Edo kissy
JF-Expert Member
- Mar 21, 2022
- 2,802
- 7,551
Now anampenda kweli , kwa aliyopitia altona Judy ndo msaada.Hao wako pamoja ila Judy sio km anapendwa kaonewa huruma na saiv yupo juu ya mawe basi dalali hana chaguo, hampendi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Now anampenda kweli , kwa aliyopitia altona Judy ndo msaada.Hao wako pamoja ila Judy sio km anapendwa kaonewa huruma na saiv yupo juu ya mawe basi dalali hana chaguo, hampendi
Angempenda asingejutia vile alivyojishusha kuomba msamahaNow anampenda kweli , kwa aliyopitia altona Judy ndo msaada.
😂😂👐 tuwaachie wenyewe, watutunzia uncle wetu.Angempenda asingejutia vile alivyojishusha kuomba msamaha
Hongera mkuu,umetoaEPS 16
Baada ya Maisha kunipiga kweli kweli, nilifanya jitihada za kina sana kumtafuta Judy mwanzoni alikuwa hataki kabisa kusikia habari ya Kurudiana na wala hata kuonana tu.
Ila mtoto alikuwa anapiga video Call namuona, mtoto alishakua mkubwa kabisa ana miaka mitano
Nilimtafuta rafiki yake aende akaongee nae ila, nilimwambia anipe Muda niongee nae tu uso kwa uso naamini hata kama hataki turudiane angalau tunaweza kuzungumzia hatma ya mtoto na maisha mengine yaendelee.
Nilijua tu nikikaa nae kwa dakika thelathini tu lazima anielewe maana nilikuwa nimeshajipanga kisawa sawa
Rafiki yake alinirudishia majbu ya kunikatisha tama kweli kweli alisema hataki kabisa Kuongea na mimi kwa jambo lolote kama nina shida na mtoto ampe mtu amlete nimuone nikae nae nikichoka Nimrudishe.
Judy aliwahi kumwambia Huyo rafiki yake niwatafute wale Malaya zangu niendelee nao, na hali ninayoipitia anamuomba Mungu ikibidi hadi nitembee barabarani naongea mwenyewe kabisa.
Siku moja alinitumia sms akaniambia uko nyumbani nikamwmabia ndio leo sijatoka siku nzima, akaniambia hata Malaya zako hawajaja kukutembelea au walishavuna wanasubiri msimu tena msimu mwingine wa mavuno.
Alikuwa ananiumiza sana na muda huo sina kazi, sina hela nawaza hata kodi ikiisha nitalipa vipi.
Nilifikiria niuze kiwanja changu kimoja ambacho kilibaki nijipange kwenye biashara ila nikaona kwa maisha yalivyo sitaweza kununua tena kingine.
Baada ya jitihada nyingi sana kufeli niliamua sasa niende mimi mwenyewe kwa Judy nyumbani niaksema hata akinifukuza Poa ila siwezi kutulia kiboya japo aliniambia siku nikikanyaga kwake au kwneye biashara yake ataniitia mwizi au ataniaibisha sana.
Nilisema liwe liwalo nikaenda kibabe asee alivyoniona nilivyokuwa nimebadilika aliishia kunione Huruma maana hakuamini kama hali ilikuwa mbaya hivyo.
Nilienda sikutaka kupoteza muda wala nilimwambia moja kwa moja ila nilijikaza sana "Judy, naomba msamaha kwa moyo wangu wote kwa maumivu niliyokusababishia. Nimejutia sana na natamani kurekebisha mambo. Tafadhali nipe nafasi ya kuzungumza nawe.nahitaji muda wako mfupi tu unisikilize kisha utafanya maamuzi wewe mwenyewe”
Alinicheki bila kusema kitu kabisa nikarudia tena hayo maneno kwa hisia kali sana zile hisia za ndani kabisa.
