MJADALA: Kwanini pale alipo mtu mweusi hali ya uchumi huwa ni tete? Nini chanzo cha umasikini?

MJADALA: Kwanini pale alipo mtu mweusi hali ya uchumi huwa ni tete? Nini chanzo cha umasikini?

Kwako choo ni nini ? na kuna aina ngapi za vyoo ?

Je unaona ni sahihi na sustainable kwa sehemu za vijiji vyenye ukame kuwa na flushing toilet au ni kama jamii hizo walivyojiwekea a dry toilet ili kuweza ku-conserve maji ? Hata huko ulaya wameshaona kwamba pa kuelekea ni kutumia water recycling...

Wewe uliopo mjini unadhani hujisaidii kwenye vyanzo vya maji..., ushaona waste water zinavyokuwa dumped kwenye vyanzo vya maji au haujui kuna meli huwa zinakuja na industrial wastes kutoka huko ili kuzileta huku na kuzi-dump (juzi tu kuna meli ilishikwa Kenya ikiwa inaelekea huku)

Moral of the story ni kwamba kutokuendelea kwetu kupo kwenye fikra kwa sasa na sio kwenye ngozi (kutawaliwa kwetu kumesababisha kuona kwamba suluhisho ni wale wanavyofanya na sio sisi kuweza kuboresha kile wanachofanya au mababu zetu walichofanya)
Mkuu Kwanini Hapa Tanzania Watu Wanasubiri Mvua Inyeshe Ndo Walime Wakati Tuna Mito Na Maziwa

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Wakati Wa Msimu Kama Ni Nyanya Au Mboga Za Majani Utakuta Mbei Ndogo Sana Mpka Ushangae Msimu Ukiisha Vitu Bei Kubwa Kwanini Tusiweze Kutengeneza Kitu Cha Kuhifadhi Kwa Muda Mrefu

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Uongozi unaanza ngazi ya familia mkuu

Unafata kwenye jamiii

Familia nyingi za kiafrika ni uchawi na huamini maendeleo yapo tu

Hapa unakuta familia haina strategy za kujikomboa kiuchumi yenyewe kwanza

Hata serikali ikipambana kumuinua mwananchi lakini kama mwananchi mwenyewe hana strategy za kujiinua kiuchumi lazima aiponde

NB Usiilaumu serikali je ngazi ya familia inakuongoza vipi kwenye kujikwamua kiuchumi?
Uongozi Usianzie Kwenye Familia, Uanzie Juu Selikarini Yani Unavyoona Watu Kuna Pahala Kuna Imani za Kishirikina Ujue Huko Maendeleo Watu Wanaishi Kama Wanyama

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Ajabu na wataalam wapo...
Tatizo ni nini unadhani!?
Tatizo lipo mpaka kwa wataalamu wetu wao wanatumia ushauri wa mazingira tunayoweza kuishi kwa urahisi akikwambia acha sukari utafurahi kusikia hivyo maana inapunguza gharama za kununua sukari kwa kisingizio sukari haifai wakati sukari ni lazima na siyo muhimu Bali ni lazima ila sukari asilia, na upande wa vitu vingine hivyo hivyo mfano niliosema wa mafuta hivyo hivyo butter original ya wanyama ni Bora kwa protein kuliko hata mayai na maziwa lakini Leo tunalia mafuta hakuna na tunajumlisha mafuta ya mgando ya kupikia yaliyotengezwa kwa mimea ni mabaya, wakati ya wanyama ni mazuri na wenzetu weupe ndo wanatumia kupikia vyakula vyao, gee imejaa tu madukani na butter na cheese vyote ni mafuta ila vinauzwa ghali kwa vile wananunua weupe tu kwa afya zao ila tungetumia na sisi na wataalamu wakashauli tungepata kwa bei ndogo na akili zetu zikawa na kiwango kizuri, hata hizo olive sijui zaituni zingelimwa kwa wingi.
 
Ndugu zangu hili ni suala tunaweza kulipatia ufumbuzi tukilijadili kwa kuangalia hali halisi ya nchi yetu na za Africa kwa ujumla.

Juzi Tanzania one alisema sisi bei yetu ni poa sana ukilinganisha na ndugu zetu wamarekani. Sidhani kama alikuwa sahihi na hakupatikana mwandishi wa kumwuliza nini hasa alimaanisha je ni ile bei ya pump pale sheli au alimaanisha tozo zilizopo katika mafuta?

