aibu kupotosha umma, yaani umepinda mgongo kuandika upupu, shwain
 
Angekuwa Sheikh Yahaya ungesema "Abracadabra"?
 
Nashangaa kuona wapo wa2 wanageuza eneo hli kuwa uwanja wa ma2c, ugomvi na fkra mgando. Coni sababu ya wao kutukanana... Mazee ths is the GREAT THINKERS FIELD. Mmeshndwa kufkr kwamba swala la kwa babu lpo kiiman zaid.. Hebu fkr kwann kama hao wanasayans waliotumwa walsema ni "sumu" iweje serkal iruhusu watu kuendelea?

Mjengwa! Hoja ya kwamba hakuna mtu aliepona na kujtokeza kukr hlo sion msing wake kwan kama umeweza kunukuu vtabu mbalmbal bas hata magazet unasoma ambayo meng yameandka ushuhuda wa weng wao, mi mwenyewe shangaz yangu alkuwa na presha na ksukar na sasa ni zaid ya mzma, kunamama (jiran yetu) alkuwa na cancer ya kzaz kwa kias kwamba hadi tumain la maisha llshapotea, sahv ni mzma na anafanya mambo yake peke yake.
Ni kwel kwamba hata biblia imeandka kuhusu siku za mwsho na mambo yatakayotokea, manabii wa uongo ni sehem mojawapo lakn biblia hyo hyo imeandka kuhusu kla m2 na kpawa alchopewa na mungu istoshe kla mtu yupo dunian kwa kusudi maalum la mungu. Na hvo Mungu pekee anajua namna ya kuwasliana na watu wake kuwatuma kutimiza kusudio lake.
Sikunym wala kukulazmisha kuwaza niwazavyo mimi
 

So wewe unaamini kwa sababu ya umati wa watu wengi unaoenda huko?
 
Maggid, abracadabra kali zaidi ni jinsi Watanzania walivyoweza kudanganyika kiasi cha kumpa mtu kama Kikwete madaraka. Angalau kwa 'Babu' wa Loliondo kuna hiari, tumaini na unafuu hata kama ni wa muda but for now who really really knows !
Well said.
 
Hivi ni lini atatokea "babu" mwingine atakaetuletea tiba ya matatizo ya kijamii? naombea atokee "babu" aje na dawa ya mgao wa umeme, foleni zisizoisha, dawa ya maji ya uhakika, utawala bora na kuutokomeza ufisadi.

Nadhani atakuwa kesha oteshwa ila time will tell.

My take.

Ya babu wa loliondo inathibitisha kuwa matatizo yetu hayataweza kuja kutatulika kisayansi ila kwa "ABRAKADABRA"
 
Magid, unapotumia kalamu yako kupotosha watu si vyema na hauwatendi haki, watu wanaoishi kiimani, wewe ni mwislamu, hata siku moja hauwezi kuishi kwenye imani ya kikristo, katika ukristo kuna maono na kuna kutokewa na roho mtakatifu, sasa ni vyema jambo usilolijuwa ukakaa kimya kuliko kudandia treni kwa mbele, hivi wewe ukiwa kama muislamu utajisikiaje mtu akisema marehemu mtume Muhamad SAW, ingawa ni kweli hayuko duniani? acha kukebehi imani za watu. sheikh Yahya miaka nenda rudi anafundisha watu hadharani jinsi ya kutengeneza majini na hatujawahi kuwasikia mkisema akadagabra, leo mchungaji anatoa dawa bure kwa sababu ya udini uliokujaa imekuwa nongwa, nakupa changamoto nenda kwa JK KWA SABABU HUWA ANAKUTUMIA SANA PALE ANAPOKUHITAJI, na umuulize ile dozi aliyokunywa kwa babu imemsaidia au hamna kitu?
 
MAGGIJ, vipi mbona umekimbia, au ndo abrakadabra
 
Inashangaza sana kwa makala hii kuwa kali kiivyo. Kwani huyu mleta mada kaingiliwa kiasi gani na mwinjilist hadi kumdamkia? Kuna msemo wa wahenga husema, waache wafu wawazike wafu wao. Tena kelele za chura hazimzuii tembo kunywa maji.
 
