Mkasa: Jinsi nilivyofunzwa uchawi na mama yangu

Nitarudi kusoma
 
Kwann max asingewek sehem ya kurecord voice ili msimuliaji asipate shida ya kuandika kama riwaya za erik shigongo??
 
SHEMU YA TATU

INAENDELEA; Niliamka asubuhi nikiwa nimechoka sana, na kwakua ilikua ni siku ja jumapili nilishukuru sana kwani niliutumia muda huo kupumzika.

nlimfuata mama akiwa katika sehemu tulivu na kutaka kumuuliza juu ya hali ya jana ambapo alinambia mzee Yule alikua na utajiri wa misukule na mbali na hapo alikua na kinga kubwa sana pia shariti lake kubwa ni kutolala kitandani, na ndio maana tulipoingia tuliona maji tu.

Nilishangaa kiukweli kwani sikutaraji kwamba uchawi unaweza kua na nguvu hiyo, nilitamani kua mchawii ili niwakomeshe maadui na yoyote atadiriki kunionea hasa shuleni.

Mama alinieleza vitu vingi sana kuhusu uchawi mweupe na mweusi kwamba uchawi mweupe ndio hugeuzwa na kua uchawi mweusi na pia kuna wanyama ambao wana uhusiano na kila aina ya uchawi.

Kwa uchawi mweupe wengi hutumia paka weupe au njiwa weupe katika ulozi lakini vile vile kwa uchawi mweusi hutumia paka weusi ambao inasadikika wana nguvu za kichawi za asili.

Baada ya kuongea na mama kwa muda mrefu alikuja dada na kutuita ili tukapate chakula cha mchana, baada ya kula mama aliniambia anataka anipeleke mahali nikajifunze namna ya kutengeneza dawa za kichawi kwa kutumia mizizi tuliyokata jana.

Tulianza safari kuelekea kwenye shamba letu kubwa la mahindi ambalo katikati lilikua na kijumba kidogo cha nyasi ambacho sikuwahi kukiona japo tulikua tukilima shamba hilo miaka yote.
Tuliingia na mama alinielekeza namna ya kutengeneza na kuzikausha papo hapo kwa kutumia uchawi.

“ukisha maliza kazi hii leo nnitaenda kukutambulisha kua mwanachama mpya”. Aliongea mama
“sawa ila mimi sitaki kuua”. Niliongea kwa woga sana.
“nani aliyekwambia wachawi wanaua? Sisi tunatumia uchawi katika kuongeza mazao mashambani”. Aliongea mama na kunifanya niwe na amani.

Masaa yalisogea hadi ilipohitimu usiku wa manane ambapo mama alikuja kuniamsha kisha tukapotea na kutua katika uwanja wa shule yetu, kwakua tuliwahi tulikuta watu wachache sana huku wengine wakiendelea kutua kila mmoja.

Nilishangaa kuwaona na baadhi ya walimu, moyo wangu ulistuka sana na nilishindwa kujizuia
“haaa, hadi mwalimu msinza”. Nilimwambia mama ambaye aliweka kidole mdomoni kuashiria ninyamaze.
Watu waiongezeka na mwisho alitua mzee mmoja wa makamo akiwa na kofia nyekundu na kaniki nyeupe na nyekundu pmoja na usinga.

Wachawi wote waliinama kwa heshima nami baada ya kuona peke ndiye nimesimama, niliinama kama wenzangu na baada ya muda wote tuliinuka.
“tumepata mgeni na tunaimani ataifanya kazi hii vizuri na kwa ushirikiano bila kutoa siri zetu”. Aliongea mzee Yule ambapo zilipigwa ngoma kisha moto mkubwa uliwashwa na nilishuhudia kina mama wawili wakija na maiti mbili za kiume na inaonesha walikua na umri usiozidi miaka 25.

Wachawi wote walishangilia na kucheza kwa furaha kisha ulifika ule wasaa wa kula nyama ambao ndio ulikua wakati mgumu kwangu katika nyakati zote nilizowahi kupitia duniani.

Kwenye foleni mimi ndiye nilikua wa kwanza, kisha alifuata mama na wa tatu alikua dada, nilipewa pande kubwa la nyama ambalo lilinifanya nitetemeke mwili mzima hadi kupelekea niidondodhe nyama ile.

Nilipogeuka niliona watu wakinikata jicho hasa mama kwani nilikua namtia aibu ambapo ilibidi niokote kipande kile kisha nilisogea walipoketi mama na dada ambao walikua washamaliza kula nyama zao mimi nikiwa bado naogopa.
Nilianza kula mpaka waliponilazimisha sana na kupelekea mimi kua wa mwisho kisha mkuu wa wachawi alipiga makofi na watu wote walinyamaza kumsikiliza.
Baada ya muda alituita mimi na mama pamoja na dada ambapo mama alipiga goti moja huku tukiwa tumesimama.
“karibu sana binti nakupa hii, hakikisha unaitunza na hailoi na maji itakuepusha na hatari, maelekezo mengine utapewa na mama yako”. Aliogea mzee Yule huku akinivisha hirizi nyekundu mkono wa kushoto kisha akamgeukia dada
“karibu na wewe katika jamii yetu ya wachawi, nina imani unajua kila kitu”. aliongea mzee Yule kisha mama aliinuka na ulikua ni muda wa kutawanyika kila mtu aendelee na shughuli zake kama kuwanga na kuroga kama kawaida.
Tulipotea na kutokea makaburini ambapo

mama aliniambia
“unatakiwa kupeleka kafara ya kukaribishwa kama mwanachama mpya, tunatakiwa kufukua kaburi”.

Je nini kilifuata
 
heee!...mara hii uzi ushafika sehemu ya tatu?.ya pili iko wapi?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…