TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

Siku moja niliku pm ila naamini uliona meseji hiyo japo haukunifeed back.

Hiki ulichokiandika hapa kiko wapi dada?
Naweka video, ni kubwa ndo mana inachukua muda

Asnt sana kwa kufatilia mjadala na maendeleo ya jimbo letu[emoji120]
 
BUKOBA[emoji24] [emoji24] [emoji24]

6cc51c1bc4c9b2bc17d383a85d2a5b05.jpg
41b680af6e202ba4cb846d03d0ce8492.jpg


Mwonekano wa mji wa Bukoba 1972, 2014 na 2016 kwa kufuata mtiririko wa picha zote tatu (3). Hakuna kilichobadilika cha maana[emoji24] [emoji24] [emoji24] [emoji24]
 
MKOA WA KAGERA TARATIBU WAANZA KUREJEA KATIKA ENZI ZA NSHOMILE KATIKA ELIMU WASHIKA NAFASI YA TANO KATIKA KUMI BORA KITAIFA DARASA LA VII

Na: Sylvester Raphael

Kutokana na usimamizi na uongozi thabiti chini ya Mkuu wa Mkoa mahili wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu kiwango cha Elimu mkoani hapa kimeanza kupanda kwa kasi na kuifanya Kagera kuanza kurejerea katika miaka ya 1980 wakati ule mkoa ulipokuwa unasifikakwa jina la “Nshomile”

Katika matokeo ya darasa la saba ya mwaka 2016 Mkoa wa Kagera umeendelea kufanya vizuri na kushika nafasi ya tano kati ya mikoa 10 bora, Aidha mwaka 2014 Kagera ilishika nafasi ya 10 kati ya mikoa kumi bora, mwaka 2015 mkoa ulishika nfasi ya 7 kati ya mikoa 10 bora na mwaka huu umepanda juu nafasi mbili za ufaulu.

Halmashauri iliyoongoza katika mkoa wa Kagera ni Ngara iliyofaulisha kwa asilimia 87.82% na kitaifa imekuwa ya 12, mwaka jana 2015 ilikuwa ya 18. Ya pili ni Biharamulo iliyofaulisha kwa asilimia 85.11% na kitaifa imeshika nafasi ya 21, mwaka jana ilikuwa ya 3. Halmashauri ya tatu kimkoa ni Muleba liyofaulisha kwa asilimia 83.69% na kitafa kushika nafasi ya 24 ambapo mwaka jana 2015 ilishika nafasi ya 43.

Halmashauri ya nne ni Manispaa ya Bukoba iliyofaulisha kwa asilimia 83.23% na kushika nafasi ya 26 kitaifa aidha, mwaka jana ilishika nfasi ya 47. Ya tano ni Missenyi liyofaulisha kwa asilimia 78.80% na kushika nafasi ya 46, mwaka jana ilikuwa ya 19. Kyerwa ya sita imefaulisha kwa asilimia 77.60% na kushika nafasi ya 53 ambapo mwaka jana 2015 ilishika nafasi ya 68 kitaifa.

Karagwe ya saba iliyofaulisha kwa asilimia 76.79% na kushika nafasi ya 54 kitaifa ambapo mwaka jana 2015 ilishika nafasi ya 72 kitaifa. Halmashauri ya mwisho ni Bukoba iliyofaurisha kwa asilimia 74.86% na kushika nafasi ya 69 kitaifa ambapo mwaka jana ilishika nafasi ya 102, aidha, imepanda nafasi 33 kitaifa japo imekuwa ya mwisho katika mkoa wa Kagera. Shuleiliyoongoza mkoani Kagera na kuwa katika shule 10 bora zilizofanya vizuri kitaifa ni St. Achileus Chiwanuka kutoka Wilaya Muleba .

Akiongelea matokeo hayo Afisa Elimu Mkoa wa Kagera Bw. Aloyce Kamamba alisema mkoa wa Kagera unaendelea kufanya vizuri na miaka ijayo mkoa huu utaweza kushika nafasi ya kwanza kama ilivyokuwa zamani. Aidha, Afisa Elimu kamamba alisema yeye na wataalam wake watafanya tathmini ya kina kujua kwanini Halmashauri ya Biharamulo imeshuka katika ufaulu ukilinganisha na mwaka jana .

