Mjadala wa Bandari ni ama tuchague kusikiliza mtaalamu Hamza Johari au mpenda sifa Tundu Lissu

Mjadala wa Bandari ni ama tuchague kusikiliza mtaalamu Hamza Johari au mpenda sifa Tundu Lissu

Kuwa Lecturer wa Chuo Kikuu ni lazima uwe na PhD. Master degree holder ataishia kuwa tutorial assistant au sana sana Assistant Lecturer.
 
Mkuu acha hasira, mie sijahukumu mtu hap, siko kwa Johari wala kwa Lissu, hoja yangu kati ya hao wawili kwenye suala la bandari twende na nani? mwenye certificate ya india ila ya usafirishaji, au mwenye LLM ya Warrick?
Huyo mwenye setifiketi ya kihindi hajawahi kusimama mahakamani Kwa kesi yoyote Kwa hiyo Hana tofauti na Mimi Kwa kukaririshwa
 
Mtu aliyesoma Ukraine hawezi kuaminika. Angalia nchi ya wajinga ilivyogeuzwa magofu kwa upuuzi wao wa kununuliwa na Marekani. Huyu wa kwetu naye kaamua kununuliwa na waarabu.
 
Huyo mwenye setifiketi ya kihindi hajawahi kusimama mahakamani Kwa kesi yoyote Kwa hiyo Hana tofauti na Mimi Kwa kukaririshwa
Mkuu tuko kwenye kuendeleza, kuboresha, na kuendesha bandari
 
Mkuu uzuri wamekekiri humu wenyewe- Lissu et al si wataalam na kama siyo wataalamu wanamaanisha kuwa ni ule upande mwingine
Lissu ana shule ya kawaida tu kakuta nchi ina wajinga wengi. Hamza hana kipaji cha mwanasiasa, hana ule ushawishi wa majukwaani ni mtu anaongea taratibu na ana upole ulio silaha mbaya katika ulimwengu wa siasa lakini ni mtaalam sana wa masuala ya sheria na uongozi kwa ujumla.

Hamza watanzania wengi wasio kwenye sekta ya anga hawamjui, mpaka mwaka jana alikuwa ni mwakilishi wa afrika wa ICAO shirika kubwa la masuala ya anga duniani makao makuu yakiwa Canada.

Chini yake TCAA ilipata asilimia 65 za ubora wa masuala ya anga na nchi ikapewa tuzo aliyokabidhiwa hayati JPM, hakuna watanzania wanaoyajua hayo achilia mbali kuyafuatilia.

Wanasema uongo hufika juu kwa kwenda na lifti na ukweli hupanda ngazi taratibu. Muda utatuambia kati ya Lissu na Hamza mkweli ni yupi.
 
Hivyo vicertificate vya huko India, kwako unaona ni vya pekee sana?

Hivi, wakiitwa wasomi wakubwa wa nchi hii, na huyu naye utamhesabia? Sasa naelewa ni kwa nini mkataba ule wa DP ni wa hovyo kiasi hiki. Huyu wa elimu ya kuunga unga ameliingiza Taifa kwenye hasara tupu.
Mwanzo nilidhani unajua unachoandika kumbe ni mtupu tu usiye na data wala ufahamu wa unachoandika.

Hamza alipambana mpaka Ziwa Malawi kwa sasa linamilikiwa nusu kwa nusu enzi za hayati Benard Membe na JK, sijui kama hilo unalifahamu.

Hamza alipambana mpaka mamlaka ya anga TCAA wakapewa tuzo maalum ya ubora baada ya kupata asilimia 65, wakati miaka ya nyuma mwisho wetu ulikuwa ni asilimia 35 na akakabidhiwa hayati JPM, sijui kama hilo unalifahamu!.

Hamza ni mmoja wa wajumbe wa bodi ya ICAO shirika linaloongoza masuala ya ndege duniani, utungaji sera wote wa masuala ya sekta ya anga unamhusu yeye pia, sijui kama hili pia unalifahamu!.

Hao maprofesa wa kibongo wanaokuzuzua kichwa wamefanya lipi la maana, usije ukataka kumvunjia mtu heshima kwa sababu humuoni sana saa mbili kamili usiku akiongea ITV au TBC, wapo wengi wenye impact zao na huwezi kuwajua kwani hawana makuu.

Mkataba wa Consession na ule wa Lease ndiyo yenye umuhimu kwani huko ndiko biashara kwa kina zinakwenda kuwekewa vifungu, hili na wewe uliingia kichwa kichwa ukadanganya watu humu!.

Leo unawaponda watu wanaopambana usiku na mchana kwa ajili ya nchi yao!.
 
Siku moja wengi wataning'iniza vichwa vyao kwa aibu watakapogundua uovu walioutetea na mashujaa waliowakejeli.
FB_IMG_1689764982599.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom