#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

Tunarudi tena kwenye mada ya msingi ambayo bado ilikuwa bado inaendelea……………….



MATUKIO YALIYOWAHI KUJITOKEZA KABLA NA BAADA YA JUNI 2018, YAANI MWEZI AMBAO ILISEMEKANA KUWA MALIMBIKIZO YALILIPWA


Kwa hiyo mnamo August 2018 baada ya BA kuwa wameshusha riba ya akaunti yake, mhusika aliamua kwenda BB na kufungua FDR nyingine na benki hiyo,

  • Hata hivyo aliendelea kuwa na akaunti mbili na BA ikiwemo ile ambayo alihamisha fedha na kuzipeleka BB
  • Kwa hiyo kwa kipindi hicho, hakupendelea kuchukua hatua ya kufunga akaunti zake na BA
Ilipofika April 2020 (mwaka jana), akiwa anataka kufungua FDR nyingine na BB baada ya ile ya mwanzo kuwa ime-expire:

  • Akabaini kuwa kulikuwa na conspiracy kati ya baadhi ya wafanyakazi wa benki hizi mbili, yaani wafanyakazi wa tawi lile jingine la BA lililoko karibu na lile la BB
  • Conspiracy hiyo ililenga kum-trigger mhusika ahamishe tena pesa yake ambayo amekuwa aki-invest na watu wa BB na kuirudisha tena BA alikowahi kuihamisha mnamo August 2018
  • Conspiracy hii ilifanyika kwa sababu wafanyakazi hawa walijua kuwa mhusika alikuwa bado ana akaunti zake mbili na BA
  • Motive hasa ya conspiracy ya wafanyakazi hawa hakuweza kuibaini vizuri kwa wakati huo
Kwa mtu yeyote yule mwenye akili timamu, ataonawazi kabisa kuwa hapa ilikuwa inatafutwa namna fulani iliyokuwa imedhamiriwa kutengeneza mazingira ya confusion ya possibly kiasi gani cha fedha ( au kiasi cha fedha ya malipo gani) ya mhusika kiko BA na kiasi gani kiko BB

Na kama “hypotheisis” ya mhusika (ya hivi karibuni aliyoiainisha hapo juu kuhusiana na swala la malimbikizo ambayo hajawahi kulipwa hadi leo) iko sahihi, basi possibly yaweza kuwa hadi kipindi hicho, kulikuwa possibly, na fedha nyingi (sustancial) ya mhusika ambayo BA walikuwa bado wanayo kwenye system yao ya benki, ila ambayo mhusika hajawahi kuwa na taarifa yake (fedha hizo). Hii inaweza kuwa ndiyo fedha ile ya malimbikizo, assuming iliwahi kutoka

Kilichkuwa kimekusudiwa na conspiracy hiyo ni kwamba Ilitakiwa sasa mhusika aendelee kuwa na pilika pilka za uteja na BA kwa kutumia fedha zake anazozijua, ili hata zile asizozijua na ambazo hafaidiki nazo, nazo pia ziendelee kupata uhalali wa kuendelea kuwepo BA, na wakati huo huo mhusika akiwa hafaidiki na fedha hizo na pia akiwa hajui kama BA wana fedha hizo



HITIMISHO


Vinginevyo basi matukio haya yanaweza kuwa coincidental tu, isipokuwa kwa namna yalivyokaa, hata mtu mwingine yeyote yule mwenye akili timamu, pindi inapotokea amekutana na matukio yenye pattern ya namna hii, lazima tu ajaribu kuyachakata kwa kwenda umbali huu kama alioenda mhusika



Kwa hali hiyo basi, kukwepa mkanganyiko huu ambao ulikuwa unaanza kupandwa na wafanyakazi hawa kichwani kwa mhusika, hatimaye aliamua kurudi tawini kwake BA na kuzifunga akaunti hizo zote mbili kwa mkupuo, mnamo April 2020. Hivyo basi akaunti hizo hazi-exist tena hadi leo hii, yaani hazipo tena.



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
DOKEZO MUHIMU

UHUSIANO UNAOONEKANA KUJITOKEZA KATI YA HAYA YOTE YALIYOELEZWA HAPO JUU; NA MKUTANO WA DHARURA WA WANAUME ULIOWAHI KUITISHWA NA KIONGOZI MKUU WA KANISA A J2 YA TAREHE 26-04-2020


  • Mkutano huu wa Kanisan A uliitishwa siku ya J2 kwenye wiki ile ya kwanza ambayo taarifa hizi za mhusika zilianza kuonekana kwenye mtandao huu kwa mara ya kwanza
  • Hadi muda huu January 2021, inaonyesha dhahiri kabisa kuwa kwa wakati huo, ilianza kuibuka hofu ya kwamba hatimaye yatakuja kubainika, haya yote ambayo tayari yamo kwenye uzi huu
  • Kwa hiyo J2 ya tarehe 26 April 2020, ikbaidi sasa uwekwe mkakati Kanisani A ukiwa umekusudiwa kuzima jitihada za kuenea kwa taarifa hizi
  • Hii inathibitishwa na ukweli kuwa Mr X alionekana ghafla Kanisani hapo na kuja kukaa karibu kabisa na mhusika
  • Kulikuwa kumepangwa kufanyika fujo, iwapo tu mhusika angefunua kinywa chake kuongea chochote
  • Mr X alikuwa amekusudiwa kuwa ni mediator kati ya mhusika; na wale wote ambao walikuwa wameandaliwa kusimama na kumzonga kwa fujo mhusika na katika namna ile ambayo walikuwa wamepanga kuzifanya fujo hizo
  • Kwa hiyo basi, Mr X ilikuwa atekeleze jukumu hilo kwa kumtaka au hata kujifanya kama anajaribu kumzuia kwa nguvu, mhusika asipigane kanisani. Alikuja kukaa naye karibu ili iwe rahisi kwake kuweza kumshika mhusika
  • Possibly angeweza kumshika kijanaj huku akimpiga ki-kelb cha kisisri siri ili kum-excite. Huyu mtu ni mtu umbile la nje, ila ndani rohoni ni kitu kingine tu ambacho Mungu aliyemuumba ndiyo anayejua ni kitu gani
  • Vile vile Mr X alikusudiwa kuwa shahidi wa fujo hizo ofisini, na possibly ku-testify kwa mwajiri kuwa mhusika yeye ndiye alianzisha fujo Kanisani, na si vinginevyo
Hivyo basi, kwa kuangalia matukio haya yote, na assuming kwamba uchambuzi wa matukio haya uko sahihi, ni dhahiri kwa asilimia mia moja (100%) au hata zaidi, kwamba TUKIO LA MSIBA WA MDOGO WA MHUSIKA LILILOWAHI KUTOKEA HUKO MWANZA MNAMO JULY 2020, HALIKUWA LA BAHATI MBAYA, BALI LA KUPANGWA!

Ni tukio ambalo litakuwa lilikuwa planned kwa muda mrefu, na utekelezaji wake nao ukawa umepangwa kufanyika baada ya muda mrefu vile vile



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
MKUTANO UNAOHUSU MASLAHI YA MHUSIKA ULIOWAHI KUITISHWA NA MR X NA KUHUDHURIWA NA BAADHI YA WAFANYAKAZI WENZAKE NA MUHUSIKA IKIWA NI PAMOJA NA MUHUSIKA MWENYEWE, PAMOJA NA MTU MWINGINE MSTAAFU KUTOKA NJE YA TAASISI

Mkutano huu nao pia ulitoa indicator fulani kwamba malimbikizo ya mhusika yalikuwa tayari yapo mikononi mwa watu na si Serikalini
Kiongozi wake alikuwa ni huyo mstaafu kutoka nje ya taasisi hiyo. Huyu ndiye alikuwa ameletwa kwa gia ya kumsaidia mhusika kulipwa maslahi yake. Hata hivyo, mtu huyu hawezi kuwa alikuwa na nia njema kiasi hicho isipokuwa alikuwa ameletwa kwa ajili ya kuwasaidia majizi wa fedha za umma, namna ya kumtandika mhusika kisawsawa.