Bw. Kamamba aliipongeza Halmashauri ya Bukoba kuwa pamoja na kushika nafasi ya mwisho katika mkoa kama mwaka jana lakini imepandisha asilimia za ufaulu aidha, imepanda nafasi 33 kitaifa. Bw. Kamamba alisema kuwa juhudi za walimu zimeonekana lakini akatoa wito kwa Halmashauri hiyo kuhakikisha inaongeza juhudi ili iweze kutoka nafasi ya mwisho kimkoa.

Katika hatua nyingine Afisa Elimu Bw. Kamamba alisema mkakati wa mkoa ni kuhakikisha Kagera inashika nafasi ya kwanza kitaifa ambapo yeye pamoja na timu yake ya Elimu chini ya uongozi wa mkuu wa Mkoa wa Kagera wataendelea kufanya usimamizi wa kina ili kuhakikisha kiwango cha elimu kinaendelea kupanda mkoani Kagera.

Mikoa kumi iliyofanya vizuri kitaifa ni Geita iliyofaulisha kwa asilimia 86.92% mwaka jana 2015 ulishika nafasi ya 6. Wa pili ni katavi uliofaulisha kwa asilimia 86.80%, mwaka jana ulikuwa 1, Iringa ulishika nafasi ya 3 na ulifaulisha kwa asilimia 82.87%, mwaka jana ulikuwa wa 10. Dar es Salaam umeshika nafasi ya 4 kwa kufaulisha kwa asilimia 82.59%, mwaka jana ulishika nafasi ya 2. Kagera numeshika nafasi ya 5 kwa kufaulisha kwa asilimia 80.99% na mwaka jana ulishika nafasi ya 7.

Mkoa wa sita ni Mwanza uliofaulisha kwa asilimia 79.13%, mwaka jana ulikuwa wa 3 kitaifa. Kilimanjaro umeshika nafasi ya 7 na kufaurisha kwa asilimia 79.10%, mwaka jana ulikuwa wa 4. Arusha umekuwa wa 8 kwa kufaurisha kwa asilimia 77.58%, mwaka jana ulishika nafsi ya 5. Njombe umekuwa wa 9 kwa ufaulu wa asilimia 77.10% na mwaka jana ulikwa wa 9. Tabora umekuwa wa 10 kwa ufaulu wa asilimia 71.35% na kushika nafasi ya 10aidha mwaka jana ulikuwa mkoa wa 25, wa pili kutoka mwisho.
 
TATHMINI YA MIEZI MITATU (3) YA HALI YA USHIRIKISHWAJI WA WAWANCHI KATIKA SHUGHULI ZA MAENDELEO TOKA KUANZA KWA MRADI WA "TUSHIRIKISHANE"


4870a13c641814fe52139134077cd7eb.jpg


Hiyo[emoji115] ndio dira ya BMC. Dira hii mpk sasa imefanikiwa kwa 10% tu kwa kuwa na halmashauri na watendaji wa mitaa na kata.

Vinginevyo, ushiriki wa wananchi katika swala zima la maendeleo si wa kuridhisha. Wananchi hawafahamu kinachoendelea katika mipango na utekelezaji wa miradi yote ya manispaa na hawana jinsi ya kupata taarifa. Hii inatokana na kwamba;

-Website ya BMC inataarifa za 2012, idara ipo na inawatumishi kadhaa wengine wana masters.

-Meya hana kurasa za mitandao ya kijamii kama JF, fb, twitter, IG ambayo angeweza itumia kutoa taarifa

-Naibu meya kwa kurasa zake zote hakuna haongelei chochote cha Bkb au Nshambya ambayo ni kata yake. Anatumia kurasa zake kuongelea mambo mengine ya kitaifa.


-Mbunge kama taasisi ana ukurasa maalum fb lkn anapost mara chache sana kwa kadirio la mara moja kwa miezi miwili au hata zaidi. Mipango, utekelezaji na ahadi haviko katika ukurasa wake.

