Mjadala kwa wanaokataa Kuoa (Ndoa)

Wewe Ni Miongoni Mwa Vijana Ninaopenda Kufuatilia Nyuzi Zenu Hapa JF
 
Huo ni mtazamo wako, hautuhusu wanaume rijali wengine. Sisi tunapambana tu na hao wanawake na tunawamudu yaani!
 
Jichanganye nasema jichanganye umrudie kuna jamaa yangu mkewe alimsumbua sana Mungu si athumani Bana akapata mwingine na Yule wakaachana si watu wakamlaghai kuwa warudiane na mkewe atakuwa kajifunza ili walee watoto kilichompata jamaa saivi ni marehemu na mke yupo anadundaa duniani, ukipata nafasi ya kuachana na mtu Kwa amani shukuru Mungu sana mwanao atakuwa vizuri kikubwa tuma matumizi ukipata nafasi nenda kamuone Ila usijichanganye kurudiana na kirusi tabia ya mtu ni ngozi ata ajichubue VIP utarudi kwenye uhalisia wake
 
Ni kweli usemayo mkuu
Ila mbali na hivyo kuna watu wanaishi maishaa yao mkuu
Wanaamani na furaha pia.
 
Mimi nafikiri wanaoishi paa moja afadhali mabaharia wanakula Kwa uoga Ila hao wanaoishi wilaya au mikoa tofauti. Mabaharia wanajilia kama wao ndio wameoa
Wewe umetoa mahali wenzako wanakula BUREEE..!!

#YNWA
 
Maisha ya ndoa hayafanani kama ambavyo maisha ya kawaida hayafanani.
Nimeoa 2016,katika maisha yangu sijawahi kujutia kuoa,Mungu alipa zawadi siyo tu mke yaani ni zawadi kabisa.

Mke wangu hana mambo mengi,siyo kwamba ni kwa sababu ni wa kawaida hapana ni pisi kali sana tu umbo maridhawa na sauti isiyochosha.
Mke wangu hajui kusema neno hapana kwake ni ndiyo na kuomba ruhusa kwa kila anachokifanya,kwake ni kutoa ushauri na kusubiri mume nitekeleze.

Mungu alinipa zawadi,mke wangu hataki kabisa kusikia jambo lolote la kusimuliwa kuhusu mume wake,yeye msimamo wake ni mmoja tu,anaangalia vile mume wake anavyoishi naye kwa amani na upendo,namna mume anavyotimiza majukumu yake.

Nimeshamfungulia kabiashara ili na yeye awe na cha kufanya,hatumii hata mia bila kupata kibali.

Aisee hata ndoa zote ulimwenguni zivunjwe ili tuoane upya nitaenda kumchumbia upya mke wangu.
Pamoja na changamoto zote za ndoa bado ndoa zenye amani na upendo zipo kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…