Mkasa wa Kweli: Namna nilivyoshirikiana na baba kwenye shughuli za Kichawi

Mkasa wa Kweli: Namna nilivyoshirikiana na baba kwenye shughuli za Kichawi

DR SANTOS

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2019
Posts
12,846
Reaction score
28,106
Kwanza nianze Kwa kutoa disclaimer kisa hiki ni Cha kweli majina yaliyotumika hapa ni ya kweli bila kubadili chochote ilirekodiwa NAMI nikaihamisha kimaandishi kama ilivyo.

MWANZO
Kwa majina naitwa justice simangwa mkazi wa mkoa wa songwe katika wilaya ya mbozi kijiji cha msia, nilizaliwa katika familia ambayo naweza kusema ni masikini ijapokua tulikua na uhakika wa kupata chakula na kula milo mitatu kabisa.

Suala la kula halikua tatizo kwani kwa maisha ya kijijini ukikosa chakula basi wewe ni mzembe kupitiliza, yaani hata kula kwa jirani umeshindwa.
Kijumba cha nyasi cha vyumba vitatu ndicho kilichonikuza hadi kufikia umri wa miaka kumi na tano na hapo nilianza kujiona ni mkubwa kwani hata shuleni tulifundishwa kwamba unapoanza kubalehe basi ndio dalili ya kuuanza ukubwa.

“hivi utakua lini wewe”. Ni sauti ya baba akiongea kwa ukali na kunifanya nikasirike sana, kwani kila siku baba huniambia mimi ni mtoto ilhali nilijiona nimeshakua sasa
“kwani nimefanyeje baba?” nilihoji kwa mshangao kwani sikuona sababu ya baba kunikoromea kiasi kile na ukizingatia ndio nikwanza nilikua narudi kutoka shuleni.

“hivi ni mara ngapi nakukanya kuhusu kuongea na asia, Yule binti wa mzee mwashilindi?” aliongea baba na safari hii macho yake yalishaanza kuwa mekundu ma ishipa yake ilimtoka kuashiria amekasirika sana na hapendi mambo ninayoyafana.
Kwa vile, namtambua baba akiwa amekasirika, sikutaka kuendelea na majibizano zaidi nilikua mpole kama nimenyeshewa na mvua kisha nikachukua begi langu na kwenda chumbani moja kwa moja.

Ambapo nilifika na kulirusha kitandani na kisha nami nilifuata na haukupita muda tangu nilipouweka mgongo wangu juu ya kitanda usingizi ulinipitia, hii ni kutokana na kuchoka na umbali kati ya shule ya sekondari wasa na makazi yetu yalipo.

Nishituka baada ya kuhisi nimeguswa na kitu Fulani, na nilipofungua macho yangu tayari nilikutana na baba ambaye aliniamuru niamke haraka kwani kulikua na kazi ya kuhamisha vitu kutoka kwenye nyumba ya nyasi na kuvipeleka kwenye nyumba yetu mpya.

Sikua na namna na nilipoangalia nje kulikua kweusi lakini giza lilikua halijatanda kabisa, na kwa kukadiria ilikua ni saa moja usiku.

Nilijiuliza sana kwanini baba hakusiema tuhamishe vitu mchana mpaka aseme tuhamishe muda ule, maswali yangu hayakuweza kuishia moyoni tu na moja kwa moja niliamua kumuuliza baba swali hilo ambaye alinikata jicho kali hadi niliogopa.

Baba hakunijibu hilo swali wala mimi sikuhitaji tena jibu la swali lile kwani nilishatambua kuwa baba hapendi.

Baada ya kumaliza kazi hio ya kuhamisha vitu mama alipika chakula na kisha tulikula, name baada ya kula nilienda chumbani na kuchukua madaftari yangu kwa lengo la kujisomea , lakini nilishangazwa na uvivu niliokua nao siku hio, niliposhika daftari nilisinzia lakini nilipoliachia nilijiona nisie na uchovu wowote.
Niliamua kupuuzia hali hio na kuyarudisha madaftari yangu kwenye begi kisha kulivuta blanketi langu tayari kwa kulala tena na nilipanga ningeamka kusoma usiku wa manane kwani huo ndio muda akili inakua imetulia na kunakua hakuna vurugu.

Majira ya saa nane usiku nilistuka ghafla kutokana na bati za nyumba kupiga makelele sana kutokana na mvua kubwa iliyokua ikinyesha usiku huo.