Tukio hili nalo pia linachangia katika nyongeza inayoendelea kutoa taswira kwamba malimbikizo ya mhusika tayari yalishatoka Serikalini siku nyingi, ila yako somesomewhere yanazagaa kwenye mikono ya wajanja
 
UPDATE: SATURDAY 9th JANUARY 2021

HALI YA AKAUNTI (STATUS) YA AKIBA YA MHUSIKA ILIYOKO BANK B (BB)


Amebaini kuwa matumizi ya Sim Banking pamoja na ATM card vyote vimekuwa blocked, yanaleta password error kwamba anakosea kuweka password

  • Hii ni mara ya sita au ya saba anakutana na tatizo lile lile, na linapokuwa limejitokeza, wanaolirekebisha ni wale wale, lakini bado linaendelea kujitokeza
  • Kila linapotokea na kuwaomba wahusika walirekebishe, huwa habadilishi password, huwa anendelea na password hiyo hiyo
  • Password hiyo amekuwa akiitumia miaka kadhaa nyuma, possibly tangu mwaka 2002 muda ambao ATM zilianza kutumika hapa nchinii kwa mara ya kwanza
  • Zaidi ni kuwa, namba yake ya kitambulisho cha NIDA ina digits ishirini na anaijua kichwani
  • Akaunti za benki pia huwa anashika kichwani kulingana na frequency ya namna ambavyo anakaa anaziandika mara kwa mara
  • Kwa hiyo ana kumbukumbu ambayo si mbaya kiasi hicho, na hivyo si rahisi hata kidogo kwake kukaa anakosea kosea password yenye digits nne tu wakati anaweza ku-acommodate kichwani digits hadi ishirini
  • Mara ya mwisho alipokuwa ameingia kwenye ATM password hiyo hiyo iligoma mara mbili
  • Hakutilia maanani sana siku hiyo kwa sababu alikuwa na haraka, na nia yake hasa ilikuwa ni kuchukua mini statement tu. Aliahirisha akaamua kuondoka bila kuchukua statement hiyo
  • SIM banking nayo amejaribu ikagoma, na kuanzia hapa akajiongeza sasa na kujua kuwa hata ATM nayo haikuwa kosa wala bahati mbaya
Kwa hiyo kinacofanywa na BB kwa mteja huu ni usanii kwa sababu hali hii kwa swala SIM Banking imekuwa hivyo tangu afungue akaunti nao mnamo August 2018. Haupo uwezekano wa mteja huyu kusahau password moja kwa mara zote hizo

Vile vile, inaonyesha kama Benki A wali-transfer restrictions zao kwa ushauri (walizokuwa wanazi-impose kwa mteja huyu), kwenda Bank B kwa sababu walijua kuwa kuna possibility hiyo siku moja kwamba mteja wao anaweza akafunga akaunti zake na BA na kuhamia BB moja kwa moja. Uwezekano huu waliu-foresee na hivyo wakashauri mtindo waliokuwa wao wanautumia kwa mteja huyu, utumike pia hata kule BB. Kwa hiyo inaonekana dhahiri kuwa kawaida sana kwake kwamba katika kila benki anayokuwa amefungua akaunti nao, akaunti zake mara zote zinakuwa na restrictions za yeye kutumia electronic banking

elly obedy

MUBARIKWE TENA NA BWANA
 
UPDATE-2: SATURDAY 9th JANUARY 2021

KUHUSU KIONGOZI MKUU (KM) KANISA A


  • Huyu ndiye aliwahi kuitisha mkutano wa dharura wa wanaume wote wa Kanisa A siku ya J2 ya tarehe 26/04/2020
  • Kikao hiki kilitarajiwa kuzaa jambo moja zito sana, ushahidi uliopo mpaka muda huu unazidi kuonyesha hivyo. Ilikuwa ni bahati mbaya tu kwake (KM) kwamba jambo hilo alilokuwa amelimekusudiwa, halikufanikiwa
Mathalani, ikitokea kwa bahati mbaya mtu akampa ushauri KM huyu tuseme kwa kumwambia TUKUKATE KICHWA HALAFU BAADA YA HAPO TUKUPE HELA, huyu mtu anaweza hata akafanya makosa akakubali. Cash is only, the only thing in his life

Huo mkutano hakuuitisha bure, alikuwa na hints za kwamba kama tukio lingefanikiwa, kulikuwa na hela nzuri mahali fulani (au “sadaka nzuri” kama ambavyo huwa anapenda kusema kanisani).

Mjane yule aliyetoa Sadaka halafu Yesu akasema kuwa alitoa kuzidi wote, kwake yeye KM mjane huyo hakutoa sadaka nzuri. Yeye akisema sadaka nzuri huwa anamaanisha ya kiwango kile kingine ambacho si kile alichotoa mjane aliyesifiwa na Yesu

Kwenye mkutano huo ulioitishwa na KM siku tajwa, Mr X atakuwa mmoja wa walio-coordinate maandalizi yake, na ndiyo maana baadaye alikuja kukaa karibu sana na mhusika. Alikuwa kazini akisaka hela, illegal cash



ANOTHER NOTABLE AND INTERESTING INCIDENCE


Kuna J2 moja siku moja hivi karibuni mhuiska alibahatika kumuona wa nail akiwa anatoka Kanisani, mmojawapo wa wafanyakazi wa BB Mama huyu alikuwa amehudhuria bada ya asubuhi hapo Kanisani A

  • Ilikuwa ni mara ya kwanza na ya mwisho kwa mhusika kumuona mama huyu kanisani hapo
  • Katika kipindi cha miaka yote ambacho mhusika amekuwa akiabudu mahali pale (tangu mwaka 2011), hakuwa amewahi kumuona mama huyo Kanisani hapo hata siku moja.
  • Huyu mama ndiyo yule aliyempa hivi karibuni mhusika risiti nyingine ya FDR (mwezi April 2020) ambayo ameshindwa kukaa nayo nyumbani kwake, ameipiga picha na kubaki na soft copy yake tu.
Baada ya hapo. siku moja mhusika akiwa BB, alibahatika tena kukutana na huyu mama na akajaribu kumuuliza kama naye pia ni muumini wa Kanisa A siku zote.

  • Mama huyu alikanusha akasema yeye huwa anaabudu Kimara kwa Mchungaji mwingine ambaye ni swahiba wa karinu sana na Kiongozi Mkuu wa Kanisa A
  • Alieleza zaidi kuwa siku alipoonekana Kanisani A, alikuwa ameamua kuabudu pale kwa sababu baada ya hapo alikuwa anatakiwa kuwa ofisini.
  • Kwa hiyo siku hiyo alikuwa yuko njiani kuelekea kazini na hivyo aliona ni zaidi convenient kwake kuabudu mahali pale siku ile badala ya kule ambako huwa anaabudu siku zote
  • Hata hivyo mhusika hana uhakika sana kama mama huyu anaweza akawa hata ameabudu kwa safari zinazoweza kuzidi idadi ya mbili kwa mwaka uliopita wa 2020
  • Ni kwa sababu inaonekana kama convenience ya mama huyu kuabdu mahali pale akiwa yuko njiani kuelekea ofisini ipo kwenye baadhi tu ya siku ambazo zinaweza kuwa ni chache sana
  • Vinginevyo mhusika angekuwa amemuona tena kwa sababu ni siku zenye idadi ya kutosha zimepita tangu alipomuona kwa mara ya kwanza
  • Kwa hiyo, tangu siku hiyo mhusika alipomuona mama huyu Kanisani A, hajawahi tena kumuona mahali pale hadi leo
  • Ilikuwa ni mara ya kwanza lakini pia ya mwisho pia kwa mhusika kumuona mama huyu mahali pale.
  • Ilikuwa ni mwaka jana, miezi kadhaa baada ya mkutano ule wa wanaume wa tarehe 26 April 2020 kuwa umepita


MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
MAREKEBISHO MUHIMU!