-Mkurugenzi wa manispaa ni mgeni. Lakini pia watendaji wengine wa BMC kama wakuu wa idara hawaongelei chochote popote na sheria haziwaruhusu

-Mkanasha huu wa JF ulilenga kusaidia mbunge na katibu wake pamoja na halmashaufi kujibu maswali na kuwapa mwelekeo wa halmashauri wananchi lkn bado haujatumika ipasavyo.

-Ukurasa wa katibu wa mbunge katika mitandao ya kijamii pia hauna msaada kwa yeyote anayetaka taarifa.

-Ukifika manispaa kupata taarifa yeyote unaambiwa uandike barua kwa mkurugenzi kwanza ili idara ziruhusiwe kutoa taarifa. Hivyo njii hii si rahisi sana kwakua inakua na mlolongo mrefu

-Viongozi hawajaweza kutumia radio zetu na Tv kuelezea chochote kuhusu BMC, maendeleo n.k

-Kuna njia zilipendekezwa kwenye warsha ya "Tushiikishane" za namna ya kuwafikishia wananchi taarifa kama kuandaa namba maalumu na kutuma jumbe fupi kupitia simu, bado hazijafanyiwa kazi

Katika kata kadhaa nilizopita kufatilia maendeleo ya mradi wa Tushirikishane, watendaji wake wote hawajawahi sikia kuhusu mradi, hawafahamu hatua zilizofikiwa katika ujenzi wa soko kuu na stand, mtendaji wa Nyaga tu ndo alikua anafahamu kuh ujenzi wa stand. Mahojiano mbali mbali niliyofanya na wananchi wa kawaida, wengi hawafahamu chochote. Nilifanikiwa kuhoji hata bodaboda wa pale nje ya ofisi za manispaa nao hawafahamu chochote

Aidha, ninampongeza na kumshukuru Mh. mbunge pamoja na halmashauri, wameahidi kulifanyia kazi swala hili kwa haraka sana. Na kwa kuanza wameahidi kuwa baraza la madiwani litakua likirushwa moja kwa moja katika radio zetu na Tv ili wananchi wengi zaidi waweze kufikiwa na taarifa. Hii ni habari njema sana[emoji120]


Bukoba Kazi, Amani na Maendeleo!
 
TAARIFA YA MRADI YA AUGUST - OCTOBER, 2016


UTANGULIZI

Tushirikishane ni mradi unaowahusisha viongozi wa kuchaguliwa (mbunge na madiwani) serikali (halmashauri) na wananchi katika kufanikisha maendeleo. Wadau wakuu wa mradi huu ni Halmashauri ambayo ndiyo kitovu cha mipango ya maendeleo na utekelezaji wake, Mbunge ambaye ni msimamizi wa serikali (halmashauri), Jamiiforums ambao ni wasimamizi wa mradi na Wananchi.

Tushirikishane ilianza rasmi mwezi August katika jimbo la Bukoba mjini kwa kukutanisha wadau husika. Kundi la wananchi liliwakilishwa na makundi yote wakiwemo viongozi wa dini, wanawake, vijana, wazee, wafanyakazi na wafanya biashara mbalimbali wakiwemo bodaboda, n.k na kupitisha vipaumbele vinne ambavyo vimetokana na ahadi za mbunge alizotoa wakati wa kampeini. Vipaumbele hivyo ni;

1. Ujenzi wa Stand Kuu ya Mabasi, ujenzi wa Soko la Kuu na Soko la Kashai

2. Urasimishaji Makazi

3. Mikopo kwa Wanawake na Vijana, na

4. Bima ya Afya

Utekelezaji wa mradi unaanzia Halmashauri ambayo inasimamia miradi yote na inayotokana na vipaumbele vyetu vinne (4). Pia inatoa taarifa kwa kila hatua inayofikiwa katika vipaumbele vyote. Mbunge katika mradi ni daraja kati ya manispaa na wananchi katika kuweka msukumo wa utekelezaji na kutoa taarifa kwa wananchi. Mbunge pia anatoa taarifa kwa JF juu ya kila hatua zinazofikiwa katika vipaumbele vya mradi. Halmashauri na mbunge wanawajibika moja kwa moja kwa wananchi. Jamiiforums ni mfatiliaji wa shughuli zote za mradi (utekelezaji wa vipaumbele) inatoa taarifa kwa wananchi juu ya mradi kupitia hapa, mitandao ya kijamii, magazeti, radio na mikutano midogo midogo katika kata zilizoko manispaa.

