TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Bukoba Mjini

Hatua Zilizofikiwa katika utekelezaji wa Vipaumbele vya TUSHIRIKISHANE; Kata Nyanga, kama anavyoeleza Mtendaji wa Kata ndugu Kamuzora



Ujenzi wa stand kuu ya mabasi utafanyika katika kata hii ya Nyanga, eneo la Kyakailabwa. Na kwa mujibu wa mtendaji wa kata hii, ndugu Kamuzora ni kwamba tayari waliohamishwa kupisha mradi wamekwisha lipwa fidia na tathmini ya kimazingira imekeisha kufanyika. Zoezi linalofuata ni ujenzi wa stand yetu mpya.

I cant wait[emoji126] [emoji126] [emoji126] [emoji126] [emoji126]
 
Ili ni wazo zuri kwa maendeleo ya Mkoa na Manispaa.. Ushauri ni kwamba ruhusu mawazo huru au tofauti na mawazo yenu na kutoa nafasi kwa watu wote maana tumezoea mambo yakishindikana kwenda kwasababu ya kumuliki hoja na mawazo..
 
Ili ni wazo zuri kwa maendeleo ya Mkoa na Manispaa.. Ushauri ni kwamba ruhusu mawazo huru au tofauti na mawazo yenu na kutoa nafasi kwa watu wote maana tumezoea mambo yakishindikana kwenda kwasababu ya kumuliki hoja na mawazo..
Ndugu Alexism, si rukhsa kutukana tu mengine yote unaruhusiwa

Karibu sana!
 
UTALII BUKOBA

f9726e2e3a772a38e3d599c19a2fce9c.jpg
530d0f64480337741bab27daf510e425.jpg


Hivyo ni baadhi ya vivutio vilivyopo ndani ya manispaa ya Bukoba. Zipo pia shughuli nyingi za kufanya za kitalii. Zipo pia kampuni kadhaa zinazotoa huduma ya utalii.

Unapokuja kusalimia wazee kamwe usiache kutembelea vivutio ili kukuza utalii katika Bukoba yetu. Unapokuja na familia hakikisha unawaonyenya uzuri wa Bukoba kwa kuwatembeza katika vivutio mbali mbali.

Karibu pia kuwekeza katika sekta ya utalii.
 
Mheshimiwa RAS
Kwa heshima na taadhima kwa niaba ya wananchi wako tunakuomba uutumie muda wako adhimu uwatembelee hawa Mabwana wakubwa wa Bukoba Water and Sanitation(BUWASA), na kuwauliza kwa nini hatupati maji?
TANESCO wasipotoa huduma hututangazia tuwe tayari! BUWASA ni wepesi kutuma bills kubwa kubwa kwetu bila kutoa huduma.
Mheshimiwa nikuambie kitu!
Tangu BUWASA wanifungie maji mwaka 1992 maji hayajawahi kukatika kwangu!
Tangu walipowaleta hawa Wahindi "eti" kuboresha huduma leo ni kilio kila nyumba.
Mheshimiwa nafahamu una majukumu mengi lakini BUWASA wamekuwa na kazi nyingi kukuzidi.
Naomba nirudie tena; Sisi tumekuwa watumishi wa BUWASA badala ya wao.
Kwa ufupi sasa mimi sipati maji na kama yatapatikaa saa kumi na moja alfajiri hadi saa mbili asubuhi. Nisielewe hawa malaika watateremshwa lini ili na wao waishi kama mashetani. Ni wepesi wa kuleta bills kubwa kuliko matumizi lakini bila kutoa wao kutoa huduma.
Wako boi wa BUWASA
Ramadhani Kingi

Mzee wangu Ramadhani Kingi
Pole sana kwa kutokutendewa haki katika kupata huduma kuu na muhimu kwenye maisha ya mwanadamu. ili ni tatizo ambalo linawakumba wengi na wengi hawajui wapeleke wapi kilio chao wanabaki kugugumia na kusononeka kisha kuitupia lawama serikali na hali kuna mtu kajitapa kuja kumaliza tatizo ili kumbe heri ya huko tulikotoka.
naomba tujiulize huu utaratibu wa kuruhusu makanjanja wajiitao wawekezaji kwenye sekta muhimu sana kama hii. je wanapopewa hii miradi kuiendesha kautaratibu ka kuwafanyia evaluation kama kile walichokiahidi wanakitekeleza au ni business as ussual. nadhani hata RC. afatwe na aelezwe na kisha afatilie na kutoa majibu kwa wananchi maana tunatambua maji ni uhai na mtu akishatambulika kama mwekezaji au mtoa huduma kwa namna yoyote ile anatakiwa afanye kile kitakachoongeza ubora na si kuwatesa wananchi na kupiga hela tu
 