Wakati mhusika anaamua kuacha kuyafuatilia maslahi yake. Baada ya kuwa amezungushwa sana, ilikuwa ni April 2019 na si April 2018 kama alivyosema hapo awali.

  • Ni katika kipindi hiki ambacho mdiyo aliwahi kuingia ofisini kwa Mkuu wa Taasisi akifuatilia appointment ya kuonana naye halafu Katibu Muhtasi wake akaanza kumpigia simu bosi huyo huku akiwa anatetema kwa kwikwi za kutaka kupasuka kilio
  • Mpaka muda huu, ulikuwa unakaribia takriban mwaka mmoja tangu mhusika ahamishe fedha zake kutoka Benki A na kuzipeleka Benki B, mnamo August 2018 baada ya Benki A kuwa wameshusha riba ya akaunti ya mhusika
 
NYONGEZA YINGINE NMUHIMU KUHUSIANA NA AKAUNTI YA AKIBA YA MHUSIKA ILIYOPO BANK B

Mwezi December 2020 alifika Benki B (BB) kwa ajili ya kuchukua pesa

  • Zilikuwa ni kiasi ambacho asingeweza kuchukua kupitia kwenye ATM kwa sababu miamala yake ingekuwa mingi kiasi
  • Kwa hiyo aliingia ndani ili akachukue kupitia dirishani
  • Baadaye ilionekana kuwa mtandao uko chini, unaleta matatizo, hivyo ilibidi kuusubiria kwa dakika kadhaa na hatimaye ulirudi
  • Kipindi akiwa bado anasubiria subiria mtandao uliokuwa ukigoma goma, na akiwa mbele kabisa ya Benki teller wa dirisha alilokuwa amepanga foleni kwa ajili ya kuchukua pesa, teller huyo alimuuliza mhusika kama ana ATM card
  • Mhusika alipokubali kuwa anayo (japo hakuwa ameichukua siku hiyo, huwa hatembei nayo mara zote), Benki teller huyo alimshauri mhusika kama anaweza kwenda kuchukua pesa kwa kutumia card hiyo kwenye ATM machine badala ya kuendelea kusubiria mtandao uliokuwa haujulikani utarudi muda gani
  • Baada ya ushauri huo, mhusika alikosa logic ya ushauri huo kwa sababu kama mtandao ulikuwa upo down kwenye sytem zingine za benki hiyo, obvious hata kwenye ATM nako pia mtandao ulikuwa uko down
  • Hilo ndiyo lilikuwa jibu lake mhusika kwa Benki teller huyo
  • Zaidi alimweleza kuwa alihitaji pesa ambayo miamala ya laki nne nne ya kwenye ATM machine ingemletea usumbufu kwake, just in case angeamua kuufanyia kazi ushauri wa benki teller huyo
Kabla hajenda kwenye queu ya kuchukua pesa, alikuwa tayari ame-lodge kikaratasi cha kuomba balance pale customer service

  • Na kwa vile mtandao ulikuwa uko down, aliamua kuelekea kwenye foleni ya dirishani kwanza ili akaendelee kuusubiria akiwa hukoi
  • Baadaye ulirudi akachukua pesa dirsishani na hatimaye kuondoka kupitia customer service (CS)
  • Kule CS kwenyewe bahati mbaya mtandao ukawa bado uko chini, unasumbua kitu ambacho alikiona kuwa ni paradox
  • Mtandao hauwezi kurudi kwa sehemu, kwamba dirishani kwa teller unakuwepo, halafu CS unakuwa haupo, hii ni paradox
  • Ilibidi aondoke bila kuchukua balance yake siku hiyo
Zaidi ni kuwa siku hiyo, akina mama wale ambao huwa wanampa balance siku zote hakuwaona, inawezekana hawakuwepo. Akina mama hawa wako wawili au watatu, mmojawapo akiwa ni yule ambaye aliwahi kumuona Kanisa A, na ambaye aliwahi kutoa risiti ya FDR kwa mhusika mwezi April 2020, mhusika alipokuwa aki-renew akaunti yake hiyo. Akina mama hawa huwa hawafanyi kazi CS lakini huwa wanakuja pale kwa ajili yake, siku inapotokea ameonekana hapo benki

Hizi ni ishara muhimu alizokuwa ameziona tangu mwanzo lakini akawa anasubiria na matukio mengine mapya yajitokeze tena mbele ya safari ili aweze ku-pin together the evidence



FREQUENCY YA MATUKIO YA MTANDAO KUWA CHINI PINDI ANAPOKUWA YUPO BENKI B


Kwa mwaka uliopita wa 2020, amekumbwa na jumla ya matukio matatu (3) yanayohusu mtandao kuwa chini pindi anapokuwa yupo BB

  • Tukio la kwanza la mtandao kuwa chini lilimtokea siku ya tarehe 26/04/2020
  • Hii ni siku ambayo aliwahi kuondoka Kanisani baada ya kuwa amekwepa kikao cha wanaume wote kilichoitishwa na Kiongozi Mkuu
  • Siku hiyo alienda BB na alipofika alikuta tena mtandao uko chini, lakini hatimaye alifanikisha shida yake iliyokuwa imempeleka hapo
  • Tukio la pili lilimtokea mwisho wa mwezi ule ambao mbele yake shule zilifunguliwa baada ya ugonjwa wa Corona
  • Mwezi huo alifika mahali pale kwa ajili kuchukua hela ya matumizi ya shule baada ya kuwa zimefunguliwa tena
  • Tukio la tatu na la mwisho limemtokea mwezi jana kwenye tarehe za katikati
Tukio hili la mwisho ndiyo lile la siku ambayo aliweza kuchukua hela ila ikashindikana kupewa balance kwa sababu mtandao haukuwepo customer service, ulirudi ukawa upo dirishani tu ila si customer service

Vile vile, siku hiyo wahusika halisi ambao wameonekana kuwa wako authorized kumpa balance mhuiska nao pia hawakuwepo, hakuwaona. Kawaida huwa hawakosi kuonekana meneo ya customer service wakishamuona mteja wao huyo hapo BB



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
NYONGEZA NYINGINE MUHIMU KUHUSIANA NA NGAZI ZA MADARAJA ALIYOWAHI KUPATA MHUSIKA KWENYE VIPINDI VIWILI TOFAUTI VYA JULY 2006 NA JULY 2012

