Mjue gwiji wa sheria nchini Dkt. Lamwai

Mjue gwiji wa sheria nchini Dkt. Lamwai

Wapo wanaomjua Dr Masumbuko kama Mhadhiri Mwandamizi wa Sheria na alifundisha na kuwawezesha wengi kuwa Wanasheria na Mawakili na wengine hadi wamefikia kuwa Majaji...
Hakika naona Kila mtu anamkanda Tu kwa mabaya wakati anamazuri mengi tu
 
ukweli ni kwamba, lamwai ni mtu aliyewafanya watu wengi sana wasomee sheria kutokana na umahiri wake, watu waliipenda sheria kwa kumwangalia yeye. hilo ameacha kama legacy.
Hakika
 
wewe umezaliwa juzi, ni manguli wachache sana walishawahi kutokea Tanzania waliomzidi Lamwai, hao siwajui. hata Tundu Lisu na wote uliowataja walijifunza na kupata moyo na uzoefu toka kwa Lamwai. huyu jamaa alikuwa noma.
Mkuu kama unawajua walipokuwa vizr kabla ya lamwai waweke wazi...

Mm ni wa kitambo mno
 
Dr Walid Aman Walid Kabourow ana record yake

1) Katibu Mkuu wa Chadema
2) Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa
3) Mbunge wa kwanza wa Jimbo wa Chadema
4) Mbunge wa Kwanza wa kutokea Upinzani baada ya kufanyika uchaguzi mdogo 1994
5) Kijana aliefungwa na kufukuzwa shule kwa kuchana kadi ya TANU na ya Baba wa Taifa, wa pili akiwa Hayati Mchungaji Christopher Mtikila
6) Kiongozi wa Kitaifa wa kwanza kutoka Chadema kuunga mkono juhudi
Ahsante Sana kwa kunijulisha mana nilikuwa namskia tu
 
Mkuu kama unawajua walipokuwa vizr kabla ya lamwai waweke wazi...

Mm ni wa kitambo mno
kabla ya Lamwai alikuwepo Shivji, alisumbua sana enzi za nyerere tangu enzi za kesi za kina Chandrakant waliokuwa wahindi wenzie, tangu enzi nyerere anataifisha hayo magorofa ya wahindi uhindini huko.
 
Ukiona msomi yeyote yeyote kaingia kwenye siasa, elewa kuwa huyo kasoma lakini hajaelimika.

Msomi kuingia kwenye siass iwe kwenye miaka yake ya kustaafu, ndipo kweli bado ana nia ya kuitumikia jamii.

Tazama kina Dr. Janabi, na fursa zote walizonazo na usomi wao lakini wamekataa kabisa kuingia kwenye siasa, Janabi alikataa mpaka uwaziri, anasema anataka kuitendea haki elimu yake. Hao ndiyo wasomi walioelimika.
Acha uongo
 
kabla ya Lamwai alikuwepo Shivji, alisumbua sana enzi za nyerere tangu enzi za kesi za kina Chandrakant waliokuwa wahindi wenzie, tangu enzi nyerere anataifisha hayo magorofa ya wahindi uhindini huko.
Daah asee ahsante Sana hakika wewe mwamba
 
View attachment 2795908

Nenda, pita pote, mji kwa mji, kijiji kwa kijiji. Uliza nani mwamba wa sheria, Tena usisahau kupita kwa Wanazuoni wa kizazi cha 21 *uliza hilo swali, Pita *Udom, Udsm, Mzumbe, Saut, Tudarco mpaka,Ruco kwa wakatoliki. Wote watakujibu Gwiji wa sheria ni Kibatala na Tundu lissu, wakienda mbali watamtaja Mnyakusa wakili Mwabukusi wa Mwanjelwa.

Sasa acha hao wote, kuna huyu mwamba ambaye kawapiku wote, Rekodi yake haijawahi kuvunjwa na wote hao. Ubaya ni kuwa Hakufanya kazi zake kipindi Watoto wa Mkapa na JK tunazaliwa.

Huyu Mwamba alizitesa mahakama za Taifa hili Mpaka zikakubali, Hayati Jaji kisanga na Nyalali waliukubali mtikiso wa Mwamba huyu haijawahi kutokea.