Yaani ili kulikwamua jimbo katika umaskini mnawaza stendi na kuwawezesha mama ntilie tu ,hapo lazima mkae tu,vp kuhusu ukusanyaji wa mapato yatokanayo na ziwa victoria?,kuwa na viwanda ili kupata ajira za uhakika,elimu juu ya kilimo cha mazao mchanganyiko maana kagera wanajua ndizi na kahawa tu wakati mkoa una mvua za kutosha na udongo mzuri kusaport mazao ya aina mbalimbali ya chakula na biashara?.Ki ukweli uwezeshaji wowote lazima uanzie kwenye akili za wawezeshwaji wenyewe -watu wa chini kabisa,lazma kuwepo na amsha amsha kwani watu wamekata tamaa ya maisha ukijumlisha na tetemeko ndo kabisa kila siku tunaona na kusikia kwenye vyombo vya habari.Vinginevyo mipango yenu itabakia kwenye makablasha yenu mwanzo mwisho na hakuna kitakachofanyika.
 
Salaam ndugu zangu wana Tushirikishane.
Ni siku nyingine tena yenye kila dalili za kuwa na baraka zote za muumba wetu hivyo tuna kila sababu ya kumshukuru na kuomba rehema zake. Ni wiki moja sasa tangu niulize juu maendeleo ya utekelezaji miradi tajwa ndani ya mradi wa Tushirikishane lakini niseme tu bado tuna tatizo la kupata habari za mrejesho toka kwa viongozi wetu. kwa wale mliofatilia mjadala niliouanzisha ni dhairi mtakubaliana na mimi kuwa hakukuwa na majibu ya kujitosheleza ya kile nilichouliza kwa lengo la kupata ufafanuzi.

Nisiwe mbinafsi sana nimshukuru Mb. Mh. Lwakatare alitoa jibu japo kama tulivyowazoea hawa wanasiasa wetu majibu yao uwa ni yale ya juu juu lakini nimshukuru kwa ilo. ombi langu kwako mh. Mb. Lwakatare wana JF especially wale walio hapa Tushirikishane tungependa kupata ufafanuzi wa kina ni figisu figisu zipi zinazokwamisha kuanza kwa miradi hiyo ambayo tunatambua wazi haiko mikononi mwa serikali kama ili kama vip tuzihoji mamlaka za juu kwanini ziweke kiza kinene kwenye miradi hiyo? Mh. ukiweza kutuhabarisha ukwamishaji huko wapi tutaweza kukupa ushirikiano wa kuwauliza wenye mamlaka ili tuje na majibu muafaka maana ni wajibu wetu na ni haki yetu ya msingi kujua kinachojiri.

Jambo la pili linaloendelea kunisikitisha ni kwa jinsi viongozi wetu wasivyoona umuhimu wa kutumia mitandao ya kijamii nimejaribu kumtafuta Meya wa Manispaa maana yeye ndiye mwenye picha nzima ya miradi hii lakini kwa bahati mbaya bado simpati kokote Ndugu yangu chief Kalumuna katika ulimwengu huu wa utandawazi bado kweli usiwe mtumiaji wa Social Network? naomba mlio na bahati ya kukutana nae mwambieni kuwa yawezekana anayakosa mengi ya ulimwengu huu kwa kutokuwa kwenye Social media. Maana yeye ndo mtoa majibu mkuu sasa endapo hapati jumbe kama hizi dah ni dhairi tunatwanga maji kwenye kinu na maendeleo tunayoyapigania yatachukua muda kutufikia wana bukoba