Madaraja haya yote yana sifa zifuatazo zinazofanana

  • Yote yalikuwa na “double impact” kwenye mshahara wake kwamba mwaka 2006, kulikuwa na mabadiliko mawili kwa wakati mmoja, kwenye ngazi/cheo cha mhusika
  • Mnamo July 2006, promotion iliambatana pamoja na kupandishwa kwa daraja kwa mhusika kutokana na kupata qualifications mpya za juu za masomo yake
  • Vile vile mnamo July 2012, promotion yake iliambatana na nyongeza ya mshahara mpya wa Serikali
  • Kwa hali hiyo mamlaka iliyokuwa inahusika na kumpandisha cheo, ilitakiwa imwandikie barua baada ya Julai mosi 2012, kipindi ambacho mshahara wake mpya tayari ungekuwa umeshajulikana
  • Mamlaka hizo hazikufanikiwa kuliona hilo na hivyo kupelekea kumpandisha cheo kwa ngazi ya juu huku zikimpa mshahara wa ngazi iliyokuwa nyuma yake, yaani ile iliyokuwa inafuata ngazi hiyo ya kupandishwa kwake, kwa chini yake
  • Madhara ya promotion hii ya mwaka 2012 ni kwamba angeendelea/ ataendelea kupata mshahara uliio pungufu mpaka siku anastaafu kwa sababu ngazi aliyopandishwa kwa mwaka 2012 ilikuwa ni ya mwisho ambayo haina promotion nyingine iliyo juu yake
Kwa hiyo matokeo ya michakato hii miwili, ule wa mwaka 2006 na mwingine ule wa mwaka 2012, michakato hii yote miwili kawaida ilitakiwa kuwa na double impact kwa mhusika lakini makosa yalifanyika na kupelekea michakato yote kuwa na single impact kwenye mshahara wake, na cheo /ngazi yake mhusika

Hii inamaanisha kuwa mwaka 2006 alipata nyongeza moja tu ya mshahara iliyotokana na promotion peke yake na alipoteza nyongeza aliyotakiwa kupata kutokana na kupata qualifications mpya za juu za masomo. Vile vile, mwaka 2012, alipata tena nyongeza moja tu ya mshahara iliyotokana na promotion peke yake, na akapoteza nyongeza nyingine iliyokuwa imetolewa na Serikali



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
KIKUNDI CHA KUSIFU NA KUABUDU CHA KANISA A KILICHOKUWA KINAIMBA VIZURI SANA:

Kipo lakini hakiimbi vizuri tena kama hapo awali

Ni kikundi ambacho linapokuja swala la uimbaji pamoja na upigaji wa vyombo vya muziki, KIILIKUWA kinaimba kwa ubora wa hali ya juu sana

  • Kama HAKIKUWA cha kwanza kwa uimbaji bora Tanzania , basi kitakuwa KIILIKUWA cha pili, hakiwezi kuvuka mamba hiyo
  • Na kama KIILIKUWA cha kwanza Tanzania, basi kinaweza kuwa hata KIILIKUWA cha kwanza Afrika
KIILIKUWA, sasa hivvi siyo tena. Kuna drums zimeongezeka kwenye mziki huo

Mhusika hapa inabidi aongee kwa kierfu sana kuhusu drums, akihusisha na experience aliyowahi kuipata alipokuwa yuko Kanisa B, kule uhamishoni alikowahi kwenda

Mziki wa ki-mbingu uliokuwepo Kanisa A umepotea haupo tena sababu ya drums. Hapa ameahidi itabidi aongee kwa kirefu sana kuhusu drums Kama alivyozifahamu tangu kipindi alipokuwa yuko Kanisa B



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: SUNDAY 10th JANUARY 2021

“KANISA B” “KANISA B” “KANISA B” “KANISA B”

BAADHI YA MAMBO KADHAA YA MUHIMU YALIYOJIRI KIPINDI MHUSIKA AKIWA UHAMISHONI KANISA B

UTANGULIZI


Msomaji wa siku zote wa taarifa jizi atakumbuka kuwa

  • Mnamo Juni 2014 mhusika alihama kutoka Kanisa A kwenda Kanisa B
  • Alichukua hatua hiyo baada ya mtandao uliokuwa Kanisa A kuwa umemubugudhi katika namna ambayo alishindwa kuendelea kukaa pale tena
  • Bugudha ilifikia kiwango ambacho alikuwa hawezi tena kukivumilia
  • Kwa hiyo aliamua kuhamia Kanisa B, ambako alikaa mpaka April 2017 kabla ya kuamua kurudi tena Kanisa A baada ya hapo
  • Sababu zilizomtoa uhamishoni Kanisa B ni zile zile sawa na zile zilizowahi kumpeleka huko akiwa anatokea Kanisa A
Kwa hiyo bugudha alizowahi kukumbana nazo pindi akiwa Kanisa B, kwa kiasi kikubwa zinashahibiana tu na zile zilizowahi kumtoa Kanisa A na kumpeleka huko, japo utofauti nao pia upo kwa kiasi fulani



MUUNDO WA UONGOZI WA KANISA B

Muundo wa Kanisa B upo sawa kabisa na ule wa Kanisa A isipokuwa:

  • Kiongozi Mkuu wa Kanisa B (KM-B) hana mamlaka makubwa kama alivyo Kiongozi wa Kanisa A (KM)
  • Yaani huyu wa Kanisa B kwa kiasi fulani huwa hana autonomy ile anayotakiwa kuwa nayo kama KM
  • Badala yake kuna kiongozi mwingine (iwapo bado yupo mpaka mda huu) ambaye yuko chini ya KM-B kwa mamlaka, lakini ambaye huwa anaonekana kuwa ana mamlaka zaidi kiutendaji Kanisani B kuliko hata KM-B mwenyewe
  • Mtu huyu alikuwa ana cheo cha Mzee Kiongozi (MZK-B)


WASIFU WA MZEE KIONGOZI (MZK-B) WA KANISA B KWA KIFUPI SANA

  • Ni mtumishi wa umma, na kwa kazi ambayo inafanana sana kama ya mtumishi wa Mungu kwenye nyumba ya Ibada
  • Mhusika yeye anaamini kuwa watu wanaofanya kazi za utabibu pamoja na zile za ulinzi na usalama, majukumu yao yanashahibiana sana kama yale ya watumishi wa Mungu kwenye nyumba za Ibada
  • Ni kwa sababu kazi zao ni za masaa 24 , kama siyo kila dakika, na zina uhusiano wa karibu sana na uhai wa binadamu
  • Kwa hiyo mhusika anaamini kuwa watu hawa ni wasaidizi wa Mungu wa karibu sana kwa kazi zao za kila siku


MAJUKUMU YA MK-B KAMA ALIVYOYAONA MHUSIKA

MZK-B huyu ndiye anayehusika na kutoa matangazo ya kila J2 Kanisani B ikiwa ni pamoja na kukaribisha wageni unless labda awe hayupo J2 husika . Kwenye swala hili la matangzo, ndipo hasa mhusika alipoanzia kubaini matatizo kadhaa kwa kioongozi huyu. Ukiangalia majukumu na umuhimu wa kazi yake aliyoajiriwa na umma halafu ukaongezea na kujtoa kwake mtu huyu kama mtumishi kwenye nyumba ya kiroho

  • Sababu hizi pekee zilikuwa zinatosha kabisa kwa mamlaka ya Kanisa B kumpa chochote, hata kama ingetokea akawa na kawaida ya kuonekana siku za Ibada ya J2 hadi J2 nyingine (yaani pasipo kuonekana siku zingine za katikatii ya wiki)
  • Hata hivyo, yeye mwenyewe ameamua kujipa mzigo huo ambao hakustahili kuubeba, mamlaka za Kanisa B zinaonekana kuwa si zile zilizompa mzigo huo wa nyongeza.
  • Ni yeye mwenyewe ameamua kuubeba kwa mapenzi yake mwenyewe
  • Sababu ya yeye kujibebesha mzigo wa aina hiyo, inaonekana kama pengine labda ni kutaka ku-justify ujira wake pale kanisani, ili ionekane kwamba kile anacholipwa (kama kipo) kinaendana na kazi anayofanya kanisani hapo
Hata hivyo, kama ilivyoelezwa hapo awali, mtu huyu anastahili kwa asilimia 100, kupata ujira kanisani hapo (kama upo) hata kama angekuwa na kawaida ya kuonekana Kanisani siku za J2 tu. Hii ni kutokana na ukweli kuwa majukumu ya umma aliyonayo ukiunganisha na moyo wake wa kukubali kutumika kwenye nyumba ya Ibada, tayari hivi vinampa sifa ya kupata ujira Kanisani hata kabla hajafanya kitu kingine cochote kile kanisani hapo

Tofauti na ilivyo kwa wazee wa makanisa wengine kama ambavyo mhusika anafahamu namna yalivyo majukumu yao, huyu MZK-B ndiye huwa:

  • anatoa matangazo ya kila J2
  • anakaribisha wageni kila J2
Wapo wazee wengine wa Kanisa chini yake lakini huwa hawawezi kutoa matangazo, unless yeye awe hayupo kanisani siku hiyo

  • Kwa hiyo anapokuwa yupo Kanisani, wazee wengine wote huwa hawana jukumu lolote la kusimama mbele ya madhabahu siku hiyo
  • Mambo yote huwa anafanya yeye, kitu ambcho siyo sahihi
Kawaida huyu yeye anatakiwa kuwa-coordibate wazee wengine walio chini yake ili wafanye kazi hizo hizo ambazo yeye huwa anafanya.