Ila kikubwa hapa kwa nini nchi za Afrika haziendelei nini tatizo rasilimali zipo, watu wapo na serikali sikivu zipo lakini hali si nzuri sasa hivi vita ipo Ukraine, Ethiopia, Somalia, madagascar hali si shwari.

Wapi Serikali au nchi zetu zinakosea?

Tafadharini tusaidiane kimawazo, Makamba akipita hapa tuwe tumemwongezea kitu. Karibuni.
Some Africans are stupid AF
 
Bora kwa nani ? Kwa macho au kwa afya ?

Tuongelee makazi kidogo.., je ni afya kujifungia kwenye kuta nne bila hewa sijui dirisha la aluminium wakati ukilifungua unapata hewa half the space ?!!!

Au tuongelee kipindi kirefu watu walijiona wajanja kutumia eti bati za kisasa (Asbestos) ila kuja kugundua madhara yake kwa afya na watu walikuwa wanajifungia humo kutwa na kuchwa !!!, Don't get me wrong ubora na kuboresha ndio maisha ila sio kila kipya ni kizuri na cha zamani ni kibaya..., Mfano nyumba ya udongo ni environmental friendly na inakupa joto kwenye baridi na baridi kwenye joto kuliko nyumba ya cement...

Unaongelea lishe bora, Mmasai anakula fresh food na sio processed food ambayo imejaa makemikali na addictives za kufa mtu (junk food)..

Kwahio perception yetu ni kwamba the grass is greener kwa jirani ila kwa mtu ambaye ameishi maisha yote huku na kule atakwambia its not so...

Umasikini upo mijini, umasikini upo sasa na utaendelea kuwepo kutokana na gap in classes kuongezeka siku baada ya siku..., Umasikini unachangiwa na sio sababu kuna less for everyone (there is enough for everyone need ila sio for everyone greed)..., kwahio kutokuweza ku-manage mazingira yetu ndio kunaleta umasikini na sio sababu mtu mweusi hana akili (la hasha) sababu ni marginalization, as well as indoctrination ambayo tumeshajengewa ya kwamba nini kinafaa na nini hakifai hence kutukuza mkate zaidi ya muhogo..., cement zaidi ya udongo, bati la msausi zaidi ya msonge n.k. (wakati hivyo vyote vingeweza kuboreshwa kuendana na wakati na mazingira yetu)...,

Don't get me wrong siongelei kila cha jirani ni kibaya hivyo tusiige mazuri (bali naongelea pia kila kilicho chetu sio kwamba hakifai na kinahitaji kuboreshwa)
Maendeleo ndio hayo ya uboreshaji wa vitu vya zamani kuwa vya kisasa mkuu......kutoka nyumba za nyasi kwenda za cement......kutoka kupanda punda mpaka magari....kutumia mitishamba mpaka dawa za hospitali.....kutuma barua mpaka kutumia simu..... Na hivyo vyote tumeletewa kutoka Ulaya ...... Mi nimeishi kijijini ambako tulikuwa tunatembea peku peku bila viatu...Kuishi nyumba za tembe..kupikia kuni..... naelewa maisha yalivyokuwa magumu......kupata mia 5 ya kununua hata sabuni ni shughuli....acha kabisa fikiria uko kwenye nyumba ya udongo yatokee mafuriko hali itakuwaje........
 
Ndugu zangu hili ni suala tunaweza kulipatia ufumbuzi tukilijadili kwa kuangalia hali halisi ya nchi yetu na za Africa kwa ujumla.

Juzi Tanzania one alisema sisi bei yetu ni poa sana ukilinganisha na ndugu zetu wamarekani. Sidhani kama alikuwa sahihi na hakupatikana mwandishi wa kumwuliza nini hasa alimaanisha je ni ile bei ya pump pale sheli au alimaanisha tozo zilizopo katika mafuta?

Ila kikubwa hapa kwa nini nchi za Afrika haziendelei nini tatizo rasilimali zipo, watu wapo na serikali sikivu zipo lakini hali si nzuri sasa hivi vita ipo Ukraine, Ethiopia, Somalia, madagascar hali si shwari.

Wapi Serikali au nchi zetu zinakosea?