Naibu Meya Ndugu Jimmy najua ni mtu active sana na kwa bahati ni mtumiaji mzuri wa mitandao lakini kimya chake kwenye masuala ya maendeleo ya bukoba kinanipa wasiwasi. maana namuona sana kuchangia kwenye masuala mengi yahusuyo uhai wa siasa na demokrasia ya Tanzania ila sio kutuhabarisha wana bukoba kwenye yale tuyatumainiayo kuyaona wana bukoba wenye fikra na mitazamo chanya kwa bukoba tuitakayo.
Ndugu yangu Jimmy. naomba nikupe mfano mdogo sana wa kiongozi ninayempenda katika nyanja za siasa na huyu si mwingine ni Mh. Nassari Mb. wa Arumeru. yuko active kwenye kila jambo na anajua namna ya kueleza umma wa wana arumeru juu ya kinachohitajika kufanyika au hatua zilizofikiwa. juhudi zake za kutoa mrejesho zinawapa nguvu wana arumeru kuchangia kwa hali na mali katika maendeleo yao.

nisiwachoshe kwa maneno mengi sana bali niseme wazi kuwa viongozi wetu vunjeni ukimya muwe watu wa kuzungumzia maendeleo msijiweke kimya maana kwa style hii ya ukimya mnaonekana kama hamko nasi. Wana bukoba tunapenda kusikia na kuona Bukoba ikipiga hatua ndani ya miaka hii minne kabla ya 2020, na hii itakuwa ni nafasi pekee kwenu kusimama mbele ya wanabukoba tena mkiwa vifua mbele kuwa tumefanya ili na linaonekana kuliko zile ahadi za miaka ya nyuma ambayo it was business as ussual

Muwe na siku njema
 
Yaani ili kulikwamua jimbo katika umaskini mnawaza stendi na kuwawezesha mama ntilie tu ,hapo lazima mkae tu,vp kuhusu ukusanyaji wa mapato yatokanayo na ziwa victoria?,kuwa na viwanda ili kupata ajira za uhakika,elimu juu ya kilimo cha mazao mchanganyiko maana kagera wanajua ndizi na kahawa tu wakati mkoa una mvua za kutosha na udongo mzuri kusaport mazao ya aina mbalimbali ya chakula na biashara?.Ki ukweli uwezeshaji wowote lazima uanzie kwenye akili za wawezeshwaji wenyewe -watu wa chini kabisa,lazma kuwepo na amsha amsha kwani watu wamekata tamaa ya maisha ukijumlisha na tetemeko ndo kabisa kila siku tunaona na kusikia kwenye vyombo vya habari.Vinginevyo mipango yenu itabakia kwenye makablasha yenu mwanzo mwisho na hakuna kitakachofanyika.
Ndugu Lind, hii ni mipango ya miezi tisa (9) ambayo ni vipaumbele vya mbunge. JF kazi yake ni kuhimiza utekelezaji wa ahadi hizi za mbunge kwa muda huo. Eneo letu la mradi ni Bukoba sio Kagera

Tukiongelea maendeleo ya Kagera kila mwanakagera ana nafasi ya kuchangia maendeleo ya kwao awe ndani ya Kagera au nje ya Kagera. Watu wa nje ya Kagera tunawategemea zaidi kwamaana wengi wao wana mitaji wanaweza kuja kuwekeza kwao. Kama tunavyokuwa na ushawishi katika siasa na chaguzi tunatamani kuona pia ushawishi wao katika shughuli nyingine za maendeleo. Kama wanavyofatilia, fadhili kampeni na chaguzi vivyo hivyo tunawahitaji wafatilie na kufadhili shughuli nyingine za maendeleo

Hata hivyo km ulivyokwisha kusema, mipango ya uwekezaji inapasa kuwa ya kumwinu mtu wa chini. Soko tunalihitaji lkn tunahitaj zaidi viwanda, uwekezaji ktk kilimo n.k

Shukrani[emoji120]
 
Ndugu Lind, hii ni mipango ya miezi tisa (9) ambayo ni vipaumbele vya mbunge. JF kazi yake ni kuhimiza utekelezaji wa ahadi hizi za mbunge kwa muda huo. Eneo letu la mradi ni Bukoba sio Kagera

