Uko sahihi mkuu. Unajua sehemu kubwa ya manispaa/mkoa kwa ujumla ilikuwa bado iko underutilised kama pamelala hivi ndo kila mtu akawa anatukebehi na wakasahau endapo vitu vyake vikianza kutumika ipasavyo itakuwa ni kimbilio la kila mtu sasa wanaanza kukana maneno yao wenyewe. Ni jambo jema sana kwamba wananchi wanao uwezo wa kujimultiply na ukizingatia raisi kasema anataka kuifanya Kager a mkoa wa uwekezaji, tulia uone. Naamini hadi mwaka huu ukaishe tutakuwa tunaongea mambo tofauti kabisa, mambo mengi yako njiani kwa kasi isiyo ya kawaidabukoba inakuja kwa kasi.mpaka raha.
Nadhani umimi umetutawala sana, ila tukiacha hayo tukashirikiana hata kwa kutoa maoni nadhani bado tuna nafasi ya kurudisha heshima ya mkoa wetu. Kujifanya mambo ya kagera hayakuhusu kisa upo mikoa ya watu haikufanyi mtu usiwe wa kagera Kwa hiyo kama kuna kitu hakiendi vizuri huko lazima watu wanaokujua watakunyooshea kidole kwamba mbona kwenu kuko hivi.Hata mi huwa nashangaa watu wanauona Uzi tena ni wa bukoba halafu wanapita tu sijui bukoba nani alituroga yaani watu tunasahau nyumbani kiasi hicho tunahitaji sala nyingi kweli
Kumbe umeona eti.hivi sasa mji unabadirika haraka na kukua kwa kasi sana sio kama zamani ila miundombinu ASA katikati ya mji bado ni changamoto kati kati kuna udongo mwekundu ,barabara sio kubwa,mitaro nk .ningeomba manispaa ijenge barabara za mjini kati kama walivyotengeneza ya rwamishenye au ya pale kanoni yaani udongo usiwepo mjini ,kuwepo na taa na traffic light,round about za maana ,nk hapo mji wa bukoba utavutia zaidi ila kimajengo yaani ujenzi wa maghorofa na nyumba speed inaridhisha kuliko miji mingi tzbukoba inakuja kwa kasi.mpaka raha.
Mkuu soko limefikia wapi ? Mbona mwaka umepita sasaUjenzi wa soko maandalizi yanakwenda vizuri. Wiki ijayo consultant na watu wa TIB watakuwa hapa Bukoba kwa mazungumzo. Kila kitu kinaendelea vizuri.
Wakuu mnakaribishwa kuleta mawazo yenu ili kuendeleza mji wa bukoba ambayo ndo sura ya mkoa wa kagera.mmepotea siku hiziBukoba isonge mbele.naimani itawezekana
Kwakweli nafurahi sana kuona mkuu Maxence Melo kwanza..ametupatia chombo huru cha habari cha kueleza maoni yetu..Pili sasa kaja hili swala la maendeleo..Kweli mkuu ubarikiwe na MUNGU na timu yako nzima.
Ratiba ya utekelezaji iko wapi ili tukienda rikizo Xmass tupitie kuona maendeleo ya utekelezaji labda tunaweza kutupia kwenye account.
Ila wewe, dah! wahenga wangelikuwepo ungepigwa adhadu, hujui ishami zamani walikuwa wanatengeneza mboga?
teh
Mkuu tunakuomba uje ujibu hoja zetu hukuTuko pamoja, michango yenu ya mawazo ni muhimu sana
Mkuu upo wapi siku hizi karibu tenaNdugu wananchi wa Bukoba,
Katika mradi wa "Tushirikishane" kwa BM tumekubaliana vipaumbele vinne ambavyo ni;
i) Ujenzi wa Soko Kuu, Soko la Kashai na Stand mpya ya Kyakailabwa
ii) Urasimishaji Makazi
iii) Mikopo kwa Wanawake na Vijana
iv) Bima ya Afya
Nitawashirikisha hatua zilizokua zimefikiwa katika vipaumbele vitatu (3) vya awali (kwa kufuata mpangilio hapo juu) kabla ya kutokea janga la tetemeko.
1. UJENZI WA SOKO KUU, KASHAI NA STAND YA KYAKAILABWA
Tayari TIB wamekubali kutoa 70% ya pesa ya kujenga soko kuu sawa na 13 billion tsh. 30% ya pesa inayobaki itatolewa na BMC ama kwa ubia au wao wenyewe.
