Mkapa kaondoka, je nani atamfunga paka Kengele?

Mkapa kaondoka, je nani atamfunga paka Kengele?

Historia ina tabia ya kujirudia, alichofanya Raisi Magufuli kwa Mzee Mkapa ndicho alichokifanya Raisi Mkapa kwa Mzee Nyerere. Mwaka 1995 ulikuwa ni mwaka wa wakina Jakaya na Malecela lakini Mzee Nyerere akatumia nguvu zake za Ubaba wa Taifa kumfanya Mkapa awe Raisi. Mkapa alinadiwa kama Mr Clean huku Magufuli kama Tingatinga na Askari wa Mwamvuli.

Haukuvuka hata mwaka Raisi Mkapa akaanza kumkera sana Mzee Nyerere, basi watu wakawa wanapeleka malalamiko yao kwa Mzee Nyerere kwasababu wanamuogopa Mkapa. Baada ya mwaka 2015 watu walianza kupeleka malalamiko yao kwa Mzee Mkapa kisa wanamuogopa Magufuli. Yaani historia imejirudia vizuri sanaa!

Mzee Nyerere alikufa kwa majonzi baada ya kugeukwa na Mkapa,
Mzee Mkapa amekufa kwa majonzi baada ya kugeukwa na Magufuli.
Historia huwa ina tabia ya kujirudia rudia tu, hivyo tuwe tunatunza kumbukumbu zetu vizuri.

NB: Baada ya Mzee Nyerere kufariki hakukuwa na mtu wa kumfunga lijamu Mkapa, akaamua kutuuza wananchi wote kwa mabepari maana alifanya kila analotaka. Raisi Magufuli naye anaelekea kulekule kwenye "ABSOLUTE POWER" ambako Raisi Mkapa alielekea baada ya kifo cha Mzee Nyerere. Hatua stahiki zisipochukuliwa na watu wenye akili timamu tutakuja siku kuikumbuka hii miaka kwa majonzi sana.
 
Historia ina tabia ya kujirudia, alichofanya Raisi Magufuli kwa Mzee Mkapa ndicho alichokifanya Raisi Mkapa kwa Mzee Nyerere. Mwaka 1995 ulikuwa ni mwaka wa wakina Jakaya na Malecela lakini Mzee Nyerere akatumia nguvu zake za Ubaba wa Taifa kumfanya Mkapa awe Raisi. Mkapa alinadiwa kama Mr Clean huku Magufuli kama Tingatinga na Askari wa Mwamvuli.

Haukuvuka hata mwaka Raisi Mkapa akaanza kumkera sana Mzee Nyerere, basi watu wakawa wanapeleka malalamiko yao kwa Mzee Nyerere kwasababu wanamuogopa Mkapa. Baada ya mwaka 2015 watu walianza kupeleka malalamiko yao kwa Mzee Mkapa kisa wanamuogopa Magufuli. Yaani historia imejirudia vizuri sanaa!

Mzee Nyerere alikufa kwa majonzi baada ya kugeukwa na Mkapa,
Mzee Mkapa amekufa kwa majonzi baada ya kugeukwa na Magufuli.
Historia huwa ina tabia ya kujirudia rudia tu, hivyo tuwe tunatunza kumbukumbu zetu vizuri.

NB: Baada ya Mzee Nyerere kufariki hakukuwa na mtu wa kumfunga lijamu Mkapa, akaamua kutuuza wananchi wote kwa mabepari maana alifanya kila analotaka. Raisi Magufuli naye anaelekea kulekule kwenye "ABSOLUTE POWER" ambako Raisi Mkapa alielekea baada ya kifo cha Mzee Nyerere. Hatua stahiki zisipochukuliwa na watu wenye akili timamu tutakuja siku kuikumbuka hii miaka kwa majonzi sana.
We have 2 problems.
1.CCM
2.Ccm voters
 
Hapa ni kimoja tu wandugu tumpe Lissu huyu bwana ataokoa ya hovyo mengi ambayo yanakuja kuanzia 2021 hadi 2025, wengi watajuta hapa.
Ni siri iliyo wazi kuwa Hayati Benjamin Mkapa alikuwa nguzo muhimu sana CCM haswa katika utawala huu wa Magufuli. Mkapa alikua mtu pekee ambae alikua haogopi kumpa Magufuli za uso. Magufuli mwenyewe alikua sio tu anamheshimu sana, bali alikua anamchukulia kama baba yake maana Mkapa ndiye aliyemsaidia kuingia kwenye ulingo wa siasa, na alichangia sana yeye kuwa Rais 2015.