Tukiongelea maendeleo ya Kagera kila mwanakagera ana nafasi ya kuchangia maendeleo ya kwao awe ndani ya Kagera au nje ya Kagera. Watu wa nje ya Kagera tunawategemea zaidi kwamaana wengi wao wana mitaji wanaweza kuja kuwekeza kwao. Kama tunavyokuwa na ushawishi katika siasa na chaguzi tunatamani kuona pia ushawishi wao katika shughuli nyingine za maendeleo. Kama wanavyofatilia, fadhili kampeni na chaguzi vivyo hivyo tunawahitaji wafatilie na kufadhili shughuli nyingine za maendeleo

Hata hivyo km ulivyokwisha kusema, mipango ya uwekezaji inapasa kuwa ya kumwinu mtu wa chini. Soko tunalihitaji lkn tunahitaj zaidi viwanda, uwekezaji ktk kilimo n.k

Shukrani[emoji120]
Dah wewe Dada hii nafasi hawakukosea kukupatia maana unajua mpaka basi. hongera
 
Salaam ndugu zangu wana Tushirikishane.
Ni siku nyingine tena yenye kila dalili za kuwa na baraka zote za muumba wetu hivyo tuna kila sababu ya kumshukuru na kuomba rehema zake. Ni wiki moja sasa tangu niulize juu maendeleo ya utekelezaji miradi tajwa ndani ya mradi wa Tushirikishane lakini niseme tu bado tuna tatizo la kupata habari za mrejesho toka kwa viongozi wetu. kwa wale mliofatilia mjadala niliouanzisha ni dhairi mtakubaliana na mimi kuwa hakukuwa na majibu ya kujitosheleza ya kile nilichouliza kwa lengo la kupata ufafanuzi.

Nisiwe mbinafsi sana nimshukuru Mb. Mh. Lwakatare alitoa jibu japo kama tulivyowazoea hawa wanasiasa wetu majibu yao uwa ni yale ya juu juu lakini nimshukuru kwa ilo. ombi langu kwako mh. Mb. Lwakatare wana JF especially wale walio hapa Tushirikishane tungependa kupata ufafanuzi wa kina ni figisu figisu zipi zinazokwamisha kuanza kwa miradi hiyo ambayo tunatambua wazi haiko mikononi mwa serikali kama ili kama vip tuzihoji mamlaka za juu kwanini ziweke kiza kinene kwenye miradi hiyo? Mh. ukiweza kutuhabarisha ukwamishaji huko wapi tutaweza kukupa ushirikiano wa kuwauliza wenye mamlaka ili tuje na majibu muafaka maana ni wajibu wetu na ni haki yetu ya msingi kujua kinachojiri.

Jambo la pili linaloendelea kunisikitisha ni kwa jinsi viongozi wetu wasivyoona umuhimu wa kutumia mitandao ya kijamii nimejaribu kumtafuta Meya wa Manispaa maana yeye ndiye mwenye picha nzima ya miradi hii lakini kwa bahati mbaya bado simpati kokote Ndugu yangu chief Kalumuna katika ulimwengu huu wa utandawazi bado kweli usiwe mtumiaji wa Social Network? naomba mlio na bahati ya kukutana nae mwambieni kuwa yawezekana anayakosa mengi ya ulimwengu huu kwa kutokuwa kwenye Social media. Maana yeye ndo mtoa majibu mkuu sasa endapo hapati jumbe kama hizi dah ni dhairi tunatwanga maji kwenye kinu na maendeleo tunayoyapigania yatachukua muda kutufikia wana bukoba

Naibu Meya Ndugu Jimmy najua ni mtu active sana na kwa bahati ni mtumiaji mzuri wa mitandao lakini kimya chake kwenye masuala ya maendeleo ya bukoba kinanipa wasiwasi. maana namuona sana kuchangia kwenye masuala mengi yahusuyo uhai wa siasa na demokrasia ya Tanzania ila sio kutuhabarisha wana bukoba kwenye yale tuyatumainiayo kuyaona wana bukoba wenye fikra na mitazamo chanya kwa bukoba tuitakayo.
Ndugu yangu Jimmy. naomba nikupe mfano mdogo sana wa kiongozi ninayempenda katika nyanja za siasa na huyu si mwingine ni Mh. Nassari Mb. wa Arumeru. yuko active kwenye kila jambo na anajua namna ya kueleza umma wa wana arumeru juu ya kinachohitajika kufanyika au hatua zilizofikiwa. juhudi zake za kutoa mrejesho zinawapa nguvu wana arumeru kuchangia kwa hali na mali katika maendeleo yao.