Eneo la muda lililopendekezwa kuhamia wafanyabiashara wa Soko kuu ni eneo la KCU jiran na Rumuli na Police. Mazungumzo baina ya BMC na TIB yanaendelea ili kupata msaada wa kujenga soko la muda
Tathmini ya mazingira imekwisha fanyika kwa Stand, Soko Kuu na soko la Kashai. BMC inasubiri tu vyeti
Waliokua wakidai fidia ya eneo litakalojengwa Stand Mpya ya Kyakailabwa tayari wamekwisha lipwa.
2. URASIMISHAJI MAKAZI
Tiyari zoezi limekwishaanza Kashai na hatua iliyokuwa ikifanyika na imekamilika ni kuunda vikundi vitatu vyenye mitaa 3 kwa kila kikundi hivyo kuleta jumla ya mitaa 9 ya kata nzima ya kashai.
Vikundi hivyo vimesajiliwa na Mkurugenzi wa manispaa ili kupata haki ya kufungua akaunti na kupata stakabadhi za malipo.
Vikundi viko kama ifuatavyo:-
1. Kashenye
Kilimahewa
National Housing
2. Mafumbo
Matopeni
Lwome
3. Kashai Halisi
Kisindi
Katotolwansi
Hatua iliyokua imefikiwa ni uhamasishaji wa nyumba kwa nyumba ili wakazi watambue umuhimu wa kupimiwa wa zoezi na waende kulipia garama ya 200000 kupitia akaunti za vikundi walivyomo ili upimaji uanze baada ya malipo kukamilika.
Zoezi lilikwisha anza na pia kata Bakoba, nyumba zilizozipimwa mpk sasa ni 724 kwa mitaa miwili ya Nyakanyasi na Mtoni. Mitaa ya Forodhani na Buyekela zoezi linaendelea
3. MIKOPO KWA WANAWAKE NA VIJANA
Uhamasaishaji wa wananchi kuunda vikundi, na elimu ya mikopo na namna gani ya kupata mikopo umeanza kata ya Bakoba na Kashai
Aidha, jitihada za kufanikisha vipaumbele vya "Tushirikishane" zimesuasua wakati huu wa janga la "tetemeko" ofisi ya Mbunge na BMC kwa pamoja zimeelekeza nguvu zao katika janga. Pia wananchi wa Bukoba wanahitaji kusikia kuhusu janga na hali ya Bukoba ilivyo kwa sasa kuliko kitu kingine chochote.
Pia kuna ishara ya kuwa baadhi ya vipaumbele havitafikiwa ndani ya miezi 9 ya mradi kama ilivyokua imetarajiwa. Mfano Urasimishaji Makazi, inawezekana kusuasusa kwasababu; Kila nyumba inatakiwa kuchangia 200000/- katika kufanikisha hili ambayo ishaonekana kuwa changamoto kwa sasa; Nyumba zilizoathirika ni nyingi sana, kuna zinazoonekana zimesimama lkn hazifai kuishi ni za kujenga upya; Jitihada za serikali hazishawishi kuwa ndani ya miezi 9 watu watakua wamerejea ktk maisha yao ya kawaida. Hivyo, inawezekana swala la Kurasimisha Makazi lisipate mwitikio mzuri kutoka kwa wananchi
====Edited====
Lakini pia inawezekana kutumia janga la 'tetemeko' kama fursa, kuhamasisha wananchi wengi zaidi kujiunga na Bima ya Afya.
Hatua za mradi wa "Tushirikishane" zilizofikiwa kabla ya "tetemeko" zinatia moyo. Ni maombi yetu kuwa kipindi hiki kigumu kipite haraka.
Bwana Atuwezeshe!
Mheshimiwa tunakukaribisha tena kujibu hoja zetu hukuView attachment 404994 LEO NIMEWASILISHA RIPOTI YA KIKAO NILICHOKIFANYA NA BAADHI YA WANA KAGERA WAISHIO JIJINI DAR ES SALAAM KWA MKUU WA MKOA KAGERA.
View attachment 405000 View attachment 405001 View attachment 405002 View attachment 405003 View attachment 405003 View attachment 405003 View attachment 405004
MH. MKUU WA MKOA,
KAGERA.