Hivyo basi kawaida yeye:

  • Hatakiwi kuwa anasimama madhabahuni kutoa matangzao kila J2
  • Anatakiwa kusimama madhabahuni kutoa matangazo maaalumu tu, na ambayo huwa yanatokea mara chache sana Kanisani
  • Matangazo anayotakiwa kutoa MZK-B ni kama yale ambayo KM-B anaweza akawa ana udhuru wa kuyatoa, hivyo yeye inabdi amsaidie huyo
  • Anatakiwa kuwasimamaia wazee wengine wafanye kazi hizo ambazo amekuwa akizifanya ikiwa ni pamoja na kukaribisha wageni Kanisani
  • Panapo nafasi, anatakiwa awakaribishe kwa staha na si kuwakashifu na kuwafokea


MZK-B HUWA ANAFUKUZA WAZIWAZI WAGENI KANISANI, YAANI KWA MAKUSUDI

Ukizingatia maelezo hayo hapo juu, kawaida MZK-B hatakiwi kuwa anasimama madhabahuni kila J2 kusoma matangazo, badala yake kazi hiyo inatkiwa ifanywe na wazee wa kanisa walioko chini yake

  • Kama ambavyo amekuwa akifanya, MZK-B akisimama kusoma matangazo, mojawapo ya matangazo hayo huwa ni lile linalohusiana na ukaribisho wa wageni waliofika kanisani hapo J2 hiyo
  • Kawaida huwa anasoma matangazo hayo kabla ya mahubiri kufanyika, na baada ya hapo ndiyo mahubiri huanza
  • Wakati akiwa anawakaribisha wageni, huwa anatoa wito wa wale wanaopenda kuokoka; kitu ambacho ni ujinga kwa sababu mtuhawezi kufika kanisani tu siku hiyo moja, hajahubiriwa chochote halafu akaamua kuokoka
  • Jukumu la waageni kukaribishwa kuokoka, kawaida na mara zote linatakiwa lifanywe na mhubiri wa siku hiyo, baada ya mahubiri kumalizika
  • Kwa hiyo mahubiri yanapomalizika J2 hiyo, kawaida huwa hakuna tena wito wa watu kuokoka kwa sababu wito huo unakuwa tayari ulishatolewa na MZK-B kabla ya mahubiri
  • MZK-B huwa anawalazimisha waokoke kipindi akiwa anatoa matangazo na huwa ana lugha chafu kwa wageni inapotokea wito huo umewachaganya
Baadhi ya wageni huwa anawaweka kwenye mkanganyiko kwa sababu

  • Pengine mtu anakuwa ni mgeni, na ni mara yake ya kwanza kabisa kufika Kanisani
  • Anakuwa ameamua kufika kanisani ili asikilize mahubiri kwanza halafu kule mwisho aweze kupima na kuona kama anaweza akaamua kuokoka
Tofauti na ambavyo mgeni alikuja kanisani akiwa amepanga, ghafla hukutana na ukaribisho wa yeye kuombwa kuokoka wakati hata kile kilichokuwa kimemleta, bado hajakipata. Hii huwa inapelekea baadhi ya wageni kushindwa kuelewa kile wanchoelezwa na MZK-B. Na inapotokea hivyo, MZK-B ni mkali kwa wageni nadhani zaidi ya alivyo mkali kwa watoto wake nyumbani. Utamsikia anasema kwa mfano

“we mama hivi wewe unaelewa Kiswahili……. ebu mlio karibu naye msaidieni huyo mama……, we mama unaelewa Kiswahili? Ungependa kuokoka?

  • Huyu mtu anafokewa hivi ni mgeni ambaye amefika kanisani kwa mara ya kwanza
  • Ni mgeni ambaye bado hajasikia hata fungu moja la maandiko matakatifu
  • Ni wakati wa matangazo tu na si wa mahubiri
  • Mahubiri yaliyomleta mgeni kanisani yanakuwa bado hayajafanyika
  • Jukumu la kutoa matangazo si la MZK-B bali la wazee walioko chini yake yeye MZK-B
  • Kukaribisha wageni ili waokoke kunatakiwa kufanywe na muhubiri wa Ibada ya siku hiyo (au kiongozi mwingine husika) BAADA YA MAHUBIRI NA SI WAKATI WA MATANGAZO KABLA YA MAHUBIRI
  • Lugha kali na yenye kuwakashifu na kuwadhalilisha wageni mbele ya waumini wote kanisani hapo, kama iliyotolewa mfano hapo juu amekuwa akiitumia mara kwa mara
Haihitaji mtu kuwa anajua kusoma na kuandika kuuweza kujua kuwa huyu mtu huwa ana mkakati wa kufukuza wageni kanisani. Badala ya Kanisa kuongezeka, huwa linaendelea kubaki vile vile, na wakati mwingine hata kupungua

Tuchukulie kwa mfano, mhusika mwenyewe alikaa Kanisani A anasikiliza mahubiri tu bila kuokoka kwa muda wa zaidi ya miezi mine. Leo mtu mzima una akili timamu, unasimama Kanisani kusoma matangazo tu halafu unalazimisha watu wageni waliofika kanisani kwa mara ya kwanza, waokoke wakati wa matangazo na si wakati wa mahubiri, na wakishindwa kukuelewa unaanza kuwafiokea na kuwakashifu mbele ya waumini, kanisa zima likiwa linashuhudia?

Kwa makusudi kabisa, huyu mtu huwa anafukuza wageni Kanisani



……………………………..itaendelea
 
UPDATE: MONDAY 11th JANUARY 2021

“KANISA B” “KANISA B” “KANISA B“KANISA B”

KUNDI LILOPELEKEA MHUSIKA KUHAMA TENA KUTOKA “KANISA B” NA KURUDI KANISA A:

KIONGOZI MKUU WA KANISA B (MK-B) HAKUHUSIKA NA UHAMAJI WA MUUMINI HUYO


Awali ya yote, mwandishi hajaenda mbali sanaa, ni kwamba mhusika wa habari hizi anapenda kuwajulisha wasomaji wa uzi huu kuwa kundi la Kanisa B lilochangia katika bugudha za kusababisha ahame tena kutoka Kanisa na kurudi tena kule alikokuwa ametoka, yaani Kanisa B,:

  • Liliongozwa na Mzee Kiongozi wa Kanisa B (MZK-B)
  • Kiongozi Mkuu wa Kanisa B (MK-B) hakuwa mmoja wapo wa watu waliokuwa kwenye kundi hilo, na hivyo basi, MK-B hakuhusika na swala la uhamaji huo
Hivyo basi MK-B, hakuwahi kuwa na mchango katika swala hili kwa sababu tafiti zake zote mhusika hatimaye zilikuja kumthibitishia pasipo shaka kuwa MK-B hakuwahi kuhusika kwenye bugudha hizi zilizopelekea ahame tena kutoka Kanisa B na kurudi Kanisa A. Tafiti hizi alikuwa anazifanya pindi alipokuwa bado yuko hapo Kanisa B na hata baada ya kuwa amehama. Hata baada ya kuhama, bado pia aliweza kuendelea na utafiti wake huo kwa sababu taarifa za kuendelea kuchakata zilizotokana na matukio yaliyowahi kujitokeza pindi akiwa hapo Kanisa B, bado alikuwa nazo.