nisiwachoshe kwa maneno mengi sana bali niseme wazi kuwa viongozi wetu vunjeni ukimya muwe watu wa kuzungumzia maendeleo msijiweke kimya maana kwa style hii ya ukimya mnaonekana kama hamko nasi. Wana bukoba tunapenda kusikia na kuona Bukoba ikipiga hatua ndani ya miaka hii minne kabla ya 2020, na hii itakuwa ni nafasi pekee kwenu kusimama mbele ya wanabukoba tena mkiwa vifua mbele kuwa tumefanya ili na linaonekana kuliko zile ahadi za miaka ya nyuma ambayo it was business as ussual

Muwe na siku njema
Changamoto ya taarifa ni kubwa ndugu!
 
CHANGAMOTO YA UPATIKANAJI WA TAARIFA

97e89391a820b9b34f6b635c47d2bab1.jpg


Changamoto ya upatikanaji wa taarifa ni dhahiri ndio sababu sitoi updates za mradi (vipaumbele vyetu) mara kwa mara kama inavyotakikana. Vile vile kuhabarisha juu ya miradi mingine inayoendelea nje ya vipaumbele vyetu ambavyo najua wananchi wangependa kufahamu

Kama niliviyokwisha eleze kwenye post za awali jinsi mradi unavyotekelezwa na nafasi ya kila mdau katika mradi huu.

1. Vipaumbele vyetu vinne ni baadhi ya ahadi za mbunge. Utekelezaji wake unaanzia BMC na taarifa za mradi zinaanzia BMC. Mbunge ni daraja la kuleta habari zilizo rasmi kuhusiana na maendeleo ya utekelezaji wa mradi kutoka BMC.

2. Mbunge anasimamia utekelezaji na ndiye anatoa taarifa rasmi kwa umma kupitia jukwaa maalum la Jf

3. Jf inahimiza na kufatilia taarifa na vipaumbele ilivyokubaliana na wananchi na mbunge kutekeleza ktk kipind cha mradi.

4. BMC na Mbunge wanawajibika kwa wananchi moja kwa moja

5. JF ni daraja la kupasha habari na kufikisha taarifa za maendeleo ya utekelezaji wa mradi kwa jamii kama zinavyowasilishwa na mamlaka husika
 
View attachment 404994 LEO NIMEWASILISHA RIPOTI YA KIKAO NILICHOKIFANYA NA BAADHI YA WANA KAGERA WAISHIO JIJINI DAR ES SALAAM KWA MKUU WA MKOA KAGERA.
View attachment 405000 View attachment 405001 View attachment 405002 View attachment 405003 View attachment 405003 View attachment 405003 View attachment 405004
MH. MKUU WA MKOA,

KAGERA.

MAAZIMIO YALIYOPITISHWA KWENYE KIKAO KILICHOITISHWA NA MH. WILFRED LWAKARATE(MB), MBUNGE WA JIMBO LA BUKOBA MJINI, KUJADILI ATHARI ZA TETEMEKO LA ARDHI MKOANI KAGERA, KUONA JINSI YA KUSAIDIA WALIOPATWA NA MADHARA.TAREHE 18 SEPTEMBA, 2016 KWENYE HOTELI YA KEBBY'S, MWENGE, DAR ES SALAAM.

1. Kwa kauli moja kikao kimetambua na kuishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua zakuridhisha kufuatia janga hili, ikiwa ni pamoja na ;
i. Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa, (Mb), Waziri Mkuu, pamoja na kiongozi mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Mh. Freeman Aikael Mbowe (Mb) kufika B ukoba mara moja kuona athari za tetemeko na kushiriki mazishi ya watu waliofariki kutokana na janga hili na pia kuwafariji waliojeruiwa na kuathirika kwa namna mbali mbali.

ii. Kuandaa mkutano wa kuishirikisha jumuiya ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na jumuiya ya wafanyabiashara kwa lengo la kukusanya misaada kwa ajili ya kukabiliana na janga hili.

iii. K uandaa matembezi ya hisani kwa ajili ya kukusanya fedha za kusaidia nakukabiliana na madhara ya janga hili.

iv. Viongozi waandamizi mbali mbali waserikali, wakiwemo Mawaziri, Viongozi mbalimbali wa kisiasa, Makatibu wakuu na wakuu wa vitengo muhimu vinavyo husiana na maafa kufika kwenye eneo la tukio kwa haraka.