Hakika mvua ile ilinishangaza sana, kwani ilikua ni majira ya kiangazi, sasa inakuaje mvua kubwa kiasi kile inyeshe majira ya kiangazi.

Nikiendelea kuwaza hayo nilishikia kishindo kikubwa maeneo ya sebleni, hakika kishindo hiki kilipelekea moyo wangu upasuke paa!
Kisha mapigo yangu ya moyo kuanza kudunda kwa kasi, kabla sijakaa sawa niliaza kusikia bati zikigonga gonga kana kwamba kuna vitu vilikua vikicheza.

Nilipata ujasiri kisha haraka niliinuka na kutoka kuelekea sebleni ambapo katika hali ya kustaajabisha niliona kibuyu cheusi chenye shanga zinazowaka kama taa na kukifanya king’ae.

Macho yangu yalinitoka pima na kisha kibuyu kile kikapotea, baada ya hapo kila kitu kilikoma, hata mvua iliyokua ikinyesha iliacha na kukawa swari kabisa.

Sikua na budi kurudi chumbani kwa hofu sana kwani nilichokiona yalikua ni maajabu kwa upande wangu na moyo wangu haukua na amani hata kidogo.
Nilifika na kuvuta shuka
langu na kujifunika gubi gubi nikiwa na hofu sana yote hii ni kuufanya usingizi uwahi kunichukua.

Baada ya kupitiwa na usingizi nilikuaja kuzinduka majira ya alfajiri kama ilivyokua kawaida yangu kuwahi kuamka kabla ya wote na kuandaa kifungua kinywa kabisa kisha kuwahi shuleni.

Na wiki hio ilikua ni ya mwalimu mkali kuliko wote pale shuleni.
Nilijinyoosha na kisha kutoka nje kwa lengo la kuwasha moto lakini nilishangaa sana baada ya kukuta nyumba yetu ya zamani ikiwa imeanguka, haraka niliingia ndani na kumgongea baba ambaye alitoka na kuangalia hali halisi lakini hakuonesha kustuka na chochote.

“tukiwaambia mnakua wabishi”.
Aliongea baba na kisha kuingia ndani akiniacha na maswali mengi sana

Je nini kilifuata
 
Kwanza nianze Kwa kutoa disclaimer kisa hiki ni Cha kweli majina yaliyotumika hapa ni ya kweli bila kubadili chochote ilirekodiwa NAMI nikaihamisha kimaandishi kama ilivyo.

MWANZO
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Kwa majina naitwa justice simangwa mkazi wa mkoa wa songwe katika wilaya ya mbozi kijiji cha msia, nilizaliwa katika familia ambayo naweza kusema ni masikini ijapokua tulikua na uhakika wa kupata chakula na kula milo mitatu kabisa.

Suala la kula halikua tatizo kwani kwa maisha ya kijijini ukikosa chakula basi wewe ni mzembe kupitiliza, yaani hata kula kwa jirani umeshindwa.
Kijumba cha nyasi cha vyumba vitatu ndicho kilichonikuza hadi kufikia umri wa miaka kumi na tano na hapo nilianza kujiona ni mkubwa kwani hata shuleni tulifundishwa kwamba unapoanza kubalehe basi ndio dalili ya kuuanza ukubwa.

“hivi utakua lini wewe”. Ni sauti ya baba akiongea kwa ukali na kunifanya nikasirike sana, kwani kila siku baba huniambia mimi ni mtoto ilhali nilijiona nimeshakua sasa
“kwani nimefanyeje baba?” nilihoji kwa mshangao kwani sikuona sababu ya baba kunikoromea kiasi kile na ukizingatia ndio nikwanza nilikua narudi kutoka shuleni.

“hivi ni mara ngapi nakukanya kuhusu kuongea na asia, Yule binti wa mzee mwashilindi?” aliongea baba na safari hii macho yake yalishaanza kuwa mekundu ma ishipa yake ilimtoka kuashiria amekasirika sana na hapendi mambo ninayoyafana.
Kwa vile, namtambua baba akiwa amekasirika, sikutaka kuendelea na majibizano zaidi nilikua mpole kama nimenyeshewa na mvua kisha nikachukua begi langu na kwenda chumbani moja kwa moja.

Ambapo nilifika na kulirusha kitandani na kisha nami nilifuata na haukupita muda tangu nilipouweka mgongo wangu juu ya kitanda usingizi ulinipitia, hii ni kutokana na kuchoka na umbali kati ya shule ya sekondari wasa na makazi yetu yalipo.

