Mkandarasi wa Uturuki, Yapi Merkezi athibitisha pengo la $1.8bn katika ufadhili wa Tanzania SGR

Mkandarasi wa Uturuki, Yapi Merkezi athibitisha pengo la $1.8bn katika ufadhili wa Tanzania SGR

Walipewa walichotaka mchina anakupa unachotaka wenyewe walikuwa janja janja.Lakini mbona Nchi nyingine mfano Indonesia aliwafadhili SGR na Vichwa vilivuopelekwa nivya mchongoko.Ukiona Mchina kafeli jua janja janja nyingi kwenye uwo mradi.
Hata hapa nchi ya kutanga na nyika tukitaka vichwa vya mchongoko vitakuja ni pesa yetu na viongozi wakiacha janja janja.
 
Ongea kitu unachokijua mkuu, China hajajenga SGR Indonesia.
Indonesia imejengwa HSR
Nashukuru kwa kuniabarisha chanzo changu cha tatifa kilinipotosha.Kikubwa mchina afeli kwenye kufinance.
 
Kama ungeelewa lengo la kuboresha na kujenga hizo bandari ni sehemu ya mradi mkubwa wa miundombinu kuweza kuitumia vizuri SGR usinge andika ulicho andika hapa.
Yaonekana ilani (manifesto) yenu ya uchaguzi hauijui.
Sgr inaenda Mwanza kufanya nini Cha maana huko? Kwa nini isingeenda Kigoma?
 
Huyu Mbarawa amekuwa ni kiongozi asieaminika, ni muongo sana na anahadaa watanzania.........serikali wanakuja na rundo la miradi na mingi inaishia kuwa white elephant huku wao mifuko yaoikizidi kunenepa
Amekuhadaa Kwa lipi? Au wewe ndio unahangaika na Mbarawa?
 
Tuliambiwa mwanzoni "Tunajenga kwa fedha zetu"
Nini hiki kinachoendelea?
Hii nchi ina ombwe la viongozi wenye nia ya dhati!
 
Haya yanafanyika katika nchi ambayo maji na umeme bado si vitu vya uhakika kwa qananchi!! Mradi wa doll Billion 10 utarejesha faida lini?
Kuna Uzi humu uliohusu ujenzi wa hiyo reli. Tulisema ni ngumu kwa Tanzania kujenga miradi miwili ya $7b+ kwa wakati mmoja kwani uwezo huo haupo. Ila enzi hizo propaganda zilikuwa na nguvu kuwa uwezo huo upo. Sasa ukweli uko hadharani.
 
Sgr inaenda Mwanza kufanya nini Cha maana huko? Kwa nini isingeenda Kigoma?
Soma nyuzi nyingi zinazo husu bandari za maziwa makuu na SGR utaona lengo ni kuunganisha na Uganda hadi South Sudan.
Shirika la chakula duniani limeshatumia reli na ziwa Victoria Mwanza kupeleka chakula maeneo ya Uganda na Rwanda jirani na Ziwa Victoria maeneo yenye njaa na wakimbizi.
Soma mkuu Soma sana utajua mengi.

Fuatilia mkakati wa EAC kuunganisha railway Ile Northern corridor.

Ni fursa kubwa ya kiuchumi.
Wenye maono walimuelewa Magufuli, wasioona mbali wanaweza kumdhihaki kama wewe ulivyo ita "miradi ya Kisengerema ipelekwe Chato".
 
Tra wanakusanyaga trillion 2 ,+++ ingekuwa yapi wanachukuwa madafu faster. Sana tungewapa [emoji3]
 
Na huko lot 3&4 wafanyakazi wameshaanza kupunguzwa inatarajiwa watu 500+ wasimamishwe na hawa ni watanzania pekee bado na waturuki watapunguzwa pia.
Niko dodoma ihumwa Hapa Niko karibu na kampu hi Ni kwamba kazi huku siyo kubwa kihvyo hbyo namuona mkandarasi akipunguza wafanyakaz kila uchao
 
Mnapoona pale juu mnaona kuna mtu pale?
Wala sio tatizo la pale juu, bali dhalimu aliingia kwenye game kichwa kichwa kusaka sifa za kishamba, lakini ukweli Tanzania haikuwa na uwezo wa kutekeleza miradi ya 20t kwa wakati mmoja.
 