2. Kwa kauli moja kumuomba Mh. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwa ndiye baba wa nchi, pamoja na shughuli zake nyingi, kutenga siku mapema itakavyo mpendeza kufika mkoani Kagera kuwapa pole wananchi wake kutokana na janga hili. Tunaamini walioathirika watafarijika sana kumuona Rais wao akiwa nao kwenye eneo la tukio.

4. Kwa kuwa janga hili la kitaifa halina itikadi ya siasa, dini, rangi, kabila wala ubaguzi wa aina yoyote ile, hivyo ushiriki wa watu wote ni muhimu sana.

5. Kwa kutambua ukweli wa walioathirika zaidi ni wananchi wa mkoa wa Kagera, inawapasa wao kuwa msitari wa mbele katika kushiriki katika juhudi zote zinazofanyika, kwa njia na jinsi yoyote inayowezekana, iwe ni kwa hali au mali, mshikamano wao katika janga hili ni muhimu sana. Mpaka sasa, imejidhihirisha kwamba ushiriki wa wana Kagera bado ni hafifu sana. Wana kagera wanahimizwa kutokukata tamaa nakuamsha hari ya kushirikiana katika kuusaidia mkoa wao kwa nidhamu ya hali ya juu . Ili kusisitiza umuhimu huo, mfano wa kwamba ili kuweza kupewa msaada wa usafiri (lift) ni lazima uwe njiani, unahusika.

6. Kwamba kutokana na mkoa wa Kagera kukumbwa na maafa makubwa na mengi mfululizo kuanzia miaka ya 1970 zilipoanza chokochoko za nduli Iddi Amini wa Uganda, vita vya Uganda , Ukimwi, mdudu wa migomba (ekiuka), madhara ya wakimbizi kutoka nchi jirani yaliyo leta ujambazi , kufa kwa Vyama vya Msingi vya Ushirika na Chama Kikuu cha Ushirika (BCU/ KCU) kulikoambatana na kuanguka kwa bei ya zao la kahawa, kuanguka kwa Shirika la Reli Tanzania (TRC), kulikosababisha bei za bidhaa za viwandani ambavyo vingi vipo Dar es salaam, kuwa juu kuliko sehemu nyingine yoyote ya Tanzania, ugonjwa wa mnyauko ambao umeangamiza kabisa migomba na zao lake ndizi, na sasa ni janga la tetemeko. Majanga hayo yote ni sababu kubwa kwa mkoa wa kagera kushuka sana kiuchumi kutoka kati ya mikoa mitatu tajiri miaka ya 70 - 80 hadi kuwa kati ya mikoa mitano masikini sana nchini. Serikali inaombwa ichukue hatua za makusudi kutoa upendeleo wa kisera wa kuusisimua upya uchumi (a stimulus package) kwa mkoa wa Kagera kwa kufanya yafuatayo :

i. Kutoa msamaa wa kodi zote kwenye bidhaa zote za ujenzi zinazouzwa mkoani Kagera kwa kipindi cha miaka kumi.

ii. K wa kutambua madhara ya mdororo wa uchumi wa mkoa wa Kagera kwa muda mrefu hivyo kuwepo tatizo kubwa la ajira na umasikini, miradi yote ya ujenzi wa miundombinu ya kijamii kama mashule, zahanati, vituo vya afya na majengo mengine ya serikali yatakayo jengwa upya au kukarabatiwa, ugawaji wa kandarasi ufanywe kwa mtindo wa uwezeshaji kwa makampuni yaliyopo na yanayoendesha shughuli zao mkoani kagera yenye uwezo, wakishirikiana na makampuni ya wana -Kagera walioko nje ya mkoa pale inapobidi . Vigezo vitaandaliwa ili vizingatiwe.