Hatua zilizokua zimefikiwa katika vipaumbele vyetu mwezi August zilikua ni za kuridhisha isipokuwa mwezi September shughuli za tetemo la ardhi zilikua nyingi zaidi kwa takriban mwezi mzima na hivyo kuchelewasha utekelezaji kwa kiasi flan. Kutokana na hili vipo vipaumbele ambavyo vimerudisha nyuma sana kutokana na athari ya tetemeko kama 'Urasimishaji Makazi'. Kutokana na hilo ripoti hii itaanzia August mpaka October ili kuweka mtiririko mzuri. Na baada ya hapa ripoti itakua ikiandaliwa ya kila mwezi.



TAARIFA

1.Ujenzi wa Soko Kuu

Lengo la Tushirikishane katika kipaumbele hiki ni angalau ifikapo April 2017, ujenzi uwe umeanza angalau kwa hatua ya msingi. Hatua zilizokwisha kukamilika mpka sasa ni zifuatazo;

- Tayari vikao vya OGM (mhandisi mshauri) na CTM vimekwishafanyika kuhusu nyaraka mbali mbali kama feasibility study, architectural drawings, engeneering drawings, geotechnical survey, bills of quantities, na tender document

- Kampuni hiyo ya OGM imekwishawssilisha taarifa yake ya utendaji kuhusu utayarishaji wa nyaraka za mradi kwa kamati ya ilinzi na usalama

- Michoro ya jengo, usanifu na upembuzi yakinifu umekamilika ukionyesha basement, ground floor ghorofa tatu na tower

- Ukokotoaji wa gharama za ujenzi uko tayari umekamilika ambapo itagharimu shilingi 13 bilion

- Upimaji wa hali ya udongo tayari umekamilika

- Uchunguzi wa athari ya mradi kimazingira umekamilika

- Nyaraka za zabuni zimeandaliwa

- Mazungumzo kati ya OGM na TIB na halmashauri juu ya kupata pesa yamekwishakufanyika. TIB wameahidi kutoa 70% ya pesa yote na halmashauri kutoa 30% katika mapato yake au kwa ubia

- Baraza la madiwan limekwishakutoa kibali cha kukopa

- Akaunti maalum imekwishafunguliwa

- Aidha business plan haijakamilika kwasababu OGM waliomba kulipwa ghrama yao ya 50,000,000/- ili kukamilisha kazi hiyo lakin manispaa haikuweza kuipata kutokana na kushuka kwa mapato. Badala yake manispaa imeiandikia barua TIB kuomba kulipa kampuni ya OGM deni lake lote la zaidi ya mil 400 kama sehemu ya pesa ya mradi wa ujenzi wa soko kuu

- Maombi ya eneo la KCU lililoko kati ya ofisi ya Mkurugenzi wa manispaa na Mkombozi Commercial Bank yalifanyika kwaajili ya kuhamishia wafanyabiashara wa soko kuu kwa muda ili kupisha ujenzi. KCU wamekubali kutoa eneo

- Hatua inauofuata ni kukaa uongozi wa halmashauri pamoja na uongozi wa soko na wafanyabiasha kuweka mikakati ya kusonga mbele, kutangaza na kupata mzabuni, kuhamisha wafanyabiashara, kutaguta pesa hiyo 30%, n.k


2. Ujenzi wa Stand ya Mabasi

Vilevile katika ujenzi wa standi tuntegegema ifikapo April 2017, ujenzi uwe umeanza angalau kwa hatua ya msingi. Zifuatazo ni hatua zilizofikiwa;

- Fidia ya jumla ya 12, 967, 735/- imekwishalipwa kwa watu watatu ambao walikua hawajalipwa

