Hello great denialists!!
Nawakaribisha katika uga wa sifa na kudumisha misimamo yetu ya kukataa ndoa na kukataa kuoa.
Kama kawaida yetu msisitizo wetu ni kusaka pesa kutafuta pesa kutumia pesa pesa zituzoee bata lituzoee tukiamka nikutafuta pesa pesa pesa ndio msingi wa maisha na jeuri ya pesa.
Hatuna muda wa kupoteza kuwaza ukurutu na miwasho ya ndoa na kuoa.
Hatuwakatazi kuoa na kufunga ndoa kila mtu afanye maamuzi yake free tusipangiane maisha.
Naomba wakataa ndoa na wakataa kuoa tufunike kwa visa na mikasa na macontent ya maana.
Tutafute pesa na pesa ndio msingi wa busara, ukomavu na jeuri yoyote, katika harakati hizi tuchangie harakati za maendeleo, tuiunge mkono serikali, tumuunge mkono ndugu Rais, na viongozi wa ngazi zote.
Sehemu yoyote ile sisi wakataa ndoa na wakataa ndoa tuwe kielelezo cha amani, utulivu, kutii sheria, kuwa mfano mzuri tusiwe wagomvi, tusitukane, tuwe wastaarabu.
Hii itasaidie wengi wajikatae na wajiunge kundi letu tukufu la sisi wakataa ndoa na wakataa kuoa maarufu hapa jukwaani na mitaani.
Tujipende tusikose mademu angalau 3 hadi 5 kwa utulivu zaidi na ubora wa saikolojia na afya ya akili katika utafutaji.
Tuiombee Arsenal FC iendelee pia kutoa upinzani na ipate ubingwa Inshallah. 🙏🙏🙏
Wadiz