Nishituka baada ya kuhisi nimeguswa na kitu Fulani, na nilipofungua macho yangu tayari nilikutana na baba ambaye aliniamuru niamke haraka kwani kulikua na kazi ya kuhamisha vitu kutoka kwenye nyumba ya nyasi na kuvipeleka kwenye nyumba yetu mpya.

Sikua na namna na nilipoangalia nje kulikua kweusi lakini giza lilikua halijatanda kabisa, na kwa kukadiria ilikua ni saa moja usiku.

Nilijiuliza sana kwanini baba hakusiema tuhamishe vitu mchana mpaka aseme tuhamishe muda ule, maswali yangu hayakuweza kuishia moyoni tu na moja kwa moja niliamua kumuuliza baba swali hilo ambaye alinikata jicho kali hadi niliogopa.

Baba hakunijibu hilo swali wala mimi sikuhitaji tena jibu la swali lile kwani nilishatambua kuwa baba hapendi.

Baada ya kumaliza kazi hio ya kuhamisha vitu mama alipika chakula na kisha tulikula, name baada ya kula nilienda chumbani na kuchukua madaftari yangu kwa lengo la kujisomea , lakini nilishangazwa na uvivu niliokua nao siku hio, niliposhika daftari nilisinzia lakini nilipoliachia nilijiona nisie na uchovu wowote.
Niliamua kupuuzia hali hio na kuyarudisha madaftari yangu kwenye begi kisha kulivuta blanketi langu tayari kwa kulala tena na nilipanga ningeamka kusoma usiku wa manane kwani huo ndio muda akili inakua imetulia na kunakua hakuna vurugu.

Majira ya saa nane usiku nilistuka ghafla kutokana na bati za nyumba kupiga makelele sana kutokana na mvua kubwa iliyokua ikinyesha usiku huo.

Hakika mvua ile ilinishangaza sana, kwani ilikua ni majira ya kiangazi, sasa inakuaje mvua kubwa kiasi kile inyeshe majira ya kiangazi.

Nikiendelea kuwaza hayo nilishikia kishindo kikubwa maeneo ya sebleni, hakika kishindo hiki kilipelekea moyo wangu upasuke paa!
Kisha mapigo yangu ya moyo kuanza kudunda kwa kasi, kabla sijakaa sawa niliaza kusikia bati zikigonga gonga kana kwamba kuna vitu vilikua vikicheza.

Nilipata ujasiri kisha haraka niliinuka na kutoka kuelekea sebleni ambapo katika hali ya kustaajabisha niliona kibuyu cheusi chenye shanga zinazowaka kama taa na kukifanya king’ae.

Macho yangu yalinitoka pima na kisha kibuyu kile kikapotea, baada ya hapo kila kitu kilikoma, hata mvua iliyokua ikinyesha iliacha na kukawa swari kabisa.

Sikua na budi kurudi chumbani kwa hofu sana kwani nilichokiona yalikua ni maajabu kwa upande wangu na moyo wangu haukua na amani hata kidogo.
Nilifika na kuvuta shuka
langu na kujifunika gubi gubi nikiwa na hofu sana yote hii ni kuufanya usingizi uwahi kunichukua.

Baada ya kupitiwa na usingizi nilikuaja kuzinduka majira ya alfajiri kama ilivyokua kawaida yangu kuwahi kuamka kabla ya wote na kuandaa kifungua kinywa kabisa kisha kuwahi shuleni.

Na wiki hio ilikua ni ya mwalimu mkali kuliko wote pale shuleni.
Nilijinyoosha na kisha kutoka nje kwa lengo la kuwasha moto lakini nilishangaa sana baada ya kukuta nyumba yetu ya zamani ikiwa imeanguka, haraka niliingia ndani na kumgongea baba ambaye alitoka na kuangalia hali halisi lakini hakuonesha kustuka na chochote.

“tukiwaambia mnakua wabishi”.
Aliongea baba na kisha kuingia ndani akiniacha na maswali mengi sana

Je nini kilifuata
Leta chap chap sio tukae tunasubili muda mrefu.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
SEHEMU YA PILI

INAENDELEA: maneno ya baba nilishayazoea na hata alivoongea nilijua huenda ni hasira tu ya nyumba kuanguka. Na alipomaliza kuongea maneno hayo alirudi ndani, nami kwakua jiko nalo lilikua limeanguka basi sikua na namna ya kufanya zaidi nilioga maji ya baridi na kwakua nilikua na akiba ya pesa niliibeba ili nikaitumie shuleni kwa masuala ya chakula endapo njaa ikiniuma.