Karma is real and her other name is a bitch, malipizo ni hapa hapa mradi wa kukomboa taifa na vizazi vyake watu wanafanya mzaha

Ofcourse si mradi wa kwanza kufanyiwa mzaha, the fact ipo mingi ilichezewa, na wanachi wenyewe wakashindwa kufanya lolote to date
Dont wait for karma , just do it
 
Wakati serikali ya Tanzania ikiendelea kuficha ukweli, Kampuni ya ujenzi ya Uturuki ya Yapi Merkezi imeripoti pengo la dola bilioni 1.8 (zaidi ya shilingi trilioni 4.5 za kitanzania) katika ufadhili wa mradi wa reli ya kiwango cha kimataifa nchini Tanzania huku ikiendelea kuwezesha Dodoma kutafuta ufadhili wa mradi huo kote Ulaya.

Makamu Mwenyekiti wa Yapi Merkezi, Erdem Arioglu, ambaye hivi karibuni alimuongoza Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba na ujumbe wa Serikali katika nchi za Hispania, Sweden na Poland kutafuta ufadhili wa mradi huo, aliliambia gazeti la The EastAfrican kuwa harakati za kuchangisha fedha hizo ni ufuatiliaji wa ahadi mbalimbali zinazofikia dola bilioni 2.2. kuelekea mradi wa dola bilioni 10.4.

Alikanusha kuwa Yapi iliongoza misheni hiyo walipochunguza Mpango B - ufadhili mbadala ili kushughulikia matatizo yake yenyewe ya mtiririko wa pesa - lakini walifanya hivyo katika nafasi zao kama mkandarasi mkuu kwa awamu nne za kwanza za mradi.

Source: THE EASTAFRICAN
Turkey contractor confirms $1.8bn gap in funding Tanzania SGR
Kwanini Serikali ya Mama Samia imeongezea Makutupora to Isaka, Isaka to Mwanza na Tabora to Kigoma wakati hakuna hela.

Kwanini tusimalize kwanza walau Dar to Dodoma.
 
Niko dodoma ihumwa Hapa Niko karibu na kampu hi Ni kwamba kazi huku siyo kubwa kihvyo hbyo namuona mkandarasi akipunguza wafanyakaz kila uchao
Ukiacha hiyo lot 2 ni kuanzia lot 3 (makutupora-tabora na lot 4 tabora -isaka) huko watu wanapunguzwa na mradi bado haujafikia ata asilimia 25.
 
Wakati serikali ya Tanzania ikiendelea kuficha ukweli, Kampuni ya ujenzi ya Uturuki ya Yapi Merkezi imeripoti pengo la dola bilioni 1.8 (zaidi ya shilingi trilioni 4.5 za kitanzania) katika ufadhili wa mradi wa reli ya kiwango cha kimataifa nchini Tanzania huku ikiendelea kuwezesha Dodoma kutafuta ufadhili wa mradi huo kote Ulaya.

Makamu Mwenyekiti wa Yapi Merkezi, Erdem Arioglu, ambaye hivi karibuni alimuongoza Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba na ujumbe wa Serikali katika nchi za Hispania, Sweden na Poland kutafuta ufadhili wa mradi huo, aliliambia gazeti la The EastAfrican kuwa harakati za kuchangisha fedha hizo ni ufuatiliaji wa ahadi mbalimbali zinazofikia dola bilioni 2.2. kuelekea mradi wa dola bilioni 10.4.

Alikanusha kuwa Yapi iliongoza misheni hiyo walipochunguza Mpango B - ufadhili mbadala ili kushughulikia matatizo yake yenyewe ya mtiririko wa pesa - lakini walifanya hivyo katika nafasi zao kama mkandarasi mkuu kwa awamu nne za kwanza za mradi.

Source: THE EASTAFRICAN
Turkey contractor confirms $1.8bn gap in funding Tanzania SGR
Hizi hela si ndo mradi mzima au .inaamaana hajalipwa hata kidogo
 
Back
Top Bottom