Akaniambi haya sema hapa kwani unataka kusemaje nikusikilize nikamjibu
Asante sana kwa kujibu, Judy. Naendelea kukuomba msamaha tena kwa jinsi nilivyokukosea na jinsi hii imetuathiri sisi na mtoto . natamani zaidi tujadili hili pamoja, kwa nia ya kujenga upya na kuhakikisha tunaweka familia yetu mbele. Maana ni jambo sasa la kujenga makosa yameshatokea lakini Mungu ametupa nafasi tena tuongee haya mamb.
Nilijieleza kwa unyenyekevu sana na upole ule wa kumaanisha japo baadae nilikuja Kuona kama nimejidhalilisha sana kujieleza sana mbele ya mwanamke.
Nikamwmabia mimi ni hayo tu nimeona nikueleze naye nikampa muda ili aongee
Alinishangaa sana hakuamini kama ningeweza kujishusha hivyo.
Alianza kuongea alianza kunikumbusha matukio ya nyuma jinsi nilivyokuwa kiburi, dharau vile nilikuwa nafuja hela na watoto wazuri bar alifungua faili moja moja hadi mwisho akaanza kutoa machozi, namimi sikuwa mbali nikamsogelea nikaanza kumfuta machozi huku nambembeleza na vimaneno maneno vya Hapa na pale vitamu.
Akaniambia basi ondoka tu tutaongea kwenye simu, Tuliendelea kuongea kwa simu kama wiki hivi tukajikuta kama tumeshaanza kurudiana tena akanaimbia kama nataka turudiane akanipa mashart mawili.
Moja tukapime afya, na sharti la pili hatarudipale home hadi niende kwao na tumalize mambo ya Harusi.
Ilibidi nikubaliane nae maana yeye ndio aliyekuwa amebaki peke yake.
Tulikuja kurudiana japo hadi sasa hatuishi pamoja maana tunafanya mchakato wa kwenda kwao ila kama nilivyowahi kusema sehemu mimi home nilitoka nasitaki kuonana na ndugu zangu ndio kipengele japo nimepanga niende home nimeamua kuwasamhe ndugu zangu ili Turudishe umoja na masuala ya ndoa yafanyike. Siku nikienda homenitawaletea Mrejesho.
Kuhusu masuala ya kazi Mwezi wanne mwaka Huu nilipata kazi sehemu nipo hapo maisha yameanza tena kuleta mwanga, nashukuru mshahara nao sio haba.
Nimeona nishee haya machache kwenu Uandishi ndio unaniangusha. Sifa kuu ya watu wa IT kuandika hatujui wala kusimulia.
Ukamgonge baba Yako labda..Wewe sura nzuri tunakugonga tu kwa vijicent
😅😅napendaga wakiteseka mimi kenge hawaPa kupigika nimepapenda pangeendelea kwa miaka mingine 2 hivi, wanaume ni ...bwaa
Mimi peke yangu nakutosha mrembo.Ukamgonge baba Yako labda..
Msongo wa Mawazo, una roho ya chuki, akili ya kimasikini na hujitambui wewe. Kwani umelazimishwa kusoma?HUJUI KUSIMULIA
STORY YAKO HAINA MVUTO
UMEJARIBU KUITUNGA UIFANYE IPENDEZE IMESHINDIKANA. NI MBAYA.
WEWE NI CERTIFICATE HOLDER HUJUI HATA KUANDIKA. USILETE TENA UCHAFU KAMA HUU
Una msongo wa mawazo, una roho ya ukilaza, akili huna, hujielewi wewe. Kwani umelazimishwa kukoment?Msongo wa Mawazo, una roho ya chuki, akili ya kimasikini na hujitambui wewe. Kwani umelazimishwa kusoma?
Yani km huyu ilitakiwa msoto uendelee 😂😂😅😅napendaga wakiteseka mimi kenge hawa
Hongera San kwa kuwakilishaEPS 16
Baada ya Maisha kunipiga kweli kweli, nilifanya jitihada za kina sana kumtafuta Judy mwanzoni alikuwa hataki kabisa kusikia habari ya Kurudiana na wala hata kuonana tu.