Kwa hiyo basi:

  • Kiongozi pekee alliye na uhakika naye kwa kiasi kikubwa kabisa kuwa ndiye alihusika na kuhama kwake (mhusika) ni MZK-B na kundi lake. MZK-B anawajaua vizuri watu wake walioko kweye kundi lake hilo
  • Tofauti na ilivyo kwa mfano, kama kwa Kiongozi Mkuu wa Kanisa A (KM-A), kule aliko sasa hivi, ambaye yeye kazi yake kubwa sana kila siku mpaka muda huu, ni kupanga mipango ile tu ya kutaka kufanikisha kumbomoa mhusika, huyu mwingine wa Kanisa B (MZK-B) aliwahi kumpa mhusika ushirikiano wa kutosha na unaostahili kabisa kama mumini wake, na anaonekana anaheshimu sana watu
  • Kipindi mhusika anahama kutoka Kanisa B, hakuwahi kumuaga KM-B kwa sababu kipindi hicho alikuwa bado ana dhana kichwani kuwa pengine na yeye alikuwa anahusika katika baadhi ya matukio yaliyokuwa yakiendelea, na piavile vile alikuwa bado anaedelea kufanya utafiti wa kina, alikuwa hajakamilisha utafiti wake
  • Utafiti huu wa kina (wa mhusika) mpaka muda huu unaonyesha kuwa KM-B hakuwa na mchango hata chembe, isipokuwa kundi hilo lilikuwa lnafanya mambo katika namma ambayo lilikuwa linatamani na yeye aonekna kuwa alikuwa mmoja wake
  • MK-B kwa maana nyingine, alikuwa anachafuliwa na kundi hilo kwa mhuiska
Na possibly, kundi hili lilikuwa linafanya hivi baada ya kuwa halipati ushirikiano liliouhitaji, kutoka kwake KM-B huyo. Mhusika hatimaye alikuja kubaini haya baada ya kukutana na scenerios ambazo zililenga kumfanya yeye (mhusika) amuone mbaya KM-B, na zile ambazo alizing’amua kuwa zilitengenezwa na kundi ili kumfanya KM-B amuone mbaya mhusika

Kwa hiyo kazi nyingine kubwa iliyokuwa inafanywa na kundi hili la MZK-B ni kuwachonganisha mhusika na KM-B na kuna incidence kama moja hivi ambayo kundi hili liliwahi kufanikiwa kufanya hivyo

Ni kwamba kuna siku MZK-B aliwahi kukiuka makubaliano yake yeye na muumini wake, yaani mhusika

  • Ukiukwaji wa makubaliano hayo ndiyo ulikuja hatimaye kupelekea mhusika kudhani kuwa pengine hata MK-B naye pia alikuwa mmoja wao wale waliokuwa kwenye kundi la MZK-B, kumbe hapana
  • Yalikuwa ni makubaliano ya kawaida tu kati ya Mtumishi wa Mungu na muumini wake
Tukio la ukiukwaji wa makubaliano hayo atakuja kulitolea ufafanuzi wa kina, hapo baadaye

KWA HIYO ALIYEHUSIKA NA SWALA LA MHUSIKA KUHAMA TENA KUTOKA “KANISA B” NA KURUDI TENA “KANISA A”, NI MZK-B NA KUNDI LAKE AMBALO MK-B HAKUWAHI KUWA MIONGONI MWAO WALIOKUWA KWENYE KUNDI HILO



…………………………….inaendelea
 
ANGALIZO MUHIMU KUHUSIANA NA WASIFU WA MZK-B:

Mzee wa Kanisa wa Kanisa B (MZK-B) na Kiongozi Mkuu wa Kanisa A (MK-A) (makanisa mawili haya) wanafanana sana katika kila kitu, na wote huwa wanafanya operesheni zao kutokea madhabahuni, yaani wanachakachua madhabahu ya Bwana Kanisani. Ndiyo maana MZK-B alishalazimisha kutoa matangazo kila siku za Ibada ya J2 wakati siyo kazi yake. Ni kazi ya wazee walioko chini yake. Huyu amejipa jukumu hili ili kuhakikisha kuwa anapata nafasi ya kukanyaga madhabahuni kila Jumapili. MZK-B anafukuza waumini Kanisani pia, sawa tu na MK-A anavyofanya. MK-A yeye huwa anafukuza waumini kijanja, siyo kwa kuwafokea kwa maneno na ndiyo maana hapendi kabisa melody ya mziki mzuri zaidi isikike ndani ya nyumba hiyo ya Ibada, na wale ambao huwa wanapita mbele ya madhabahu kila J2 kwamba wameamua kuokoka, baadhi ya hao zaidi ya 90% huwa ni mamluki. Wale wanaopita mbele kila J2 wangekuwa ni watu ambao wamenuiwa kuwa waumini halisi mbele ya safari sasa hivi Kanisa hilo lingekuwa linajaa waumini hadi barabara ya Morogoro. Labda kwa ufafanuzi zaidi katika hili, mwandishi inabidi akatize kidogo maswala ya Kaniisa B halafu arudi Kanisa A na kuelezea incidence nyingine iliyojitokeza hapo jana tu siku yaJ2 tarehe 10/01/2021. Atarudi kidogo kuelezea incidence hii ya Kanisa A iliyotokea jana, halafu atendelea tena na maswala ya Kanisa B





…………………………….inaendelea
 
UPDATE-2: MONDAY 11TH JANUARY 2021

(TUNARUDI KIDOGO KULE KWA SIKU ZOTE, “KANISA A”)

TUKIO LILILOTOKEA JANA KANISA A, (LA TATU) NA LINALOSHAHIBIANA NA MENGINE MAWILI AMBAYO YAMEWAHI KUTOKEA NYUMA ILA KATIKA KIPINDI CHA HIVI KARIBUNI


Kuna J2 moja mara baada ya kumalizika kwa Ibada ya pili, kiongozi mmoja (mhusika wa manunuzi ya Sanitizer), alisimama madhabahuni kutoa tangazo muhimu lililohusiana na zone za waumini wote wa Kanisa A

  • Zone hizi huwa ni vikundi vidogovidogo vya waumini kwa ajili ya maombi na kujifunza neno la Mungu, na wanaoishi eneo moja au sehemu moja kama vile labda tuseme Riverside au Ubungo Kisiwani
  • Zone hizi huwa zinahusisha vikundi vya familia kuanzia takriban tano na kuendelea, na huwa zina ukubwa kulingana na idadi ya waumini ilivyo kwenye eneo husika wanaloishi
  • Waumini wakizidi idadi ya juu inayotakiwa kwenye vikundi hivi, zone hiyo husika hupelekea kuzaliwa kwa zone nyingine mpya; yaani zone hiyo hutakiwa kugawanywa mara mbili
J2 ya tangazo husika, kiongozi huyo alisimama madhabahuni na kuanza kusoma majina ya zone zilizopo Kanisa A na hatimaye kuwaomba washiriki wa kila zone husika kukusanyika sehemu moja kwenye eneo ambalo kiongozi huyo alielekeza, ila ndani ya uzio wa nyumba hiyo ya Ibada