Majira ya saa kumi na mbili nilianza safari ya kwenda shuleni na njiani nilikutana na wanafunzi wenzangu waliokua na baisikeli ambapo mmoja alinipa lifti kwani alikua ni rafiki yangu, na lengo lilikua ni kuwahi kufika shule ili tuepukane na adhabu ya mwalimu chimota, ambaye alikua akiogopeka kwa bakora zake.

“pole rafiki, naona nyumba yenu imeanguka, mmepona”. Aliongea rafiki yangu thabiti tukiwa tumepakizana kwenye baisikeli yake
“dah asante sana rafiki yaani hata sielewi, maana mvua kubwa imenyesha usiku wa kuamkia leo, hadi kupelekea nyumba yetu ya zamani kuanguka”.

Niliongea maneno ambayo yalimshangaza sana thabiti, kwanza alishangaa kusikia kwamba mvua imenyesha usiku wa kuamkia siku ya leo.
“mmmh, huku ni noma ndugu, maana mimi nimeamka saa nane usiku niliua nasoma sasa hio mvua wewe umeisikia saa ngapi”. Alihoji thabiti na kunifanya nimsimulie kila nilichokisikia usiku lakini ajabu nilipotaka kuongea juu ya kibuyu cheusi, nilimuona asia pembeni yangu akinikata jicho kali kisha kuweka ishara ya kidole mdomomoni akimaanisha nisiseme chochote.

Hakika nilistuka sana na mstuko huo uliambatana na kigugumizi ambayo kilimfaya thabiti ashangae pia kwani sikua na kigugumizi kabisa.

“vipi chalii, mbona huendelei kuongea?” alihoji thabiti ana wakati huo tulishafika shuleni.
Sauti ya mwalimu chimota ndiyo iliyonistua ikituamuru tusimame kwani wote tulikua tumechelewa, hapo nilishuka kwenye baisikeli kisha thabiti akaenda kuiegesha mahali ulipokua mti wa kivuli kisha tukajikusanya na kukamilisha idadi ya wanafunzi ishirini kwa makaridirio.
Baada ya hapo niliweza kumuona asia nae akisogea kwenye kundi hilo na kuzidi kuongeza idadi.

Nilipomuona asia moyo wangu ulistuka sana na kufanya kumbukumbu ya tukio lililotokea muda mfupi wakati nazungumza na thabiti linirudie akilini, na kunifanya ghafla nipate hofu ambayo ilinifanya kijasho chembamba kinitoke.
“ina maana na huyu amechelewa, hivi asia ana nini huyu? Mbona najikuta nampenda sana tena ghafla”.
Nilijiongelesha mwenyewe maswali ambayo hayakua na mtu wa kunijibu hivyo yaliishia hewani tu.

Kisha macho yangu yalimwangalia asia ambaye nae aligeuka na kufanya macho yetu yagongane, lakini niliona kitu cha tofauti sana kwenye macho ya asia ambapo almanusura nizimie.

Nikiwa katika hali ya sintofahamu mwalimu chimota alituamuru tuanze kupita mmoja mmoja na kupigwa bakora kama adhabu ya kuchelewa.
Alianza thabiti ambapo alifika na kuinama au kama ilivozoeleka kupinda saba
Mwalimu chimota aliinua fimbo yake lakini kabla haijatua kwenye makalio ya thabiti, shati la mwalimu chimota lilichanika kwenye kwapa na zipu ya suruali ikakafuata kufunguka.

Vicheko vya wanafunzi ndivyo vilivyomstua sana mwalimu chimota kwani hakuelewa ni kitu gani kimetokea, na alipokuja kugundua alighafirika sana, jasho lilianza kumtoka kisha mikono yake ilianza kutetemeka.

“ooo…ndo kkeni hapa haraka”. Aliongea chimota huku nae akiondoka na kwenda nyumbani, na hakurudi tena shuleni siku hio.

Hakika wanafunzi walicheka sana na ilikua burudani sana siku hio na hio ndiyo ilikua stori ya siku kwa kila mwanafunzi ukizingatia hakuna mwanafunzi aliyempenda mwalimu chimota.

Baada ya kufanya shuguli za usafi kila mwanafunzi aliruhusiwa kwenda darasani lakini baada ya muda tulitole

wa kwa kengele ambayo iligongwa na kuashiria wote tukutane , mbele ya ofisi ya mkuu wa shule.