MAAZIMIO YALIYOPITISHWA KWENYE KIKAO KILICHOITISHWA NA MH. WILFRED LWAKARATE(MB), MBUNGE WA JIMBO LA BUKOBA MJINI, KUJADILI ATHARI ZA TETEMEKO LA ARDHI MKOANI KAGERA, KUONA JINSI YA KUSAIDIA WALIOPATWA NA MADHARA.TAREHE 18 SEPTEMBA, 2016 KWENYE HOTELI YA KEBBY'S, MWENGE, DAR ES SALAAM.
1. Kwa kauli moja kikao kimetambua na kuishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua zakuridhisha kufuatia janga hili, ikiwa ni pamoja na ;
i. Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa, (Mb), Waziri Mkuu, pamoja na kiongozi mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Mh. Freeman Aikael Mbowe (Mb) kufika B ukoba mara moja kuona athari za tetemeko na kushiriki mazishi ya watu waliofariki kutokana na janga hili na pia kuwafariji waliojeruiwa na kuathirika kwa namna mbali mbali.
ii. Kuandaa mkutano wa kuishirikisha jumuiya ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na jumuiya ya wafanyabiashara kwa lengo la kukusanya misaada kwa ajili ya kukabiliana na janga hili.
iii. K uandaa matembezi ya hisani kwa ajili ya kukusanya fedha za kusaidia nakukabiliana na madhara ya janga hili.
iv. Viongozi waandamizi mbali mbali waserikali, wakiwemo Mawaziri, Viongozi mbalimbali wa kisiasa, Makatibu wakuu na wakuu wa vitengo muhimu vinavyo husiana na maafa kufika kwenye eneo la tukio kwa haraka.
2. Kwa kauli moja kumuomba Mh. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwa ndiye baba wa nchi, pamoja na shughuli zake nyingi, kutenga siku mapema itakavyo mpendeza kufika mkoani Kagera kuwapa pole wananchi wake kutokana na janga hili. Tunaamini walioathirika watafarijika sana kumuona Rais wao akiwa nao kwenye eneo la tukio.
4. Kwa kuwa janga hili la kitaifa halina itikadi ya siasa, dini, rangi, kabila wala ubaguzi wa aina yoyote ile, hivyo ushiriki wa watu wote ni muhimu sana.
5. Kwa kutambua ukweli wa walioathirika zaidi ni wananchi wa mkoa wa Kagera, inawapasa wao kuwa msitari wa mbele katika kushiriki katika juhudi zote zinazofanyika, kwa njia na jinsi yoyote inayowezekana, iwe ni kwa hali au mali, mshikamano wao katika janga hili ni muhimu sana. Mpaka sasa, imejidhihirisha kwamba ushiriki wa wana Kagera bado ni hafifu sana. Wana kagera wanahimizwa kutokukata tamaa nakuamsha hari ya kushirikiana katika kuusaidia mkoa wao kwa nidhamu ya hali ya juu . Ili kusisitiza umuhimu huo, mfano wa kwamba ili kuweza kupewa msaada wa usafiri (lift) ni lazima uwe njiani, unahusika.
6. Kwamba kutokana na mkoa wa Kagera kukumbwa na maafa makubwa na mengi mfululizo kuanzia miaka ya 1970 zilipoanza chokochoko za nduli Iddi Amini wa Uganda, vita vya Uganda , Ukimwi, mdudu wa migomba (ekiuka), madhara ya wakimbizi kutoka nchi jirani yaliyo leta ujambazi , kufa kwa Vyama vya Msingi vya Ushirika na Chama Kikuu cha Ushirika (BCU/ KCU) kulikoambatana na kuanguka kwa bei ya zao la kahawa, kuanguka kwa Shirika la Reli Tanzania (TRC), kulikosababisha bei za bidhaa za viwandani ambavyo vingi vipo Dar es salaam, kuwa juu kuliko sehemu nyingine yoyote ya Tanzania, ugonjwa wa mnyauko ambao umeangamiza kabisa migomba na zao lake ndizi, na sasa ni janga la tetemeko. Majanga hayo yote ni sababu kubwa kwa mkoa wa kagera kushuka sana kiuchumi kutoka kati ya mikoa mitatu tajiri miaka ya 70 - 80 hadi kuwa kati ya mikoa mitano masikini sana nchini. Serikali inaombwa ichukue hatua za makusudi kutoa upendeleo wa kisera wa kuusisimua upya uchumi (a stimulus package) kwa mkoa wa Kagera kwa kufanya yafuatayo :
i. Kutoa msamaa wa kodi zote kwenye bidhaa zote za ujenzi zinazouzwa mkoani Kagera kwa kipindi cha miaka kumi.