Ila mtoto alikuwa anapiga video Call namuona, mtoto alishakua mkubwa kabisa ana miaka mitano
Nilimtafuta rafiki yake aende akaongee nae ila, nilimwambia anipe Muda niongee nae tu uso kwa uso naamini hata kama hataki turudiane angalau tunaweza kuzungumzia hatma ya mtoto na maisha mengine yaendelee.
Nilijua tu nikikaa nae kwa dakika thelathini tu lazima anielewe maana nilikuwa nimeshajipanga kisawa sawa
Rafiki yake alinirudishia majbu ya kunikatisha tama kweli kweli alisema hataki kabisa Kuongea na mimi kwa jambo lolote kama nina shida na mtoto ampe mtu amlete nimuone nikae nae nikichoka Nimrudishe.
Judy aliwahi kumwambia Huyo rafiki yake niwatafute wale Malaya zangu niendelee nao, na hali ninayoipitia anamuomba Mungu ikibidi hadi nitembee barabarani naongea mwenyewe kabisa.
Siku moja alinitumia sms akaniambia uko nyumbani nikamwmabia ndio leo sijatoka siku nzima, akaniambia hata Malaya zako hawajaja kukutembelea au walishavuna wanasubiri msimu tena msimu mwingine wa mavuno.
Alikuwa ananiumiza sana na muda huo sina kazi, sina hela nawaza hata kodi ikiisha nitalipa vipi.
Nilifikiria niuze kiwanja changu kimoja ambacho kilibaki nijipange kwenye biashara ila nikaona kwa maisha yalivyo sitaweza kununua tena kingine.
Baada ya jitihada nyingi sana kufeli niliamua sasa niende mimi mwenyewe kwa Judy nyumbani niaksema hata akinifukuza Poa ila siwezi kutulia kiboya japo aliniambia siku nikikanyaga kwake au kwneye biashara yake ataniitia mwizi au ataniaibisha sana.
Nilisema liwe liwalo nikaenda kibabe asee alivyoniona nilivyokuwa nimebadilika aliishia kunione Huruma maana hakuamini kama hali ilikuwa mbaya hivyo.
Nilienda sikutaka kupoteza muda wala nilimwambia moja kwa moja ila nilijikaza sana "Judy, naomba msamaha kwa moyo wangu wote kwa maumivu niliyokusababishia. Nimejutia sana na natamani kurekebisha mambo. Tafadhali nipe nafasi ya kuzungumza nawe.nahitaji muda wako mfupi tu unisikilize kisha utafanya maamuzi wewe mwenyewe”
Alinicheki bila kusema kitu kabisa nikarudia tena hayo maneno kwa hisia kali sana zile hisia za ndani kabisa.
Akaniambi haya sema hapa kwani unataka kusemaje nikusikilize nikamjibu
Asante sana kwa kujibu, Judy. Naendelea kukuomba msamaha tena kwa jinsi nilivyokukosea na jinsi hii imetuathiri sisi na mtoto . natamani zaidi tujadili hili pamoja, kwa nia ya kujenga upya na kuhakikisha tunaweka familia yetu mbele. Maana ni jambo sasa la kujenga makosa yameshatokea lakini Mungu ametupa nafasi tena tuongee haya mamb.
Nilijieleza kwa unyenyekevu sana na upole ule wa kumaanisha japo baadae nilikuja Kuona kama nimejidhalilisha sana kujieleza sana mbele ya mwanamke.
Nikamwmabia mimi ni hayo tu nimeona nikueleze naye nikampa muda ili aongee
Alinishangaa sana hakuamini kama ningeweza kujishusha hivyo.
Alianza kuongea alianza kunikumbusha matukio ya nyuma jinsi nilivyokuwa kiburi, dharau vile nilikuwa nafuja hela na watoto wazuri bar alifungua faili moja moja hadi mwisho akaanza kutoa machozi, namimi sikuwa mbali nikamsogelea nikaanza kumfuta machozi huku nambembeleza na vimaneno maneno vya Hapa na pale vitamu.
Akaniambia basi ondoka tu tutaongea kwenye simu, Tuliendelea kuongea kwa simu kama wiki hivi tukajikuta kama tumeshaanza kurudiana tena akanaimbia kama nataka turudiane akanipa mashart mawili.
