TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

hehhehe hivi ule mpango wenu wa kuigeuza bikoba kuwa dubai umefikia wapi? naomba updates plz
 
Sasa hebu tupeni kidogo, kuna hatua yoyote ambayo labda ishaanza katika ujenzi rasmi wa mradi wowote kati ya stand na soko make kama ni michoro kwenye tumeiona mda mrefu, vikao vimeshakaa vya baraza la madiwani n.k .Tujulishe mkuu kuna hata jiwe moja limeshawekwa kama starting point ya kujenga msingi? Asante!
Ujenzi wa stand mpya maendeleo yaliyofanywa karibuni ni kulipa fidia kwa watu watatu waliokuwa wamegoma sh 12,000,000 kama walivyokubali baadae na watu wa Nemc kuja kufanya tathimini tayari. Tunasubiri kupata certificate yao soon. Hatutakuwa na kikwazo zaidi.
 
Sasa hebu tupeni kidogo, kuna hatua yoyote ambayo labda ishaanza katika ujenzi rasmi wa mradi wowote kati ya stand na soko make kama ni michoro kwenye tumeiona mda mrefu, vikao vimeshakaa vya baraza la madiwani n.k .Tujulishe mkuu kuna hata jiwe moja limeshawekwa kama starting point ya kujenga msingi? Asante!
Ujenzi wa soko maandalizi yanakwenda vizuri. Wiki ijayo consultant na watu wa TIB watakuwa hapa Bukoba kwa mazungumzo. Kila kitu kinaendelea vizuri.
 
Ratiba ya utekelezaji iko wapi ili tukienda rikizo Xmass tupitie kuona maendeleo ya utekelezaji labda tunaweza kutupia kwenye account.
Nimeeleza hatua tulizofikia katika utekelezaji nikijibu hoja ya mjumbe mmoja wapo humu
 
Mtani

Tupo pamoja kabisa, pia nawasifu nyie kwa kuungana na team ya JF kujaribu kupiga hatua kupitia huu utaratibu wa kujipima.

Naamini kama ulivyosema tuanze na hayo madogo then tuone tutafikia wapi na tutaanza vipi kwa yale makubwa.

Hongereni sana, ila nisadie kumuuliza Melo - why huku kwa babu zenu hajafika?
Anaweza kuja kujibu mwenyewe lkn taarifa ni kwamba mradi umeanzia kwa majaribio ndani ya majimbo 8 kama sio 9 kwa tanzania nzima, then ikionyesha inaleta tija basi majimbo yote yatafikiwa. Jifunze kwanza kupitia huku kwetu.
 
  • Thanks
Reactions: bdo
Suala la mbwembwe si kwetu tu bali hata serikali kuu, umeona maamuzi mangapi ya kila aina ya mbwembwe yametolewa lakini yanaishia hewani.

Ujenzi wa Soko na Stendi kuu ya mabasi ni vitu ambavyo tumekuwa tukivitaka miaka yote, kila mbunge anayeingia anakuja na ahadi hizo lakini mwisho wa siku mnaingiza siasa na miradi kama hiyo inakufa zaidi tunaoneshwa ramani za miradi hiyo, sasa sijui ramani zinatusaidia nini!!! Tunataka miradi ikamilike. Siasa za kukomoana hatutaki tena Bukoba maana zinazidi kutuumiza sisi wananchi.
Kwa kipindi hiki figisu figisu hazina nafasi. Kazi zinaendelea, ondoa shaka.
 
Asante sana Jamii Forums,,,,,
kwa hili najua maendeleo lazima yapatikane,,,
Asante pia wakuu viongozi husika kwa kukubali wito maana kwa kufanya hivyo ndiyo njia pekee ya kuweza kufikia malengo
Asante sana, michango yenu ya mawazo ni muhimu pia ili tushirikishane kikamilifu kuhakikisha tunasonga mbele
 
Ndugu wananchi wa Bukoba,

Katika mradi wa "Tushirikishane" kwa BM tumekubaliana vipaumbele vinne ambavyo ni;

i) Ujenzi wa Soko Kuu, Soko la Kashai na Stand mpya ya Kyakailabwa

ii) Urasimishaji Makazi

iii) Mikopo kwa Wanawake na Vijana

iv) Bima ya Afya

Nitawashirikisha hatua zilizokua zimefikiwa katika vipaumbele vitatu (3) vya awali (kwa kufuata mpangilio hapo juu) kabla ya kutokea janga la tetemeko.

