Mkasa wa Kweli: Namna nilivyoshirikiana na baba kwenye shughuli za Kichawi

😃😃😃Sasa ya nn kutishiahiana maisha
Wawili nimesha waadhibu akiwemo umugaka mwenyewe nimemshusha kabusha kadogo tu siku mbili tatu kamsumbue ili arudishe heshima. Alianza jisahau sana yule dogo. Sasa wanaonitishia maisha nimewaonya tu wasifikiri mi wa mchezo.
 
Mimi ni novel author. Kuhusu kisa ni Cha kweli haya mambo yapoe na yalishatokea
 
Wawili nimesha waadhibu akiwemo umugaka mwenyewe nimemshusha kabusha kadogo tu siku mbili tatu kamsumbue ili arudishe heshima. Alianza jisahau sana yule dogo. Sasa wanaonitishia maisha nimewaonya tu wasifikiri mi wa mchezo.
🤔🤔Ulimfanyia kama yule mfanyakazi wa kazini kwako😱😱
 
Haya mengine nisiseme sana maana mshasema tunatumia majini n.k ila dogo nimempokea mimi town na kumfundisha anakuja kuponda huku JF?ambako nlimuingiza mimi mwenyewe.
Kuna mengi yamejificha kwenye ule Uzi, ngoja tuone Hadi mwisho😃😃
 
SEHEMU YA NNE -04

SASA ENDELEA; baba aliniangalia usoni kabla ya kusema jambo lolote na wakati huo nilikua nimeegamia ukuta.
“hebu njoo hapa”. Aliniambia baba kama ishara ya kuwa nisogee mahali alipo name sikusita nilisogea.

“umeona haya maji? Angalia kwa makini, alafu utakachokiona litakua jiu lako”. Aliongea baba nami nilitii, na kisha kuyakaza macho yangu kwenye moja ya chungu kilichokua na maji ndani yake.
“mbona sioni kitu?” nilimhoji baba aliyekua amekaa pembeni yangu akinitazama ninachokifanya.

“angalia kwa makini, mbona mimi naona? Hautakiwi kuwa na mawazo mengine. Jitahidi kuweka akili yako yote kwenye tukio hili”. Baba alimaliza kunielekeza na kisha nilirudia kukitazama chungu kile kilichokua na maji.

Gafla zilitikea radi kwenye chungu kile na kisha nilianza kumuona asia akiwa anaongea na sauti ya ajabu ambayo ilimjibu pasipo mtu anayeongea kuonekana. Hakika nilishangaa sana kwani asia hakuonekana kuogopa chochote kile.

Asia alivaa nikabu nyeusi na vazi aina ya kaniki nyeusi pia na kumfanya awe na mwonekano wa kutisha na kuogofya pindi ukimtazama.

“unahitaji damu ya kujaza kibuyu hiki ili upate kuwa mchawi mwenye nguvu ya kufanya jambo loloote lile pasipo kuonekana na mwisho utapotea kabisa katika ulimwengu wa dunia hii”.
Mazungumzo hayo niliweza kuyapata vema kwani yalisikika barabara kwenye ngoma za masikio yangu, na kunifanya nichoke mwili hadi akili. Licha ya hayo yote nilifikiria sana kuhusu baba kwani mara nyingi amekua akiniambia kwamba yeye ni mtaalamu wa dawa za kienyeji, licha ya hivyo mara kadhaa tuliongozana porini kuchimba dawa ambapo alinielekeza mambo mengi sana kuhusu dawa za kienyeji a aliniambia angependa sana niwe mrithi wake ili niweze kuendesha mambo ya tiba za kienyeji pindi atakapokufa.

“vipi mbona umeduwaa?” alihoji baba baada ya kuona nimekaa muda mrefu bila kusema chochote
“hivi baba umewezaje kuyajua yote haya?” nilihoji swali ambapo baba hakunijibu zaidi ya kuanza kunisema tena kwamba mimi bado sijakua.

Na siku hio nilitaka kumdhihirishia baba kwamba nimekua na sitaki aendelee kunidharau tena
“nitamuua huyo asia kabla hajafanya jambo lolote”. Niliongea kwa ujariri
“huwezi kumuua pasipo kupata dawa ya ulinzi, na pia kama sio mchawi huwezi kumzuia asifanye anachokifanya”. Alingea baba huku akinitazama aone nitasema kitu gani name nilibaki kimya tu.