  • Zone ya mhusika iliposomwa, wao walielekezwa wakutane upande wa kulia wa madhabahu, au kushoto kwake yeye aliyekuwa amesimama madhabahuni
  • Ili mtu aliyekaa ndani ya nyumba hiyo ya Ibada aweze kufika sehemu hiyo aliyoelekeza kiongozi huyu Zone ya mhusika wakutane, inabidi apite na kukanyaga sakafu ya mbele ya madhahabu, ambapo watu huwa wanasimama pindi wanapokuwa wameitwa kupita mbele ya madhabahu
  • Mhusika alinyanyuka kutokea pale alipokuwa amekaa na kuelekea kule ambako alikuwa ameelekezwa kukutana na wenzake, yaani kulia mwa madhabahu, akiipita na kuikanyaga sakafu iliyoko mbele ya madhabahu hiyo
Kabla ya tangazo hilo, awali siku hiyo mhusika alipokuwa amewasili Kanisani hapo akiwa anatokea nyumbani, alipitia kwanza kwenye banda au Kanisa la watoto, kabla hajaingia Kanisani ndani

Hilo likawa tukio la kwanza


Tukio la pili la iana hiyo lilitokea tena siku ambayo wanaume walitakiwa kukutana kwa dharura J2 moja, ili watoe sadaka ya elfu kumi (au chochote kile walichokuwa nacho hata chini ya hiyo pesa). Tukio hili ameshawahi kulitolea ufafanuzi wake wa kina ndani ya uzi huu

  • Sadaka hiyo walitakiwa kuitoa wanaume wote ndani ya mwaka 2020 kabla haujapita
  • Ni kwa sababu sadaka hiyo ilikuwa inaonekana kuchelewa na hivyo ndiyo maana tangazo la dharura lilikuwa ni muhimu
  • Ilikuwa ni mara baada ya Ibada ya kwanza
  • Mhusika alikuwa amehudhuria Ibada ya pili lakini wakati tangazo linatolewa, alikuwa tayari ameshafika Kanisani
  • Kikapu cha sadaka kiliwekwa mbele ya madhabahu siku hiyo na watu wakaanza kupita mbele wakitoa sadaka
  • Mhusika naye pia aliipita mbele ya madhabahu akikanyaga sakafu iliyoko mbele ya madhabahu na kwenda kutoa sadaka hiyo
Siku hiyo vile vile, alipowasili akiwa anatokea nyumbani, alipitia kwanza kwenye banda au Kanisa la watoto, kabla hajaingia ndani Kanisani, sawa sawa kabisa na kama alivyowahi kufanya kwenye tukio lile la kwanza ambalo amelielezea hapo juu

Hilo likawa sasa ni tukio la pili

Tukio la tatu na la mwisho limetokea jana JUMAPILI YA TAREHE 10/01/2021

MAELEZO YA TUKIO LENYEWE: ILIKUWAJE?


Mara baada ya Ibada ya pili kumalizika, kuna tangazo muhimu lilitolewa ambalo details zake mhusika asingependa kuziongelea humu. Na illi mtu aweze kutimiza matakwa ya tangazo hilo jana, ilikuwa inambdi apite mbele ya madhabahu halafu, apititlize hadi kulia kwa madhabahu, kule ambako Zone ya mhusika iliwahi kukutana kwenye lile tukio la kwanza ambalo ameshalielezea hapo juu. Wakati tangazo linatoka, lilielekeza pia kwa uwazi kabisa kuwa sehemu aliyokuwa yupo ndani ya nyumba hiyo ya Ibada mtu aliyehusiana na tangazo hilo, ni hiyo

Kwa hiyo jana pia mhusika alipita mbele ya madhabahu akikanyaga sakafu iliyoko mbele ya madhabahu hatimaye kwenda kuonana na mtu ambaye tangazo hilo lilikuwa na uhusiano naye

Jana pia vile vile, mhusika alikuwa mepitia kwenye banda au Kanisa la watoto, kabla hajaingia ndani Kanisani



MAZINGIRA MENGINE YALIYOJITOKEZA JANA J2 YA TAREHE 10/01/2021 YANAYOZIDI KUTOA IUSHAHIDI WA KILICHOELEZWA HAPO JUU


  • Mhubiri alikuwa ni kiongozi yule ambaye ameanza kubuni mtindo wa kuhubiri maandiko matakatifu, mafungu yaliyo mengi au yote anayotumia, yakiwa yanasomwa na mmojawapo au baadhi ya watu awanaokuwa wamekaa kwenye hadhira ya waumini
  • Katika kipindi chote ambacho mhusika amekuwa akimfahamu na kumuona mtumishi huyu akiwa amesimama madhabahuni, jJana ilikuwa mara ya pili kwa mtumishi huyu kuonekana akifundisha maandiko matakatifu kwa mtindo huu mpya
Wakati akiwa anahitimisha Ibada, mtuishi huyu alifanya mambo yafuatayo:

  • Aliitoa wito wa wageni waliohitaji kuokoka na walijitokeza (mmoja au waiwili) na kupita mbele ya madhabahu
  • Baadaye tena alitoa wito wa muumini mwingine yeyote yule mwenye hitaji lolote lile, kupita mbele ya madhabahu
  • Walijitokeza waumini wengi kiasi wakapita mbele
  • Mhusika yeye hakupita, japo mahitaji alikuwa nayo
  • Ni kutokana na ukweli kwamba ilikuwa ni surprise kubwa kwake, kiasi kwamba mwanzoni hakuwa ameamini kama masikio yake yalikuwa yamesikia sawasawa
  • Ni kwa sababu alikuwa hata hakumbuki ni lini mara ya mwisho aliwahi kuusikia wito wa namna hii ukitoka kinywani mwa mhubiri aliyesimama madhabahuni, kanisani hapo
Ni nadra muno kwa wito wa namna hii kutolewa Kanisani A siku hizi. Tangu mhusika alalamike kuhusiana na swala la wazinzi kuonekana walikuwa wame-dominate madhabahu kipindi kirefu nyuma, tangia pale staili ilibadilika na kuwa dominated na wito za wageni wanaotaka kuokoka, ambao ameshawaongelea huko nyuma kwamba takribani asilimia tisini (90%) huwa ni mamluki, na wahubiri ambao wamekuwa wakitoa wito hizo muda wote huo, nao pia wanajua hilo siku zote. Vinginevyo kwa muda huu, Kanisa A lingekuwa linajaa hadi kwenye barabara ya morogoro

Kwa hiyo kwa ufupi J2 ya jana walianza wakaitwa wageni waliotaka kuokoka, baadaye tena wakaitwa waumini wote kwa shida yoyote ile.