1. UJENZI WA SOKO KUU, KASHAI NA STAND YA KYAKAILABWA

Tayari TIB wamekubali kutoa 70% ya pesa ya kujenga soko kuu sawa na 13 billion tsh. 30% ya pesa inayobaki itatolewa na BMC ama kwa ubia au wao wenyewe.

Eneo la muda lililopendekezwa kuhamia wafanyabiashara wa Soko kuu ni eneo la KCU jiran na Rumuli na Police. Mazungumzo baina ya BMC na TIB yanaendelea ili kupata msaada wa kujenga soko la muda

Tathmini ya mazingira imekwisha fanyika kwa Stand, Soko Kuu na soko la Kashai. BMC inasubiri tu vyeti

Waliokua wakidai fidia ya eneo litakalojengwa Stand Mpya ya Kyakailabwa tayari wamekwisha lipwa.

2. URASIMISHAJI MAKAZI

Tiyari zoezi limekwishaanza Kashai na hatua iliyokuwa ikifanyika na imekamilika ni kuunda vikundi vitatu vyenye mitaa 3 kwa kila kikundi hivyo kuleta jumla ya mitaa 9 ya kata nzima ya kashai.

Vikundi hivyo vimesajiliwa na Mkurugenzi wa manispaa ili kupata haki ya kufungua akaunti na kupata stakabadhi za malipo.

Vikundi viko kama ifuatavyo:-
1. Kashenye
Kilimahewa
National Housing

2. Mafumbo
Matopeni
Lwome

3. Kashai Halisi
Kisindi
Katotolwansi

Hatua iliyokua imefikiwa ni uhamasishaji wa nyumba kwa nyumba ili wakazi watambue umuhimu wa kupimiwa wa zoezi na waende kulipia garama ya 200000 kupitia akaunti za vikundi walivyomo ili upimaji uanze baada ya malipo kukamilika.

Zoezi lilikwisha anza na pia kata Bakoba, nyumba zilizozipimwa mpk sasa ni 724 kwa mitaa miwili ya Nyakanyasi na Mtoni. Mitaa ya Forodhani na Buyekela zoezi linaendelea

3. MIKOPO KWA WANAWAKE NA VIJANA

Uhamasaishaji wa wananchi kuunda vikundi, na elimu ya mikopo na namna gani ya kupata mikopo umeanza kata ya Bakoba na Kashai

Aidha, jitihada za kufanikisha vipaumbele vya "Tushirikishane" zimesuasua wakati huu wa janga la "tetemeko" ofisi ya Mbunge na BMC kwa pamoja zimeelekeza nguvu zao katika janga. Pia wananchi wa Bukoba wanahitaji kusikia kuhusu janga na hali ya Bukoba ilivyo kwa sasa kuliko kitu kingine chochote.

Pia kuna ishara ya kuwa baadhi ya vipaumbele havitafikiwa ndani ya miezi 9 ya mradi kama ilivyokua imetarajiwa. Mfano Urasimishaji Makazi, inawezekana kusuasusa kwasababu; Kila nyumba inatakiwa kuchangia 200000/- katika kufanikisha hili ambayo ishaonekana kuwa changamoto kwa sasa; Nyumba zilizoathirika ni nyingi sana, kuna zinazoonekana zimesimama lkn hazifai kuishi ni za kujenga upya; Jitihada za serikali hazishawishi kuwa ndani ya miezi 9 watu watakua wamerejea ktk maisha yao ya kawaida. Hivyo, inawezekana swala la Kurasimisha Makazi lisipate mwitikio mzuri kutoka kwa wananchi

====Edited====

Lakini pia inawezekana kutumia janga la 'tetemeko' kama fursa, kuhamasisha wananchi wengi zaidi kujiunga na Bima ya Afya.