“sahizi kunywa hii kisha nenda kapumzike, usiku kuna mahali nitakupeleka ila tambua unahitaji kuwa na kifua kwani ni kazi hatari sana”. Aliongea baba akinisisitiza juu ya suala la kuwa msiri
Tulipomaliza mazungumzo nilitoka na kwenda moja kwa moja chumbani huku nikimuacha baba kwenye chumba kile, ambapo nilifika na kujilaza.

Mwalimu chimota alifika paredi akiwa hana wasi kabisa, huku kila mwanafunzi akimshangaa kwani alikua kama alivyozaliwa, alifika moja kwa moja na kusimama mbele ya wanafunzi na kisha kuanza kuongea mambo ambayo kila mmoja alionekana kuyashangaa na mwisho mwalimu chimota alionekana ni kama aliyechanganyikiwa.

“halafu hii tabia ya kurogana tutakuja kuonana wabaya jamani”. Aliongea kwa mikwara mwalimu chimota ambapo wanafunzi hawakuelewa kabisa ambacho mwalimu wao alikua anakizungumza.
Kisha alipomaliza kuyasema hayo maneno alienda kwa mkuu wa shule na kumnong’oneza jambo Fulani na kisha kuondoka.

Wazo alilokuanalo chimota kwa wakati huo ni kwenda kwa mtaalamu wa tiba asilia aliyekuwepo kitongoji jirani cha msia, alijiandaa haraka na kisha kuwasha gari lake kwa lengo la kuwahi kwa mganga.

Aliendesha gari kwa kasi sana chimota ambapo alitumia dakika kumi tu kufika msia,kisha alipaki gari maeneo ya zahanati na kuanza kutembea mita kadhaa hadi alipofika nyumbani kwa mganga.

“mwakata?” (habari ya saa hizi) aliongea chimota kwa lugha ya kinyiha
“mwakata huli?”. (ni nzuri, habari yako) alijibu mke wa mzee simangwa ambaye ndiye mganga
“hansi! Nimemkuta mtaalamu”. Alihoji chimota
“ndio, yupo ndani karibu!”. Aliongea bi zulfa mke halali wa simangwa kisha alimkaribisha ndani mwalimu chimota.

“mzee nimekuja, niko na shida sana na ninahisi kuna mwalimu mwenzangu ni mchawi ananiroga”. Aliongea chimota akimweleza mganga,

“sio mwalimu, ni mwanafunzi mchawi na msipokaa sawa walimu wote mtakufa kwani anachokitafuta ni nguvu ya kufanya mambo ya giza pasina kuonekana”.

Aliongea mzee simangwa kwa umakini wa hali ya juu kumfanya mzee chimota astuke sana na kutoa mguno ambao ulioonesha dhahiri amestuka.

“haaaaaaa!”.
“hapa nitakupa dawa lakini kuna kazi kubwa ambayo tutaifanya siku ya kesho majira ya usiku ili tuweze kuvunja mitego yake yote kwako, lakini nitahitaji jogoo mweupe na tetea mweusi kwa kazi hiyoo”.
Aliogea mganga.

“hilo sio tatizo mkuu”. Alijibu chimota kwa shauku, kwani alishachoshwa na mauzauza yaliyokua yanamtokea.
Baada ya mazungumzo hayo mganga alipekua vitu vyake na kutoa moja ya mzizi na kumkabidi chimota na kumwambia aupokee kwa mkono wa kushoto, nae alifanya hivyo.

“pindi utakapoweka mzizi huu kwenye mfuko wako wa kushoto, hakikisha hauogi wala kubadili suruali yako mpaka tutakapokutana tena”. Mganga alitoa maelekezo kisha mwalimu chimota aliacha kiasi cha pesa na kuahidi kutimiza masheriti yote kisha kutoka nje ya chumba kile.

Baada ya kuchoka kulala, nilitoka nje japo nipate kuotea jua la mchana, nje nilikuta gari ambalo nililifahamu kabisa na mara nyingi lilikua likiegeshwa nje ya nyumba ya mwalimu chimota.

