Mkasa wa Afande Mwasifiga alivyopoteza kazi baada ya kubishana na hayati Rais Magufuli

Mkasa wa Afande Mwasifiga alivyopoteza kazi baada ya kubishana na hayati Rais Magufuli

Logical non sequitur fallacy.

Hataishi milele ila Magufuli katangulia kufa kamuacha afande analifaidi jua bado.

Magufuli na mabobish yake yote ya "Naweza kukuvua manyota" hayakumsaidia kukishinda kifo.

Cheo ni dhamana, usikitumie kujimwambafy na kutishia watu.

Duniani wote tunapita tu.
Kifo Pia kisikuogopeshe kufanya Maamuzi yalipohitajika Maamuzi kwa wakati sahihi.
Kifo ni Hatima.
Kifo ni sheria ya mwisho itakayomhukumu kila Mwanadamu haijalishi aliishi maisha gani duniani.
Bila kuchoka,
Yesu Alikufa akawaacha Wenye dhambi wanakula jua la dunia.
Kwa Mbope ndio uone ajabu!
 
Aliebarikiwa anaacha mfumo imara ambao utaendelezwa na watakaofuatia,tofauti na hapo huo uthubutu,uzalendo,kutetea wanyonge na kumtanguliza Mungu mbele havitaendelezwa.Hivyo nae ataingizwa kwenye kundi la walioshindwa.
Sawa.
Kwahiyo Mbepo Alishindwa nini?
Je, yeye ni wa kwanza kufariki?
Je, hakuna washindi waliotangulia mbele za haki?
 
Jpm sijawahi kumpenda kwa sababu ni mtumia mihemko huku Mungu kambariki akili
Haujakosea, jpm alikuwa ni mtu mwenye akili nyingi sana, hiyo ilipelekea pia awe ni mfuatiliaji wa mambo mengi sana ya nchi, so ktk muktadha huo kukosea ktk maamuzi isingekuwa jambo la kushangza maana alikuwa binadamu mwenye hisia na utashi pia.
 
Aliebarikiwa anaacha mfumo imara ambao utaendelezwa na watakaofuatia,tofauti na hapo huo uthubutu,uzalendo,kutetea wanyonge na kumtanguliza Mungu mbele havitaendelezwa.Hivyo nae ataingizwa kwenye kundi la walioshindwa.
Mbona Babu yako mzaa Baba yako alibarikiwa, lakini wewe mjukuu wake umekuwa kilaza. Kwa hiyo na wewe umekuwa kundi la mavilaza Acha kukariri wewe
 
Leo nimekumbuka mkasa mmoja uliotokea enzi ya awamu ya tano!

Ilikuwa ni Julai 16 ya mwaka 2019 Jumanne tulivu tu ndani ya jiji la Mwanza, ghafla Gereza Kuu la Butimba likapata ugeni wa Amiri Jeshi Mkuu, Rais Magufuli.

Basi baada ya maofisa wa juu kutonywa kuwa Rais angeweza kufika pale, wakajipanga kumpokea.

Punde si punde, hayati Magufuli akawasili na bila kupoteza muda akaomba kuongea na wafungwa ili asikie matatizo yao kama ilivyoada yake.

Wafungwa walifurahi sana kumuona Rais, basi wakaambiwa watoe kero zao. Wakazungumza wengi mpaka ilipofika kwa mfungwa mmoja aliyeamua kumwaga mchele kwenye kuku wengi.

Mmoja ya wafungwa waliopata nafasi ya kuongea na hayati Magufuli alikuwa ni Kalikenye Thomas Nyamboge, mfungwa mwenye ulemavu wa ngozi, aliyekuwa anatumikia kifungo cha Miaka 30 jela.

Mfungwa Kalikenye yeye akatoa kero yake kuhusu Afisa Usalama wa Gereza hilo, Afande Mwasifiga kuwa anashirikiana na wafungwa wengine kwa kuwapa simu waongee na watu wa nje ya Gereza kinyume na utaratibu uliowekwa lakini pia anashirikiana na baadhi ya wafungwa wenye hela kuingiza simu kwenye Gereza hilo la Butimba.