Hatua za mradi wa "Tushirikishane" zilizofikiwa kabla ya "tetemeko" zinatia moyo. Ni maombi yetu kuwa kipindi hiki kigumu kipite haraka.

Bwana Atuwezeshe!
 
Mradi wa Tushirikishane (JamiiForums yazindua rasmi mradi wa "Tushirikishane") umeanza rasmi jimbo la Bukoba mjini chini ya Uongozi wa Mheshimiwa Mbunge Wilfred Lwakatare.

Tokana na misingi ya TUSHIRIKISHANE iliyoelemea katika kuwawezesha wabunge wa kuchaguliwa kutekeleza ahadi 4 kati ya jumla ya ahadi walizotoa wakati wa uchaguzi kwa urahisi kwa kushirikiana na wananchi; mada hii itatumika kuwasilisha, kujadili na kupeana taarifa ya kile kinachojiri Bukoba mjini.

Ahadi walizochagua kufuatilia wananchi wa Bukoba mjini kwenye mradi wa TUSHIRIKISHANE

a. Ujenzi wa soko kuu la Bukoba, soko la Kashai na Stendi kuu ya mabasi Bukoba

b. Mikopo ya vikundi vya kijasiriamali vya akina mama na vijana

c. Urasimishaji wa makazi

d. Bima za afya kwa wananchi angalau​

View attachment 389799

Mawazo ni mazuri ingawa wengi wetu tulitegemea haya mambo tuyaone kama taarifa katika utekelezaji wake na wala siyo kukusanya mawazo kupitia JF.
USHAURI WANGU
Kwa viongozi wa halmashauri mnaohusiki msipo angalia mtamaliza vipindi vyenu hata kufanya chochoe. Hii ni kwa Mhs Mbunge na Mayor etc.
Cha kufanya kwa mwendo wa KASI, ninapendekeza kwa issue ya SOKO na Stand, weka mikakati kwa kushirikiana na Bank mojawapo ili mpate mkopo wenye uafadhari wa masharti na kusimamia nyie hizo projects. Isimamiwe kama unavyosimamia ujenzi wa nyumba yako mwenyewe otherwise watu wa BKB ni watu wa deal na mtaanguka. Na mkicheza bila kufanya haya hata katika chaguzi zijazo hamna lenu, maana tunawasubiri katika hili. Nafasi mnayo na sasa fanya kazi.
NB: Tafuta mchumi mzuri na alipwe ili aifanyie kazi. Ikishindikana kaangalie halmsahauri zilizofanikiwa hapa Tanzania na copy ili haya mambo yafanyike haraka sana.
Haya tunawasubiri.......

Meya wa Manisapaa ya Bukoba, Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini na Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media wakisaini makubaliano ya kushiriki katika utekelezaji wa Mradi wa Tushirikishane


Mada hii itatumika zaidi na Wana Bukoba kutupa taarifa.

Baadhi ya Washiriki watakuwa:-

1. Mh. Mbunge Wilfred Lwakatare
2. Katibu Alex Xavery (Katibu)
3. Happiness Essau (Afisa habari Bukoba)
4. Chief Karumuna (Mayor wa Bukoba)
5. Jimmy Kalugendo (Naibu Mayor)
6. Na washiriki wote wa Warsha hiyo na wale wote wenye mapenzi ya Maendeleo ya Bukoba mjini.

Karibuni...
 
Taarifa imekaa vizuri sana, Tumuombe Mungu atutoe haraka katika janga hili la tetemeko la ardhi ili turudi kwa pamoja kupiga kazi.
 
Suala la Tetemeko sasa hivi kama limepoa, watu wanaishi maisha ya tabu misaada bado haijawafikia. Sijui kama wanabukoba tuna msaada gani kwa wahanga maana rais ametuambia tetemeko halijaletwa na serikali.

Mambo mengine serikali inajichanganya. Kuna wafanyabiashara walisema kukarabati shule zilizokumbwa na tetemeko (Ihungo na Nyakato), serikali nayo ikasema itakarabati. Ukweli sielewi hapa.
 
Back
Top Bottom