  • Baada ya waumini wote kuwa wameitwa hatimaye waliitwa watoto waliokuwa wanatarajia kuanza shule kesho yake, yaani leo
  • Hawa wao hawakujitokeza hata mmoja na ilionyesha wazi kabisa kuwa mpango wa kuwaita watoto hawa ulikuwa ni wa dharura. Yaani ni mpango uliobuniwa ndani ya siku hiyo
  • Ungekuwa umebuniwa kabla, watu wa aina hii wasingekosekana kwa sababu wangekuwa tayari wana taarifa in advance, lazima wangepatikana japo wachache
Baada ya miito yote hiyo kupita, hatimaye wakati wa matangazo ndiyo lilitoka tangazo ambalo liliwahusu baadhi ya waumini kuonana na mtu ambaye, kwa mtu yeyote yule mwenye akili timamu, ilikuwa ni muhimu kuonana naye, japo haikuwa lazima. Mtu huyo alikuwa amekaa upande wa kulia kwa madhahabu na katika sehemu ambayo ili mtu aweze kumfikia, lazima apitie madhabahu mbele



HITIMISHO

Wito wa pili uliotolewa kwa muumini mwenye hitaji lolote lile kupita mbele ya madhabahu wakati wa Ibada J2 hiyo, ulikuwa unam-qualify pia mhusika kufanya hivyo, ila hakufanya hivyo. Bado pia hapa anasisitiza kuwa hakumbuki ni lini mara ya mwisho, wito wa aina hiyo uliwahi kutolewa na mhubiri aliyesimama madhabahuni

Baada ya mhusika kuahirisha kupita mbele ya madhabahu kwa wito huu wa hitaji lolote lile, baadaye Ibada hiyo iilifika mwisho na hatimaye tangazo jingine tena ambalo nalo pia lilikuwa linam-qualify mhusika kupitia mbele madhabahuni, likatolewa.

Kwa hiyo, baada ya watu kutawanyika, mhusika alitembea akipita mbele ya madhabahu na baada ya hapo alipitiliza hadi upande ule wa kulia wa madhabahu ili kuonana na mtu husika na tangazo hilo.

Iwapo kama mhusika asingefanya hivyo, picha ambayo wangeipata watu walio wengi Kanisani hapo ni kwamba aidha ni kuwa mhusika tayari alishaonana na kuongea na mtu huyo kabla ya tangazo hilo, wakati kumbe hapana. Na kwa wale ambao walikuwa wanajua kuwa mhusika hakuwa amewahi kuonana na mtu huyo hadi kipindi tangazo hilo linatoka; kama wangemuona mhusika akiondoka bila kwenda kuonana na mtu huyo wakati tangazo alilisikia, basi watu hao wangeweza hata kudhani kuwa pengine mhusika ana tatizo fulani kichwani siku hizi ambalo bado hajaweza kuulifahamu



MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 

EBR. 6:4-6 SUV​

Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.
 
UPDATE: TUESDAY, 12th JANUARY 2021

UFAFANUZI WA NYONGEZA KUHUSIANA NA MAELEZO YA “KANISA A” YALIYOTOLEWA HAPO JUU


Ni kwamba baada ya mhusika kuwahi kulalamika huko nyuma kuhusiana na madhabahu ya Kanisa hilo kuwa domibated na wazinzi pekee

  • Badala ya kuendelea kuwa dominated na wazinzi hatimaye madhababhu hiyo ilianza kuwa dominated na watu wageni ila wanaopenda kuokoka
  • Hawa ndiyo wamekuwa wakiitwa kupita mbele ya madhabahu karibia kila J2
  • Hapo awali, Idadi ya watu hawa wakati mwingine ilikuwa inakuwa kubwa kidogo
  • Na kwa sababu wengi wao wamekuwa ni mamluki ambao wanakuwa wamealikwa rasmi kwa ajili ya jambo hilo tu na kwa makubaliano maalum, baadaye waalikaji hao walikuja kubaini kwamba iwapo wangeendelea na mtindo wao huo wa kualika idadi ambayo ni kubwa kidogo, siri yao waliyokuwa wameficha kwenye jambo hilo, ingeweza kuja kubainika baadaye
  • Ni kwa sababu baada ya kipindi kirefu, itaonekana kuwa wanaopita mbele kuokoka kila J2 ni wengi lakini idadi ya waumini kanisani inaendelea kuwa ni ile ile
  • Kwa hiyo ukabuniwa utaratibu mwingine wa kupunguza idadi ya waalikwa wao, kwamba angalau kila J2 awe anakuwa amealikwa mtu mmoja au wawili
  • Huo ndiyo utaratibu mpya ambao umekuwa ukitumika tangu kipindi kirefu nyuma mpaka sasa
Walio dominant kwenye madhabahu kwa sasa ni watu wanaopenda kuokoka, na huwa hawakosekani kila Jumapili miaka kadhaa sasa, na idadi yao ikiwa ni ya watu wachache

Hata hivyo, hii haimaanishi kuwa hapo kabla wageni waliopenda kuokoka hawakuwa dominant hapana. Ni kwamba walikuwa dominant isipokuwa na waumini wengine nao pia walikuwa dominant at the same time. Tofauti iliyopo sasa na wakati huo wa zamani ni kwamba kwa kipindi hiki, zinaweza zikapita wiki sita au hata saba mfululizo, kila J2 inapofika wanaoitwa kupita mbele ya madhabahu ni wageni wanaopenda kuokoka tu na si mtu mwingine yeyote yule nje ya hao

EBR. 6:4-6 SUV​

Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.


MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Mtu mwingine aliyewahi kujikuta yuko kati yao bila ya kuwa mmoja wao huyu hapa:

 
UPDATE: THURSDAY 14th JANUARY 2021

WASOMAJI WA UZI HUU ANAOMBA AWSHIRIKISHE JAMBO MOJA JINGINE LA NYONGEZA, NJE YA MADA ZINAZOENDELEA KWENYE UZI HUU:




Mhusika wa taarifa hizi anauliza swali akiwa anahitaji msaada kutoka kwa wasomaji kwamba: Je website hii aliyokuwa akiitumia kipindi kirefu nyuma kupata Salary Slips zake, ni kweli ilikuwa ya Serikali?

Website yenyewe ni hii hapa:


Ni website ambayo aliwahi kujisajili na hatimaye akawa ana-print salary slips zake kutoka kwenye site hiyo kuanzia March 2017

  • Ni baada ya taasisi anayofanyia kazi kuacha kutoa Salary Slips na kuwashauri watumishi wake wajisajili kwa ajili ya kupata salary slips hizo online, kutoka Serikalini moja kwa moja
  • Baada ya kuwa amejisajlili, Salary slip ya kwanza ailiyopata kutoka kwenye website hii ni ya March 2017
  • Aliendelea kupata Salary slip hizi hadi December 2018
  • Baada ya hapo, kuanzia February 2018 site ikawa inarudisha ujumbe kuwa iko kwenye matengenezo hadi leo
  • Salary slips alizowahi kupata anazo soft copies zke hadi leo, yaani za kuanzia march 2017 mpaka December 2018
  • Kuanzia pale hana tena Salary Slip yoyote hadi leo kwa sababu site hiyo inaonekana iko kwenye matengenezo muda wote
  • Ameshajaribu kujisajili kule kwingine Wizara ya Fedha, lakini anapata ujumbe kuwa Chek Namba, e-mail address pamoja na namba yake ya simu alivyotumia tayari vilishatumika na mtu au watu wengine
Attachment mbili zilizopo hapo chini zinaonyesha home page au login page ya website hiyo namna ilivyotokea alipojaribu kuitafuta jana tarehe 13/01/2021, lakini hakuweza ku-login, ilikuwa inaleta time-out error. Amejaribu tena leo tarehe 14/01/2021, imeanza tena kumletea ujumbe ule ule wa zamani ukisema

“MFUMO HUU KWA SASA UPO KWENYE MATENGENEZO SAMAHANI KWA USUMBUFU ULIOJITOKEZA. ASANTE”.

Huu ndiyo ujumbe ambao amekuwa aikiupokea tangu February 2018 na hana Salary Slips tena kuanzia pale hadi leo

Je, ni kweli kwamba hii site ilikuwa genuine na ni ya Serikali?
 

Attachments

BREAKING NEWS: FRIDAY 15 JANUARY 2021

SENIOR MSTAAFU WA KIUME ALIKUWA AMEPANGA KUFANYA KITU OFISIN MUDA HUU ASUBUHI HII YA LEO NA WAKATI HUU, ANA WATU WAKE
 
Back
Top Bottom