ii. K wa kutambua madhara ya mdororo wa uchumi wa mkoa wa Kagera kwa muda mrefu hivyo kuwepo tatizo kubwa la ajira na umasikini, miradi yote ya ujenzi wa miundombinu ya kijamii kama mashule, zahanati, vituo vya afya na majengo mengine ya serikali yatakayo jengwa upya au kukarabatiwa, ugawaji wa kandarasi ufanywe kwa mtindo wa uwezeshaji kwa makampuni yaliyopo na yanayoendesha shughuli zao mkoani kagera yenye uwezo, wakishirikiana na makampuni ya wana -Kagera walioko nje ya mkoa pale inapobidi . Vigezo vitaandaliwa ili vizingatiwe.
7. Kwa kutambua kuwa serikali imeunda kamati za maafa za Kitaifa na Mkoa ambapo Wabunge wa mkoa wa Kagera wameshirikishwa, ni vyema ushiriki kwenye kamati hizo upanuliwe na kuzijumuisha taasisi za dini ambazo mkoani kagera zimekuwa na mchango mkubwa katika utoaji wa huduma za jamii kwa miaka mingi. Hatua hii itasaidia kuongeza ufanisi katika zoezi zima la uthamini wa madhara, ukusanyaji wa taarifa na usambazaji wake. Aidha kwenye hizo kamati uwepo umuhimuwa ku wahusisha wataalam wa habari kuongeza ufanisi katika upashanaji wa habari .
8. Kwa kuzingatia mamlaka ya Mbunge anayopewa na katiba ya jamhuri ya Muungano wa T anzania, mifuko ya majimbo pia itumike kusaidia kwenye majanga yamaafa kama haya.
9. Kwa kukubali kwamba bado uitikiaji na ushiriki wa wana -Kagera bado ni hafifu sana, juhudi mpya zifanyike kwa kuishirikisha Serikali ya mkoa wa Kagera, Wabunge wote wa mkoa na viongozi wa dini zote kuitisha mkutano/ kusanyiko jingine haraka iwezekanavyo hapa dar es salaam kwa lengo la kuwashirikisha wana-Kagera na wadau wengine wote wenye mapenzi mema, katika kuonyesha kuguswa kwetu kama jamii na tatizo hili, tukusanye rasilimali kusaidia kwenye janga hili. Ndiyo njia pekee ya kuonyesha kuwa tunahitaji kupatiwa msaada wa usafiri (lift), hivyo ni vyema tukawa njiani.
NB : Katika kikao hicho cha wana kagera ahadi za jumla ya Tshs. 6,780,000/= zilitolewa na pesa taslimu Tshs. 1,480,000/= na kuleta jumla ya Tshs. 8,260,000/=
Sekretarieti iliyoundwa inaendelea kuratibu ukusanyaji wa michango hiyo ili itakapokamilika iwasilishwe sehemu husika.
Imewasilishwa leo tarehe 22/09/2016
Ofisi ya mkuu wa mkoa.
Wilfred Muganyizi Lwakatare (Mb)
Jimbo la Bukoba Mjini.
K. N.Y Wana Kagera wanaoishi Dar es Salaam (Waliohudhuria kikao hicho).
NAKALA KWA;
Mh. Waziri Mkuu.
Viongozi wakuu wa madhehebu ya kidini.
Viongozi wa vyama vya siasa.
Waheshimiwa wabunge wote wa mkoa Kagera.
Waandishi wa Habari.
Umepotea mkuuSisi tuna nyumba pale mtaa wa uswahilini.
Ni ya late bibi.nimejaribu kuwashauli Mama zetu ambao ni warithi watuachie sisi watoto wao. Tuijenge iwe ya kisasa na vizazi vyetu baadae nao kila likizo wawe na sehemu nzuri ya kufikia. Nimegonga mwamba.
Wamepiga hesabu zao nani kabaki bk na kuna ambaye anahitaji kurudi bk kati yao.wameamua kuiuza. Kwa kuwa wao wapo Dar na majumba mazuri they dont care.
Imagine utajili tuliouweka nje ungekuwa pale town Bk ingekuwaje?
Elimu imetuharibu.
Ndio maana mchaga ambae hana elimu ya mzungu akibahatisha town anainvest kwao.
Now Moshi pana heshima sio only ya mashule bali pia uwekezaji ukilinganisha na sisi ambao tunaongoza kuwa na civilized elimu ya mzungu.