Mkuu wa shule alianza kuguna kama ishara ya kuweka koo lake sawa kisha akaanza kuongea.

“poleni kwa usumbufu, pia poleni kwa nitakachowaambia sasa”. Aliongea mkuu kisha akapumzika na kuendelea kuongea.
“mwalimu wenu chimota amepatwa na ukichaa wa ghafla, na hivi sasa amekimbilia kusikojulikana, yatupasa kumuombea sana pia hali hii inahusishwa na nguvu za giza moja kwa moja”.
Alipoongea masuala ya nguvu za giza moyo wangu ulipasuka pa! kisha nikakumbuka yale niliyoyaona kwa asia hakika, niliogopa sana

“ina maana asia ni mchawi au? Na kile kibuyu je”.
Nilipokua nikiendelea kuwaza hayo ghafla nilimuona asia akiwa pembeni ya mkuu wa shule akicheka na kumzomea kwa kuweka mikono yake kichwani kisha kuichezesha kama popo na kutoa ulimi kisha kicheko kikali kilifuata name sikuweza kuvumilia nilizimia papo hapo.

Je nini kilifuata
 
SEHEMU YA PILI

INAENDELEA: maneno ya baba nilishayazoea na hata alivoongea nilijua huenda ni hasira tu ya nyumba kuanguka. Na alipomaliza kuongea maneno hayo alirudi ndani, nami kwakua jiko nalo lilikua limeanguka basi sikua na namna ya kufanya zaidi nilioga maji ya baridi na kwakua nilikua na akiba ya pesa niliibeba ili nikaitumie shuleni kwa masuala ya chakula endapo njaa ikiniuma.

Majira ya saa kumi na mbili nilianza safari ya kwenda shuleni na njiani nilikutana na wanafunzi wenzangu waliokua na baisikeli ambapo mmoja alinipa lifti kwani alikua ni rafiki yangu, na lengo lilikua ni kuwahi kufika shule ili tuepukane na adhabu ya mwalimu chimota, ambaye alikua akiogopeka kwa bakora zake.

“pole rafiki, naona nyumba yenu imeanguka, mmepona”. Aliongea rafiki yangu thabiti tukiwa tumepakizana kwenye baisikeli yake
“dah asante sana rafiki yaani hata sielewi, maana mvua kubwa imenyesha usiku wa kuamkia leo, hadi kupelekea nyumba yetu ya zamani kuanguka”.

Niliongea maneno ambayo yalimshangaza sana thabiti, kwanza alishangaa kusikia kwamba mvua imenyesha usiku wa kuamkia siku ya leo.
“mmmh, huku ni noma ndugu, maana mimi nimeamka saa nane usiku niliua nasoma sasa hio mvua wewe umeisikia saa ngapi”. Alihoji thabiti na kunifanya nimsimulie kila nilichokisikia usiku lakini ajabu nilipotaka kuongea juu ya kibuyu cheusi, nilimuona asia pembeni yangu akinikata jicho kali kisha kuweka ishara ya kidole mdomomoni akimaanisha nisiseme chochote.

Hakika nilistuka sana na mstuko huo uliambatana na kigugumizi ambayo kilimfaya thabiti ashangae pia kwani sikua na kigugumizi kabisa.

“vipi chalii, mbona huendelei kuongea?” alihoji thabiti ana wakati huo tulishafika shuleni.
Sauti ya mwalimu chimota ndiyo iliyonistua ikituamuru tusimame kwani wote tulikua tumechelewa, hapo nilishuka kwenye baisikeli kisha thabiti akaenda kuiegesha mahali ulipokua mti wa kivuli kisha tukajikusanya na kukamilisha idadi ya wanafunzi ishirini kwa makaridirio.
Baada ya hapo niliweza kumuona asia nae akisogea kwenye kundi hilo na kuzidi kuongeza idadi.

Nilipomuona asia moyo wangu ulistuka sana na kufanya kumbukumbu ya tukio lililotokea muda mfupi wakati nazungumza na thabiti linirudie akilini, na kunifanya ghafla nipate hofu ambayo ilinifanya kijasho chembamba kinitoke.
“ina maana na huyu amechelewa, hivi asia ana nini huyu? Mbona najikuta nampenda sana tena ghafla”.
Nilijiongelesha mwenyewe maswali ambayo hayakua na mtu wa kunijibu hivyo yaliishia hewani tu.

Kisha macho yangu yalimwangalia asia ambaye nae aligeuka na kufanya macho yetu yagongane, lakini niliona kitu cha tofauti sana kwenye macho ya asia ambapo almanusura nizimie.

