Mjadala kuhusu Babu wa Loliondo na dawa yake.

Mjadala kuhusu Babu wa Loliondo na dawa yake.

...non sense stuff, from clue-less padre, for the sleeping masses.
 
Mimi jamaa yangu ana ngoma ameenda kwa Babu akanywa dawa baada ya wiki ambayo ni jana amepima bado hajapona hivyo tunasubiri muda zaidi tukiwa na imani
 
Mdondoaji na watu wengine mnaodadisi hii 'tiba' ya babu!
Hii sio mara ya kwanza na wala haitakuwa mara ya mwisho kwa watu wa aina hii ya babu wa Loliondo kujitokeza. Mnamo miaka ya 2003 (sina uhakika na kumbukumbu zangu) sehemu za Moshi vijijini alijitokeza mtoto aliyekuwa anatibu kama huyu babu.... kwa kutumia imani na unapewa maji aliyokuwa anayaita ya 'baraka' unakunywa. Alifanikiwa kuvuta umati mkubwa wa watu (japo si kwa kiwango cha babu) lakini japo mwanzoni kulikuwepo na shuhuda za kupona lakini kwa sasa sijui alikoishia. Mambo nililoligundua kuhusu 'watabibu' wa aina hii:
1. Hudai wametokewa na Mungu
2. Huanza kuvuta watu polepole, baada ya muda watu huongezeka sana na mwisho huanza kupungua na 'wanapoishia' hakuna anayekumbuka kuwafuatilia wao wala wagonjwa wao, jambo linatoa mwanya kwa 'waganga' wapya wanapoibuka watu wasifanye rejea ya nyuma.
3. Mara nyingi hutaka kutoa dawa wenyewe kwa mikono yao na wanywaji hunywea papo hapo.
4. Gharama zao zinakuwa ndogo sana au bure.
Mwisho nataka kusema tu hizi ni dalili za watu tuliokata tamaa na tunajaribu kutumia upenyo wowote kutatua matatizo yetu.

mh Macho! huenda una point!
 
kama ni kwa jina la Yesu angewahubiria watu waokoke sio tu kupewa kikombe cha dawa na kuondoka bila wokovu.pole uliyedanganyika. Yesu wetu anataka watu wote waokoke na waijue kweli bwana.

Mbona hatujasikia mahubiri yoyote pale! PALE YESU HAYUKO .IKO MIZIMU YA KWAO NDIYO INAYOTIBU!
 
Dah!!! Mungu wabariki watumishi wako!!! Ushukuriwe Mungu kwa kuwa shauri lako tu ndilo linalosimama. Na mambo yote tunayakabidhi mikononi mwako, ukweli wa mambo haya unaujua wewe Mungu. Utupe neema yako ili tusije tungaamia kwa kukosa maarifa. Ni wewe Mungu uliyetuumba kwa sura na mfano wako, na ni wewe pia unayetulinda na kutuponya nafsi zetu na magonjwa na hila mbaya za shetani.

Ninachokiamini kwako wewe ni wa huruma na Neema huwezi kutuacha tungaamia kwa kutojua ee Mungu. Tulinde sisi na wagonjwa tulio nao uwape afya na nguvu. Utakapofika wakati ulio uamuru wewe mwenyewe uhukumu hukumu ya haki juu ya haya mambo, utupe kuujua ukweli ili huo ukweli utuweke huru.

Amen!!!!
 
padre ana hoja ya msingi. wakristo hawpaswi kushabikia jambo na kilikimbilia kama majuha. padre amewapa vipendele vya kuzingatia kama checklist kabla hawajakurupuka kukimbilia loliondo. najua watampuuza na wameishampuuza sana huyo padre lakini yeye katimiza wajibu wake. Mungu ambariki sana

tatizo watu wameishalewa na mrigariga hawataki tena kusikia maneno ya Mungu yanasemaje!

ooh Lord have mercy on your people. amen

Glory to God

Miss, hata wakati wa Yesu watu walikimbilia miujiza na wakati mwingine mikate na vipande vya samaki. cha msingi ni wewe mwenyewe kulijua, kuliishi na kulitenda Neno.
 
Tanzania mambo ya mmpito ni mengi mmno,
miaka ya 80-90's kulikuwa na imani ya kakakuona ,kuwa anatabiri mambo makuu na muhimu,viongozi wa serikali walishiriki ktk hilo zoezi,wanaanchi tukaaminishwa juu ya umuhimu wa kaka kuona na utabiri wa Mvua,Njaa etc
Then ilikuja product moja inaitwa OKO ,inaziba pancha ya gari likiwa in motion,kwamba ukiweka oko ktk gari lako hupati pancha tena,nayo hii ikapita,so kwa babu ni moja ya mozonge ya Tanzania na upeo wetu mmdogo kitaifa wa kupambanua mambo.
 