Huyu Ndiyo Dr Masumbuko Mahunga Selasini Lamwai. almarufu Dr Lamwai, mzaliwa wa mkoa adhimu wa kilimajaro aliyezikataa zile mbichi na kuiheshimisha tasnia ya uwakili nchini.

Kwanza ni Genius vibaya mno, Alipoenda kusoma Chuo kikuu Cha Oxford- Uingereza aliwapiga na kitu kizito wazungu, aliwaambia yeye anao uwezo wa kusoma miaka miwili kozi ya miaka minne. Wakamjaribu, Mwamba akagraduate na kuwaacha wazungu wakomae na miaka minne.

Alihitimu PhD ya Criminal & Procedural law kwa miaka miwili tu badala ya minne. huu utaratibu ulikuwepo pale chuoni.

Mpaka sasa anatajwa kuwa ndiye Mwanafunzi pekee kutoka afrika aliyewahi kuhitimu hiyo fani kwa Miaka miwili.

Dr Lamwai alikuwa wakili matata Sana. Aliingia Bungeni kama Mbunge wa jimbo la ubungo mwaka 1995. Akiwa Bungeni aligoma kuapa kiapo cha utii kwa Rais. Akatoa hoja kuwa Bunge ni muhimili unaojitegemea, hivyo, sio Sawa mbunge kuapa kiapo cha utii kwa Rais, mwamba akamfundisha Spika dhana ya Separation of power, akampa vifungu konki Spika Pius Msekwa.

Spika Msekwa, akaamuru sheria ya kiapo cha utii irekebishwe na kufuta kipengele cha wabunge kuapa utii kwa Rais, wabunge wote walirudia kuapa upya mwaka huo na mpaka sasa wabunge hawaapi kiapo cha utii kwa Rais kwasababu ya ufundi wa Dr lamwai.

Dr Lamwai aliwahi kumshikisha adabu waziri mmoja aliye kuwa mwanamama. Alimpiga cross examination ya kichokozi kinoma, alimuuliza; "Inaonekana wewe ni Malaya Sana?", waziri akachukia, akaanza kutukana hovyo hovyo mahakamani.

Mwamba akatoa picha za Watoto wanne wa yule waziri akamuuliza; "Hawa ni wanao?", Waziri akakubali. Wakili lamwai akatoa picha za wanaume wanne akamwambia; iambie mahakama Hawa ni Akina nani?. Waziri akainamisha kichwa kwa aibu. Basi umalaya ukathibitishwa na wakili lamwai, kwani kila mtoto alikuwa na Baba yake kwenye zile picha. Yaani waziri alizaa na wanamume wanne tofauti. Huu ni utundu wa Dr lamwai.

Dr lamwai aliwahi Kusimamia kesi maarufu ya kupinga ushindi wa ubunge jimbo la temeke mwaka 1996 Ambapo alishinda na kumng'oa kitini mh Ramadhan kihiyo kwa tuhuma za kudanganya elimu yake.

Dr lamwai alikuwa kivutio kikubwa kwa vijana enzi za miaka ya 90. Inasemekana watu walilala kwenye stesheni za treni kumsubili lamwai.

Lamwai alikuwa mbunge wa kwanza wa chama cha upinzani NCCR-mageuzi katika jimbo la ubungo, aliitumia Taaluma ya sheria kushinikiza mambo nyeti na muhimu Bungeni.

Baada ya kuitesa serikali kwa muda mrefu, kisasi kikamfikia. Dr lamwai alifukuzwa kazi pale Udsm alipokuwa akifundisha sheria, akafanyiwa figisu akapoteza ubunge, akaporwa leseni ya uwakili, Mali zake zikataifishwa. akabaki yeye na nguo zake tu. Akaishi kwa dhiki muda mrefu hadi alipoamua kujiunga na chama tawala-CCM ndipo akarudishiwa leseni ya uwakili na mali zake.

Dr lamwai ametoa vipanga wa sheria nchini. Mfano mzuri ni wakili Msomi John Malya. Hiki kichwa kiliandaliwa na Dr lamwai pale chuo kikuu Cha Tumaini - dar es salaam.

Dr lamwai alifariki mwaka 2020 kwa maradhi.
Hii history ina walakini mkubwa sana, history ya Dr Lamwai umekosea sana
 
Back
Top Bottom