- Eneo la hekta 6.53 limetengwa na kupimwa

- Mchoro umekwishaandaliwa

- Uchunguzi wa athari ya kimazingira umekwishafanyika

- Shirika la Mzinga Holding Cooperatio Ltd tawi la Morogoro limeingia makubaliano na manispaa lifanye kazi ya kuandaa feasibilitu study, ramani ya michoro na majengo, business plan, na kusaidia kutafuta mbia au mfadhili wa mradi

- Kazi zinazofuata ni kuandaa andiko la mradi na kutafuta fedha kwa wabia wau wafadhili ( Bank ya Dunia wameonyesha nia)


3.Mradi wa Ujenzi Soko Kashai

Ujenzi wa soko la Kashai tunatarajia uwe umeanza ifikapo April 2017. Zifuatazo ni hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wake;

- Michoro na usanifu tayari

- Andiko la mradi limekamilika

- Uchinguzi wa athari ya mrafi kimazingira umekamilika

- Nyaraka za zabuni zimekamilika

- Fedha za ujenzi bado zinaombwa kutoka bank ya dunia

4.Urasimishaji Makazi

Katika kipaumbele hiki tunatarajia kuwa zimesajiliwa nyumba zipatazo 10000 igikapo April 2017. Hizi ni hatua zilizofikiwa katika kipaumbele hiki;

- Zoezi la kuunganisha mitaa katika vikundi limekwishakamilika Kashai na Bakoba.

Kashai imewekwa katika vikundi vitatu;
i. Kashenya
Kilimahewa
National Housing

ii. Mafumbo
Matopeni
Lwome

iii. Kashai
Kisindi
Katatolwansi

Bakoba mitaa ni miwili;

i. Nyakanyasi
Mtoni

ii. Forodhani
Buyekela

- Gharama za kupima ni 200000 kwa kila nyimba ambazo zinawekwa katika akaunti za vikundi

- Tayari akaunti maalumu zimekwisha kufunguliwa kwa kata hizo mbili

- Wananchi wanaendelea kuelimishwa

Aidha, zoezi hili limeathiriwa sana na tetemeko la ardhi.

5.Mikopo kwa wanawake na Vijana.

Tunatarajia ifikapo April 2017, vikundi 250 viwe vimepata mkopo wa pesa ya 10% ya mapato ya manispaa inayotengwa kila mwezi na kupelekwa SACCOS kwaajili ya wanawake na vijana kukopa. Hizi ni hatua zilizofikiwa;

- Halmashauri inatenga 10% ya mapato yake ya kila mwezi na kupeleka SACCOS kwaajili ya mikopo ya wanawake na vijana

- Uhamasishaji wa wanawake na vijana kujiunga katika vikundi unaendelea katika ngazi ya kata

- Elimu ya ujasiriamali inatolewa

- SACCOS mbili zitakazotoa mikopo kwa wanawake na kwa vijana zimekwisha ainishwa

- Maombi ya mkopo yanaendelea kuwasilishwa katika SACCOS husika


6.Bima ya Afya

Zoezi hili halijaanza ila tunategemea ifikapo April 2017, ziwe zimetolewa bima si chini ya 5000 na makampuni mbali mbali


HITIMISHO

Hiyo ndiyo taarifa fupi ya maendeleo ya mradi na hatua zilizofikiwa katika vipaumbele vyetu vyote kwa mwezi August mpk October.
Kama hukuweza kuona taarifa ya mradi ni hii hapa[emoji115]
 
Hivi kuna tofauti gani leo ukiiangalia manispaa chini ya CDM na ile ikiwa chini ya CCM (2010-2015)?, kuna tofauti gani kati ya Lwakatare na Kagasheki (2010-2015)?, kuna tofauti gani kati ya wapinzani na CCM?

Nikiwasema hawa jamaa watu wapuuzi wanakimbilia kwenye vyama na kuanza kusema we fulani eti uko CCM, maendeleo hatuhitaji tena kuanza kuchunguzana vyama, ili iweje? Usikosoe, utaitwa hivi. Usisifie, utaonekane vile, basi tu ilimradi u-vyama wao.