Moja tukapime afya, na sharti la pili hatarudipale home hadi niende kwao na tumalize mambo ya Harusi.
Ilibidi nikubaliane nae maana yeye ndio aliyekuwa amebaki peke yake.
Tulikuja kurudiana japo hadi sasa hatuishi pamoja maana tunafanya mchakato wa kwenda kwao ila kama nilivyowahi kusema sehemu mimi home nilitoka nasitaki kuonana na ndugu zangu ndio kipengele japo nimepanga niende home nimeamua kuwasamhe ndugu zangu ili Turudishe umoja na masuala ya ndoa yafanyike. Siku nikienda homenitawaletea Mrejesho.
Kuhusu masuala ya kazi Mwezi wanne mwaka Huu nilipata kazi sehemu nipo hapo maisha yameanza tena kuleta mwanga, nashukuru mshahara nao sio haba.
Nimeona nishee haya machache kwenu Uandishi ndio unaniangusha. Sifa kuu ya watu wa IT kuandika hatujui wala kusimulia.
Nimekutana na huu uzi wako mwingine, hongera sana mkuu una visanga sanaEPS 14
N.B Udalali niliacha kuna sehemu nilipata ajira nafanya hapo tangu mwezi wanne mwaka Huu lakini hata hivyo nilikuwa nimeshaacha. Sasa hivi nafanya mara chache sana inapobidi. Nimeweka sawa ili kupunguza maswali.
Kama wewe ni mpangaji au ulishawahi Kununua nyumba kwa watu au kiwanja bila shaka ulishawahi Kukutana na kisa cha Ushirikina hasa Uchawi kwenye Shughuli zako.
Miongoni mwa visa nilivyokutana navyo katika pilikapilika pilika za Udalali ni kazi hii Kuhusishwa na vitendo vya Ushirikina.
Kabla sijaingia kwenye udalali nilikuwa nafikiri kwamba Wenye nyumba ni washirikina sana kumbe visa Vingine vinafanywa na baadhi ya madalali wasiokuwa na maadili.
Kuna visa vingi sana vya watu kufanya Ushirikina asee.
Kisa kimojawapo siku moja Tupo bar na dalali mmoja anaitwa Rama, wakati huo ndio nilikua Nimeshakaa sana kwenye udalali lakini tukawa tuna share Experience za kazi zetu.
Nlimwambia rama Ilivyo ngumu Kumshawishi mteja hadi akubaliane na kazi yako
Rama akaniambia tatizo lako wewe Ni wale wa “MUNGU NISAIDIE” kutoboa ni ngumu sana lazima utembee kidogo kwa wazee.
Aliniambia kwamba madalali wengi wana wa wini wateja kwa sababu ya ushirikina.
Alinisimulia namna ilivyo kwamba ili uweze kupata mteja na hata kumbadilisha akili aache chaguo lake na akubaliane na chagu lako sio kazi rahisi.
Hivyo kuna Bibi ambaye wanamtumia yupo Kihesa Iringa anatoa dawa ya mvuto ambayo ukiitumia ukimshawishi mteja hata nyumba ambayo ipo bondeni anakubali hata kama nyumba aliyokuwa anahitaji yenye sifa Fulani, unaweza kumbadilisha
Huyo bibi wa Kihesa anakupa dawa ambayo ni kama kimzizi ambacho unatakiwa kukiweka mfuko wa nyuma wa suruali yako kila siku unapoenda kwenye mishe mishe zako au kama una kiofisi kuna kidawa anakupa unakiweka kwenye droo unachanganya anhela nyingine zinaitahela tu na watu.
Sikutaka kumbishia maana lengo langu ilikuwa nimsikilize tu ila mimi huwa simaini hayo mambo japo yapo ila sitaki kuyategemea kabisa madhara yake ni makubwa mkuu wala usiyatamani.