7. Kwa kutambua kuwa serikali imeunda kamati za maafa za Kitaifa na Mkoa ambapo Wabunge wa mkoa wa Kagera wameshirikishwa, ni vyema ushiriki kwenye kamati hizo upanuliwe na kuzijumuisha taasisi za dini ambazo mkoani kagera zimekuwa na mchango mkubwa katika utoaji wa huduma za jamii kwa miaka mingi. Hatua hii itasaidia kuongeza ufanisi katika zoezi zima la uthamini wa madhara, ukusanyaji wa taarifa na usambazaji wake. Aidha kwenye hizo kamati uwepo umuhimuwa ku wahusisha wataalam wa habari kuongeza ufanisi katika upashanaji wa habari .

8. Kwa kuzingatia mamlaka ya Mbunge anayopewa na katiba ya jamhuri ya Muungano wa T anzania, mifuko ya majimbo pia itumike kusaidia kwenye majanga yamaafa kama haya.

9. Kwa kukubali kwamba bado uitikiaji na ushiriki wa wana -Kagera bado ni hafifu sana, juhudi mpya zifanyike kwa kuishirikisha Serikali ya mkoa wa Kagera, Wabunge wote wa mkoa na viongozi wa dini zote kuitisha mkutano/ kusanyiko jingine haraka iwezekanavyo hapa dar es salaam kwa lengo la kuwashirikisha wana-Kagera na wadau wengine wote wenye mapenzi mema, katika kuonyesha kuguswa kwetu kama jamii na tatizo hili, tukusanye rasilimali kusaidia kwenye janga hili. Ndiyo njia pekee ya kuonyesha kuwa tunahitaji kupatiwa msaada wa usafiri (lift), hivyo ni vyema tukawa njiani.

NB : Katika kikao hicho cha wana kagera ahadi za jumla ya Tshs. 6,780,000/= zilitolewa na pesa taslimu Tshs. 1,480,000/= na kuleta jumla ya Tshs. 8,260,000/=

Sekretarieti iliyoundwa inaendelea kuratibu ukusanyaji wa michango hiyo ili itakapokamilika iwasilishwe sehemu husika.

Imewasilishwa leo tarehe 22/09/2016

Ofisi ya mkuu wa mkoa.

Wilfred Muganyizi Lwakatare (Mb)

Jimbo la Bukoba Mjini.

K. N.Y Wana Kagera wanaoishi Dar es Salaam (Waliohudhuria kikao hicho).

NAKALA KWA;

Mh. Waziri Mkuu.

Viongozi wakuu wa madhehebu ya kidini.

Viongozi wa vyama vya siasa.

Waheshimiwa wabunge wote wa mkoa Kagera.

Waandishi wa Habari.
nimekupenda sana mheshimiwa kwakuwa karbu sana na mkuu wa mkoa na kushirikiana naye vizur ..napenda sana kuwa huru na kiongozi mwngne sio mambo ya kutunishiana misur kila mtu anajiona yupo juu
 