Tafadharini tusaidiane kimawazo, Makamba akipita hapa tuwe tumemwongezea kitu. Karibuni.

Kwanini hapo hapi Mzungu, mhindi mwaraabu anatajirika, fursa?
 
Mtu Mweusi ?!!!

Unamjua Mansa Kankan Mussa ??

Ukishamjua huyo na kumfuatilia rudi tena tuendelee na mjadala....

Umasikini mwingi ni Man Made na unatokana na Marginalization na unyonyaji fulani na ukiunganisha na mentality ya watu / mtu...,

Huwezi kuniambia mmasai ni masikini wakati ana chakula chake, natural AC na anayamudu mazingira alafu eti jamaa anayeishi huko New York kwenye one bedroom flat na maisha yake yote yupo kwenye cubicle 24/7 anatafuta senti ya kuweka kumuweka kwenye one bedroom flat yake ambayo hakai sana sababu muda mwingi anatumia kwenye traffic..., eti huyu ni tajiri in comparison na huyu mwingine....

It's just your perception....
Ndo umejibu nini hapa.huyo mansa mussa naye mwenyewe huo utajiri wake ulitokana na kujimilikisha mali za Mali empire.Hoja ya mtoa mada haiwezi kujibiwa kwa hoja rahisi hivyo kwasababu hali ya waafrika ni ngumu zaidi ukilinganisha na jamii zingine.Tatizo letu halitatuliki kwa kuangalia mtu mmoja mmoja bali jamii nzima.
 
uitolee mfano nchi yetu. Mimi leo nimeamka, nimetoka nyumbani kuja mjini. Njiani ninakutana na magari, kwa kukadiria si chini ya 300 na yote yanatumia mafuta na wanalipa kodi. Lakini maajabu ni kuwa nilipotoka nje ya geti, nilikutana na madimbwi na mashimo kwenye asilimia 80 ya njia niliyopita mpaka kufika mjini. Mashimo na madimbwi haya huharibu magari kwa kiwango kikubwa hivyo kulazimu matumizi ya mabilioni ya pesa kwenda nje ili spea ziletwe zitengeneze tena hayo magari.
WEWE UNAPASWA KUTUMIA PUNDA KUJA MJINI, WALA SI GARI
KWA VILE HUKO UNAPOISHI HAKUJAKUWA NA BARABARA BADO.
Hiyo ni njia ya punda na magari ya punda na Ngombe.
Unafosi kupitisha gari kisha unawalaumu Wazungu , au Viongozi.
Kweli Waafrika tunashindwa hata kuwa na fikara sahihi.
 
Uzalendo haupo, kila mtu anapigania tumbo lake. Angalia waliopewa mashirika ya Umma wakati wa mwalimu, kila mtu alichukuwa chake mapema, SU= soma ule.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fanya Research kidogo angalia Nchi za Watu wanaokula Ugali for Breakfast,Lunch n Dinner angalia na Umasikini na IQ zao.

After all huu Ugali tumeletewa na Wareno i mean Wamisionari wa Kireno.
Mkuu umesoma biochemistry? Unaijua kazi ya thiamine?
 
Chanzo cha umasikini ni laana za mababu waliojiconnect na mizimu.Ili kuutokomeza umasikini ni kukata connection na mizimu. Familia zote au Jamii zote zisizona connection na mizimu zipo njema. Kwann.
Mizimu haitaki maendeleo kwani kupitia maendeleo watu wataelimika na kustaarabika nao wataacha kuabudu mizimu.
Hivyo umasikini ni negative power nayo uambukiza uthibisho ukikaa na watu au mitaa masikini baada ya mda utaaiga tabia zao nawe utacopy automatic utakuwa masikini. Umasikini ni tabia na sio asilia.
 
Kwanza ieleweke watawala wa kiafrica wote wanafanana uongo na propaganda ndio sifa yao kuu. Wao huwa awaangalii asili ya tatizo bali kudakia tatizo Ili kujifichia udhaifu wa kushindwa kwao. Vita upiganwa ukraine ni mbali mafuta uagizwa toka middle east, kwa akili ya kawaida tu ni uongo.
 
Sababu ni zilezile:
1: ignorance and encompitance
2: Lack of capital
3: poor leadership and governance
4: infeliority complex
5: lazyness and lack of self discipline
 
Back
Top Bottom