Sasa akaniambia kwamba yeye anacho kizizi akiongea na mteja yeyote lazima atakubali tu hata kama alihitaji nyumba Ubungo atampanga atampa ya Kimara au mbezi na atakubali.
Lakini pia unaweza ukawa unahitaji nyumba au kiwanja na mtu akakupeleka abondeni kabisa, au jirani na dampo au sehemu yenye makelele kama bar au kule wanakouza K, unajikuta uekubaliana nae na kulipia ukishalipia ndio akili zinaanza kukufunguka kumbe dawa yenyewe ndio inakuvuta.
Siku ukimkuta mtu amepanga vingunguti machinjoni na ni mtu mwenye akili timamu au amepanga mabondeni mvua ikinyesha tu anaingia ankutoka akiwa anogelea usije kushangaa ujue ni ushirikina unafanya kazi nah ii ni kazi inayofanywa na madalali njaa.
Rama alinaimbia wengine wanachanjiwa dawa kwenye Uume, wanapeleka majina yao kwa waganga kisha wanafanya wanachojua wanakuchanjia dawa kwenye Uboo au shingoni., huyo akikushawishi huchomoki mzee.
Kisa kingine cha Ushirikina hiki nilisimuliwa na Dalali Tumwite Tall wa Tabata Segerea yeye aliniambia sasa hivi dalali mkuu una connection sana na mabosi mpumbaze mmoja uanze kuzifaidi Kodi usikubali kukaa kizembe.
Iko hivi kuna mzee mmoja wa malamba mawili Mwisho, Alikua ndio mtaalam wa hayo mambo ilikuwa ukimkabidhi funguo tu na hauishi hapo anafanya ushirikina wa kukupeperusha anakufanya unasahau kabisa nyumba yako utakumbuka lakini kila ukipanga kwenda unaahirisha, mzee alikuwa anpanga anakula kodi tu kila mwezi na mwenye nyumba hajui chochote kinachoendelea.
Huyu mzee alikuwa an nyumba yake Malamba mawili Alikuwa anaiuza kwa taarifa za watu wa karibu ni kwamba alishawahi kuiuza kwa watu kadhaa alafu wakishalipia anabaki nayo.
Sasa yeye alikuwa na dawa zake alikuwa akishakuuzia nyumba unafanya malipo na anakuambia umpe wiki moja ahamie kwenye nyumba yake nyingine ila ukishalipia hutarudi tena huko na wala hutakumbuka mzee anaendelea kula hela na nyumba anabaki nayo.
Inasemekana yeye watu walikuja kugundua siri kuna jamaa alitaka kununua nyumba hiyo majirani wakamtonya kuhusu hilo swala mnunuzi akasema sasa huu ndio utakuwa mwisho wake. Jamaa akanunua nyumba wakafuata michakato yote kisha akampa hela yake akaondoka mzee akasemaapew siku tatu ahamishe vitu. Usiku akatengeneza dawa zake kama kawaida akafanya ya kufanya, Kesho yake asubuh mnunuzi akarudi akammabia ulichofanya umeshashindwa hama leo leo na ndio ikawa mwisho wa ufalme wa Yule mzee baada ya kuumbuliwa, Kumbe jamaa alikuwa amejipanga sana kiroho alikuwa na kinga zake za kichawi uwezo ukazidiana.
Kwa ambao wanasema uchawi haupo nawashangaa sana, ndio maana tunaomba Mungu kila siku ili atuepushe na hayo mambo.
Tall akaa ananishauri na mimi niitumie hiyo dawa kupeperusha mabosi angalu na mimi nipate nyumba moja niwe nalia kivulini jasho la mtu hiyo siku nilicheka sana nikaona sasa hii kazi sio. Sikuwahi kujaribu kabisa hilo jambo japo alinipa shuhuda nyingi sana.
Kuna mama nyumba moja ilikuwa kibaha ni Apartment nzuri sana, lakini kila wapangaji walikuwa wakikaa pale miezi sita wanaondoka wengine hata hawamalizi hata hiyo sita wanaondoka.
Kuna Familia moja walipanga hapo ilikuwa ikifika kila siku usiku wanasikia watu wanacheka sebuleni wakichungulia ahwaoni mtu.