Mkapa ndiye alimnadi Magufuli jukwaani 1995 wakati anaomba ubunge Chato ambao Magufuli alishinda. Akamteua kuwa Naibu Waziri na baadae kuwa Waziri kamili. Tunajua Mkapa alizungumza wazi uchapakazi wa Magufuli mpaka kumuita Askari wake wa Mwavuli, hali iliyosababishwa Magufuli kunyweshwa sumu na "watu" waliodhani anaandaliwa na Mkapa kuwa Rais 2005. Mkapa aliendelea kumlinda na hata kumpa ulinzi wa usalama wa taifa.

Mchakato wa Urais 2015
Tunajua Lowassa alikatwa 2015 sababu Kikwete alitaka Membe amrithi Urais. Vyanzo mbalimbali ndani ya chama vinasema Kamati ya Wazee, kwa ushawishi mkubwa wa Mzee Mkapa, vilionya Membe asingeweza kumshinda Lowassa sababu wananchi wangeona ni muendelezo wa miaka mitano wa Rais Kikwete. Ndipo jina la Magufuli likapendekezwa na Mkapa, na alitetea kuwa Magufuli ni mtu ambae amefanya kazi zake "consistently" na kuwa ni mtu ambae hana "roots" ndani ya chama hivyo itakua rahisi CCM kunadi sera za Rushwa ambayo ndio ilikua agenda kuu ya Upinzani. Kikwete ikabidi akubali, na kilichofuata ilikua tu itifaki ya kupitisha jina la mgombea.

Baada ya Urais 2015
Mkapa alifurahishwa na jinsi Magufuli alivokuwa anaendesha nchi mwanzoni, ila baada ya kama mwaka hivi, akaona jinsi mtu aliempigania alivokuwa ameaza kubadilika. Alikua ananadi mafanikio ya serikali kama ya kwake (Magufuli) binafsi na sio ya CCM. Pia, Magufuli, mara kadhaa alikua anaponda jinsi MaRais wezake walivyoendesha nchi na mida mengine aliponda sera za Mkapa za ubinafsishaji.

Hata hivyo, uhusiano kati ya hawa ulizorota sana kwa takribani mwaka hivi maana Magufuli aliona anamuingilia sana katika kazi zake. Mkapa akanawa mikono. Waliohudhuria mkutano wa Mkapa kule kigamboni 2018 mnajua alisema kuwa anaomba asihusihwe na mambo yanayoendelea nchini maana kama mstaafu amejaribu kwa nguvu zote kutoa mchango wake ila hausikilizwi.

Kwa mnaofuatilia kwa ukaribu sana siasa za nchi mtajua kuna wakati, Rais Mkapa alikuwa haonekani katika hafla za kitaifa, ni kwa sababu alikuwa anagomea mialiko. Magufuli, kuona mtu anaemuheshimu hampi support, alijirudi, akaongea nae na uhusiano wao ukaanza kurudi taratibu.

Baada ya hapo alikua moja wa watu wachache sana ambao Magufuli alikua anawasikiliza. Hata baadhi ya wazee (kina Kikwete) walikua wanamtumia yeye kuwasilisha madukuduku yao. Kama unakumbuka ile audio ya Kinana iliyovuja mtandaoni, Kinana alisikika akimwambia Nape kuwa Mkapa alitaka kumuona Magufuli kuongea nae kuhusu maswala ya Chama, ila Magufuli alikua anamkimbia. Hii ilidhiirisha influence ya Mkapa kwenye uRais wa Magufuli.

Nini sasa baada ya kifo?
Wastaafu waliobaki tunajua hawana nguvu kama aliyokuwa nayo mzee Mkapa kumshauri Magufuli kwenye maswala mbalimbali, Kikwete analinda maslai ya familia yake - mtoto na Mke wake waendelee kuwa Wabunge, na pia kulinda baadhi ya bishara zake. Mwinyi anataka mwanae awe Rais wa Zanzibar na pia ukweli ni kuwa amekua mzee sana na hata mawazo yake (kama lile la kutaka Magufuli apewe zawadi ya kuongezewa muda wa uongozi) hayachukuliwi kwa uzito.

