Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Una faida KWA shetani pekeeUchawi hauna faida
Mwendelezo ni lini? Ni vyema ukiimwaga yote kwa wakati mmoja, sio mbaya ukimuiga Deeppond ktk utoaji simulizi mkuu hakuna cha 'itaendelea'clara unataka kufanya nini?” iliskika sauti hio
Je nini kilifuata
Nitarudi kusomaSEHEMU YA KWANZA.
Nikiwa nimerudi kutoka shuleni nilikutana na mama nje ambaye alinambia tumepata mgeni ambaye atakua akitusaidia kazi za ndani yaani dada wa kazi, kutokana na uchovu na fimbo za siku hio hata sikua na hamu ya kutaka kujua zaidi kuhusu jambo hilo nilimjibu mama kwa kifupi.
“haya”. Huku nikielekea ndani ambapo nilifika na kumkuta dada mmoja aliyekua na umri kati na miaka kumi na saba hadi ishirini ambaye alinichangamkia kama mtu tuliyejuana siku nyingi.
“mambo clara habari ya shule”. Aliongea dada Yule. Na kunifanya nishangae kalijuaje jina langu lakini nilihisi huenda mama alishamwambia kwamba ana mtoto anaeitwa clara.
“nzuri shikamoo dada,”. Niimjibu kwa heshima kwa kua alikua ameninzidi ki umri hivyo alistahili heshima kwani mimi nilikua darasa la nne tu, baada ya kumjibu nilielekea ndani na kulitua begi langu pia nilikuta mizigo ya dada Yule ambaye ilionesha hakua amefika muda mrefu.
Kwakua tulikua tukipata chakula shuleni nilipitiliza kulala ambapo usingizi ulinipitia na nilikuja kustuka majira ya saa sita usiku ambapo nilimuona dada Yule akiwa ameketi kitandani uchi wa mnyama huku akiwa ameinguanisha mikono yake kama mtu aliyekua akisali.
Moyo wangu uliogopa sana na nililazimika kufikicha macho ili nijue kwamba ilikua ndoto au la na niligundua kwamba haikua ndoto bali ilikua ni ukweli kabisa.
Kisha dada Yule akasimama na kuanza kutembea tembea ndani ya chumba changu huku mikono akiwa ameikunja vile vile na macho yake yakiwa yamefungwa, na kisha baada ya muda, alirudi kitandani na kuketi kama alivyokua awali.
Baada ya dakika tano nilimshuhudia mama nae akija chumbani akiwa amevaa kama dada Yule, hapo nilishindwa kujizuia na kutamka.
“haaa, mama kumbe nawe mchawi”. Niliongea kwa mashangao kauli ambayo ilimstua sana mama na kisha akanisogelea bila uwoga na kuniambia.
“shhhhhhhhh, hakuna haja ya kujificha sasa mimi ni mchawi ndio na hata wewe ni lazima uwe mchawi au laa nikuue kama nilivyomfanya baba yako”.aiongea mama maneno ambayo yalinistua sana na kunifanya nianze kutetemeka.
“unaogopa nini? Mimi ni mchawi toka nilipokua na umri kama wewe umewahi kunigundua? Umewahi kuniona nikitisha? Acha ujinga mwanangu”. Aliongea mama na baada ya muda tulimshuhudia dada Yule wa kazi akiinuka huku macho yake yakiwa yanawaka kama tochi. Na hapo nilimshuhudia mama akipiga goti na kuanza kumsujudu dada Yule.
“naam mkuu, nimekuletea binti huyu akiwa kama mwanachama mpya”. Aliongea mama ambapo dada Yule alinitazama kwa makini sana kisha kumgeukia mama.
“inabidi tumfundishe taratibu kabla ya kumtambulisha kwa wenzetu”. Aliongea dada Yule kisha nilimshuhudia mama akiinuka na kunigeukia.
“mwanangu clara, wewe ndiye wa pekee kwangu na nimekuteua wewe upate kujua vitu vyangu vya ndani, na mbona sikuwaambia kaka zako? Naomba uniisitiri”. Aliongea mama na kunipa mtihani mgumu sana katika umri mdogo na mpaka apo sikua nimesema jambo lolote.