Mfungwa wa miaka 30 Jela, Bwana Thomas Kalikenye akaendelea kumsagia kunguni Afande kuwa, msako ukipita simu hazionekani na wao akina Thomas wasiohusika na kuingiza simu wanamwagiwa vitu vyao kama vile Karanga, Sukari, Sabuni na saa nyingine vinachukuliwa kwa nguvu na team ya Afande Mwasifiga.

Ghafla hayati Magufuli anabadilika na kuuliza yuko wapi huyo Afande Mwasifiga? Afande anatokea na kupiga saluti na kuanza kujibu shutuma.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Afande Mwasifiga anaanza kubishana na Rais Magufuli kuhusu suala la uwepo wa simu kwa wafungwa katika Gereza la Butimba.

Afande Mwasifiga katika ubishani wake akamuambia Rais Magufuli, “huyu alitaka kuniinua” Maneno hayo yalimchefua sana Rais.

Magufuli akamwambia afande kuwa”inaonekana una dharau sana wewe” akawa ameshakasirika huku wasaidizi wa Rais wakimtonya Afande Mwasifiga aombe msamaha kwa Rais. Kweli akaomba msamaha huku akipiga saluti, lakini haikusaidia kitu.

Kama utani Rais Magufuli akamwambia ninaweza nikang’oa hizo nyota zako hapo (huyu Afande alikuwa na nyota mbili).

Basi Rais akaachana nae akamalizia kuongea na wafungwa kama alivyopanga ana akatoa agizo kwa Mkuu wa Gereza la Butimba, ole wake mfungwa yoyote aliyetoa kero anyanyaswe, basi atachukua hatua mara moja. Akamaliza akaaga akaondoka zake.

Usiku wake, Afande Mwasifiga akapokea maelekezo kuwa ameondolewa Gereza la Butimba na kupewa uhamisho wa kwenda Ukerewe.

Sambamba na hilo, akavuliwa nyota yake moja alitoka kuipata siku chache kabla ya kubishana na Rais. Hivyo basi akabaki na nyota moja tu badala ya mbili kama hatua ya kinidhamu iliyochukuliwa dhidi yake.

Kama haitoshi, baada ya miezi sita akiwa katika kituo chake kipya cha kazi, akastaafishwa kwa maslahi ya umma na utumishi wake ndani ya Jeshi la Magereza ukawa umefikia kikomo.

Ikumbukwe alipewa miaka mitano ya ziada jeshini baada ya kupewa nyota ya pili kabla ya kuipoteza nyota hiyo kutokana na kubishana na Rais.

Ukawa ndio mwisho wa Afande Mwasifiga, aliyepata kuwa Mkuu wa Usalama ndani ya Gereza la Butimba na waliopata kufanya nayr kazi wanakwambia alikuwa ni mjivuni, kiburi kwelikweli.

Kwasasa amerudi kwao Mbeya akiwa ni mkulima akiendeleza maisha baada ya kustaafishwa kwa maslahi ya Umma!View attachment 3164402
Mkuu uandishi na usimulizi wako ni mzuri sana..kongole
 
Huyo mfungwa kama hajamaliza kifungo chake hadi leo basi hana bahati lazima kahamishiwa kwenye yale magereza magumu ya kilimo
 
Sawa.
Kwahiyo Mbepo Alishindwa nini?
Je, yeye ni wa kwanza kufariki?
Je, hakuna washindi waliotangulia mbele za haki?
Yeye sio wakwanza kufariki,je katuachia nini tunachokiishi? Ni hizi amri alizokua anazitoa kwenye majukwaa? Na baada ya kuondoka yeye nini kimefuata? Vipi angetuachia bunge lenye meno ambalo lingekua linaihoji serikali kila inapofanya vitu visivyoeleweka? Yeye ndio katuachia haya matatizo ya kujaza wabunge wanaobenuka sarakasi.
 
Back
Top Bottom