Ndio maana Kikwete amesikitika sana, anajua jinsi huyo mzee alivokuwa na nguvu katika kutoa kauli ya wastaafu. Mkapa alikua moja ya watu wachache sana ambao walikua hawamwogopi Magufuli, and he spoke his mind whenever necessary.

Kwa hali ya siasa ilivyo nchini, kilichobaki ni kumuomba Mungu tu, maana kizingiti kikubwa kilichokuwa kimzuie Magufuli (kama alikua na mpango wa kubadilisha katiba atawale zaidi ya 2025) kimeondoka. Tuwaombee wastaafu waliobaki wasimame kwa umoja na nguvu moja kusemea maswala muhimu ya nchi, la sivyo tunapoelekea naona giza tu.
Kweli sauti ya mamlaka imeondoka
Wee unafikiri alivyokuwa ana mkaripia magu alifurahi moyoni wakati magu uwezo anao?
Aliondoka Nyerere mwl wa Nkapa, eti ndio tujiulize mwanafunzi wake kuondoka itakuwaje?
Kama unawasiwasi washauri wamuweke kwenye machine kama Ariel Sharon wa Israeli.

Faida niliyo ipata hapa ni kujua madhumuni ya kitabu cha marehemu kwamba ni kujaribu kudhibiti kauli ile ya mambo ya hovyo na nchi kufanywa shamba la bibi na watangulizi wa incumbent. Si ajabu wale Wazee wa watakao, wastaafu walio Sifiwa na Bashiru wakati ule walikuwa wanatumiwa kuendeleza mchakato maalumu ulio anzishwa na uandishi wa kitabu cha marehemu.
Umeongea jambo la maana sana
JPM kapata pigo kubwa sana…tumfariji
Muda wa kumfunga paka kengele haupo. Paka apigwe manati ya utosi
Wakati ni ukuta Mungu atotuacha yatima
 
Paka...
DbEjGegX4AAzkLw.jpg

0b257f060fe7fb239d15bf885e362caf.jpg

1265b3c63f741ce2c9d3ebcbf63f9aef.jpg
 
Hapa ni kimoja tu wandugu tumpe Lissu huyu bwana ataokoa ya hovyo mengi ambayo yanakuja kuanzia 2021 hadi 2025, wengi watajuta hapa.

Lissu alijimaliza mwenyewe alipounga mkono ujio wael cdm. Haya mengine yote anayo ya fanya ni yale ya mfa maji. Dhambi ya ulaghai wao kwetu wananchi kamwe haita waacha salama. Wameanza kuvunjika/kuvunjwa miguu mwisho wake ni mioyo. Labda watubu kwa Mola wao wala si kushupaza shingo. Nikuulize siku hizi za karibu ulisha wasikia wakiongelea juu ya wale wahanga wa Arusha kati ya wengi walio waponza kwa kuwajaza ujinga? Wanachoongelea sasa ni kukumbatia ubeberu na ushoga maana ndiko ulaji uliko.
 
Historia ina tabia ya kujirudia, alichofanya Raisi Magufuli kwa Mzee Mkapa ndicho alichokifanya Raisi Mkapa kwa Mzee Nyerere. Mwaka 1995 ulikuwa ni mwaka wa wakina Jakaya na Malecela lakini Mzee Nyerere akatumia nguvu zake za Ubaba wa Taifa kumfanya Mkapa awe Raisi. Mkapa alinadiwa kama Mr Clean huku Magufuli kama Tingatinga na Askari wa Mwamvuli.

Haukuvuka hata mwaka Raisi Mkapa akaanza kumkera sana Mzee Nyerere, basi watu wakawa wanapeleka malalamiko yao kwa Mzee Nyerere kwasababu wanamuogopa Mkapa. Baada ya mwaka 2015 watu walianza kupeleka malalamiko yao kwa Mzee Mkapa kisa wanamuogopa Magufuli. Yaani historia imejirudia vizuri sanaa!

Mzee Nyerere alikufa kwa majonzi baada ya kugeukwa na Mkapa,
Mzee Mkapa amekufa kwa majonzi baada ya kugeukwa na Magufuli.
Historia huwa ina tabia ya kujirudia rudia tu, hivyo tuwe tunatunza kumbukumbu zetu vizuri.