Hod hodi Jf mimi ni mgeni humu nawasalimia.

Nimevutiwa na hii topic ya Babu wa Loliondo. Baba yangu mzazi ameenda huko siku tatu iliyopita. Anaugua cancer ya mifupa na kisukari. Mimi nimeokoka na baba yangu ni mkatoliki. Baba yangu aliombewa na kupona maumivu yaliisha na afya yake ikawa inaendelea kutengamaa. Sasa kwakua giza na mwanga haviwezi kukaa pamoja nilimshauri baba asiende kwani mm nilikuwa naona anahisi tu kwamba hajapona kutokana na ukubwa wa magonjwa aliyokuwa nayo kwahiyo hisia zake ndo tatizo. Ilikuwa aende wiki moja iliyopita. Nikaomba Mungu, anipe ishara kama hayo si mapenzi yake na tukatukabaliana na Mungu itokee pingamizi, kesho yake serikali ikatangaza imesitisha huduma ya babu. Hiyo ikawa kwangu uhakika kuwa hapo kuna walakini. Nikamshukuru Mungu kwa hilo. Baada ya siku mbili hilo tangazo sijui ikawaje nikaona baba na kaka yangu wanapanga safari. Nikamsihi sana baba asijepoteza utukufu wa Mungu kwa kuabudu miungu mingine asiyoijua, baba akakubali kaka yangu akakataa. Sasa nimewaambia kati ya Mungu wa Loliondo na wakwangu kama hawatendi kazi na roho mmoja mmoja lazima awe mwongo na kama ni roho ile ile basi baba afya yake itatengamaa. Kama sivyo lazima ugonjwa uzidi kuliko ulivyo mwanzo nahapo Mungu wangu mimi nitamwita kushuhudia kuwa ndiye Abba na Yehova Yire (Mungu mponyaji).

Nitaleta huu ushuhuda. Iwapo baba atapona basi huyo Mungu atakuwa ndiye Mungu wangu pia hivyo nitarudi kumshuhudia hapa na nitampa sifa na utukufu na aibu yangu nitaitangaza ili yeye abakiye mwenye kuabudiwa na kutukuzwa. Kama siye basi hali ya baba nitaithibisha kwenu na baada ya hapo nitamwombea na kuondoa huyo pepo wa maradhi. Na shukuru Mungu haya kutokea maana baada ya hapa injili itajithibitisha nyumbani kwetu na nguvu ya udini itaondoka.

Mbarikiwe na bwana.
 
Hana anayempotosha, ukisoma jina lake tu hapo chini unaelewa ndo wale waleeee, wanaokwendaga kwenye mihadhara kutukana dini za wenzao. Hana ajualo wala analoelewa. Baba mwenye nyumba mwenyewe kakimbilia huko na keshapata dozi, kamuulize. Looh! Watu wengine wadhani kuandika saaaaanaaaa kurasa kitabu ndo tutakubali hadithi yako iliyojaa udini na kutoelewa usemacho??? Toka lini Muislamu ukayajua ya Ukristo kama sio kutaka kuleta upupu tu hapa ukumbini??? Acha niishie hapa nisiendelee maana.... :smash:

Kama limetoka kwa Bwana hata uje na nguvu gani hutaweza kulizuia na waliokusudiwa watapata baraka zao. Kalagabaho!
 
Huyu majid ni vuvuzela la mambo ya udini na si lolote wala chochote kama imani yako haihusiki kinakuuma nini?shut up!!!!
 

...one time i agree with Matola!!
 


Haueleweki hata unachotaka kutuambia, mara unataka kumuombea baba yako mara aende akirudi ndio utoe ushuhuda, hivi ni lini babu wa Loliondo aliwahi kujitangaza kwamba yeye ni mungu? wewe huna cha ulokole wowote, ni mtu tu ambaye umeshakuwa brain washed na wajanja wachache wanaoishi kwa kutegemea fungu la kumi kwa gia ya ulokole, in short wewe ni mjinga tu kama wajinga wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…