Naamini kabisa, hawa nao ni kama wengine tu, hawana kipya, manispaa nzima iko chini yao lakini hamna kitu. Sijuhi kwanini hawaendi hata kujifunza kwa sugu kidogo ama kwa dogo janja? Lwakatare ni mtu hasiye jituma na mwoga wa kuwasiliana, ni mbunge asiye na ubunifu hata kidogo. Kwanza miradi wanayohangaika nayo ilibuniwa wakati wa CCM, yeye ni kitu gani kawahi kubuni na kakisimamia kikazaa matunda? Tumefeli sana, it's another downfall upon our mission and vision, hatuwezi kuendelea kwa aina ya viongozi wa (kisiasa) walio chini ya mbunge ukianza na mbunge mwenyewe kwasababu hawaelewi vitu vingi sana kuanzia mawasiliano mpaka uongozi kwa ujumla. Huyo meya hata exposure hana, sasa atajifunza wapi na kwa nani?

Vyama vya siasa havina tija Tz, ni mzigo na ni upuuzi mtupu.
 
Kama hukuweza kuona taarifa ya mradi ni hii hapa[emoji115]
Kama utapata kilichoongelewa jana kwenye kikao cha maendeleo cha mkoa tunaomba utupenyezee ili tuelewe wenzetu walipokutana waliongea nini make nimemwona Prof. Tibaijuka, Meya, mb.wa karagwe n.k
 
Ahaaaaaaah! do we have any more?
Mwaka unaisha hivi hivi, kama utani vile. Every thing is just centered around bwana yule a.k.a Lwakatare.

Bwana huyu alianza mashindao aso yaweza, habari za mpango wake mwenyewe zinamzidi kilo, kawa mwepesi wa kuubeba mkonga wake mwenyewe na sasa anajificha uvunguni mwa meza kila uchao. Aje tu apulize firimbi ili mchezo uishe.
 
Suala la misaada ya waathirika wa tetemeko limeishia wapi?

Sioni kinachoendelea zaidi, au mshanogewa na senene?
 
Ahaaaaaaah! do we have any more?
Mwaka unaisha hivi hivi, kama utani vile. Every thing is just centered around bwana yule a.k.a Lwakatare.

Bwana huyu alianza mashindao aso yaweza, habari za mpango wake mwenyewe zinamzidi kilo, kawa mwepesi wa kuubeba mkonga wake mwenyewe na sasa anajificha uvunguni mwa meza kila uchao. Aje tu apulize firimbi ili mchezo uishe.
Punguza machungu mkuu, muda ndio utakaoamua. Mji wa Bukoba eti tunazidiwa na Kigoma... Inakujia akilini kweli?
 
[emoji441]Taarifa ya Mkutano wa 'TUSHIRIKISHANE'

Napenda kutumia fursa hii kuwajulisha kuwa siku ya kesho Ijumaa Dec 2, 2016 nitakuwa mwenyeji wa Mbunge wa Bukoba Mjini, Mh. W. Lwakatare katika mkutano wa kujadili hatua za maendeleo ya vipaumbele vya Mradi wa TUSHIRIKISHANE.

Mkutano huu utafanyika kwenye ukumbi Halmashauri ya Manispaa kuanzia saa 8 mchana.

Wadau wenye maslahi na Jimbo la Bukoba Mjini mnakaribishwa kuhudhuria au kushiriki kwa njia zingine za Mawasiliano.

Asanteni kwa ushirikiano katika kuijenga Bukoba Mpya.
 
Kwanza miradi wanayohangaika nayo ilibuniwa wakati wa CCM, yeye ni kitu gani kawahi kubuni na kakisimamia kikazaa matunda?

Naomba kibali cha kudandia treni kwa mbele kuhusiana na mada 'quoted' hapo juu.

Mtazamo wangu ni, si vibaya kuendeleza miradi iliyoanzishwa na waliokutangulia ali mradi ilikuwa ya manufaa kwa jamii inayokuzunguka. Haina mantiki kubuni miradi mipya ilhali iliyokuwepo ambayo ilihitaji usimamizi wako tu inakufa kwa kisingizio cha aidha ilianzishwa na wapinzani wangu au natakiwa kubuni mipya.