NB: Baada ya Mzee Nyerere kufariki hakukuwa na mtu wa kumfunga lijamu Mkapa, akaamua kutuuza wananchi wote kwa mabepari maana alifanya kila analotaka. Raisi Magufuli naye anaelekea kulekule kwenye "ABSOLUTE POWER" ambako Raisi Mkapa alielekea baada ya kifo cha Mzee Nyerere. Hatua stahiki zisipochukuliwa na watu wenye akili timamu tutakuja siku kuikumbuka hii miaka kwa majonzi sana.
hvi ni kweli haya maneno uliyoyaandika?
 
Historia ina tabia ya kujirudia, alichofanya Raisi Magufuli kwa Mzee Mkapa ndicho alichokifanya Raisi Mkapa kwa Mzee Nyerere. Mwaka 1995 ulikuwa ni mwaka wa wakina Jakaya na Malecela lakini Mzee Nyerere akatumia nguvu zake za Ubaba wa Taifa kumfanya Mkapa awe Raisi. Mkapa alinadiwa kama Mr Clean huku Magufuli kama Tingatinga na Askari wa Mwamvuli.

Haukuvuka hata mwaka Raisi Mkapa akaanza kumkera sana Mzee Nyerere, basi watu wakawa wanapeleka malalamiko yao kwa Mzee Nyerere kwasababu wanamuogopa Mkapa. Baada ya mwaka 2015 watu walianza kupeleka malalamiko yao kwa Mzee Mkapa kisa wanamuogopa Magufuli. Yaani historia imejirudia vizuri sanaa!

Mzee Nyerere alikufa kwa majonzi baada ya kugeukwa na Mkapa,
Mzee Mkapa amekufa kwa majonzi baada ya kugeukwa na Magufuli.
Historia huwa ina tabia ya kujirudia rudia tu, hivyo tuwe tunatunza kumbukumbu zetu vizuri.

NB: Baada ya Mzee Nyerere kufariki hakukuwa na mtu wa kumfunga lijamu Mkapa, akaamua kutuuza wananchi wote kwa mabepari maana alifanya kila analotaka. Raisi Magufuli naye anaelekea kulekule kwenye "ABSOLUTE POWER" ambako Raisi Mkapa alielekea baada ya kifo cha Mzee Nyerere. Hatua stahiki zisipochukuliwa na watu wenye akili timamu tutakuja siku kuikumbuka hii miaka kwa majonzi sana.
Aisee..
Ngoja nikae kimya..
Huwenda Ricin imehusika kulingana na maelezo yako..
 
Huu ndio ukweli.Sio tu kuwa waliobaki hawawezi kumfunga gavana aliyeko kilingine, ila pia kwa sababu mbalimbali hawana msimamo wa kuwafanya wathubutu kumyooshea kidole ...
 
Mtu pekee ni JK, sema watu hawataki kumkubali kwa sababu anaonekana soft lakini ni mtu mwenye mizizi sehemu zote za za serikali kuanzia JWTZ ambako wengi wa wakubwa amewafundisha pale monduli.


Cha msingi tuombe Mungu, na kumwamini Magufuli kwamba sasa atawaza kama baba mwenye nyumba na nchi ikiharibika laana itakua juu yake.
Kuwafundisha siyo hoja,
Hoja ni kauli yenye mamlaka
 
Mtu pekee ni JK, sema watu hawataki kumkubali kwa sababu anaonekana soft lakini ni mtu mwenye mizizi sehemu zote za za serikali kuanzia JWTZ ambako wengi wa wakubwa amewafundisha pale monduli.


Cha msingi tuombe Mungu, na kumwamini Magufuli kwamba sasa atawaza kama baba mwenye nyumba na nchi ikiharibika laana itakua juu yake.
Watu wanamchukulia kikwete mwepesi sana lakini huyu mzee Ni mtu mzito sana sana sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwezi Iona thamani ya mtu angali bado anaishi Ila akishakufa ndo utajua thamani na umuhimu wake.

Ukweli nikwamba Taifa la Tanzania tumepoteza mtu mhimu Sana na hata CCM imepoteza mtu mhimu Sana ambae alikuwa yupo tayari alale njaa ili CCM ipate ushawishi na kura za kutosha kutoka kwa wananchi.
Oh basi sawa.
 
Back
Top Bottom