Nijuavyo mimi furaha ya mgonjwa uwa kubwa apatapo uponyaji, sasa ni vipi hadi sasa kuwe kimya? Naamini ni zaidi ya waTZ milioni sasa wamefika kwa babu na BABU kaweka wazi kisukari upona kwa siku 7 ukimwi siku 21 sasa mbona wagonjwa husika hawasimami kutoa USHUHUDA wa kupona kwao? Naona magazeti tu ndio yana nukuu taarifa za watu kupona au kutopona, jamani kuna tbc,itv na star tv nendeni mkatoe ushuhuda wa kupona kwenu ili wasio amini tiba ya babu waamini hata magazetini basi hata picha za wahusika ziwekwe. kuna mgonjwa wa kisukari yupo hoi kcmc ICU wakati amepiga kikombe cha BABU sasa mtu kama mimi kuniaminisha kupitia magazeti inakuwa ngumu, waliopona wajitokeze ili imani yetu kwa BABU iongezeke.
 
ndugu yangu huyu mtu anahitaji evidence ili awa na uhakika! Jibu ulilotoa ni sahihi kweli? Acha hasira mtu anapouliza swali. Kama huna jibu ungenyamaza tu. Sasa amekosea wapi kuuliza hilo swali? Kwani wewe umeenda? Wapo watu waliokwenda ndio wana jibu. I've seen no mistake in this question.

Hilo ndio jibu nililoona linamfaa kwa mtizamo wangu.
Kwani watu wengi wamekuwa wa siri na magonjwa yao. Yeye kwa kuwa anataka kupata scientific result aende yeye aje atuwekee matokeo
 
Kwani tatizo nini,hata kama siyo Yesu yeye na Imani yake Itatosha na kama watu wanapona mim sioni shida yyote.kama imani yako haipo hulazimishwi kuamini
 
kama ni kwa jina la Yesu angewahubiria watu waokoke sio tu kupewa kikombe cha dawa na kuondoka bila wokovu.pole uliyedanganyika. Yesu wetu anataka watu wote waokoke na waijue kweli bwana.

Mbona hatujasikia mahubiri yoyote pale! PALE YESU HAYUKO .IKO MIZIMU YA KWAO NDIYO INAYOTIBU!

Mizimu bomba hii inatibu magonjwa sugu . Mungu aizidishie marifa mizimu ya mwasapile iweze kutibu na matatizo mengine ya wa Tanzania
 
yetu macho, na kila mtu awe na msimamo wake,, una imani ya babu nenda kapate kikombe, huna endelea na maisha yako!!!!
 
Tanzania mambo ya mmpito ni mengi mmno,
miaka ya 80-90's kulikuwa na imani ya kakakuona ,kuwa anatabiri mambo makuu na muhimu,viongozi wa serikali walishiriki ktk hilo zoezi,wanaanchi tukaaminishwa juu ya umuhimu wa kaka kuona na utabiri wa Mvua,Njaa etc
Then ilikuja product moja inaitwa OKO ,inaziba pancha ya gari likiwa in motion,kwamba ukiweka oko ktk gari lako hupati pancha tena,nayo hii ikapita,so kwa babu ni moja ya mozonge ya Tanzania na upeo wetu mmdogo kitaifa wa kupambanua mambo.

Ndugu umenikumbusha mbaaaaali miaka ileeeeeee!! OKO!! Kulikuwa na tangazo lake redio!! Kweli sikumbuki ilienda wapi nailiishaishaje!! Sasa na huyu babu sijui ila kauli yangu: Mwisho wa babu mbaya
 
Hilo ndio jibu nililoona linamfaa kwa mtizamo wangu.
Kwani watu wengi wamekuwa wa siri na magonjwa yao. Yeye kwa kuwa anataka kupata scientific result aende yeye aje atuwekee matokeo

Na kama haumwi aende tu kupata kinga au? Babu amepiga marufuku watu wanaoenda kupata kinga sasa jamaa afanyeje? Ugumu wa watu kutoa ushahidi uko wapi. Wakitoa ushahidi itasaidia sana
 
Dah!!! Mungu wabariki watumishi wako!!! Ushukuriwe Mungu kwa kuwa shauri lako tu ndilo linalosimama. Na mambo yote tunayakabidhi mikononi mwako, ukweli wa mambo haya unaujua wewe Mungu. Utupe neema yako ili tusije tungaamia kwa kukosa maarifa. Ni wewe Mungu uliyetuumba kwa sura na mfano wako, na ni wewe pia unayetulinda na kutuponya nafsi zetu na magonjwa na hila mbaya za shetani.

Ninachokiamini kwako wewe ni wa huruma na Neema huwezi kutuacha tungaamia kwa kutojua ee Mungu. Tulinde sisi na wagonjwa tulio nao uwape afya na nguvu. Utakapofika wakati ulio uamuru wewe mwenyewe uhukumu hukumu ya haki juu ya haya mambo, utupe kuujua ukweli ili huo ukweli utuweke huru.

Amen!!!!

Am blessed by your prayer. Thanx
 
Miss, hata wakati wa Yesu watu walikimbilia miujiza na wakati mwingine mikate na vipande vya samaki. cha msingi ni wewe mwenyewe kulijua, kuliishi na kulitenda Neno.

mkuu, kumbuka kuwa wakati wa Yesu kulikuwa hakuna wakristo. ukristo umezaliwa wakati wa mitume (apostolic era). zingatia sana hili please.

glory to God
 
mkuu, kumbuka kuwa wakati wa Yesu kulikuwa hakuna wakristo. ukristo umezaliwa wakati wa mitume (apostolic era). zingatia sana hili please.

glory to God

did I mentioned wakristo anywhere? nimesema watu sikusema Wakristo.
 
Back
Top Bottom