Ni kama niliotea sahihi kwani haukupita muda mwalmu chimota alitoka nje na aliponiona alistuka sana, hata mimi pia nilishituka na kubaki na maswali moyoni.

Je nini kilifuata
 
Ndani ya nyumba. Jamaa wataku mind sana kwa nini umeniita.....😂
Kumbe wewe ni mpemba Ndiomana ulimvaaa Umughaka kweli lol! Kwani nawewe ni mutu ya shirki mkuu??? Au wapenda wote ni watu wa shirki???
Nimeuliza tu natanguliza samawani
 
SEHEMU YA TANO (05)

ENDELEA; “SHIKAMOO!” nilimsalimu mwalimu chimota naye alijibu bila wasi huku akiingia kwenye gari lake.
“marahaba dogo hujambo”. Alijibu
“sijambo tu mwalimu”.

Baada ya salamu mwalimu chimota aliondoa gari maeneo ya nyumbani na safari yake iliishia kwa mzee simfukwe aliyekua akisifika kwa ufugaji wa kuku kijijini pale.

Alifika na kukaribishwa mpaka ndani nae hakusita kuingia na kumuelekeza kuwa alikua na shida ya kuku, jogoo mweupe na tetea mweusi.

“wapo wengi tu unataka wangapi?” alihoji mzee simfukwe
“nataka kuku wawili tu, jogoo mweupe na tetea mweusi”. Aliongea mwalimu chimota
“kuku wameshatoka nje, naomba jioni uje wajukuu zangu watakukamatia”. Aliongea mzee simfukwe
Mzee wa makamo anaeendesha maisha yake kwa ufugaji wa kuku pamoja na kilimo.

Bada ya makubaliano hayo mwalimu chimota hakuweza kukaa tena nyumbani kwa mzee huyo zaidi aliacha pesa na kuwasha gari kisha kuondoka kwenda nyumbani kwake ambako ndiko shule ya wasa sekondari ilipo.

Alifika na kuwakuta wanafunzi wakiwa paredi, lakini kwa mbali aliweza kumuona kiumbe akiwa mrefu kuliko wanafunzi wote huku akipitiliza hata jengo la ofisi ya walimu.

Hakika walimu chimota alistuka sana na almanusura angonge ukuta wa darasa, mwalimu chimota alienda moja kwa moja nyumbani ambapo alifika na kukuta nyumba yake ikiwa chafu na yenye matakataka mengi nje.

Aliyapuuzia kwani alitambua huenda takataka zile zimeletwa na kimbunga ukizingatia yalikua ni majira ya kiangazi, alizipiga hatua zake kuelekea ulipo mlango wa kuingilia ndani, alipofika mlangoni alishangaa kukutana na ujumbe ulioandikwa kwenye karatasi nyeupe na ilionesha dhahiri iliandikwa kwa damu.

Hakika maneno yaliyoandikwa kwenye karatasi ile ilikua na maneno mazito ambapo hata ungelikua wewe ungetetemeka baada ya kuyasoma.
“maandishi haya nimeyaandika kwa damu yako mwenyewe, achana na jambo hili kabisa la sivyo nitakumaliza na hilii ni onyo la mwisho kabisa”.

Chimota alistuka sana mstuko alioupata hauwezi kulinganisha na kitu chochote kwani almanusura azimie, tumbo la kuhara lilimpata ghafla na alijikuta akitamani kwenda uwani kwaajili ya kujisaidia.

Haraka alichota maji kwenye bomba lililokua pembeni ya nyumba yake na moja kwa moja kwenda maliwatoni, alistuka sana pindi alipoingia maliwatoni baada ya kuona moshi mweusi wenye harufu kali ukitoka kwenye tundu la shimo la choo.

Moshi ule ni kama ulikua na sumu kwani mwalimu chimota alizimia na kuanguka chooni punde tu baada ya kuivuta hewa ile.

Chimota alizinduka na kujikuta akiwa chooni majira ya jioni, viungo vilimuuma sana pia harufu mbaya ya kinyesi ndiyo ilimchefua kwani kila mahala alipoenda nzi walimfuata.