Pili, ubunifu si kuunda tairi jipya. Ubunifu waweza pia kuongeza ubora kwenye tairi lililoundwa na mwingine ili kulipa maisha marefu ya kutumika, usalama, nk.

Baada ya kusema hayo naomba kusimamisha treni nishuke.

Nawasilisha,
Mentor.
 
Punguza machungu mkuu, muda ndio utakaoamua. Mji wa Bukoba eti tunazidiwa na Kigoma... Inakujia akilini kweli?
Ndugu yangu kuna mda nikiongea unanipinga sana lakini naamini kuna baadhi ya maeneo tunaelewana walau. Nikisema nchi hii wapinzani ni maneno tu na hawana tofauti na CCM unahisi nawachukia, hawa jamaa tujukubali tukatae ni mizigo na hawajitambui. Wanadai waruhusiwe kuandamana wakati mipango tu ya jimbo inawashinda kuisimamia, watu wa hivi wana faida gani? tuwatofautisheje na wale wa kijani?
 
[emoji441]Taarifa ya Mkutano wa 'TUSHIRIKISHANE'

Napenda kutumia fursa hii kuwajulisha kuwa siku ya kesho Ijumaa Dec 2, 2016 nitakuwa mwenyeji wa Mbunge wa Bukoba Mjini, Mh. W. Lwakatare katika mkutano wa kujadili hatua za maendeleo ya vipaumbele vya Mradi wa TUSHIRIKISHANE.

Mkutano huu utafanyika kwenye ukumbi Halmashauri ya Manispaa kuanzia saa 8 mchana.

Wadau wenye maslahi na Jimbo la Bukoba Mjini mnakaribishwa kuhudhuria au kushiriki kwa njia zingine za Mawasiliano.

Mwenye swali, maoni au mapendekezo yoyote kuhusiana na maendeleo ya Bukoba Mjini awasilishe kwangu kupitia no. 0620-883020

Asanteni kwa ushirikiano katika kuijenga Bukoba Mpya.
Dada Happy habari ya mchana!
Naelekea moja kwa moja kwenye mada yako.

1. Tumeshaongea na kushauri sana kupitia chombo hiki, tunachoweza kusema ni; wewe pitia kurasa kwenye mada hii tokea nyuma utaona hayo mengi tuliyokuwa tunasisitiza, kushauri na kuchangia kwa ujumla ...ni mengi sana kusema kweli.

2. Tunaomba na tunasisitiza, mbunge na meya watambue rasmi nguvu ya mitandao ya kijamii, wajifunze kuongea, kupokea na kutoa habari pasipo shuruti. Wajifunze kwa wenzao kwasababu sie wengine hatupati nafasi kufika hapo BMC lakini kwenye mitandao tuko active kweli kweli, waache kujifungia maofisini na kujipoteza mbele ya jamii.

3. Naleta wazo la kimaendeleo. Hii ni kuhusu Uwanja wa Kaitaba. Navyojua mie ule uwanja uko chini ya BMC na si wa chama kama vingine mfano ule wa Kirumba, Kambarage n.k. Huu uwanja ni kitega uchumi, huu uwanja ni mradi mzuri sana kimaendeleo. Ukiutumia huu uwanja utawasaidia sana kukuza mapato ya BMC, hawatashindwa kupata mamilioni ya sh. kwa mwaka. Sasa nini kifanyike, watafute watu wajenge majukwaa kwa kuwekeza pale, waweke maduka n.k, waweke hotel/restaurant n.k. Waweke taa na mambo ya namna hiyo, watu wanakosa kuja kwasababu huduma nzuri hazipo. Uwanja uvutie na iwe sehemu ya kivutio cha kitega uchumi, tusikimbilie vikubwa tu wakati hivi vilivyopo vinaachwa hovyo. Tayari TFF wamesaidia vya kutosha sasa baraza la madiwani waangalie wavutie michezo, hili litasaidia ukuaji wa mapato, mji, mahoteli, utalii n.k. Michezo sahivi ni uchumi na ni fursa, wakae kimichezo na wawaze kifursa zaidi.
 