Mwisho mama alichukua unga mweupe na kunipaka katika paji la uso kisha tulijikuta sehemu nyingine kabisa ambayo ilikua ngeni kabisa lakini iionesha ilikua ni katika msitu uliopo kando ya barabara.
Kwani magari yalikua yakisikika yakipiita,
“mwanangu, huu ni msitu wa wachawi msitu ambao ukiingia kama si mchawi basi huwezi toka na utafanywa kafara”. Aliongea mama kauli ambayo ilinifanya niwaone wachawi ni watu wabaya.
“Watu wengi wamepotea katika msitu huu na vifo vyao vilikua vya kutatanisha , hiii ni kwasababu wanachukuliwa na mizimu na kufanywa kafara lakini mchawi si mtu mbaya ila wapo ambao wanautumia uchwi vibaya kwa kufanya visasi na mauaji”. Aliongea mama mambo mengi kuhusu uchawi kisha alinifundisha dawa nyingi sana za kichwawi ikiwemo za kupotea na kiini macho.
Kwakua muda ulikua umekwenda tulirejea nyumbani ambapo bado nilikua na maswali mengi sana na siku hio nilipanga ktoka na kwenda kwa rafiki yangu zuwena nipate kumuuliza mambo kadhaa kuhusu hali iliyonitokea jana usiku.
Nilimuaga mama vizuri na kumwambia nilikua nikienda kwa rafiki yang na alichonisisitiza ni kuwahi kurudi.
Nilipofika nyumbani kwa rafiki yangu kulikua kimya sana ambapo nilibisha hodi mara tatu na kufunguliwa na zuwena mwenyewe
“mambo clara”. Alinisalimu zuwena huku akinikaribisha ndani ambapo tulipiga storiza hapa na pale mwisho niliamua kumuuliza swali.
“eti unawafahamu wachawi”. Nilihoji
“eee, ni wanatisha sana na ni wabaya, wauaji na hawana huruma”. Zuwena aliongea kana kwamba ni mtu anaejua mambo mengi sana kuhusu uchawi.
“basi nikwambie kitu zuwena, mwenzio mama yangu ni……”. Kabla sijamaliza ilikuja sauti kichwani mwangu ambayo niliitambua kwamba ni ya mama.
“clara unataka kufanya nini?” iliskika sauti hio
Je nini kilifuata
heee!...mara hii uzi ushafika sehemu ya tatu?.ya pili iko wapi?.SHEMU YA TATU
INAENDELEA; Niliamka asubuhi nikiwa nimechoka sana, na kwakua ilikua ni siku ja jumapili nilishukuru sana kwani niliutumia muda huo kupumzika.
nlimfuata mama akiwa katika sehemu tulivu na kutaka kumuuliza juu ya hali ya jana ambapo alinambia mzee Yule alikua na utajiri wa misukule na mbali na hapo alikua na kinga kubwa sana pia shariti lake kubwa ni kutolala kitandani, na ndio maana tulipoingia tuliona maji tu.
Nilishangaa kiukweli kwani sikutaraji kwamba uchawi unaweza kua na nguvu hiyo, nilitamani kua mchawii ili niwakomeshe maadui na yoyote atadiriki kunionea hasa shuleni.
Mama alinieleza vitu vingi sana kuhusu uchawi mweupe na mweusi kwamba uchawi mweupe ndio hugeuzwa na kua uchawi mweusi na pia kuna wanyama ambao wana uhusiano na kila aina ya uchawi.
Kwa uchawi mweupe wengi hutumia paka weupe au njiwa weupe katika ulozi lakini vile vile kwa uchawi mweusi hutumia paka weusi ambao inasadikika wana nguvu za kichawi za asili.
Baada ya kuongea na mama kwa muda mrefu alikuja dada na kutuita ili tukapate chakula cha mchana, baada ya kula mama aliniambia anataka anipeleke mahali nikajifunze namna ya kutengeneza dawa za kichawi kwa kutumia mizizi tuliyokata jana.