Alipokumbuka masheriti aliyopewa ya kutokuoga alichoka sana, kwani aliwaza angewezaje kufika siku ya kesho pasina kuoga wala kubadili nguo?
Akili yake ilimtuma kuangalia dawa aliyoiweka mfukoni, na alipopapasa tu hakuiona, na hakuishia hapo bali aliingiza mkono mfukoni na alikuta ujumbe badala ya ile dawa.

“huwezi zima moto kwa moto zaidi utachochea moto uwake na ukolee zaidi, chimota ni lazima ufe”.
Moyo wa chimota ulipasuka paaaaah! Kwani alijiona kwamba tayari ameshakufa japo yapo alikua buheri wa afya.
Mikono yake ilitetemeka kwa wasiwasi, mdomo wake pia ulianza kutetemeka kama mtu anayesikia baridi kali sana.
Chimota hakutaka kulala tena nyumbani kwake na aliamua kupiga simu kwa mganga, ambapo simu iliita na kisha kupokelewa.

“kosa ulilolifanya ni kupita kwa yule mzee”. Aliongea mganga kabla hata ya salamu kisha kukata simu na kumuacha chimota akiwa kwenye hali ya sintofahamu .
………………………………………………………………………………………………………………………………………………....................
“karibu sana justice simangwa kwenye

ulimwengu huu jisikie uko nyumbani na haujapotea njia kabisa”.
Ilisikika sauti ya mzee mmoja wa makamo ambaye nilimfahamu kabisa na alikua wa pale pale mtaani
“baba yako amenieleza kila kitu kuhusu wewe, name nitakupa nguvu ya kuweza kuangamiza uchawi mweusi ambao unatufanya wachawi wote tuonekane wabaya”.
Aliongea mzee huyo wakati huo mimi nikiwa kimya kabisa, mazingira tuliyokuepo niliyafahamu kwamba ni ya uwanja wa shule ya wasa.

Niliona aibu sana na muda mwingi nilikua nikificha jogoo wangu kwani tulikua uchi wa mnyama lakini hakukua na mtu aliyeonekana kujali mambo ya mwenzake.

Baada ya kusema maneno hayo mzee Yule alichukua usinga wake na kuanza kuupepeza kisha ghafla kilitokea kibuyu chenye angi ya njano kilichonakshiwa na shanga nyeusi.

Mzee Yule alinisogelea mimi na kuniamuru nisimame name nilitii, kisha akaanza kuupepeza usinga wake kwenye paji langu la uso huku akiongea maneno ambayo sikuyaelewa kabisa.

Alipomaliza kuyasema maneno hayo, alinyoosha mkono wake juu na kisha kikatokea chungu cheusi ambacho ndani kilikua na damu kisha akaniamuru ninywe.
Hakika ulikua ni mtihani mgumu sana, kabla ya kufanya jambo lolote nilimtazama baba yangu ,ambaye alinipa ishara ya kwamba ninywe na nisimuangushe.

Nilipiga moyo konde na kuinywa damu iliyokua kwenye chungu kile ambapo baada ya kumaliza, shangwe zilisikika si kina mama wala kina baba wote walishangilia kwa nguvu na ngoma zilipigwa.

“hatimaye tumekamilisha zoezi la kumpokea mwanachama mpya katika chama chetu cha uchawi, tutajipongeza kwa kula nyama na mwisho kila mmoja ataenda kwake”.
Baaada ya kusema maneno hayo moto mkali uliwaka na kisha kina mama wawili waliokua ndani ya vazi la kaniki walisogea mbele wakiwa wamebeba miili miwili ambayo sikuelewa ni ya kina nani lakini ilionesha ni maiti mbili za kiume.

Kisha bila huruma walikata vipande vipande na kila mmoja alokua eneo lile alipanga foleni kwaajili ya kupata kipande cha nyama.

Mzee Yule mwenye ndevu nyingi na mvi nyeupe aliniamuru niwe wa kwanza kupata kipande cha nyama.

ambapo nilisogea pia baba alifuata na alikua nyuma yangu alihakikisha nafanya kila jambo linalotakiwa kwa usahihi.

Baada ya kupokea kipande cha nyama nilikaa pembeni nikisubiri kuelekezwa ijapokua nilijua kabisa kinachofuata ni kula nyama ile ya binadamu mwenzangu.

Je nini kilifuata
 
GoPPiii.
 
Duh hii ni balaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…