Dada Happy habari ya mchana!
Naelekea moja kwa moja kwenye mada yako.

1. Tumeshaongea na kushauri sana kupitia chombo hiki, tunachoweza kusema ni; wewe pitia kurasa kwenye mada hii tokea nyuma utaona hayo mengi tuliyokuwa tunasisitiza, kushauri na kuchangia kwa ujumla ...ni mengi sana kusema kweli.

2. Tunaomba na tunasisitiza, mbunge na meya watambue rasmi nguvu ya mitandao ya kijamii, wajifunze kuongea, kupokea na kutoa habari pasipo shuruti. Wajifunze kwa wenzao kwasababu sie wengine hatupati nafasi kufika hapo BMC lakini kwenye mitandao tuko active kweli kweli, waache kujifungia maofisini na kujipoteza mbele ya jamii.

3. Naleta wazo la kimaendeleo. Hii ni kuhusu Uwanja wa Kaitaba. Navyojua mie ule uwanja uko chini ya BMC na si wa chama kama vingine mfano ule wa Kirumba, Kambarage n.k. Huu uwanja ni kitega uchumi, huu uwanja ni mradi mzuri sana kimaendeleo. Ukiutumia huu uwanja utawasaidia sana kukuza mapato ya BMC, hawatashindwa kupata mamilioni ya sh. kwa mwaka. Sasa nini kifanyike, watafute watu wajenge majukwaa kwa kuwekeza pale, waweke maduka n.k, waweke hotel/restaurant n.k. Waweke taa na mambo ya namna hiyo, watu wanakosa kuja kwasababu huduma nzuri hazipo. Uwanja uvutie na iwe sehemu ya kivutio cha kitega uchumi, tusikimbilie vikubwa tu wakati hivi vilivyopo vinaachwa hovyo. Tayari TFF wamesaidia vya kutosha sasa baraza la madiwani waangalie wavutie michezo, hili litasaidia ukuaji wa mapato, mji, mahoteli, utalii n.k. Michezo sahivi ni uchumi na ni fursa, wakae kimichezo na wawaze kifursa zaidi.
Shukran sana ndugu Rweye kwa kushiriki[emoji120]
 
BAADHI YA MAFANIKIO YA MRADI WA TUSHIRIKISHANE

a70fd2b0c56005c95042f72a4e229d44.jpg
90314275906286ffeb492753ebb59045.jpg
36bce4a9baf6a8da9c5d73aec9a52088.jpg


Msingi wa mradi huu ni Ushirikishwaji wa wananchi katika shughuli za maendeleo ya Bukoba yao kama jina la mradi linavyosadifu. Hivyo pamoja na vipaumbele vyetu vinne (rejea taarifa za nyuma) ambavyo tulikubaliana kutekeleza kwa pamoja, msisitizo hasa wa mradi uko katika UTOAJI na UPATIKANAJI wa taarifa kwa wananchi ili waweze kufahamu kinachoendelea na kushiriki katika hatua zote za maendeleo.

Tumefurahi na tunampongeza Mbunge Wilfred Lwakatare kwa kuanza kulifanyia kazi swala hili mtambuka. Tunasisitiza Halmashauri pia kufuata nyayo zake. Wito huu wa kutoa taarifa pia uwafikie wadau mbali mbali wa maendeleao ya Bukoba.

Wananchi pia wanapaswa kufatilia, kuhoji na kushiriki kikamilifu kwamaana maendeleo hayataletwa na viongozi tu
 
Tangia huu mradi uanze ni mda sasa, kuna kipi ambacho tayari kimefanyika? siulizi kwa mabaya ila tu kwa maendeleo! Tuliona mmetuwekea vipaumbele vya kufanya!

Ndio tunajua kuwa mambo ya tetemeko yalirudisha michakato nyuma ila haizuii kutoa taarifa ya maendeleo ya Mradi.
Asanteni na Nawatakia utekelezaji mwema
 
Back
Top Bottom