Ningeshauli ipite kwanza elimu ya kujua uthamini wa nyumbani kwanza
Umepotea mkuu tunakaribisha hoja zakoNaipenda Bk yangu mitaa niliyochezea komborela sasa haipo kila kitu kimebadilika nahisi nikija Hamgembe nitapata kichaa niacheni nipumzike hukuhuku Lindi[emoji27]
Unakaribishwa mkuu tena kutoa hojapia katibu wa mbunge pamoja na meya hawapo hapa?
kiukweli miundombinu mjini ndo inatuangusha wanaousika sijui ndo manispaa jengeni barabara jitahidini zamu yenu kuonesha uwezo mlionao then udongo mwekundu unaharibu taswira ya mji.na ikiwezekana wanapojenga barabara za lami wahakikishe wanaondoa kabiasa huu udongo mazingira ya barabara.kama ingekuwa mimi nimgetafuta ufumbuzi namna gan wa kuuondoa hata kwa kuleta udongo/au mchanga from one place to another japo zipo njia nyingi za kuuondoa kama wahusika wakiwa wabunifu.ni mawazo yangu kama kijana mwenye uchungu na maendeleo hasa ya bukoba na kagera kwa ujumla.Kumbe umeona eti.hivi sasa mji unabadirika haraka na kukua kwa kasi sana sio kama zamani ila miundombinu ASA katikati ya mji bado ni changamoto kati kati kuna udongo mwekundu ,barabara sio kubwa,mitaro nk .ningeomba manispaa ijenge barabara za mjini kati kama walivyotengeneza ya rwamishenye au ya pale kanoni yaani udongo usiwepo mjini ,kuwepo na taa na traffic light,round about za maana ,nk hapo mji wa bukoba utavutia zaidi ila kimajengo yaani ujenzi wa maghorofa na nyumba speed inaridhisha kuliko miji mingi tz
Hivi ujenzi umeshaendelea baada ya hizi sikukuu? Tupia kapicha kengine mkuu tuendelee kufurahia Bkb yetuUmepotea mkuu tunakaribisha hoja zako
Hivi sasa rwamishenye udongo mwekundu hauonekani kwa sababu ya barabara kuwa kubwa na sehemu za waenda kwa miguu zina lami wakifanya hivyo mjini kati patavuta na kupendeza sanakiukweli miundombinu mjini ndo inatuangusha wanaousika sijui ndo manispaa jengeni barabara jitahidini zamu yenu kuonesha uwezo mlionao then udongo mwekundu unaharibu taswira ya mji.na ikiwezekana wanapojenga barabara za lami wahakikishe wanaondoa kabiasa huu udongo mazingira ya barabara.kama ingekuwa mimi nimgetafuta ufumbuzi namna gan wa kuuondoa hata kwa kuleta udongo/au mchanga from one place to another japo zipo njia nyingi za kuuondoa kama wahusika wakiwa wabunifu.ni mawazo yangu kama kijana mwenye uchungu na maendeleo hasa ya bukoba na kagera kwa ujumla.
Sijaenda huko tena ila nitaenda jnne ila watakuwa wanaendelea kwa sababu kwa Maelezo ya meya first phase inabidi ikamilike February kadri ya mkataba itahusishwa pavement ya base ya stendi.choo na police station .na chakufurahisha zaidi wanajenga stendi mbili ya mabasi. Na daladala za mikoani zinaonekana hivyo kabla ya ChristmasHivi ujenzi umeshaendelea baada ya hizi sikukuu? Tupia kapicha kengine mkuu tuendelee kufurahia Bkb yetu
Aisee, umefanya la mbolea sana kwa hizi picha. Hiyo ghorofa ya Bkb shopping mall linajengwa maeneo gani mkuu?Jengo jipya la benki ya finca lililofunguliwa bukobana hili linajengwa barabara ya kashura jengo la wanajeshi chemba rwamishenye sijui watafikia ghorofa ya ngapi wamefikia ya nne nadhani ndo litakuwa jengo refu zaidi bk bukoba shopping mall inayojengwa na mmiliki wa prince motel kimsingi kimajengo bukoba inabadirika mno tunazidi kuwahamasisha wazawa warudi zaidi kujenga mji speed hii isipunguwe
maeneo ilipo prince hotel karibu na hotel ya walkguard transit Uganda roadAisee, umefanya la mbolea sana kwa hizi picha. Hiyo ghorofa ya Bkb shopping mall linajengwa maeneo gani mkuu?