Tulianza safari kuelekea kwenye shamba letu kubwa la mahindi ambalo katikati lilikua na kijumba kidogo cha nyasi ambacho sikuwahi kukiona japo tulikua tukilima shamba hilo miaka yote.
Tuliingia na mama alinielekeza namna ya kutengeneza na kuzikausha papo hapo kwa kutumia uchawi.
“ukisha maliza kazi hii leo nnitaenda kukutambulisha kua mwanachama mpya”. Aliongea mama
“sawa ila mimi sitaki kuua”. Niliongea kwa woga sana.
“nani aliyekwambia wachawi wanaua? Sisi tunatumia uchawi katika kuongeza mazao mashambani”. Aliongea mama na kunifanya niwe na amani.
Masaa yalisogea hadi ilipohitimu usiku wa manane ambapo mama alikuja kuniamsha kisha tukapotea na kutua katika uwanja wa shule yetu, kwakua tuliwahi tulikuta watu wachache sana huku wengine wakiendelea kutua kila mmoja.
Nilishangaa kuwaona na baadhi ya walimu, moyo wangu ulistuka sana na nilishindwa kujizuia
“haaa, hadi mwalimu msinza”. Nilimwambia mama ambaye aliweka kidole mdomoni kuashiria ninyamaze.
Watu waiongezeka na mwisho alitua mzee mmoja wa makamo akiwa na kofia nyekundu na kaniki nyeupe na nyekundu pmoja na usinga.
Wachawi wote waliinama kwa heshima nami baada ya kuona peke ndiye nimesimama, niliinama kama wenzangu na baada ya muda wote tuliinuka.
“tumepata mgeni na tunaimani ataifanya kazi hii vizuri na kwa ushirikiano bila kutoa siri zetu”. Aliongea mzee Yule ambapo zilipigwa ngoma kisha moto mkubwa uliwashwa na nilishuhudia kina mama wawili wakija na maiti mbili za kiume na inaonesha walikua na umri usiozidi miaka 25.
Wachawi wote walishangilia na kucheza kwa furaha kisha ulifika ule wasaa wa kula nyama ambao ndio ulikua wakati mgumu kwangu katika nyakati zote nilizowahi kupitia duniani.
Kwenye foleni mimi ndiye nilikua wa kwanza, kisha alifuata mama na wa tatu alikua dada, nilipewa pande kubwa la nyama ambalo lilinifanya nitetemeke mwili mzima hadi kupelekea niidondodhe nyama ile.
Nilipogeuka niliona watu wakinikata jicho hasa mama kwani nilikua namtia aibu ambapo ilibidi niokote kipande kile kisha nilisogea walipoketi mama na dada ambao walikua washamaliza kula nyama zao mimi nikiwa bado naogopa.
Nilianza kula mpaka waliponilazimisha sana na kupelekea mimi kua wa mwisho kisha mkuu wa wachawi alipiga makofi na watu wote walinyamaza kumsikiliza.
Baada ya muda alituita mimi na mama pamoja na dada ambapo mama alipiga goti moja huku tukiwa tumesimama.
“karibu sana binti nakupa hii, hakikisha unaitunza na hailoi na maji itakuepusha na hatari, maelekezo mengine utapewa na mama yako”. Aliogea mzee Yule huku akinivisha hirizi nyekundu mkono wa kushoto kisha akamgeukia dada
“karibu na wewe katika jamii yetu ya wachawi, nina imani unajua kila kitu”. aliongea mzee Yule kisha mama aliinuka na ulikua ni muda wa kutawanyika kila mtu aendelee na shughuli zake kama kuwanga na kuroga kama kawaida.
Tulipotea na kutokea makaburini ambapo
mama aliniambia
“unatakiwa kupeleka kafara ya kukaribishwa kama mwanachama mpya, tunatakiwa kufukua kaburi”.
Je nini kilifuata
Na ukiwaogopa ndo unawapa nguvu.Wachawi wote ni SAwa na mende, kunguni viroboto tu, zaidi ya propaganda hawana nguvu kubwa zaidi ya vitisho tu.