Kuna watu walikuwa wakilala kuna mapaka yanalia kweli kweli nje ya nyumba yanatoa sauti za ajabu sana, wakati mwingine wakitoka wakirudi wanaona kama matone ya damu mlangoni lakini walikuwa hawaelwi kabisa ni nini kinafanyika.
Mwanzoni walifikiri kwamba labda ni ugeni mawazo na woga ndio unawafanya wanasikia hivyo.
Na aliyekuwa akisikia mara nyingi ilikuwa ni mke wa jamaa sasa siku wamekaa sebuleni TV ikawa inajiwasha na kujizima alafu inatokea kama sauti ya vicheko hivi vya kukera.
Walikuwa wamekaa sebeleni wote woga uliwaingia sasa la mwanaume alikausha kwamba sio uchawi kuna hitilafu baadae kweli ikatulia na wakasahau.
Vile visa vikazidi sasasiku hadi siku nyumba akawa haikaliki kuna wakati walikuwa wanasikia pia kama watu wanarusha mawe kwneye mabati lakini wakauliza majirani wanasema wao hawakusikia.
Majini yakawa yanawavamia usiku yanawanyonga sana jamaa akaona visa vimezidi wakati mwingine wanalala kitandani wakiamka wanajikuta wamelala chini sebuleni tena wakiwa watupu.
Jamaa ilibidi aanze kutafuta ushauri kwa wadau wake wakamwambia atumie dawa za kienyeji mara maji ya upako lakini wapi mateso yakawa ni makubwa sana usiku ni heka heka hakuna kulala. Mwisho wa siku jamaa ikabidi ashauriane na mke wake ahame na stori zikasambaa mtaani mwneye nyumba ni mshirikina na ndani kwake kuna majini.
Ila mwenye nyumba alikuwa ansikia akafikiri majirani wanamzushia au hawampendi kwa hiyo mambo ya Kiswahili wanasambaza kwa watu ili nyumba yake wapangaji wasidumu.
Taarifa zilisambaa sana hivyo akaaamu na yeye kufanya tafiti zake za tiba huko kwa wataalam ndio wapiga Ramli wakamtaji jina la mtu Fulani hivi kumbe ndio alikuwa dalali wake anayemletea wateja.
Kwanini dalali alifanya vile, kwa sababu ile nyumba ilikuwa ni nzuri na watu wanavutiwa nayo na kodi yake ilikuwa sio ndogo na kila akileta mteja anpewa kamisheni yake.
Hivyo kuna madawa alikuwa amesindika huko ili wapangaji wasiwe wana dumu wahame apelike wengine apige hela tu kirahisi, maana unaambiwa kuna wapangaji wengine walikuwa Wanaka hata wiki tu na kodi wanasamehe wanasema wamepata mchongo mkoani wanahama kumbe wamekimbia mbilinge mbilinge za majini.
Baadae waganga walikuja kutoa hayo mazindiko na nyumba kwa sasa sijui ikoje il naamini iko vizuri.
Hivi ni visa ambavyo kwenye udalali nilikutana navyo, Wenye nyumba na wapangaji umakini unahitaji Kama una Sali Sali sana ombea eneo lako kabla ya kuhamia, Wakristo wanafanya maombi yao ya kuteka na kumiliki sijui maombi ya vita n.k ili uweze kuishi vizuri, washirikina wanaweka pia mamlaka zao.
Kwenye uuzaji wa viwanja dalali akifika kwenye uwanja wako ukimpa kazi lakini akigundua unataka kumzunguka au kumpa mtu mwingine unaweza kuuza hicho kiwanja hata laki na kisipate mteja hadi yeye aamue.
Unaweza kuuza kiwanja hicho kwa mwaka mzima kila mteja akija munakubaliana bei anakubali kulipa akiondoka hata simu hapokei tena.
Hiki ni kisa kingine tena kwenye udalali na ni matukio ya kweli sio ya kusadikika. Nitarudi kuhitimisha kesho muda kama huu.