WAATHIRIKA WA TETEMEKO KAGERA WAENDELEA KUTESEKA
-------------------
Hadi leo tarehe 27/10/2016 ni Zaidi ya Siku 46 tangu Maafa ya Tetemeko la ardhi Kagera yatokee. Waathirika wameendelea kuteseka kwa kulala kwenye mabanda yaliyojengwa kwa kutumia Sheeting. Mateso haya makubwa yamesababishwa na kitendo cha kusikitisha cha kuwanyima Waathirika misaada ya Vifaa vya Ujenzi na Fedha. Wanawake mama Wajawazito na Watoto wamekabiliwa na mateso haya kwa muda wa Siku zote hizi zaidi ya Siku 46.
Leo nazungumzia athari zinazo weza kusababishwa na kulala kwenye Sheeting kwa Siku nyingi.
Sheeting utengenezwa kwa kutumia Mafuta machafu, na zimetengenezwa kwa ajili ya kutumika kwa kuanika Mazao au kufunikia mazao au kutumika kama Matulubai kwenye Magari.
Malighafi hii ya Mafuta machafu inaweza pia kuleta mazala kwa Binadamu. Lakini pia Sheeting wakati wa jua inakuwa na Joto Kali sana ambalo pia siyo Sala kwa Binadamu kutokana na Malighafi iliyotumika kutengeneza Sheeting, wakati wa baridi kama nyakati za usiku Sheeting inakuwa na baridi Kali ambayo pia siyo Sala kwa Binadamu kwani inaweza kusababisha magonjwa kama vile ya Nimonia n.k
Kwa sababu ya kujua athari hizi ndiyo maana yatengenezwa Mahema kwa ajili ya Nyumba za dhalura ambayo yanakuwa yametengenezwa kwa Malighafi ambayo haiwezi kuleta madhala kwa Binadamu, Mahema haya utumiwa sana na Watali na ata Majeshi. Kwa hapa Tanzania tunacho kiwanda cha CANVAS MOROGORO utengeneza Mahema kwa ajili ya Nyumba za dhalula,
Katika picha nilizo weka hapa utaona hilo hema lenye rangi nyekundu. Hema hili ndilo lililo sahihi kwaajili ya Makazi ya dhalula,
Kwakuwa Kamati ya Maafa imekusanya misaada ya Waathirika, na kwakuwa mpaka sasa Kamati haijatoa misaada ya Vifaa vya ujenzi na Siku sasa zimekuwa nyingi, na Waathirika wanaendelea kulala kwenye Masheeting jambo ambalo linaweza kuwasababishia athari nyingine. Kamati ya maafa inunue Mahema au iazime Mahema kwenye Majeshi yetu na kuwagawia Waathirika wote

Na Victor Sherejey

1160fbcef31b10c67f12c22a209d4014.jpg
578f8449344b7d87c82878608b692c49.jpg
27b742315c22fd39efb4d4eca1583977.jpg
5814d0d0e0b910433dc521917ea04e0a.jpg
 
Uwasilishaji wa Tushirikishane katika Radio

91c58bb739a9dad4e4a4f69e57228771.jpg
4ced4e4e7d6cded0e1a7441c40e95cf5.jpg
521fa6171b94c42be442a9c46d5ba1b0.jpg
c87bb700eab29e367cccfbc9ddcd8b6e.jpg
74e13bc74090be3fc144934adc40fc27.jpg
eb427e120c5f256d70bb6d6c66624223.jpg
a1633f7d02bf93f13a6af3747ea5f343.jpg


Katika kuhakikisha wananchi wote wa Bukoba wanashirikishwa katika shughuli za maendeleo yao, mradi wa Tushirikishane una mikakati mbalimbali ya kuhakikisha taarifa zinawafikia wananchi. Moja ya mikakati hiyo ni kwenda radioni kila mwezi kuwajuza wananchi kinachoendelea lakini pia kupata maoni kwa kundi ambalo halifiki kwenye mitandao ya kijamii.

Jana tar 27 October, Tulianza rasmi mpango wa kuwafiki wananchi kupitia radio. Tulianza na Vision Radio FM iliyoko Manispaa ya Bukoba. Tulifanya mahojiano ya saa moja na nusu tukielezea Jamiiforums, Tushirikishane, na namna gani wananchi wanaweza shiriki katika shughuli za maendeleo ya jimbo lao. Lakini pia tulipokea ushauri, pongezi na maoni ya wananchi juu ya mradi n.k

Pichani ni mimi Afisa Habari wa Jamiiforums - Bukoba, Mkurugenzi wa Jamiiforums Bw. Maxence Mello na Mtangazaji wa Vision FM Radio Bi. Matilda Leopord
 
Huyu mbunge ni jipu na janga jingine. Alitaka tumsaidie kwa pamoja lakini sasa hivi kila akiulizwa haonekani kokote na wala hafungui kinywa chake, yale yale na ameanza kurudia mle mle. The means justifies the end!
 
Binafsi napongeza uongozi wa jf maana nimekuwa kati ya wana warsha walio shiriki katika uzinduzi wa program hii kigamboni ingawa nimegundua mengi ambayo kimsingi jimbo ili nadhani dr ndungulire atajitaidi kufanya alivyo aidi. Si haba nikachangia kwa upande wa kagera maana ni kwetu ila jambo msingi hapa ni kuwa kila mwanakagera ashiriki kikamilifu na sio kumwachia mbunge.ningeoenda nione ahadi za mbunge hyu walau nishiriki kumkumbusha pale atakaposahau
 
Back
Top Bottom