Nikiwa katika hali ya sintofahamu mwalimu chimota alituamuru tuanze kupita mmoja mmoja na kupigwa bakora kama adhabu ya kuchelewa.
Alianza thabiti ambapo alifika na kuinama au kama ilivozoeleka kupinda saba
Mwalimu chimota aliinua fimbo yake lakini kabla haijatua kwenye makalio ya thabiti, shati la mwalimu chimota lilichanika kwenye kwapa na zipu ya suruali ikakafuata kufunguka.

Vicheko vya wanafunzi ndivyo vilivyomstua sana mwalimu chimota kwani hakuelewa ni kitu gani kimetokea, na alipokuja kugundua alighafirika sana, jasho lilianza kumtoka kisha mikono yake ilianza kutetemeka.

“ooo…ndo kkeni hapa haraka”. Aliongea chimota huku nae akiondoka na kwenda nyumbani, na hakurudi tena shuleni siku hio.

Hakika wanafunzi walicheka sana na ilikua burudani sana siku hio na hio ndiyo ilikua stori ya siku kwa kila mwanafunzi ukizingatia hakuna mwanafunzi aliyempenda mwalimu chimota.

Baada ya kufanya shuguli za usafi kila mwanafunzi aliruhusiwa kwenda darasani lakini baada ya muda tulitole

wa kwa kengele ambayo iligongwa na kuashiria wote tukutane , mbele ya ofisi ya mkuu wa shule.

Mkuu wa shule alianza kuguna kama ishara ya kuweka koo lake sawa kisha akaanza kuongea.

“poleni kwa usumbufu, pia poleni kwa nitakachowaambia sasa”. Aliongea mkuu kisha akapumzika na kuendelea kuongea.
“mwalimu wenu chimota amepatwa na ukichaa wa ghafla, na hivi sasa amekimbilia kusikojulikana, yatupasa kumuombea sana pia hali hii inahusishwa na nguvu za giza moja kwa moja”.
Alipoongea masuala ya nguvu za giza moyo wangu ulipasuka pa! kisha nikakumbuka yale niliyoyaona kwa asia hakika, niliogopa sana

“ina maana asia ni mchawi au? Na kile kibuyu je”.
Nilipokua nikiendelea kuwaza hayo ghafla nilimuona asia akiwa pembeni ya mkuu wa shule akicheka na kumzomea kwa kuweka mikono yake kichwani kisha kuichezesha kama popo na kutoa ulimi kisha kicheko kikali kilifuata name sikuweza kuvumilia nilizimia papo hapo.

Je nini kilifuata
Shusha episode za kutosha mkuu.huko songwe ni noma sana kwa ulozi.
 
@wew boya Chizi Maarifa njoo huku jamaa ako anakuita

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Nashukuru sana bob. Mimi nlivyo na ustaarabu nliofundishwa home.... Mtu akiniita boya, choko n.k huwa siumii nacheka tu. Yaani kama leo Umuite simba paka. Simba hawezi kasirika atacheka tu. Haya nimefika niambie wewe dr namugari sijui ni ID nyingine ya Umughaka... I dont know. Karibu Bob. Mimi nipo nimejaa tele... Niambie wewe mtaalamu, the big man, n.k na sifa zote nzuri.
 
Nashukuru sana bob. Mimi nlivyo na ustaarabu nliofundishwa home.... Mtu akiniita boya, choko n.k huwa siumii nacheka tu. Yaani kama leo Umuite simba paka. Simba hawezi kasirika atacheka tu. Haya nimefika niambie wewe dr namugari sijui ni ID nyingine ya Umughaka... I dont know. Karibu Bob. Mimi nipo nimejaa tele... Niambie wewe mtaalamu, the big man, n.k na sifa zote nzuri.
Duuh mkuu umekuja tena na huku.chonde chonde usituharibie na huku ndg yangu.
 
Nashukuru sana bob. Mimi nlivyo na ustaarabu nliofundishwa home.... Mtu akiniita boya, choko n.k huwa siumii nacheka tu. Yaani kama leo Umuite simba paka. Simba hawezi kasirika atacheka tu. Haya nimefika niambie wewe dr namugari sijui ni ID nyingine ya Umughaka... I dont know. Karibu Bob. Mimi nipo nimejaa tele... Niambie wewe mtaalamu, the big man, n.k na sifa zote nzuri.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]mnaelewana nyie
 
Back
Top Bottom